STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL:
thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
SONGA NAYO................
Jambo hilo ndilo lilimfanya usiku huo huo kusafiri mpaka Kibaha Maili moja, huko ndiko alifanikiwa kumficha mzee Hasheem huku akimpatia walinzi na wafanyakazi wa kike warembo ambao muda wote walihakikisha mzee huyo anapata kile ambacho anakihitaji. Ulikuwa ni usiku mzito lakini alihitaji mzee huyo aamshwe, jambo ambalo alikuwa nalo lisingeweza kusubiri mpaka asubuhi ndipo waongee ilikuwa ni mhumu wamalizane nalo muda huo kabla mambo hayajaanza kuwa magumu zaidi.
“Unanisumbua na usiku saivi wakati unajua kabisa nilikuwa nateseka kulala kule gerezani na wakati huu natakiwa kufidia yale mateso” alifoka mzee huyo akiwa anajifunga vizuri nguo yake ya kulalia akiwa anaisogelea meza ambayo ilitakiwa kutumika kwa ajili ya kufanyia mazungumzo.
“Jambo ambalo limenileta hapa sio la kulala”
“Ni wewe umemuua mke wa raisi?”
“Ndiyo”
“Alikupa nani hiyo kazi?”
“Aurelia”
“Kuna jambo gani ambalo linakupa hofu kiasi kwamba unatekeleza kile ambacho anakuagiza yeye?”
“Sipo hapa kuanza kukupa mambo yangu binafsi mzee na unalijua hilo”
“Nakusikiliza”
“Leo raisi alienda kumtisha Aurelia na baadae nadhani alituma watu kwa ajili ya kwenda kumuua” mzee huyo alisikitika kidogo.
“Ni raisi ndo kafanya hivi?”
“Ndiyo”
“Na kimetokea nini?”
“Mimi nimerudi usiku huu ili nimwambie nimeifanya kazi yake kwa usahihi lakini sijampata ndipo nikakutana na matatizo kwenye ile nyumba yake”
“Mmepoteza vijana wangapi?”
“Wewe unajuaje kama tumepoteza vijana?”
“Hakuna mtu anaweza kumgusa yule mwanamke Gavin akiwa mzima wa afya kwa sababu anaweza kuua kila mtu”
“Wamekufa tisa na mmoja ambaye ni mlinzi mkuu wa raisi yupo kwenye hali mbaya sana anaonekana amemuacha makusudi kabisa”
“Kwamba raisi amemtuma mlinzi wake eneo lile?”
“Ndiyo”
“Hivi hawa viongozi wananchi huwa wanawachaguaje? Kiongozi gani hana hata uwezo wa kufikiria mara mbili kabla ya kutumia mihemko kufanya maamuzi ya kipuuzi namna hiyo?”
“Kwa hilo sijui mwisho wa siku ndiye bosi wetu hatuna namna, mimi kuna mambo nataka kuyafahamu sina muda wa kusubiri, tunako elekea haya mambo yanaenda kuwa mabaya sana”
“Kwanza anayetakiwa kujiwazia sana kwa sasa ni huyo raisi wako kwa sababu Gavin hawezi kuacha hili lipite, hakuna mtu aliyewahi kumtishia mama yake akamuacha akiwa hai. Mlitakiwa kutumia zaidi akili bwana Savato na tunako elekea ni kwamba unanihitaji sana nikiwa hai kwa sababu sikuoni ukiwa na maisha marefu huko mbele”
“Nataka kujua kwamba Gavin haya mambo anayafanya mwenyewe au kuna watu wengine nyuma yake? Kwa mpangilio wa matukio ni kama inashindikana kabisa kimahesabu kuyatekeleza kwa wakati mmoja”
“Oooh usiniambie umekuja hapa kuhitaji nikumalizie simulizi ya maisha yake”
“Hiyo ndiyo sababu nipo hapa, najua unahisi kwamba naweza kuyabeba maisha yako lakini kwa sasa siwezi kwa sababu naona kabisa wewe ndiye akili yangu ya mwisho iliyo bakia na wewe ndiye unaweza kuwa msaada mkubwa kwangu kuliko mtu yeyote yule hivyo naomba sana unimalizie maelezo ya maisha yake ili niweze kutembua kwamba ni sehemu ipi ambayo inabakia wazi ili nianze kubeba tahadhari mapema”
“Gavin hayupo mwenyewe, kuna vijana wake ambao anafanya nao kazi na mmoja miongoni mwao ndiye mlinzi wa mama yake. Wakati raisi anaenda kwake leo mmewakuta walinzi wangapi?”
“Tumemkuta mmoja mbaye alitufungulia geti, ila mwingine alijitokeza baadae baada ya raisi kumnyooshea bastola mama huyo naye bila uoga akamnyooshea bastola raisi”
“Unaona kosa ambalo mmelifanya bwana Savato?”
“Kivipi?”
“Ukiwa vitani usidharau watu, siku zote watu hatari ni wale ambao huwa wanaonekana wa kawaida mbele ya macho ya wajinga”
“Unamaanisha nini kusema hivyo?”
“Unamkumbuka huyo mmoja ambaye unasema kwamba aliwafungulia geti?”
“Ndiyo”
“Alibeba silaha gani kwenye mkono wake?”
“Kama sikosei ni gobole lile”
“Yule ndiye mlinzi wake”
“Hapana, ni kijana wa kawaida yule tena mfungua geti na hata kama angekuwa hivyo basi asingekuwa anatumia silaha ya kipuuzi namna ile kumlinda yule mama”
“Mhhhhhhh nina uhakika haujui hata kile ambacho unakizungumza wewe, hivi kwa akili yako unahisi kwamba Gavin ni mpuuzi kumuacha yule mwanamke kuishi kwenye mazingira kama yale bila kuwa na uhakika na usalama wake? Yule ndiye mwanamke ambaye amemlea yeye hivyo hawezi kuruhusu mtu kumgusa kijinga kama ambavyo unafikiria wewe ila mwanamke yule amewekwa pale kama chambo kwenye safari ya kumtafuta mtu ambaye alitoa amri ya ile familia kuuawa na kama jina lako limefika kwenye mikono ya Luca kwamba nawewe ulihusika basi fanya ambalo unaliweza kuhakikisha kwamba anakufa kabla hajakufikia au uwe na majibu mazuri ya kumpa na kumshawishi aweze kukuacha hai” mzee Hasheem baada ya kuongea alitoa tablet ambayo ilikuwa kwenye droo kwenye meza hiyo na kuifungua video moja huku mkuu wa majeshi akiwa makini kumsikiliza;
“Huyu ndiye kijana ambaye wewe mwenyewe uliniambia kwamba pekeyake alimvamia waziri wa mambo ya ndani tena mchana wa juakali, kwenye hiyo video ukiangalia unaona kabisa kwamba hata hauna kabisa vijana wenye uwezo wa namna hii. Huyu Othman chunga ni miongoni mwa vijana wake na huyu ndiye huwa anawaongoza Gavin anapokuwa mbali kwahiyo huyo ambaye unasema kwamba alilegea mlangoni ndiye mwenzake na huyu Othman sasa umepata picha aina ya watu ambao unaingia nao vitani bwana mkubwa”
“Wapo wangapi wa namna hii”
“Mimi binafsi sijui kwa sasa kwa sababu ni muda sijapata taarifa zao”
“Sasa umejuaje kwamba huyo kijana wa getini ndiye alikuwa yeye?”
“Wakati mnaondoka hapo ulimuona tena?”
“Hapana, wakati tunaingia ndiye alifungua geti ila wakati wa kuondoka hakuwepo”
“Unahisi kwanini?”
“Alikuwa anasubiri mfanye kosa moja tu awaibukie kwenye uhalisia wake, wanavaa nguo nyeusi kama maninja na ndio utambulisho wao mkubwa lakini kiongozi wao huwa ana utofauti kwenye kufanya matukio yake kwa sababu yeye ana shilingi ambayo ndiyo utambulisho wake lakini ukiacha shilingi aina ya mauaji ambayo yeye huwa anayafanya ni tofauti”
“Bado haujanijibu kwamba umefahamje kwamba wa getini ndiye alikuwa mlinzi wake”
“Huwa wanafanya hivyo, kuna mtu mmoja ambaye huwa wanaamini kwamba hata maadui wakifika hawatamzingatia kwa namna anavyo jiweka kwahiyo ukifanya kosa tu anaondoka na maisha yako ndiyo maana ulivyo nielekeza tu nikajua huyo ndiye kwa sababu siku zote huwa wanafanya hivyo”
“Na unajua wanako patikana?”
“Wapo kila sehemu bwana Savato hata kwako watafika ni suala la muda tu”
“Ebu naomba tuanzie tulipo ishia wakati tupo ndani ya gereza”
“Wapi unataka tuanzie?”
“Baada ya kuzaliwa kwa wale mapacha ndipo tuliishia, nahitaji kujua kile kitu kwamba ni kwanini ilikuwa vile, kwanini ilifanyika siri na baadae hao mapacha waliishi vipi mpaka kutuletea huu muunganiko wa Gavin Luca”
“Unataka kuniua baada ya hapa?”
“Naonekana kama nipo hapa ili kuuua?”
“Sikuamini”
“Ningeweza kukutesa ukaniambia kwa ulazima, hivyo mpaka nakuja hapa ili tuongee kistaarabu ujue kabisa nakuhitaji. Mtu ambaye alinipa maagizo ya kukutafuta wewe mpaka sasa anajua kabisa kwamba umekufa jambo ambalo ni hatari kwangu siku akigundua kwamba upo hai lakini nakuweka hai kwa sababu naona tunaweza kufanya kazi siku za hapo mbeleni natakiwa kujitengenezea njia yangu kwa sababu nahisi hawa wote yakinifika kichwani sitawaona tena” mzee Hasheem alihema ili kuendelea na simulizi ya maisha ya mwanaume wa kuitwa Gavin.
“Kuzaliwa kwa wale watoto kuliongeza furaha kubwa lakini pia kulileta majukumu mapya kwenye familia kwa sababu Lucas alitakiwa kuanza kuangalia pande mbili za shilingi, moja ilikuwa ni pande yake yeye lakini upande mwingine ulikuwa ni kwa ajili ya familia yake. Kumbuka bwana yule hakuwa na maelewano mazuri na baadhi ya watu na alijua kabisa biashara yake ilimpatia maadui wengi kila kona wengine wakiwa viongozi wa serikali ambao hawakuwa upande wake hivyo alijua kwamba kuna siku ingekuja kufika mambo yangeenda vibaya ndiyo maana akataka kujiandaa mapema.
Aliamini siku moja familia yake ingekuja kuingia kwenye matatizo makubwa ndiyo maana kwanza hakutaka kabisa mkewe aweze kufahamika kwa watu kumlinda yeye pamoja na mkwewe ambaye alikuwa waziri mkuu bwana Hassan hivyo kwa ajili ya kulinda hilo akaamua kuwatenganisha watoto hao wawili. Sasa alitakiwa kuwatenganishaje? Ndipo hapa ulikuja mpango wa pili wa kumpata mama mlezi wa mtoto mmoja na jina ambalo lilitua mezani lilikuwa ni jina la Aurelia Vicent ambaye alikuwa kanali wa jeshi kipindi kile.
Sehemu ya arobaini na moja inafika tamati.
FEBIANI BABUYA.