Siri kubwa kuliko zote kuhusu dunia yetu tambarare

Siri kubwa kuliko zote kuhusu dunia yetu tambarare

JE Dunia ina umbo gani?


  • Total voters
    710
Wewe umekariri vya kuambiwa ila kushughulisha akili yako hutaki,...yaani ingewezekana tuwe ana kwa ana kisha tuchukue Mpira nikuonyeshe physically & practically kwamba mpira una ukomo nadhani ungeacha ubishi usioingia akilini.


Tafakari,..
Jibu Kwa hoja acha kusema nimekariri, ulichoandika hapo mwisho umekielewa au umekopi na kupaste tu?
 
Nani kakudanganya?

Na kwanini Ndege zina fly horizontally bila ku bend down over the so called curvature of the earth?


Ushawahi kuona Ndege Ina fly vertically downward/upward?........

Ndege zina fly horizontally over the flattened earth kwasababu Dunia ni flat.
Kwahy unakataa ndege hazitumii hii route?? Kwahy wanatudanganya??

Speaking about ndege kufly vertically ni uongo ndege zinafata curvature of the earth,
yaani unataka nione ndege ipo vertically downward kivipi??
 
So its better kila side itoe proof zake za kisayansi na sio kusema kuwa kuna interests wanayopata wanapoaminisha watu kuwa dunia ni round angali dunia ni flat.I got u.
Yap upo sahihi,. Hicho ndiyo cha msingi haijalishi kwamba kuna interests au hamna ila kinachotakiwa ni evidence(s) ambazo zitatuthibitishia kwamba:-
1. Dunia ni tufe 🌎
2. Dunia Ina move.

Kwamba tuone uthibitisho jinsi maji yanavyoweza ku stick kwenye round object ambayo haipo contained (yaani sio container) na inazunguka.

Uthibitisho ndiyo kitu ambacho kinakosekana.....
 
Sijaona swali la kujibu hapo,..
Kwa sababu huwezi kujibu miaka yako yote, na hii inathibitisha uzaifu wa hoja yako.

Kama umeshindwa kujibu hili swali basi no wazi sasa usiendelee kutudanganya humu eti Dunia ni flat. OVER
 
Kwahy unakataa ndege hazitumii hii route?? Kwahy wanatudanganya??

Speaking about ndege kufly vertically ni uongo ndege zinafata curvature of the earth,
yaani unataka nione ndege ipo vertically downward kivipi??
Ndege kutumia hiyo route, hakuthibitishi kwamba Dunia ni tufe,....

Sasa kama Dunia ni tufe, 🌎 ikiwa Ndege inataka ifike Destination ambayo Ipo Southern in reference kutoka pale ambapo Ipo,...unategemea itafikaje? Si lazima iende vertically downward? Maana ikinyoosha Horizontally haitoweza kufika destination husika!!


Au nakosea? Nirekebishe ukiweza.
 
Kwa sababu huwezi kujibu miaka yako yote, na hii inathibitisha uzaifu wa hoja yako.

Kama umeshindwa kujibu hili swali basi no wazi sasa usiendelee kutudanganya humu eti Dunia ni flat. OVER
Hujauliza swali kisha unataka nijibu,...umeweka picha bila ya swali,..uliza ulichokusudia.
 
Hujauliza swali kisha unataka nijibu,...umeweka picha bila ya swali,..uliza ulichokusudia.
Nimeweka picha nikauliza elezea inawezekana vipi hicho kitu kwenye tambarare? Au hukuelewa nn? Mpk ukaniuliza hivi👇

Kwahiyo wewe unaona Jua linaibuka chini hapo....Hhahh
 
Sasa kama Dunia ni tufe, 🌎 ikiwa Ndege inataka ifike Destination ambayo Ipo Southern in reference kutoka pale ambapo Ipo,...unategemea itafikaje? Si lazima iende vertically downward? Maana ikinyoosha Horizontally haitoweza kufika destination husika!!
Sasa Mimi muda huo nipo upande Gani mpk niione ndege ipo vertically down?
Je, nipo sourthen? Kama nipo sourthen siwez kuona hivyo Kwa sabab muda huo ndege itakuwa overhead, nikiwa northern siwezi hata kuiona hiyo ndege.
 
Sayansi ni somo linalodili na ulimwengu mzima ni pana sana kuna laws za universe humo huwezi sema shetani ndo kazitengeneza kuna biology study ya living things kuna chemia huwezi sema shetani ndo katunga hivyo labda useme shetani ana manipulate elimu ya sayansi ila sio yeye ndo katunga somo la sayansi.
(Ni Somo Ni pana Mno) bila hilo somo na upana wake katika kuishi ungeathirika na nini? vipi yatokanayo na upana wasomo hilo, yamekurahisishia kuishi au yameongeza ugumu wa wewe kuishi? aliyetaka usome hilo somo mpaka ujue hizo law za universe alikua anatafuta nini kiasi asingekipata kipi kingetokea katika maisha. Yote hayo kwa uwezo wa Muumbaji yalishaumbika ili kusapoti maisha ya kila alichokiumba, ndio maana leo kuna watu wanasifiwa kwa ugunduzi na si kwa uumbaji. maana kila kitu kilikuwepo na walikikuta kipo. sasa shetani kwakutaka sifana wanadamu tumsifu akatumia wafuasi wake walete masomo watu tumuamini yeye kuliko aliyeviumba.

kama unaamini kuna uumbaji wa ulimwengu na vitu vyote vilivyomo basi unapingana na sayansi moja kwa moja. na kama unaamini yatokanayo na sayansi ujue unapingana na uumbaji. Vita ya Muumbaji Na Mgunduzi. Yaani Mungu Na shetani.
 
duuu kaka hizi picha umeziona kweli?

1. em angalia hii picha ya mwisho inayoonesha mzunguko wa jua. Hivi ni kweli visiwa vikivyo katikati ya Greenland na Europe vyenyewe havina usiku? Maana kwa picha inavoonesha hiyo sehem hakuna muda ambao jua linaondoka completely.

2. Tukija point nyingine mbona hizi picha hazioneshi Ramani au mabara yakiwa yamenyooka (as you said flat), bali yanaonesha kama threeD vile. Yaani kama mabara yamenyoka kama yapo kwenye sahani na picha ingeonesha ni ramani iliyo flat pia. Don't you think?
Kama unataka kubishana, maswali yako yanahoja. ila kama unataka kuelewa hakuna gumu lisiloeleweka hapo. hiyo picha ni katika kukuonesha Jua linavyoizunguka Dunia hadi tunapata usiku na mchana ili wewe na waliouliza waelewe. pia hiyo si picha halisi itokanayo na Camera yoyote ile. Na ni kweli hivyo visiwa kuna miezi huwa havina usiku na kuna miezi huwa havina mchana na hiyo inajulikana hata katika elimu ya Dunia Mviringo.

Kwa elimu ya Dunia Tambarare kuna namna ya Jua huwa linasogea katika Mzunguko wake ili kupata majira ya mwaka na ndio kipindi hali hizo hutokea katika Visiwa hivyo. Na katika swali lako la pili jibu ni ndio hauyaoni kama unavyofikiria utayaona kwasababu hizo si picha halisi ni 3D kweli. Kua tayari kujifunza kwa kuihoji elimu uliyonayo juu ya Umbo la Dunia hapo utakua na nafasi yakujifunza na kuyatafakari mengi.
 
Sasa kama unalijua Hilo kuwa sayansi ipo kuthibitisha iliyoyakuta why unapinga ilichokithibitisha???
Namaanisha hivi. Sayansi Inathibitisha Bomu linaua watu wengi kupitia kwenye Movie za kivita tunazoziangalia, Je Niamini wale wanaokufa huwa wamekufa kweli?
 
Ndo maana upo hapa tutoe tulichofundishwa lete hoja zako kuhusu umbo la Dunia tambarare zenye logic, me nakujaji kulingana na unachosema ww.
Hapo tutabaki tunazunguka tuu maana mimi nilikijaji nilichokisoma Juu ya Umbo la Dunia kuwa ni Mviringo, sasa wewe ukinijaji mimi utakosa kuifahamu elimu nyingine juu ya Umbo la Dunia kuwa ni Tambarare. unachokosea unajaji Watu badala ya Elimu. Chakufanya tafuta elimu ya Dunia Tambarare halafu njoo uijaji kupitia sisi tunaoiamini. maana si kitu tunachokitunga kupitia Jukwaa hili. Ni Somo pana tuu kama Tulivyoisoma Dunia Mviringo.

Kuna maswali tukiyauliza juu ya Umbo la Dunia mviringo mtayakimbia kama mnavyofanya.
Mfano nipe jibu Linalothibitisha Dunia, Jua Na Mwezi Havitembei au Vinatembea pindi tuangaliapo kwa Macho.
Nikimaanisha, Je Nikiangalia Nini Nitajua Hivi vitu Vipo katika Mwendo Au Vimesimama.?
 
Explain this, how is it possible kwenye Dunia tambarare?
View attachment 3174372
Hio Iinawezekana kwakuthibitisha kua Jua ni dogo kuliko Dunia na linamove kuizunguka Dunia...
Au wewe ukionaga Hivyo huwa unafeel kipi Kinachomove kati ya Dunia na Hilo Jua?

Na kama unaamini huo ni mwinuko na Hilo Jua lipo Chini. Tuambie ni umbali gani toka hiyo Camera ilipokua mpaka kwenye huo mwinuko ili tukuthibitishie umbali huo utakaoutaja hauwezi kukuta mwinuko.

Soma elimu ya Dunia Tambarare hayo majibu yapo na uthibitisho kupitia tafiti mbalimbali zilizofanywa ili kuthibitisha je ni kweli umbali usemwao kuwa mviringo wa dunia utaanza kuonekana ni kweli? jibu Uwezo wa Macho yetu ndio hutengeneza hizo shape. kama ambavyo unapoingia katika mji nyakati za usiku kuna umbali ukiwepo taa zote za mji zitakupa shape ya kama mviringo hata kama ni tube light.
 
wazungu walichunguza na wakagundua kuna mabara yana mali nyingi na waliweza kuvuka maji ya kutisha na kuyafikia mabara hayo na kuyatawala na kufanikiwa kuhamisha mali za huko hadi kwao.

ukiangalia hata ramani zote za barabara zinazotumika kwenye bara la africa bado wanatumia ramani zilezile za wazungu wakoloni.watu weusi tumeshindwa hata kubuni njia zetu za kututoa sehem moja hadi nyingine iwe nchi kavu,bahari hata anga.

wazungu haohoa leo wamefikia kufika mwezini na kutuletea picha za dunia yako kama ilivyo. na sasa wanachanja mbuga miaka sio mingi wanaingia sayari ya mars.
kwamafanikio haya wenzetu wazungu sio wa kubezwa hatakidogo.kama una cha kuwapinga zaidi toa ushahidi wako ambao haugusi kabisa ushahidi wa wazungu katika utafiti wao.

KITU PEKEE AMBACHO MIMI NAWEZA KUWAPINGA WAZUNGU NI KUTULETEA DINI ZAO TU. pamoja vitabu vya dini ndio vitabu walivyoweka kumbukumbu zao na kuendeleza utafiti wao wa kidunia na maisha ya wanadamu,wakati sisi tunaendelea kuwa wajinga wa kuto kugundua mtego huu.
Ok, Unaweza kunitajia Kitabu Cha historia kilichoandikwa na Mtu mweusi na kikatumika kufundishia watu weusi? Umesoma sisi tumetokana na Nyani, Je na hao wazungu wanaundishwa hivyo?

Mengine yasitutoe nje ya mada, kwa milango yako ya fahamu uliyoumbwa nayo. unajihisi upo katika dunia inayozunguka au Jua linalotembea.? kwanini ufundishwe Darasani kupingana na kile ukionacho na kukihisi?
 
hateeb10 naona hili swali limekuwa gumu sana kwako??? Kabla sijauliza linguine jibu kwanza hili.


View attachment 3177073
Tatizo lako upo kubishana Kutaka Ushindi, ningekujibu hili vizuri tuu.
Swali Langu ni kwanini Unauliza Maswali yatokanayo na elimu ya Dunia mviringo kwa watu wa elimu ya dunia tambarare. Yaani umuulize Mkristo maswali yatokanayo na kitabu cha Kiislam au Kinyume chake. ndivyo ufanyavyo wewe, hapo itakua ni kubishana na si kuelimishana.

maana yangu, soma shape za mwezi zinaelezewaje katika FlatEarth then uje na maswali yatokeayo huko ueleweshwe, maana hapa unataka kujulishwa kitu usichokielewa, LAZIMA UTABISHA TUU.
 
Sasa hao wanaosema dunia ni duara wanapata faida gani,na kwa nini watufiche kuwa dunia ni duara!?
KWANZA KINADHARIA DUNIA ZOTE NI DUARA, ila kuna Mviringo kama Chungwa au yai, hii ndio inafundishwa madarasani na Kuna hii ya Duara kama sahani au Disk isiyofundishwa Darasani.
So Wanaosema Ni mviringo au kufundisha hivyo, lengo lao ni KUMTOA MUNGU katika UUMBAJI na faida waipatayo ni Kutumikiwa na wanadamu badala ya Wanadamu kumtumikia Mungu Muumbaji. Yaani hiyo ni Kazi ya Shetani na Wafuasi wake.

Ni Somo Lingine pana sana.
Dunia ikiwa Mviringo tunaambiwa chanzo chake ni BingBang so Haijaumbwa, lakini iliyoumbwa ni ya flat na haizunguki Bali jua na mwezi ndivyo vinavyoizunguka kama uonavyo kwa macho yako.
 
Cha kufanya thibitisha kwamba Dunia ni tufe linalozunguka,. Hizo ishu za New World Order Wala hazihusiki kwenye kuthibitisha......

Mwaka unaisha, cha ajabu mpaka leo umeshindwa kuthibitisha:-
1. Dunia ni tufe 🌎
2. Dunia inazunguka.

Ungekua na uthibitisho usingepata shida,. ungethibitisha muda mrefu sana., TATIZO HUNA UTHIBITISHO, TATIZO HUWEZI KUTHIBITISHA.
Hapo hapo Anathibitisha Jua linamove kama Mwezi ila anabishana na Ukweli alionao yeye mwenyewe. ajabu Sana.
 
Back
Top Bottom