Sipendezwi na jinsi inavyolazimishwa sasa CDF kuwa chini ya Waziri wa Ulinzi 'Kiprotokali' wakati Waziri wa Ulinzi ndiyo anapaswa kuwa chini ya CDF

Sipendezwi na jinsi inavyolazimishwa sasa CDF kuwa chini ya Waziri wa Ulinzi 'Kiprotokali' wakati Waziri wa Ulinzi ndiyo anapaswa kuwa chini ya CDF

Amiri jeshi mkuu anapopokea taarifa ile asubuhi,je huwa yupo CDF tu,akimpa taarifa za vyombo vya ulinzi na usalama au huwa yupo IGP,CDF na DGI?Sikubishii,ninataka kujua ili nijue na mafunzo yao kama yanakua chini ya CDF au IGP
Mambo yanakanganya kidogo ila nitajitahidi kufafanua vile navyofahamu, amiri anapokea taarifa tofauti tofauti kutoka kwa kila jeshi kila moja kwa wakati wake. Lakini nakala za taarifa (isipokuwa zile nyeti) lazima zitue mezani kwa CDF. Yaani lazima CDF afahamu hali ya usalama wa nchi pamoja na hali za majeshi yaliyo chini yake.
 
Duniani Kote nchi ni ya Jeshi . Nchi yenye Jeshi Kubwa ndiyo nchi imara. Tanzania hatuoni umuhimu wa majeshi yetu Kwa sababu Mwalimu alikua msomi Halisi wa siasa na jamii na Dunia aliijua vizuri Kwa alikua ni Msomi aliyeelimika Kwa kiwango kikubwa sana. Nyerere hakuwa mjinga alipokua analitumia Jeshi lake kwenye vita za Ukombozi na kusaidia nchi nyingine. Aliwaweka Wanajeshi Bize na mambo ya nje na kuwasaidia majirani. Na hicho ndicho wanachofanya Marekana ni nchi za NATO. Nchi za Kiraia zinapaswa kulitumia Jeshi Kwa umakini mkubwa. Huwezi ukasikia Rais wa Marekani anawakoromea wanajeshi Kwa lugha za kudhalilisha. Hata Kagame analiheshimu sana Jeshi lake ikiwemo Jeshi la Polisi. Huku Afrika na hata Tanzania ni rahisi kusikia Rais au mwanasiasa analidhalilisha Jeshi au Polisi wakati huo huo anategemea kuiba kura Kwa sababu Majeshi yatamlinda. Yani ni Hopeless kabisa.

Jeshi ni serikali Mbadala ndio maana imepewa jukumu la kulinda Katiba Muda wote. Kuna maana kubwa uliyojificha nyuma ya Jukumu Hilo . Wanasiasa UCHWARA HAWAWEZI KUELEWA MAANA YAKE. IPO SIKU AMBAYO HAIPO MBALI WATAJUA MAANA YAKE. Historia Duniani Kote hua inatabia ya kuwapitisha wanadamu kwenye nyakati zinazofanana endapo hawatajifunza Kwa waliowatangulia katika nyakati zinazofanana.
Afrika maendeleo ya pamoja yatatokea Kwa mapinduzi na sio Kwa kugonga meza. Afrika ikiwa na Marais 5O kama Kagame na Museveni na Museveni Hakika Kwa utajiri uliopo tungekua tunauza mtungi wa Gesi KG 15 Kwa sh. 20000 na mafuta Petroli Sh. 1200/- kwa Ltr.

Kutoliheshimu Jeshi na kulipa heshima yake inatokana na matatizo ya nchi jirani.Hali inayopelekea wanajeshi wetu angalau kupata sehemu wanapoweza kwenda kuweka roho zao rehani ili wapate anagalu fedha za kuboresha maisha yao na hivyo kutulia na kuwaachia wanasiasa wa ndani ya nchi zao wakilamba asali na kuwakejeli wanajeshi wao . Hiyo ipo pia Kwa majeshi ya Polisi Afrika wanaachwa kama Kuku wa Kienyeji waishi Kwa rushwa na kubambikia watu Kesi ili waweze kuendesha maisha yao na kusomesha watoto wao ili watoto wao wasije wakarithi matusi na kejeli Toka Kwa wanasiasa kuwa hawajasoma ,hawana uwezo wa kuchanganua mambo ,hawajui kupeleleza, ni wababaishaji,wasumbufu, hawajui Sheria n.k lakini ndio wanaowatumia kuiba kura na kuchafua Hali ya utulivu kisiasa na wakishaingia madarakani wanawakejeli na kuwaona hawana maana yoyote na hawastahili kulipwa mishahara ya kuwafanya waendeshe maisha yao Kwa misingi ya Haki na uadilifu . Matokeo yake ni kuwa na mifumo isiyoeleweka na yenye mikanganyiko mikubwa. CDF ni International Rank na vyeo vingine vyote vya Kijeshi chini yake. Hawatakiwi kuwa watumwa wa kisiasa . Wanapaswa kuwa huru mbali na siasa. Raia mmoja TU ndiye mwenye kauli juu ya Jeshi ,yaani Rais basi mana ana mamlaka ya kumteua CDF na Kumtengua muda wowote. Wengine wote hawana jambo lolote la kiutendaji juu ya Jeshi na hivyo hawana maelekezo yoyote Kwa Jeshi zaidi ya blabla za sijui ilani sijui Nini wakati Jeshi na ilani ni vitu visivyoendania Kwani Jeshi linapaswa kulinda Mipaka ya nchi na Katiba ya nchi hata kama hakuna Rais Wala Chama. Yaani hata ikatokea Serikali yote wakaangamia Kwa baridi Kali au Upepo mkali wa kisulisuki Ukalizoa Jengo la Bunge la Kameruni Bado Jeshi litalinda mipaka ya nchi na Katiba mpaka Hali itakapokaa sawa. Hivyo nakubaliana na wewe kabisa kuwa Jeshi linahitaji kuheshimiwa na kuepuka jambo lolote linaloweza kuwafanya wanasiasa kujiweka juu ya Taratibu za Kijeshi Kwa namna yoyote ndani ya nchi zetu za Afrika.

Ni bahati TU Afrika Kuna nchi zenye Vita kama Kongo ,Sudani,Somalia ,Msumbuji, Burundi n.k. Hali inayowapa fursa baadhi ya wanajeshi wa nchi nyingine kufadhiliwa na Mabeberu wa nchi za magaharibi Kwa kulipwa fedha ili wakalinde kile wanachokiita amani. Hapo wanaopata fursa hiyo wanajipatia nafasi ya kuboresha maisha yao na kuvumilia manyanayaso ya wanasiasa waliojaa dharau na kejeli Kwa kushiba asali na kujiona wao wanajua kila kitu mpaka Medani za kivita Kwa sababu TU ya kuangalia Move za Kina Rambo wanadhani kuwa kumbe inawezekana mtu mmoja akalinda mipaka ya nchi[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]


Nakuunga mkono hata kama hawatakuelewa lakini Iko siku watakuelewa. Siku Sudani na Kongo wakipata amani akili zitakaa sawa Kwa wanasiasa wa nchi za Kiafrika ,Watajua kuwa hakuna Serikali bila majeshi,hakuna heshima ya mahakama bila Majeshi ,hakuna heshima ya Bunge bila Majeshi. Hakuna amani bila Majeshi. Hakuna kula Bata na starehe bila Majeshi. Watu wamwagilia mioyo yao Kwa sababu Kuna majeshi yanayolinda usalama wa nchi.
Unaweza kutuambia kwanini wanajeshi hupiga saluti viongozi kama madc ma RC, Rais nk.
Acha kupotosha, wao jeshi hilinda nchi, na kufanikisha hilo huheshimu walioshika hatamu za nchi, kama hamtaki waliopo waheshimiwa na jeshi subirini uchaguzi mchague wa kupigiwa saluti wapya
 
Mambo yanakanganya kidogo ila nitajitahidi kufafanua vile navyofahamu, amiri anapokea taarifa tofauti tofauti kutoka kwa kila jeshi kila moja kwa wakati wake. Lakini nakala za taarifa (isipokuwa zile nyeti) lazima zitue mezani kwa CDF. Yaani lazima CDF afahamu hali ya usalama wa nchi pamoja na hali za majeshi yaliyo chini yake.
Ok! naehukuru kwa kunieleza kulingana na uelewa wako.Mimi kwa experience yangu,huwa naona polisi wanaenda kwenye shughuli za amani nje ya nchi kivyao,hali kadhalika na JW kivyao,na bilashaka polisi huwajibika kwa IGP,na JW huwajibika kwa CDF,na majukumu yao yako tofauti isipokua wanaposhirikiana hasa labda wanapodhibiti uhalifu,kama ilivyotokea majuzi hapa.Polisi wao huhusika na mambo ya ndani ya nchi,JW huhusika na ulinzi hasa kwenye mipaka ya nchi.Polisi husoma sheria na haki za binadamu,upande wa JW sijui.Na nimewahi kushuhudia askari wa JW akimpigia afisa wa polisi saluti,sijajua kiundani kama mkuu wa majeshi hupigiwa salute na IGP,nadhani wote hata wakati wa utambulisho,hutambulishwa kama 'na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama mliopo hapa',ikimaanishwa IGP,CDF,DGI n.k.
 
Wanasiasa wanaogopa kutandikwa na jeshi.

Lazima waweke mtu wao juu pale ili kulinda uhai wao. [emoji1787]
 
Kitu Ambacho watu hawaelewi ni neno MAJESHI kama linavyotumika Kwa Mkuu wa Majeshi,
MAJESHI kama ilivyo/inavyo tumika Kwa CDF ni Vile vikosi vyote vilivyochini ya JWTZ,
Mfano Kikosi cha Anga, Maji, Nchi kavu nk ni vikosi vyenye yadhi ya kuwa jeshi kamili na inatambulika hivyo, Kwa hyo Neno MAJESHI halina Maan ya kwamba ni Majeshi mengine kama Polisi,Magereza,Uhamiaji nk isipokuwa kama nilivyoandika hapo juu, na Wakuu wa vyombo hivi haviwajibiki wa CDF isipokuwa Kwa Mamulaka za uteuzi (Rais).
Kwa Kifupi CDF ni Mkuu wa JWTZ na si vinginevyo.
Hivi vyombo vyote vya ulinzi na Usalama vinafanya kazi Kwa Kushirikiana sana,
Na Kutokana na ushirikiano huo, JWTZ kikapewa Hadhi kubwa Kwa Sababu ya Ulinzi wa Katiba na Mipaka ya Nchi na CDF kama Mkuu wa JWTZ akapewa Hadhi ya kuwa Mwenyekiti wa hivi hasa pale vinapotekeleza Majukum yake.
Na Hata ukiangalia wanavyokuwa wamekaa kama (watakutana pamoja) anaanza Mkuu wa JWTZ anafuata wa Polisi nk,
Kama Polisi wamefanya kazi ambayo inahitaji Ushirikishwaji wa JWTZ basi watafanya hivyo Hali kadhalika na vyombo vingine,
Kwa hyo Hakuna Mkubwa Kati ya Wakuu wa vyombo hivi Ila Mkubwa wao ni Rais,
Isipokuwa CDF amepewa Hadhi Kwa Sababu ya Hadhi ya chombo anachokisimamia,
Ni kama Wakuu wa Mikoa,
Hakuna Mkuu wa Mkoa Mkubwa kuliko mwenzie,
Isipokuwa muda Mwingi Mkuu wa Mkoa DSM anapewa Hadhi Kutokana na Mkoa wake lakin haina Maan kwamba ni Mkubwa kuliko Wenzie,
Kuhusu CDF kuwa chini au kwenda kujitambulisha Kwa Waziri nafikili ni Kwa sababu ya Katabia kalikozuka Awamu iliyopita Maan Viongozi wa kisiasa ilifikia hatua wakaona kama wako juu ya kila kitu.
Na Katabia haka kanaendelea Kwa Kasi Sana japo Muanzilishi wake hayupo,
Miaka ya Huko nyuma hatukuwahi kuona Maajabu kama haya ya kujitambulisha,
Ila Kutokana na Kwamba CDF ni mwanajeshi itabidi Tu akajitambulishe Kwa waziri wa Wanajeshi,
Maan Wizara ya Ulinzi ni Wizara ya Wanajeshi.
 
Kuna oparesheni ambazo majeshi yetu yakiwa nje yanazifanya kwa pamoja, wakifika huko polisi wanafanya kama wanavyofanya hapa na JW wanafanya kama wanavyofanya hapa. Yaani yale ya ndani kuhusu raia wanafanya polisi na ulinzi dhidi ya uvamizi wanafanya JW.

Kuhusu afisa wa polisi kupigiwa saluti na askari wa JW iko sahihi, inategemea askari wa cheo gani amekutana na askari wa cheo gani katika jeshi lipi. Kuna polisi kwa cheo chake anampigia au hampigii askari wa JW kulingana na cheo chake. Somo la saluti linachanganya sana, ndio somo linalochukua muda mrefu kwa baadhi ya majeshi.

Kuhusu kutambulishwa wanapokaa pamoja wakatambulishwa 'wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama' mara nyingi wakiwapo pamoja basi rais yupo, na ndiye mwenye majeshi yake wewe unayetambulisha vyombo unataka kumpa nani mwingine maana katika mzingira hayo mkuu wa majeshi anakuwa amiri. Sijawahi kuwaona kwa pamoja na rais asiwepo

Ni vitu fulani vinachanganya taaluma nyingi nyingi kuvifahamu zaidi
 
Kitu Ambacho watu hawaelewi ni neno MAJESHI kama linavyotumika Kwa Mkuu wa Majeshi,
MAJESHI kama ilivyo/inavyo tumika Kwa CDF ni Vile vikosi vyote vilivyochini ya JWTZ,
Mfano Kikosi cha Anga, Maji, Nchi kavu nk ni vikosi vyenye yadhi ya kuwa jeshi kamili na inatambulika hivyo, Kwa hyo Neno MAJESHI halina Maan ya kwamba ni Majeshi mengine kama Polisi,Magereza,Uhamiaji nk isipokuwa kama nilivyoandika hapo juu, na Wakuu wa vyombo hivi haviwajibiki wa CDF isipokuwa Kwa Mamulaka za uteuzi (Rais).
Kwa Kifupi CDF ni Mkuu wa JWTZ na si vinginevyo.
Hivi vyombo vyote vya ulinzi na Usalama vinafanya kazi Kwa Kushirikiana sana,
Na Kutokana na ushirikiano huo, JWTZ kikapewa Hadhi kubwa Kwa Sababu ya Ulinzi wa Katiba na Mipaka ya Nchi na CDF kama Mkuu wa JWTZ akapewa Hadhi ya kuwa Mwenyekiti wa hivi hasa pale vinapotekeleza Majukum yake.
Na Hata ukiangalia wanavyokuwa wamekaa kama (watakutana pamoja) anaanza Mkuu wa JWTZ anafuata wa Polisi nk,
Kama Polisi wamefanya kazi ambayo inahitaji Ushirikishwaji wa JWTZ basi watafanya hivyo Hali kadhalika na vyombo vingine,
Kwa hyo Hakuna Mkubwa Kati ya Wakuu wa vyombo hivi Ila Mkubwa wao ni Rais,
Isipokuwa CDF amepewa Hadhi Kwa Sababu ya Hadhi ya chombo anachokisimamia,
Ni kama Wakuu wa Mikoa,
Hakuna Mkuu wa Mkoa Mkubwa kuliko mwenzie,
Isipokuwa muda Mwingi Mkuu wa Mkoa DSM anapewa Hadhi Kutokana na Mkoa wake lakin haina Maan kwamba ni Mkubwa kuliko Wenzie,
Kuhusu CDF kuwa chini au kwenda kujitambulisha Kwa Waziri nafikili ni Kwa sababu ya Katabia kalikozuka Awamu iliyopita Maan Viongozi wa kisiasa ilifikia hatua wakaona kama wako juu ya kila kitu.
Na Katabia haka kanaendelea Kwa Kasi Sana japo Muanzilishi wake hayupo,
Miaka ya Huko nyuma hatukuwahi kuona Maajabu kama haya ya kujitambulisha,
Ila Kutokana na Kwamba CDF ni mwanajeshi itabidi Tu akajitambulishe Kwa waziri wa Wanajeshi,
Maan Wizara ya Ulinzi ni Wizara ya Wanajeshi.
Nilipokuwa namjibu mdau pale nilisema ni mkuu wa majeshi kwasababu anasimamia vyombo vingine vya ulinzi na usalama nikaongezea ZIKIWEMO BRIGADE zake zote.

Nilijua kuna mtu ataibua hoja hii nisipotaja brigade. Uko sahihi, lakini ni sahihi pia tunaposema ana 'uenyekiti' wa majeshi yote
 
Kitu Ambacho watu hawaelewi ni neno MAJESHI kama linavyotumika Kwa Mkuu wa Majeshi,
MAJESHI kama ilivyo/inavyo tumika Kwa CDF ni Vile vikosi vyote vilivyochini ya JWTZ,
Mfano Kikosi cha Anga, Maji, Nchi kavu nk ni vikosi vyenye yadhi ya kuwa jeshi kamili na inatambulika hivyo, Kwa hyo Neno MAJESHI halina Maan ya kwamba ni Majeshi mengine kama Polisi,Magereza,Uhamiaji nk isipokuwa kama nilivyoandika hapo juu, na Wakuu wa vyombo hivi haviwajibiki wa CDF isipokuwa Kwa Mamulaka za uteuzi (Rais).
Kwa Kifupi CDF ni Mkuu wa JWTZ na si vinginevyo.
Hivi vyombo vyote vya ulinzi na Usalama vinafanya kazi Kwa Kushirikiana sana,
Na Kutokana na ushirikiano huo, JWTZ kikapewa Hadhi kubwa Kwa Sababu ya Ulinzi wa Katiba na Mipaka ya Nchi na CDF kama Mkuu wa JWTZ akapewa Hadhi ya kuwa Mwenyekiti wa hivi hasa pale vinapotekeleza Majukum yake.
Na Hata ukiangalia wanavyokuwa wamekaa kama (watakutana pamoja) anaanza Mkuu wa JWTZ anafuata wa Polisi nk,
Kama Polisi wamefanya kazi ambayo inahitaji Ushirikishwaji wa JWTZ basi watafanya hivyo Hali kadhalika na vyombo vingine,
Kwa hyo Hakuna Mkubwa Kati ya Wakuu wa vyombo hivi Ila Mkubwa wao ni Rais,
Isipokuwa CDF amepewa Hadhi Kwa Sababu ya Hadhi ya chombo anachokisimamia,
Ni kama Wakuu wa Mikoa,
Hakuna Mkuu wa Mkoa Mkubwa kuliko mwenzie,
Isipokuwa muda Mwingi Mkuu wa Mkoa DSM anapewa Hadhi Kutokana na Mkoa wake lakin haina Maan kwamba ni Mkubwa kuliko Wenzie,
Kuhusu CDF kuwa chini au kwenda kujitambulisha Kwa Waziri nafikili ni Kwa sababu ya Katabia kalikozuka Awamu iliyopita Maan Viongozi wa kisiasa ilifikia hatua wakaona kama wako juu ya kila kitu.
Na Katabia haka kanaendelea Kwa Kasi Sana japo Muanzilishi wake hayupo,
Miaka ya Huko nyuma hatukuwahi kuona Maajabu kama haya ya kujitambulisha,
Ila Kutokana na Kwamba CDF ni mwanajeshi itabidi Tu akajitambulishe Kwa waziri wa Wanajeshi,
Maan Wizara ya Ulinzi ni Wizara ya Wanajeshi.
Nimekuelewa sana,Asante kwa ufafanuzi wako mzuri,hapa umejibu na kusaidia hata wenzangu kuelewa,nilikua sijui kuhusu (majeshi)vikosi.Asante sana
 
Nadhani siyo kwamba hauelewi itifaki za serikali zinavyofanya kazi.

Umeandika kwa malengo yako maalumu unayoyajua mwenyewe.

Tangu lini Cdf kiitifaki akawa juu ya Waziri wa ulinzi?

Si Waziri wa ulinzi tu pekee ambaye yupo juu ya Cdf kiitifaki, ni kwa waziri yeyote.
Waziri wa juu Sana. Hadi mkurugenzi hupigiwa saluti na cdf.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Niwaambie ukweli aliyeleta hii hali ni baba wa Taifa kwa kuliingiza jeshi kwenye siasa.Wakati ule kulikuwa na kitu kinaitwa mkoa wa majeshi.Yote sababu ilikuwa chama kimoja.
Mimi kwa upande wangu Jeshi ni taasisi ya kipekee kabisa.Ukitaka kulijua hilo kuna mihimili mitatu Bunge,Serikali na Mahakama lakini jeshi halikutajwa katika mhimili wowote hapo hii inaonyesha ni jinsi gani ilivyo taasisi nyeti.
Jeshi japo haijaandikwa kikatiba mihimili yote hii mitatu jeshi likidinda hakuna kinachofanyika na kufanikiwa.

Kwa waziri wa ulinzi sina usemi hapo kwa kweli mi ninachojua tu CDF huwa hampigii salute mtu yeyote bali ni Raisi ambaye ni amiri jeshi mkuu,maiti(marehemu yeyote hata kama ni raia) haya basi na waziri wa ulinzi maana kumteua CDF waziri wa ulinzi anaweza husika.

Lakini kitendo cha CDF kumpigia salute mkuu wa wilaya kisa tu ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa wilaya hii sio sawa kabisa ni mambo ya siasa haya hayana mashiko.Na ukute huyo CDF ana nishani nyingi kiasi kwamba bega lake linataka kuvunjika eti anampigia salute mkuu wa wilaya hata hajawahi kupitia angalau mgambo au JKT.Ukitaka kujua tulikosea ni kwanini ilifika mahali jeshi likatolewa kwenye siasa? ikaonekana kama ukiamua kubaki na nyadhifa za kisiasa ujitoe jeshini ndio wakatoka kina Kinana,Kikwete,Makamba n.k.Miaka ile unaweza kuta askari flani mkubwa ni mkuu wa mkoa

CDF ni mtu wa kipekee sana na mzito maamuzi yake yanaweza leta mtafaruku raisi mwenyewe anamuheshimu sana.Jeshini hakuna vyama vya wafanyakazi,hakuna ilani wao ni amri tu.Mambo yakiharibika hawa jamaa wanaacha familia zao na wake zao wanakwenda uso kwa uso kwenye mvua za risasi kutupambania sisi tukiwa tume starehe na watoto wetu na wake zetu.Sisi tukiwa tumefunga mkanda kwenye suruali zetu wao mikanda kwao ni ule mkanda wa risasi.Kumbukeni Iddi Amini alivyotuvamia kama sio hawa jamaa leo historia ya nchi hii ingekuwa ni ingine kabisa si ajabu ungesikia bandari ya Tanga ni bandari ya Uganda.

Naomba nirekebishwe kama nimekosea na mimi ni binadamu
Wateule woote wa
rais Ni budi kupigiwa saluti

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Kitu Ambacho watu hawaelewi ni neno MAJESHI kama linavyotumika Kwa Mkuu wa Majeshi,
MAJESHI kama ilivyo/inavyo tumika Kwa CDF ni Vile vikosi vyote vilivyochini ya JWTZ,
Mfano Kikosi cha Anga, Maji, Nchi kavu nk ni vikosi vyenye yadhi ya kuwa jeshi kamili na inatambulika hivyo, Kwa hyo Neno MAJESHI halina Maan ya kwamba ni Majeshi mengine kama Polisi,Magereza,Uhamiaji nk isipokuwa kama nilivyoandika hapo juu, na Wakuu wa vyombo hivi haviwajibiki wa CDF isipokuwa Kwa Mamulaka za uteuzi (Rais).
Kwa Kifupi CDF ni Mkuu wa JWTZ na si vinginevyo.
Hivi vyombo vyote vya ulinzi na Usalama vinafanya kazi Kwa Kushirikiana sana,
Na Kutokana na ushirikiano huo, JWTZ kikapewa Hadhi kubwa Kwa Sababu ya Ulinzi wa Katiba na Mipaka ya Nchi na CDF kama Mkuu wa JWTZ akapewa Hadhi ya kuwa Mwenyekiti wa hivi hasa pale vinapotekeleza Majukum yake.
Na Hata ukiangalia wanavyokuwa wamekaa kama (watakutana pamoja) anaanza Mkuu wa JWTZ anafuata wa Polisi nk,
Kama Polisi wamefanya kazi ambayo inahitaji Ushirikishwaji wa JWTZ basi watafanya hivyo Hali kadhalika na vyombo vingine,
Kwa hyo Hakuna Mkubwa Kati ya Wakuu wa vyombo hivi Ila Mkubwa wao ni Rais,
Isipokuwa CDF amepewa Hadhi Kwa Sababu ya Hadhi ya chombo anachokisimamia,
Ni kama Wakuu wa Mikoa,
Hakuna Mkuu wa Mkoa Mkubwa kuliko mwenzie,
Isipokuwa muda Mwingi Mkuu wa Mkoa DSM anapewa Hadhi Kutokana na Mkoa wake lakin haina Maan kwamba ni Mkubwa kuliko Wenzie,
Kuhusu CDF kuwa chini au kwenda kujitambulisha Kwa Waziri nafikili ni Kwa sababu ya Katabia kalikozuka Awamu iliyopita Maan Viongozi wa kisiasa ilifikia hatua wakaona kama wako juu ya kila kitu.
Na Katabia haka kanaendelea Kwa Kasi Sana japo Muanzilishi wake hayupo,
Miaka ya Huko nyuma hatukuwahi kuona Maajabu kama haya ya kujitambulisha,
Ila Kutokana na Kwamba CDF ni mwanajeshi itabidi Tu akajitambulishe Kwa waziri wa Wanajeshi,
Maan Wizara ya Ulinzi ni Wizara ya Wanajeshi.
Asee nashukuru kws kulielewesha Hili mkuu.
Wengi wakisikia mkuu wa majeshi wanajua Ni pamoja na Yale ambayo kwa sheria za Sasa yametajwa kuwa majeshi eg polisi, magereza,uhamiaji nk.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna Kitendo Kimenishangaza na Kimeniuma kama kuona Juzi CDF na Chief of Staff wake wakienda Kiunyonge na Kiuhuruma kwa Waziri wa Ulinzi Kujitambulisha.

Sijawahi kuona popote pale Waziri wa Ulinzi anakuwa Juu ya Jeshi tena Kiprotokali wakati Jeshi ni Serikali Kificho ya Kimedani na inayojitegemea na ambayo ikiamua muda wowote ule ichukue hatamu ya nchi inaweza na huyo ( huyu ) Waziri wa Ulinzi anakuwa si lolote wala si chochote.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Hayati Mkapa na kidogo Mzee Kikwete waliwaheshimu mno CDF's wa Vipindi vyao na walihakikisha hawalazimishi Jeshi kuwa ni sehemu ya Siasa na Utawala wa Kiserikali.

Hayati Rais Dkt. Magufuli alianza kwa mbaali kutaka Kummiliki CDF (japo alikumbana na Ugumu kidogo) kwakuwa CDF Mstaafu Mabeyo anajitambua na ameiva Kimedani (Kijeshi ) pamoja na Protokali zake zote.

Kama kuna Kitu kimenishangaza na naona HATARI fulani mbeleni huko ni kuona Awamu hii ya Rais Samia huyu Waziri wa Ulinzi Bi. Stegormena Tax akipewa Madaraka makubwa juu ya Jeshi na CDF wake kitu ambacho si Kizuri na siyo cha Kiutaratibu kabisa.

Kwa Kawaida ilitakiwa baada ya CDF Kuteuliwa basi Kiitifaki Waziri wa Ulinzi ndiyo alipaswa kwenda kwa CDF ila siyo CDF na Chief of Staff kwenda kwa Waziri wa Ulinzi huku wakiwa na Nyuso za Huruma kana kwamba Wameamrishwa na Mtu wakati Wao ndiyo wana Mandate ya Kuamrisha.

Namalizia kwa Kuwaasa na Kuwaonya enyi Watawala ( Wanasiasa ) kuwa chezeni na Vitu vyote ila msicheze na Taasisi Nyeti kama ya Jeshi na kutaka nao wawe Wanasiasa kama nyie wakati Kiuhalisia wao ni Wanamedani na wako kwa ajili ya Ulinzi na Usalama Uliotukuka wa Taifa letu hili la Tanzania.

Nichukieni, ila yafanyieni Kazi yote!!!
Kuna tatizo la afya ya akili hapa!
 
Hakuna Kitendo Kimenishangaza na Kimeniuma kama kuona Juzi CDF na Chief of Staff wake wakienda Kiunyonge na Kiuhuruma kwa Waziri wa Ulinzi Kujitambulisha.

Sijawahi kuona popote pale Waziri wa Ulinzi anakuwa Juu ya Jeshi tena Kiprotokali wakati Jeshi ni Serikali Kificho ya Kimedani na inayojitegemea na ambayo ikiamua muda wowote ule ichukue hatamu ya nchi inaweza na huyo ( huyu ) Waziri wa Ulinzi anakuwa si lolote wala si chochote.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Hayati Mkapa na kidogo Mzee Kikwete waliwaheshimu mno CDF's wa Vipindi vyao na walihakikisha hawalazimishi Jeshi kuwa ni sehemu ya Siasa na Utawala wa Kiserikali.

Hayati Rais Dkt. Magufuli alianza kwa mbaali kutaka Kummiliki CDF (japo alikumbana na Ugumu kidogo) kwakuwa CDF Mstaafu Mabeyo anajitambua na ameiva Kimedani (Kijeshi ) pamoja na Protokali zake zote.

Kama kuna Kitu kimenishangaza na naona HATARI fulani mbeleni huko ni kuona Awamu hii ya Rais Samia huyu Waziri wa Ulinzi Bi. Stegormena Tax akipewa Madaraka makubwa juu ya Jeshi na CDF wake kitu ambacho si Kizuri na siyo cha Kiutaratibu kabisa.

Kwa Kawaida ilitakiwa baada ya CDF Kuteuliwa basi Kiitifaki Waziri wa Ulinzi ndiyo alipaswa kwenda kwa CDF ila siyo CDF na Chief of Staff kwenda kwa Waziri wa Ulinzi huku wakiwa na Nyuso za Huruma kana kwamba Wameamrishwa na Mtu wakati Wao ndiyo wana Mandate ya Kuamrisha.

Namalizia kwa Kuwaasa na Kuwaonya enyi Watawala ( Wanasiasa ) kuwa chezeni na Vitu vyote ila msicheze na Taasisi Nyeti kama ya Jeshi na kutaka nao wawe Wanasiasa kama nyie wakati Kiuhalisia wao ni Wanamedani na wako kwa ajili ya Ulinzi na Usalama Uliotukuka wa Taifa letu hili la Tanzania.

Nichukieni, ila yafanyieni Kazi yote!!!
Waziri ni mwakilishi wa Rais au wa serikali . Serikali ni lazima iwe na mwakilishi popote pale ili kuratbu yanayofanyika na yatakayofanyika. CDF ni mtaalam wa Mambo ya kijeshi tu, hivyo ni lazima awe chini ya Serikali ambayo inawakilishwa na Waziri. Asante Kwa mada wengine watajazia zaidi. Ila hata ukijaona CDF anampigia saruti Jokate mwegelo usijeshangaa Kwa kuwa yeye ni mwakilishi wa Raise wilaya ya Temeke.
 
Waziri ni mwakilishi wa Rais au wa serikali . Serikali ni lazima iwe na mwakilishi popote pale ili kuratbu yanayofanyika na yatakayofanyika. CDF ni mtaalam wa Mambo ya kijeshi tu, hivyo ni lazima awe chini ya Serikali ambayo inawakilishwa na Waziri. Asante Kwa mada wengine watajazia zaidi. Ila hata ukijaona CDF anampigia saruti Jokate mwegelo usijeshangaa Kwa kuwa yeye ni mwakilishi wa Raise wilaya ya Temeke.
"saruti' ndiyo nini?
 
Back
Top Bottom