Sipendezwi na jinsi inavyolazimishwa sasa CDF kuwa chini ya Waziri wa Ulinzi 'Kiprotokali' wakati Waziri wa Ulinzi ndiyo anapaswa kuwa chini ya CDF

Sipendezwi na jinsi inavyolazimishwa sasa CDF kuwa chini ya Waziri wa Ulinzi 'Kiprotokali' wakati Waziri wa Ulinzi ndiyo anapaswa kuwa chini ya CDF

Vijana msome katiba, mtu pekee ambae yupo juu ya CDF ni raisi wa nchi ambae ndie amiri jeshi mkuu
Mkuu Wewe unadhani GENTAMYCINE ninavyokuwa Nawadharau Wapumbavu wengi hapa kama huyo uliyemjibu hapo na Wenzake huwa nakosea?

Na cha Kusikitisha zaidi hao Wapumbavu wengi wamefikà hadi Vyuo Vikuu ila angalia walivyo Watupu Vichwani mwao.

Kama kwa hili tu la CDF limewashinda Kulijua na Kulielewa unadhani Mambo muhimu ya Nchi watayajua, watayaweza na wataweza kuwa na Tija ya Kimaendeleo ya Kulikomboa Taifa la Tanzania hasa Kiuchumi na Kijamii?
 
Hakuna Kitendo Kimenishangaza na Kimeniuma kama kuona Juzi CDF na Chief of Staff wake wakienda Kiunyonge na Kiuhuruma kwa Waziri wa Ulinzi Kujitambulisha.

Sijawahi kuona popote pale Waziri wa Ulinzi anakuwa Juu ya Jeshi tena Kiprotokali wakati Jeshi ni Serikali Kificho ya Kimedani na inayojitegemea na ambayo ikiamua muda wowote ule ichukue hatamu ya nchi inaweza na huyo ( huyu ) Waziri wa Ulinzi anakuwa si lolote wala si chochote.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Hayati Mkapa na kidogo Mzee Kikwete waliwaheshimu mno CDF's wa Vipindi vyao na walihakikisha hawalazimishi Jeshi kuwa ni sehemu ya Siasa na Utawala wa Kiserikali.

Hayati Rais Dkt. Magufuli alianza kwa mbaali kutaka Kummiliki CDF (japo alikumbana na Ugumu kidogo) kwakuwa CDF Mstaafu Mabeyo anajitambua na ameiva Kimedani (Kijeshi ) pamoja na Protokali zake zote.

Kama kuna Kitu kimenishangaza na naona HATARI fulani mbeleni huko ni kuona Awamu hii ya Rais Samia huyu Waziri wa Ulinzi Bi. Stegormena Tax akipewa Madaraka makubwa juu ya Jeshi na CDF wake kitu ambacho si Kizuri na siyo cha Kiutaratibu kabisa.

Kwa Kawaida ilitakiwa baada ya CDF Kuteuliwa basi Kiitifaki Waziri wa Ulinzi ndiyo alipaswa kwenda kwa CDF ila siyo CDF na Chief of Staff kwenda kwa Waziri wa Ulinzi huku wakiwa na Nyuso za Huruma kana kwamba Wameamrishwa na Mtu wakati Wao ndiyo wana Mandate ya Kuamrisha.

Namalizia kwa Kuwaasa na Kuwaonya enyi Watawala ( Wanasiasa ) kuwa chezeni na Vitu vyote ila msicheze na Taasisi Nyeti kama ya Jeshi na kutaka nao wawe Wanasiasa kama nyie wakati Kiuhalisia wao ni Wanamedani na wako kwa ajili ya Ulinzi na Usalama Uliotukuka wa Taifa letu hili la Tanzania.

Nichukieni, ila yafanyieni Kazi yote!!!
Sio kweli,mamlaka zote zinatakiwa kuwa chini ya supervision ya raia,
Waziri ni Mbunge,amechaguliwa na watu,Anawakilisha maslahi ya watu,anasimamia sera!CDF kachaguliwa na nani?
Na ulikuwepo utaratibu hata muhasibu wa jeshi anakuwa Raia,sio mwanajeshi!,akiwa mwanajeshi si atatii maagizo kwa kufata vyeo?
Majeshi yote yanatakiwa kulipoti kwa mamlaka za kiraia,wewe unataka jeshi lijipangie bajeti,matumizi,lijiamulie pesa kiasi gani likachukue hazina?
 
Kama hawajitambui watamilikiwa tu.
Kama umeteuliwa kimagumashi utamilikiwa tu.
Kitendo cha kuifanya TISS iwe kwenye ofisi ya rais ikakosa meno.
Hii nayo inatakiwa iwe independent organ. Kwa usalama wa nchi
 
Ni Imani yangu hao watu wa AMRI hawasomi mambo haya ya siasa.

Mungu ibariki Tanzania. Amen
 
Mkuu you are dead WRONG!
CDF siku zote yupo chini ya Waziri wake wa Ulinzi kiserikali.
Hii ni licha ha ukweli kwamba Waziri wa Ulinzi hana mamlaka wala madaraka ya kumuingilia CDF na jeshi kwa ujumla.
Waziri wa Ulinzi ni kama muwakilishi wa jeshi kiserikali ila hawezi kuliamrisha jeshi kwa aina yoyote.
Kiutendaji CDF yupo chini ya Commander in Chief moja kwa moja.

Waziri Maokola Majogo alijaribu kuliamrisha jeshi wakati fulani, cha moto alikipata, na akaondolewa unceremoniously uwaziri.
Mnajisumbua tu
 
Hii taasisi ya Jeshi ni ya kipekee inayotakiwa kuheshimiwa.
Jeshini kuna kila taaluma iliyoko uraiani kasoro taaluma ya Magereza japo wana jela zao. wana mahakama zao zinaitwa court martial kule hakimu ni mkuu wa kikosi na hakuna kujitetea wala wakili

Jeshinia wapo ma prof na ma dr wa phD.Ukitaka kujua jeshini kuna kila taalama kuna siku ma dr Muhimbili waligoma wanajeshi wakaenda kuchukua hatamu kusaidia maisha ya watu.Kuna siku waoongoza ndege waligoma wataalamu wa jeshi wakaenda uwanjana kukamata hatamu.
Jeshini kuna madaktari wa kutibu,wahasibu,walimu,ma injinia uwa umeme,majengo mechanical,chemicla nk wataalamu wa IT.Iddi Amini alivobomoa daraja la Kagera ma injinia wa Jeshi walijenga la muda kwa mda wa chini ya wiki moja kazi ikaendelea ingekuwa ma injia wa uraiani wa 10% lingechukua muda mrefu na Iddi Amini angeikalia Kagera vizuri zaidi.
Nchi ya Marekani na Urusi pia mambo makubwa ya kiutafiti yanafanywa na wanajeshi.Hata waliokuwa wanakwenda anga za mbali hadi mwezini walikuwa na wanajeshi kila Neil Armstrong huyu alikuwa ni profesa na mwanajeshi na alikuwa ndio mission commander ya kwenda mwezini.

Nimeona niongezee haya kuonyesha msisitizo taasisi hii ilivyo muhima sio taasisi ya kuchukuliwa ki spot spot kwa waziri ulinzi kupigiwa salute hapo sina objection ninachokataa mkuu wa wilaya eti CDF anampigia salute kisa tu eti ni mkuu wa ulinzi na usalama kwenye wilaya yake wakati CDF ni mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa maana changa vikorokoro vingine polisi,magereza,uhamiani, vyote yaya ndio mkuu.
Hili halijakaa sawa mkuu wa wilaya kupigiwa salute na CDF
Kwamba CDF ni mkuu wa majeshi yote ambayo ni Magereza,Polisi,Uhamiaji,Zimamoto,TISS au?Sijawahi kuona IGP akimpigia salute CDF au DGI akimpgia saluti CDF,hapo kuna mkanganyiko.
 
Kwamba CDF ni mkuu wa majeshi yote ambayo ni Magereza,Polisi,Uhamiaji,Zimamoto,TISS au?Sijawahi kuona IGP akimpigia salute CDF au DGI akimpgia saluti CDF,hapo kuna mkanganyiko.
Ni kwa sababu hujawahi kuona lakini utaratibu ndio uko hivyo kiprotokali majeshi yote yanamsalute CDF, Vivyo hivyo magereza na wengine wanamsalute IGP

Na ni sahihi kwamba CDF ni mkuu wa majeshi yote uliyoyataja kutia ndani bregade zake zote , ndio sababu anaitwa mkuu wa majeshi sio mkuu wa jeshi
 
Ni kwa sababu hujawahi kuona lakini utaratibu ndio uko hivyo kiprotokali majeshi yote yanamsalute CDF, Vivyo hivyo magereza na wengine wanamsalute IGP

Na ni sahihi kwamba CDF ni mkuu wa majeshi yote uliyoyataja kutia ndani bregade zake zote , ndio sababu anaitwa mkuu wa majeshi sio mkuu wa jeshi
Kwanini unapoteza muda na Nitwits?
 
Ni kwa sababu hujawahi kuona lakini utaratibu ndio uko hivyo kiprotokali majeshi yote yanamsalute CDF, Vivyo hivyo magereza na wengine wanamsalute IGP

Na ni sahihi kwamba CDF ni mkuu wa majeshi yote uliyoyataja kutia ndani bregade zake zote , ndio sababu anaitwa mkuu wa majeshi sio mkuu wa jeshi
Kwahiyo kwa kusema hivyo,CDF anaweza akatoa amri kwa IGP na akatii,wakati majukumu yao yako tofauti?
 
Kwahiyo kwa kusema hivyo,CDF anaweza akatoa amri kwa IGP na akatii,wakati majukumu yao yako tofauti?
Tofautisha jina Mkuu wa majeshi na mkuu wa jeshi la polisi.Natamani JKT irudi humu tunabishana na watu ambao hata ukimuambia apangilie vyeo vya JWTZ kuanzia private hadi General na mabegani anavaaa nini hawezi kukuambia kitu.
 
Hakuna Kitendo Kimenishangaza na Kimeniuma kama kuona Juzi CDF na Chief of Staff wake wakienda Kiunyonge na Kiuhuruma kwa Waziri wa Ulinzi Kujitambulisha.

Kumuweka CDF chini ya waziri wa ulinzi ni kuonesha kuwa mamlaka ni ya Raia na si jeshi, Kuonesha Jeshi ni chombo kinachotumika na Raia kwa maslahi yao. Jambo ambalo ni sawa kabisa, Serikali zote za kiraia zinafanya hivi.

Hii ni nchi yenye serikali inayoendeshwa kiraia, kwa maana wananchi ndiyo wenye mamlaka. Mamlaka yao yanawakilishwa na Rais aliyechaguliwa kwa ‘popular vote’.

Waziri wa Ulinzi anateuliwa na Rais (aliyechaguliwa na wananchi) kutoka Bungeni. Huko Bungeni amechaguliwa na wananchi au kuteuliwa na Rais.

Sijawahi kuona popote pale Waziri wa Ulinzi anakuwa Juu ya Jeshi tena Kiprotokali wakati Jeshi ni Serikali Kificho ya Kimedani na inayojitegemea na ambayo ikiamua muda wowote ule ichukue hatamu ya nchi inaweza na huyo ( huyu ) Waziri wa Ulinzi anakuwa si lolote wala si chochote.
Siyo kweli, USA, INDIA na URUSI nimetaja kwa uchache Wizara za Ulinzi ziko juu ya jeshi, kwa maana Jeshi hupokea maelekezo toka wizarani.

Kweli jeshi likitaka shika hatamu linaweza fanya hivyo mifano ni mingi.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Hayati Mkapa na kidogo Mzee Kikwete waliwaheshimu mno CDF's wa Vipindi vyao na walihakikisha hawalazimishi Jeshi kuwa ni sehemu ya Siasa na Utawala wa Kiserikali.
Siyo kweli, kwa Tanzania Jeshi limekuwa ni sehemu ya siasa na Utawala kwa kipindi cha Mwalimu, na Jeshi limeendelea kuwa sehemu ya Utawala kwa marais wote waliofuata.

Wakati wa Mwalimu, Ofisi za TANU zilipatikana mpaka kambini! Jeshi lilihimiza kudumu kwa fikra za mwenyekiti kila walipokusanyika.

Wakati wa Mwalimu na marais wengine bado watu kutoka jeshini wanapewa nafasi katika serikali, wanateuliwa kuwa Wakuu wa wilaya, Mikoa na wengine mabalozi.

Hii ina faida sana ktk kuboresha uhusiano wa Jeshi na Serikali na inatajwa kuwa moja ya mbinu inayozuia mapinduzi ndani ya Tanzania.

Mifano:
Balozi wa TZ nchini SA🇿🇦- Meja Gaudence Milanzi (mstaafu)
Aliyekuwa mwaka jana Balozi wa TZ nchini Misri 🇪🇬- Meja Anselm Shigongo (mstaafu)
Mkuu wa mkoa wa Kagera- Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti

Kama kuna Kitu kimenishangaza na naona HATARI fulani mbeleni huko ni kuona Awamu hii ya Rais Samia huyu Waziri wa Ulinzi Bi. Stegormena Tax akipewa Madaraka makubwa juu ya Jeshi na CDF wake kitu ambacho si Kizuri na siyo cha Kiutaratibu kabisa.

CDF ni lazima awe chini ya kiongozi wa kiraia. JESHI NI CHOMBO CHA WANANCHI, SI ‘PARALLEL GOVERNMENT’, hatuwezi kuwa na Dola ndani ya Dola.
JESHI linawajibu kwa Raia-wanaowakilishwa na Rais-anayemteua Waziri wa Ulinzi- anayetoka Bungeni!!

Na Mkurugenzi Mkuu wa TISS anawajibika moja kwa moja kwa Waziri wa Ulinzi.

Kwa Kawaida ilitakiwa baada ya CDF Kuteuliwa basi Kiitifaki Waziri wa Ulinzi ndiyo alipaswa kwenda kwa CDF ila siyo CDF na Chief of Staff kwenda kwa Waziri wa Ulinzi huku wakiwa na Nyuso za Huruma kana kwamba Wameamrishwa na Mtu wakati Wao ndiyo wana Mandate ya Kuamrisha.

Hiki kikitokea jua wazi tunapoteza serikali ya Kiraia. Jeshi litashika hatamu ktk ‘scenario’ mbili tu.

1. Wakati wa dharura (State of Emergency)

2. Wakipindua serikali, hii ni kinyume na katiba.
 
Tofautisha jina Mkuu wa majeshi na mkuu wa jeshi la polisi.Natamani JKT irudi humu tunabishana na watu ambao hata ukimuambia apangilie vyeo vya JWTZ kuanzia private hadi General na mabegani anavaaa nini hawezi kukuambia kitu.
Amiri jeshi mkuu anapopokea taarifa ile asubuhi,je huwa yupo CDF tu,akimpa taarifa za vyombo vya ulinzi na usalama au huwa yupo IGP,CDF na DGI?Sikubishii,ninataka kujua ili nijue na mafunzo yao kama yanakua chini ya CDF au IGP
 
Kwahiyo kwa kusema hivyo,CDF anaweza akatoa amri kwa IGP na akatii,wakati majukumu yao yako tofauti?
Anatii, nitakupa mfano, nyakati ngumu kama ishu za magaidi wanaotuvamiaga mchongo ukiwa mgumu basi CDF huwa incharge kusimamia show nzima, na katika zoezi zima yapo ambayo jw hawayafahamu bali polisi na polisi yapo ambayo hawayamudu ila jw kwahiyo wakiwa katika mapambano wanashirikiana na kushauriana ila mchongo mzima unakuwa chini ya CDF, hata yeye juzi hapa alipoenda kuaga katika kipindi cha dakika 45 itv alipoulizwa nyakati ambazo zilikuwa ngumu alitolea mfano magaidi wa kibiti na kwingineko ndio ujiulize alitoa mfano yeye kama nani ikiwa ishu ilikuwa ya kipolisi zaidi.

Vivyo hivyo katika vita mfano ile ya kagera, majeshi yote yanasonga front na CDF ndio analead mchongo mzima japo wanashirikiana na wakuu wenzie.

Chukua hii achana na watafuta umaarufu
 
Back
Top Bottom