Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Mlipita njiani laini sana....marangu! Hongera kwa kukuza jiografia yako.......
Mie nilishapanda kwa kupitia njia machame

Sent using Jamii Forums mobile app

Njia ya Machame sina hamu nayo kabisa, vyoo vibovu, mnalala kwenye mahema tu, hakuna kuoga, mnajifuta na tishu tu zile za watoto (Whipes). Mnatumia siku nyingi kuliko wanaopita Marangu.

Uzuri wa kule mambo ya jinsia hayana nafasi, tofauti kati ya mwanamke na mwanaume haipo. Mnaweza kulala hema moja na mwanamke wala usiwe na habari kabisa.
 
Kwa hio Kasie mpaka umri huo ulionao haujawahi kufika kileleni?

Sent from my GT-P5200 using Tapatalk

Wewe umewahi??
Mi nilipanda 2013 nikapata na cheti kabisa njia ya marangu nlikua nafanya field kinapa..ule mlima kinachowaua watu ni change of altitude hautaki harakaharaka mwili unaweza shindwa stahimili..ila ni mlima hata mtu wa miaka 12 anapanda..nmepanga nipande tena mwezi wa nne Mungu saidia

READERS ARE LEADERS

Safi sana, nikutakie kila la kheri kwenye safari ijayo. Mie sijapanga bado....
 
MY JOURNEY TO THE ROOF OF AFRICA

Kabla ya mwaka kuisha napenda ku share na nyie experience yangu ya kupanda mlima Kilimanjaro nitaambatanisha baadhi ya picha na video za safari yangu yote. Kama kuna watu wamewahi kupanda Mlima Kilimanjaro wanaweza ku share pia uzoefu wao.


Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails.. Kundi letu tulikua 21, Njia niliyotumia ni MARANGU.. Cost ilikua ni 560$ hii ili include kila kituu.. kuanzia usafiri Dar-Moshi Dar, chakula, hoteli.. vifaa.. fees za getini... personal guides... etc etc.. gharama zinapungua kutokana na huduma unayohitaji..

c449ae42b836bcda5f243c52a04c237b.jpg


MAANDALIZI YA SAFARI.

Baada ya ku confirm ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro. Jambo la kwanza nilifanya Medical check up.. nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni... Nikaanza mazoezi nakimbia uwanja nazunguka mara 7-10. Mazoezi ya kupandisha ngazi wanaojua jengo la UHURU HEIGHTS.. Nimepanda na kushuka hizo ngazi saana.. Pia tulikua tunafanya SEA CLIFF WALK haya yalikua matembezi kutoka Upanga hadi Sea cliff kwenda na kurudi kila jumamosi Kwa mwezi mara mbili. Kim beach kigamboni kutembea katika michanga Etc etc.

Pia nilijisajili na kitengo cha Flying Doctors Africa wako chini ya Amref.. wanatoa huduma ya helicopter kwa ajili ya ku rescue mlimani incase of emergency. Kusema ukweli nilikua muoga saana kwa sababu ya stories unazosikia so ilikua ni tahadhari maana ilikua ndio first time kupanda mlima.. & you never know nini kitatokea huko juu milimani. Fee ni 50$ kwa mtu mzima.

Nilisoma kila habari kuhusu kilimajaro na kupanda Mlima.. vifo vinavyotokea.. risk ukiwa mlimani..


KUPANDA MLIMA ULUGURU:Uluguru height ni kama 8600ft na hii ilikua ni moja ya majaribio kabla ya kupanda Mlima... Uluguru was the easiest tulienda Ijumaa.. Jumamosi tukapanda Mlima... Jumapili tukarudi Dar.. Mandhari ya Uluguru ni bomba sana...Kuna memories nyingi ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls...... Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale.. Nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikua siwezi. I wonder kwanini SUA hawarekebishi.

Tent tulizotumia kulala
181393d9af06585dd377fcf76f9b607e.jpg



Hii ndio camp kunaitwa Morning Site..tulikofikia.. humo kuna chata za watu wengi

e388057a293813c80ee7f191631c286c.jpg


The View
16bc00a84e515adb383cf530a5c579ce.jpg


3f673959c9f79e081a5f7c6109e53c62.jpg



Nitaendelea Next post.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Hongera mrembo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njia ya Machame sina hamu nayo kabisa, vyoo vibovu, mnalala kwenye mahema tu, hakuna kuoga, mnajifuta na tishu tu zile za watoto (Whipes). Mnatumia siku nyingi kuliko wanaopita Marangu.

Uzuri wa kule mambo ya jinsia hayana nafasi, tofauti kati ya mwanamke na mwanaume haipo. Mnaweza kulala hema moja na mwanamke wala usiwe na habari kabisa.

Aahahahahahahahhahaaaa looh.
Mnakuwa kama mpo bustani ya eden.
 
Njia ya Machame sina hamu nayo kabisa, vyoo vibovu, mnalala kwenye mahema tu, hakuna kuoga, mnajifuta na tishu tu zile za watoto (Whipes). Mnatumia siku nyingi kuliko wanaopita Marangu.

Uzuri wa kule mambo ya jinsia hayana nafasi, tofauti kati ya mwanamke na mwanaume haipo. Mnaweza kulala hema moja na mwanamke wala usiwe na habari kabisa.
Ahahahaha, machame kiboko bana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi na wanangu tulifanikiwa kupanda milima mitatu ya pale Kibondo,.... Twabagondozi, Nabuhima na Nengo 😀😀. Yote hiyo Nengo Kiboko kwani umechongoka na ni hatari😡, Nawapongeza mabinti zangu kwa kufanikiwa kupanda milima yote😉😉 ingawa hatukupewa vyeti na mtu yeyote😛😛.
 
Nimepanda huo mlima zaidi ya mara tano (5) wengi wa wanaobabuka ngozi zao zinakuwa zimeathirika kwa namna moja ama nyingine, mfano wanaojichuna ngozi n.k
.
KINAPA hawashauri mwendo wa haraka hapa ndipo tulipokuwa tunakosana nataka niende haraka nikitembe taratibu nitachoka, ilifikia wakati nikagombana na tour guides sijawahi kurudi tena.
.
Mwanamke atembee taratibu na kila Stopping center tupumzike huu ujinga ulinishinda, mara mia Mt Margarita Uganda fanya unachoweza.

Sio kweli wanaobabuka ni kujichubua..wengi asubuh wanataka nawa maji ya moto..tatizo kule hewa inamgandamizo so boiking point kubwa ..unaweza ona maji ya baridi kumbe kama kunyonyoa kuku...kuhusu polepole..mi nlivyopanda tulipata case mzungu kufariki....ile haraka mapafu yanashindwa stahimili na ukisema ukae chini ile baridi ikiingia kwe mapafu shida especially kutoka horombo to mandara to gilmans point,.,,anayejua zaidi anaweza jazia
 
Ahahahaha, machame kiboko bana

Sent using Jamii Forums mobile app

Ukitaka ufaidi, fuata taratibu zao tu, hata kama unajisikia bado una nguvu, usiongeze mwendo, nenda taraibu kwa kasi ile ile.
Tulipofika Lava Tower ndio tumbo lilianza kuvuruga na kukumbuka kwamba chakula kikiingia kinatakiwa kitoke kwenye mwili.

Vile vile siku ya mwisho inabidi kujitahidi kupata chakula cha kutosha, hata kama haujisikii kula na mara zote hamu ya kula inakosekana kabisa. Ile ni siku ngumu kuliko zote. Mnaanza safari saa tano usiku, mtafika kileleni kwenye saa mbili asubuhi (kutokana na ukubwa wa kundi lenu). Mkifika huko mnaanza kushuka hadi pale mlipolala, mnakula na kuanza safari ya kuja kulala kituo cha chini. Unaweza kuona siku nzima ni harakati tupu.

Lakini pamoja na shida zote, asikudanganye mtu, kileleni kuzuri sana. Ukifika unasahau shida na taabu zote. Nilichukua JIWE kule juu kama kumbu kumbu, lakini lile JIWE liko tofauti na Jiwe la Dar es Salaam.
 
Sio kweli wanaobabuka ni kujichubua..wengi asubuh wanataka nawa maji ya moto..tatizo kule hewa inamgandamizo so boiking point kubwa ..unaweza ona maji ya baridi kumbe kama kunyonyoa kuku...kuhusu polepole..mi nlivyopanda tulipata case mzungu kufariki....ile haraka mapafu yanashindwa stahimili na ukisema ukae chini ile baridi ikiingia kwe mapafu shida especially kutoka horombo to mandara to gilmans point,.,,anayejua zaidi anaweza jazia

Tulifika sehem (Tulitumia njia ya Machame) wakasema Mlima umepumua, unatoa gesi flani inaumiza vichwa sana, watu wengi wanakua na hali mbaya kuliko maelezo. Kuna mzungu kidogo amalize mitungi yote ya oxygen. Alishushwa kwa machela hadi chini.

Ila wale wagumu hawana mapafu ya kawaida. Kule sio kwa kuishi au kufanya kazi muda mwingi.
 
Sio kweli wanaobabuka ni kujichubua..wengi asubuh wanataka nawa maji ya moto..tatizo kule hewa inamgandamizo so boiking point kubwa ..unaweza ona maji ya baridi kumbe kama kunyonyoa kuku...kuhusu polepole..mi nlivyopanda tulipata case mzungu kufariki....ile haraka mapafu yanashindwa stahimili na ukisema ukae chini ile baridi ikiingia kwe mapafu shida especially kutoka horombo to mandara to gilmans point,.,,anayejua zaidi anaweza jazia
Nimesema "Mfano" ili nipate kueleweka na sio sababu ya moja kwa moja inayosababisha hilo tatizo.
 
Nmepanda sana mlima kama porter kuanzia miaka ya 2005...nmepita Machame Route na Rongai ila sikuwahi kupanda na mbongo kama mtalii
Nakumbuka siku moja tukiwa school tulitoroka tukadakwa na askari, kipindi hicho kuna watu walikuwa wanaenda kuvuna asali mlimani, wakawasha moto ule moto ukawazidi wale wavunaji na asali wakakimbia moto ukawa mkubwa sana, vijana wengi walio kuwa mtaani bila kazi walikamatwa na askari tukapandishwa mlimani kwenda kuzima moto aisee, kuna raia walikuwa balaa, tulipitia njia ya rongai, sijui kama hadi sasa hvi bado wanawasha moto
 
Tulifika sehem (Tulitumia njia ya Machame) wakasema Mlima umepumua, unatoa gesi flani inaumiza vichwa sana, watu wengi wanakua na hali mbaya kuliko maelezo. Kuna mzungu kidogo amalize mitungi yote ya oxygen. Alishushwa kwa machela hadi chini.

Ila wale wagumu hawana mapafu ya kawaida. Kule sio kwa kuishi au kufanya kazi muda mwingi.
Ukifanya kazi za milimani mda mrefu, ukifikisha miaka 55 kwenda juu ndiyo utaanza kuona madhara yake, joint za viungo vya mwili vinaanza kufail kufanya kazi
 
Back
Top Bottom