Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Kuna kitu kimoja ambacho nadhani watu wote ambao washapanda mlima kilimanjaro na kufika uhuru height lazima tukubaliane.Huu mlima unakupa sense of accomplishment kiasi kwamba unahisi hamna kitu kinachoweza kua kigumu kwako maishani.katika vitu ambavyo proud ni hiki cheti nlichopata aisee..ndo maana mwezi wa 5 nataka panda tena


Na hiyo ndio sababu kuu ilinifanya nichukue maamuzi ya kupanda huo mlima. Kama ntaweza kupanda, ntaweza kufanya jambo lolote hata liwe gumu ntapambana nalo tu. Ilifika mahali nikachoka sana, nikasema nikirudi bila kufika kwenye kilele cha mlima, ntasingizia kitu gani sasa, siumwi, kama ni uchovu wote tunaupata, nikajipa moyo kuendelea na safari.
 
Eh eh maguide huwa wanabebaga sana madem wa kizungu ..,,,kwe hizo emotional distress nakumbuka mi nlimtoa sana jamaa nliekuanaye mpunga tuliposhuka
 
Mi nilipanda 2013 nikapata na cheti kabisa njia ya marangu nlikua nafanya field kinapa..ule mlima kinachowaua watu ni change of altitude hautaki harakaharaka mwili unaweza shindwa stahimili..ila ni mlima hata mtu wa miaka 12 anapanda..nmepanga nipande tena mwezi wa nne Mungu saidia
Hivi kuna rekodi wanakufa wapajdaji wangapi kwa mwaka?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee nlifika gilmans point..naambiwa hamna mhindi ashawahi papita nshachoka mbaya kama napanda ngazi ghorofa ya 100 dah ila guide na zile energy drink zilikua zinanipa nguvu kama popeye yaani..ukipiga maenergy na glucose unasimama mbele hatua kadhaa nguvu imekata dah...ila nlifika aisee...toka hapo sijawahi ogopa assignment kwe maisha hadi ofisin hawanielewi...mi kila kazi lete tu
Na hiyo ndio sababu kuu ilinifanya nichukue maamuzi ya kupanda huo mlima. Kama ntaweza kupanda, ntaweza kufanya jambo lolote hata liwe gumu ntapambana nalo tu. Ilifika mahali nikachoka sana, nikasema nikirudi bila kufika kwenye kilele cha mlima, ntasingizia kitu gani sasa, siumwi, kama ni uchovu wote tunaupata, nikajipa moyo kuendelea na safari.
 
SAFARI YA ZEBRA ROCKS - ACCLIMATIZATION DAY

078fa31d626341b788a6ee01e95ef626.jpg


Hapa tunakaa one day kwa ajili ya Acclimatization. Sijui kiswahili wanasemaje. Ukipita njia ya Marangu lazima uwe na siku moja ya kukaa hapo ili kuzoea hali ya hewa ya mlimani.. hii pia wanasema inaongeza chance ya kufika summit

Asubuhi nikawa fresh sio kama yule mtu nilikua naumwa usiku. Tangu tuanze safari hii ndio siku naingia kuoga.. Kuna baridi saana yaani maji yanatoka katika bomba ila yanaganda na kuwa barafu.. ila niliona bora kuoga. Kama huogi unajisafisha na wet wipes ama wet towels na kubadili nguo tu.


NAKUMBUKA ilikua birthday wa mmoja wa crew yetu wale ma guide walifanya suprise ya cake, wakaimba nyimbo zao fresh saana, mimi mwenyewe nikawa mmoja wa waimbaji baada ya breakfast mood ikawa zero kabisaa, nikaenda kuongea na guide mkuu akanambia nisiwe na wasi wasi I will be okay. machozi yakaanza kunilenga lenga Mim nikaona kama hanitendei haki ataniambiaje niko sawa wakati mimi namwambia naumwa.

DIAMOX:Hizi ni dawa tulishauriwa kununua zinasaidia kama mtu ukipata altitude sickness na mimi kwa vile nilivyokua najisikia nikazinywa kwa mara ya kwanza.

I was so emotional and sensitive..nikapanda juu tunakolaa nikaanza kulia, ila nalia sitak mtu ajue kama nalia.. Ilivyoanza safari ya Zebra Rock nikawa wa mwisho kabisa kutoka hapo niko na FRED.. Mtu akiniongelesha ndio nahisi nipaze sauti nilieee .. Nilitembea kidogo then nikakaa katika jiwe nikaanza kulia.. Fred na porter mwingine wamesimama pembeni yangu kimya wananiacha tu nilie.. Nikaliaaa weee hapo nikawa nalia kwa sauti... hiyo point pia kuna network nikaomba simu nipige.. Nikawaza kumpigia Baby huo muda hatukua vizuri I was like what if asipokee au apokee asiniambie maneno ya kunifariji ninayotaka. Sikumpigia. I called kiwatengu maana yeye ndio alikua kama guide wangu mkubwa katika safari hii. Alipopokea tu sim aka notice kuwa nalia.. Akaanza kunishauriii wee akanipa moyoo... Ikanisaidia kiasi chake.

Tulienda Zebra rocks na kurudi Horombo. Ni kama 4500m kufika. Kufika kule nikawa poa kabisa kama sio yule niliekua nalia huko chini.. nikajumuika na watu na pia nikapanga mawe kule. Ukitembea Zebra Rocks pembezoni watu wamepanga Mawe na hawashauri kupangua hayo mawe if you want unaweza kupanga ya kwako.

One thing nili notice watu wengi tulikua tunapata emotional break down bila sababu ya msingi.. sio mimi tu nilililia kuwa wengine pia.. na kila mtu alikua na namna alivyo i handle.




Sent from my iPhone using JamiiForums
Kwa nini wanapanga mawe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilitoboa japo kwa taabu sana, nilipofika kituo cha stella whether ikanigomea kabisa nikashauriwa kurudi....
Jiwe la kubusu sitalisahau, nilimkumbuka mtoto wangu wa miaka minne niliyemuacha home chozi likanitoka[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
Pole sana, mimi nilipitia Umbwe route ila nilipofika Barranco Camp uzalendo ukanishinda na nilibakiza vituo viwil tu yaani Karanga camp na Barafu Hut.... [emoji1482][emoji1482]
 
tupe stori mkuu hilo jiwe la kubusu ndo likoje, ukifika unalibusu au ndo nini?
Yaani Kuna mahali unafika huko juu njia imebana na unapita sehemu ambayo unapiga mgongo korongo na unakumbatia jiwe au mwamba ili uweze kupita hiyo sehemu ....hii nilihadisiwa na guide japo sijapanda huo mdude

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
Pole sana, mimi nilipitia Umbwe route ila nilipofika Barranco Camp uzalendo ukanishinda na nilibakiza vituo viwil tu yaani Karanga camp na Barafu Hut.... [emoji1482][emoji1482]
Barafu mkifika hiyo saa kumi kumi na moja mnakula then mnaambiwa mlale, safari ya summit inaanza saa tano usiku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom