Sinema sakata la LUGUMI: Mashine za utambuzi wa alama za vidole zaanza kufungwa kimya kimya

Mkuu unaambiwa Lugumi kapiga Dili Wizara nyingi tena huko kapiga pesa nyingi zaidi , lakini sasa wapo busy kuficha ushahidi wote hawataki ya kitwanga yawakute Majipu yapo mengi sana Nchi hii , hili ni JIPU gumu Kwa Magufuli Kama lilivyokuwa JIPU la kivuko feki, mabehewa chakavu ya Mwakyembe , Dau wa NSSF , IPTL , Chenji ya Bunge la katiba na ya Rada , pesa za NIDA nk , Haya Majipu Magufuli anayaogopa Kama Ukoma .
 
Kwa hiyo kila kelele zinazopigwa na UKAWA mnataka Rais azifanyie kazi? Toka lini UKAWA wakawa washauri wa Serikali?
Mkuu unaushabiki wa kijinga hata kwenye mambo ya kitaifa
 
Mkataba ulisainiwa mwaka 2011 leo ni 2016 je Mkataba unasemaje kuhusu ukomo wa ufungwaji wa hizo mashine
Kama wangekuwa serious ni kazi ya miezi 8 mpaka mwaka ina maana mwaka 2012 walipaswa wawe wamekabidhi kazi ,
 
Hii nchi raha Sana.Ukiwa mwizi wa mabilion unalindwa lakini mwizi wa kuku unachomwa moto.
Tatizo ni kuwa hizo adhabu ie. kuchoma moto vibaka wa kuiba kuku na mwizi wa mabilioni ziko tofauti. Hata "mahakama" zinazotoa hizo hukumu ni tofauti pia
 
Kwa hiyo kila kelele zinazopigwa na UKAWA mnataka Rais azifanyie kazi? Toka lini UKAWA wakawa washauri wa Serikali?
Bado unalala gheto Kwa Lugumi ? Njaa zitakua Wewe endelea kutetea wizi mpaka Laana zikunase .
 
Kama wangekuwa serious ni kazi ya miezi 8 mpaka mwaka ina maana mwaka 2012 walipaswa wawe wamekabidhi kazi ,
Tutajie vipengele vya Mkataba Baina ya Lugumi na Police juu ya ni lini haswa ukomo wa ufungwaji wa hizo mashine
 
Endeleeni kupiga makofi na kuimba mapimbio!
Umeishiwa kweli. Nini kwenda jikoni? Mbona kamati ipo kwa ajili yetu itatuletea taarifa tu. Toka 2012 hivyo vifaa vipo Dom vikisubiri mkongo wa taifa ufike ndipo ifungwe kwa matumizi.
 
Mtumbua majipu anajifanya hana taarifa!Ama kweli mungu hamfichi mnafiki!!
Acha upuuzi, Rais akichukua maamuzi nyumbu wa chadema mtakuja kulalamika hapa kuwa rais hafuati utaratibu wa kamati ya bunge..

Wazungusha mikono ni janga la taifa.
 
Hili jipu la kwapa ambalo halifichiki lazima ukitembea utatanua mikono hata kama umevaa koti lazima watu watajua.
La utosi angalau utavaa kofia. Hapa kazi tu ya kulindana hakuna lolote.
Hahahahaha la kwapa ni kiboko
 
Wezi wa kuku wanakutana na mob justice ila wezi wa mabilioni wanakutana na court justice
mkuu Lugumi yeye analindwa sana licha ya kupewa mapesa mengi kinyume na bei halisi bado wanabariki Uongo , Yaani anapita mda huu anafunga vifaa kwenye baadhi ya vituo kisha watakuja na maneno kuwa vilifingwa zamani tena vipo kwenye vituo vyote.
 
CCM ni ile ile Oooghh Ni ile ile Mawaziri Leo hawataki kuulizwa Maswali ya kipuuzi na kijinga.... Dharau hii
 
Acha upuuzi, Rais akichukua maamuzi nyumbu wa chadema mtakuja kulalamika hapa kuwa rais hafuati utaratibu wa kamati ya bunge..

Wazungusha mikono ni janga la taifa.
Nyumbu ni ccm ambao woote ni wanafurahia wizi wa pesa za umma kisha wanaterea wizi Kama Wewe, Nani kakuambia Rais hafuati kamati za Bunge? Kama angekuwa hafuatilii Kwa nini wanahaha Usiku na mchana kufunga mashine ? Zingine wanahama hama nazo wakisikia kamati inaenda huko wanapeleka mashine chapchap kamati ikipita wanaipeleka kamati itapokwenda.
 
Hahahahaha la kwapa ni kiboko
JIPU la Lugumi ni kubwa mpaka limezaa Majipu kibao mfano kitwanga , said mwema nk , na sasa kuna JIPU lingine wanalitengeneza bila kujua ni JIPU kubwa zaidi Yaani hii sinema ya kufunga mashine chapchap na Uchakachuaji wa nyaraka kule brela kumtoa kitwanga kinyemela kwenye kampuni ya infosys .
 
Kamati ya bunge italeta report bungeni..

Hicho kihelehele cha kumtaka rais achukue maamuzi unakitolea wapi.

Ndio maana mnaitwa kuku wa kizungu.
 
Wanasiasa ni watakatifu, watumishi ndiyo mashetani
 
Tutajie vipengele vya Mkataba Baina ya Lugumi na Police juu ya ni lini haswa ukomo wa ufungwaji wa hizo mashine
Mifumo hiyo kuifunga ni rahisi kinoma. Cha msingi ni networking tu ili mashine zote ziwe synchronised na server. Sasa siasa zenu za kihafidhina ndio zinafanya muwe munauliza idiotic questions.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…