Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Kabisa uzi huu umetupa picha kamili ya huko maana nilikuwa nasikia tu watu "WANAKATA MOTO aka KURUDISHA NAMBA" wakiwa wanapanda mlima klm nikawa najuliza maswali mengi why wakate moto? Kumbe sio mchezo lazima upate ABCs za huku sio kuenda kichwa kichwa mwanangu(In Bishop Maboya's voice)

Watch "Climbing Kilimanjaro: Tips & Tricks" on YouTube


Nafikiri hiyo itatusaidia tunapofanya maandalizi.
Ila imesheheni na ni ndefu. 1 hour.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana Heaven on Earth kwa simulizi yako nzuri inayohamasisha.

Nimeishi moshi kwa karibu miaka 5 hivi, sikuwahi kuhamasika kuhusu kupanda mlima kama ilivyotokea kwa simulizi yako. Zaidi ilikua tukipata videm basi marangu falls.

Moshi nilikua na marafiki maporters, madereva na mpaka jamaa mwenye ubia na kampuni ya tours. Sikuwahi kuhamasika kama leo hadi nimeshinda YouTube kusakanya details. Very fun.

Nilichogundua wenyeji wengi wa maeneo husika huambukizwa kimazingira na kujiona na wao ni sehemu ya wamiliki au wafanyakazi au wenyeji wa eneo. Hivyo wao hawahusiki zaidi ya wanaopaswa kwenda huko ni wageni nje ya moshi (something kama washamba au wakuja)

Hii ni sawa na mtu wa mtwara kumkuta anahangaika kutafuta korosho au mwanza mtu anachanganyikiwa na sangara.

Nafikiri mamlaka husika zinatakiwa zibadirishe namna ya kutangaza utalii hapa ndani. Iwe kwa video na story zaidi kwenye mikusanyiko ya watu ili watamani kama ulivyotutamanisha.

Asante sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilimanjaro hiking ni more than experience. Nilipanda August 2018 na tukalala kilimanjaro crater. Nikiwa mlimani niliulizwa utapanda tena nikajibu never. Kwa sasa natamani kupanda tena na tena ingawa kucha zangu za vidole gumba vya miguu ziling'oka kwasababu ya mlima

Natamani kila mtu apande Kilimanjaro

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana Heaven on Earth kwa simulizi yako nzuri inayohamasisha.

Nimeishi moshi kwa karibu miaka 5 hivi, sikuwahi kuhamasika kuhusu kupanda mlima kama ilivyotokea kwa simulizi yako. Zaidi ilikua tukipata videm basi marangu falls.

Moshi nilikua na marafiki maporters, madereva na mpaka jamaa mwenye ubia na kampuni ya tours. Sikuwahi kuhamasika kama leo hadi nimeshinda YouTube kusakanya details. Very fun.

Nilichogundua wenyeji wengi wa maeneo husika huambukizwa kimazingira na kujiona na wao ni sehemu ya wamiliki au wafanyakazi au wenyeji wa eneo. Hivyo wao hawahusiki zaidi ya wanaopaswa kwenda huko ni wageni nje ya moshi (something kama washamba au wakuja)

Hii ni sawa na mtu wa mtwara kumkuta anahangaika kutafuta korosho au mwanza mtu anachanganyikiwa na sangara.

Nafikiri mamlaka husika zinatakiwa zibadirishe namna ya kutangaza utalii hapa ndani. Iwe kwa video na story zaidi kwenye mikusanyiko ya watu ili watamani kama ulivyotutamanisha.

Asante sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Another exciting video kwa wale ambao hatujafika. Muone "breakfast" na "kissing stone" kama wadau walivyosimulia

Watch "What is it really like to climb Kilimanjaro? (Lemosho route) - Follow Alice" on YouTube


Enjoy!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilimanjaro hiking ni more than experience. Nilipanda August 2018 na tukalala kilimanjaro crater. Nikiwa mlimani niliulizwa utapanda tena nikajibu never. Kwa sasa natamani kupanda tena na tena ingawa kucha zangu za vidole gumba vya miguu ziling'oka kwasababu ya mlima

Natamani kila mtu apande Kilimanjaro

Sent using Jamii Forums mobile app
Kung'oka kucha tena?? Arghhhhh.......

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kucha za vidole vya miguu ziling'ookaje? ulikuwa umevaa kandambili au? manake kabla ya kupanda mlima Kilimanjaro ni lazima ufanye preparation ya vitu vifuatavyo:
1.Viatu vigumu (Boots) lakini viwe vyepesi ili kukusaidia kutembea bila kuchoka.
2.Soksi pair 4 ndefu safi na nzito.
3.Mycotta powder.
4 Gloves safi zenye sufi ndani.
5.Jacket au pullover zito.
6.Boshori lile kofia la sweta linalofunika kichwa na kuacha sehemu ya macho tu.
7.Miwani nyeusi kupunguza mng'ao wa theluji.
7.Climbing stick
8.Kibuyu au chupa ya maji.
9.Back pack kwa ajili ya kuhifadhi vitu vidogo vidogo kama glucose,biscuits,juice n.k.
Hayo ndio mahitajio ya msingi unayotakiwa kuconsider kabla ya kuanza safari ya kupanda mlima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
STELLA POINT.
e43ceb86210e16086d81156551c61482.jpg


Nilivyofika Gilmans nilipata some sort ya relief.. Na kwa mimi nafikiria Gilmans was the hardest part. Watu wengi huwa wanaishia hapo anakosa nguvu ya kuendelea mbele. Wote katika group yetu tulipumzika then tukaanza safari ya kuelekea Stelle.

Njiani kulikua na barafu saana.. The wind is blowing hatari.. tulikua tunatembea juu ya barafu.. Problem nyingine ni kwamba tulikua hatuwezi kuonana kutokana na ukungu..Mtu yuko hatua tatu mbele ila huwezi kumuona kwasababu kuna ukungu wa kufa mtu. To be honest ilikua inatisha..

Shida inakuja kuwa hewa inakua ndogo saana. Nikaanza kuona hali tete kabla hatujafika...baada ya Masaa kadhaa tukafika Stella... Pale Kibaoni tukapiga picha haraka ili tuendelee mbele.

f88521fdd08c07bd253e06eb7726140c.jpg




Sim yangu haikuweza kuwaka.. We only took group photos

8539d6d4096127f29fe7bbc33369ec6e.jpg



UHURU PEAK.


Baada ya pale tukaanza kuitafuta Uhuru..Ambayo ni kama 30mints.. hizi dakika kuzitamka hapa unaona chache ila ukiwa kule juu ni kama mwaka...Yaani hali ya hewa ilikua mbaya saana. Nilikua nime sha give up nimechoka na nilikua sijielewi yaani natembea tu.. Sielewi kitu. Niliambiwa nilipata Hallucination..

Kuna baba mmoja mwanzoni niliwaambia kuwa yeye kapanda mara 18 ila alisema katika kipindi choote alichopanda hakuwahi kukutana na hali tuliyokutana nayo sisi kule juu. Storm inayopiga ni ya hatari..... Upepo unapiga mnakimbilia katika jiwe kubwa ili atleast upepo upungue kidogo ndio tuendelee mbele. Jamani nilikua kama naiona jehanam. It was life and death experience kule juu. Upepo ukivuma ukija hivi uso wote unafunikwa na barafu... Nilikuja kuambiwa baadae kuwa storm tuliyokutana nayo huko juu haijawahi kutokea for decades

Tukaanza kupotezana hapo.. Guide mkuu akasisitiza hali ni mbaya turudi tusiendelee mbele..kiongozi wetu anasema haiwezekani.. Mimi nilikua sielewi kitu siwezi kuongea nawatizama tu.... hata haya mengine nilikuja kuhadithiwa Yeye alikua anasisitiza hakuna mtu anarudi.... Yaani hapo hadi ulitokea ugomvi kati yetu na guide mkuu anaetuongoza. Storm ni ya hatari inapuliza mpaka unasikia jiwe kubwa linatikisika hapo nawaza hili jiwe si linaweza kubiringita hapa then litudondokee ndio iwe bye bye


I reached Uhuru Peak.. kufika summit was one of the best experiences of my life. The summit view was absolutely stunning and I don’t think any words could really give a justice... Unapaswa ushuhudie mwenyewe mtu asikuhadithie. Yaani nilisahau hata ile dhoruba tuliyokutana nayo...

Niliona mazoezi na jitihada zangu zimezaa matunda mwisho wa siku, I felt a sense of achievement kwa kutimiza kile ambacho nilijiwekea kwamba i want to STAND ON THE ROOF OF AFRICA. Nakumbuka nililia saana.... Nikiwa summit na pia wakati wa kurudi ni machozi ya furaha na relief. Mind you sisi hatukuchuka hata dakika pale juu tuligeuza muda ule ule kutokana na hali ya hewa.


4d30f6deb3d8dd89ae4b96c4086403f6.jpg


Group yetu wote hatukufanikiwa kukigusa kibao wala kupiga picha katika kile kibao.. Hii ni kutokana na barafu nyingi. Wote tulikubaliana as long as tumefika Peak hiyo inatosha... It was sad thing kutokupiga picha pale lakini pia ukifikiri ulikotoka na pale tulipofika unaona IT was okay

Nikipokea certificate yangu

daa9cf6211f80256f29dd4d894cd559b.jpg


Ukumbusho wa cheti.

f351a28485629dae51e0af9feaf946f6.jpg


Next post ya mwisho nitamalizia kushuka.
Nimefuatilia post zote pamoja na michango yote inayofikia 500.

Nimekuwa na hamu sana ya kuupanda huo mlima na nimefurahi mno kuona ushuhuda huu. Heaven on Earth Mwenyezi Mungu akubariki sana kwa ushuhuda huu.

Mipango yangu ni mwakani lazima nipande panapo uzima.

BTW, you are a good story teller. Nikikamilisha maandalizi ya kimwili (physical) ntahitaji ushauri wako pamoja na kiwatengu kuhusu tour guides na mambo yanayohusiana na hayo.

Cheers.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Interesting.....

-Ningependa kujua kuna njia ngapi(Routes) za kufika Kilele cha mlima kilimanjaro?

-Mwanzoni tulifundishwa Kibo na Mawenzi ndio vilele vya mlima kilimanjaro ila kwenye hii thread nimeona vilele zaidi ya 10 na kingine naambiwa Uhuru peak,Je Uhuru ndio Kibo au Mawenzi?

-Inachukua siku ngapi kwa kupanda hadi kufika kilele cha mlima k/njaro? Kwa Routes zote.

-Tupeni faida/changamoto za routes zote za kufika kwenye peaks.

-Gharama za kufika huko either personal au kutumia agents.

-Vitu gani vya kuzingatia ukitaka kwenda huko gears/facilities.

-Hali ya kiafya,je inatakiwa uwe katika situation gani ya kiafya ili usipate makandokando ya kufika peak,maana wamezungumzia afya general iwe nzuri,kwahiyo watu wenye HIV,pressure,kisukari etc hawewezi kuruhusiwa kwenda?
HIV sio ugonjwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom