Siri niliyoipata katika kufunga siku 21 kila mwanzo wa mwaka

Siri niliyoipata katika kufunga siku 21 kila mwanzo wa mwaka

Kuwa mwanga au mchawi ni application ya spiritual power. Unafanya mida ya usiku kwa sababu hali ya hewa na kuna utulivu.
Mkuu sorry, uzi wako una hang sana. Sijafahamu hata una base kwa Mungu au miungu ufundishapo hapa kuingia katika ulimwengu wa kiroho ili kupata matokeo.
 
Ngoja nianze kwa kusema.
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.

Kisha niongezee kwa kusema Andiko linaua bali Roho anahuisha.

Sasa hebu soma katika biblia upate kujua mzimu wa Samweli ulivyopandishwa.
11 Ndipo yule mwanamke aliposema, Je! Ni nani nitakayekupandishia? Naye akasema, Nipandishie Samweli.
1 Samweli 28:11

13 Mfalme akamwambia Usiogope; waona nini? Yule mwanamke akamwambia Sauli, Naona mungu anatoka katika nchi.
1 Samweli 28:13

14 Naye akamwuliza, Ni mfano wa nini? Akajibu, Ni mzee anazuka; naye amefunikwa vazi. Basi Sauli akatambua ya kwamba ndiye Samweli mwenyewe, akainama uso wake mpaka nchi, akasujudia.
1 Samweli 28:14
Mkuu samahani bado sijaelewa yaani swali langu hujaninibu...Hilo la Sauli kumwendea mwanamke mchawi ili Kujua ya Rohoni Ni baada ya Mungu kutokumjibu Sauli kwa Lolote....ndipo saulinakaamua kuwaendea wenye pepo wa Utambuzi

Sasa tuko kwenye Agano lililo Bora zaidi...na njia ya Kupakaribia patakatifu uko wazi kwa kila aaminiye....

Sasa Ni Jambo gani au siri gani ambayo Roho Mtakatifu ameshindwa kutufunulia Mpaka tukaitafute kwa Kuzungumza na Wafu??

Na Ni Siri gani ambayo Roho Mtakatifu haijui Mpaka kufikia Hatua ya Kuzungumza na Wafu??

Hata Bwana Yesu alituambia Huyo Roho atawafunulia Yote hata Siri na Mafumbo ya Mungu

1 Wakorintho 2:10
[10]Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.
But God hath revealed them unto us by his Spirit: for the Spirit searcheth all things, yea, the deep things of God.
 
Mkuu sorry, uzi wako una hang sana. Sijafahamu hata una base kwa Mungu au miungu ufundishapo hapa kuingia katika ulimwengu wa kiroho ili kupata matokeo.
Mkuu, Mungu ana_operate kwenye ulimwengu wa kiroho na miungu pia ni hivyo hivyo. Kwahiyo itategemea dhamira/nia yako ipi. Na ndio maana mwenye uzi ameweka wazi kuwa mmoja anaweza kutumia hizo nguvu kwa nia ovu na mwingine akazitumia kwa nia njema.
 
Mkuu samahani bado sijaelewa yaani swali langu hujaninibu...Hilo la Sauli kumwendea mwanamke mchawi ili Kujua ya Rohoni Ni baada ya Mungu kutokumjibu Sauli kwa Lolote....ndipo saulinakaamua kuwaendea wenye pepo wa Utambuzi

Sasa tuko kwenye Agano lililo Bora zaidi...na njia ya Kupakaribia patakatifu uko wazi kwa kila aaminiye....

Sasa Ni Jambo gani au siri gani ambayo Roho Mtakatifu ameshindwa kutufunulia Mpaka tukaitafute kwa Kuzungumza na Wafu??

Na Ni Siri gani ambayo Roho Mtakatifu haijui Mpaka kufikia Hatua ya Kuzungumza na Wafu??

Hata Bwana Yesu alituambia Huyo Roho atawafunulia Yote hata Siri na Mafumbo ya Mungu

1 Wakorintho 2:10
[10]Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.
But God hath revealed them unto us by his Spirit: for the Spirit searcheth all things, yea, the deep things of God.
Nadhani hapa unaongelea kitu tofauti kabisa na kile ninachokiongelea.

Hapa ninaongelea vitu vinavyotokea baada ya kufunga ukiwa serious.
Kwenye maongezi yangu hapa niliongelea kuwa unapofunga lazima uwe na lengo. Nikasema katika ulimwengu wa Roho kwa ninavyofahamu upo katika levels 6.

Nilieleza kuwa level ya kwanza ipo na kelele nyingi. Nikaendelea kusema katika level hiyo utaweza kukutana na watu waliokufa.

Hapa ninaongelea matokeo ya kufunga.
Hata hivyo hebu soma hapa:-

2 Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.
2 Wakorintho 12:2

3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua);
2 Wakorintho 12:3

4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene.
2 Wakorintho 12:4
 
Mkuu, Mungu ana_operate kwenye ulimwengu wa kiroho na miungu pia ni hivyo hivyo. Kwahiyo itategemea dhamira/nia yako ipi. Na ndio maana mwenye uzi ameweka wazi kuwa mmoja anaweza kutumia hizo nguvu kwa nia ovu na mwingine akazitumia kwa nia njema.
Asee! Sikua nafahamu hili. Mtu afunga tatu kavu kwa Bwana halafu anaingia ulimwengu wa kiroho kufanya ushirika na miungu na kuongea na marehemu.
 
Nawasalimia wana JF wote.

Katika mwendelezo wangu wa kuwafundisha na kuwafungua macho watu, leo nimeonelea nilete siri iliyomo katika kufunga.

Kwanza kabisa nawaomba muelewe kwamba, kuna namna nyingi sana ya kufunga lakini nitaongelea namna tatu:-
1. Kufunga kwa malengo
2. Kufunga kwa mujibu wa utaratibu au sheria
3. Kufunga kwa mkumbo

Sitaelezea kila moja maana lengo la waraka huu ni kuongelea siri iliyomo katika kufunga.

Kuna njia nyingi ambazo hutumika katika kufunga lakini mimi leo ninaongelea njia moja ambayo huwa naitumia katika kufunga siku 21.

Mara ya kwanza kabisa nilifunga siku tatu mfululizo pasipi kula wala kunywa. Nilikuwa nimefunga na nimejifungia sehemu kwa ajili ya kusali na kuomba. Katika mfungo huo niligundua kuwa:-
1. Unapofunga unaufanya mwili uweze kukutii na kuanza kusikiliza kutoka ndani

2. Unapofunga unapata muda wa kuwasiliana na high self.

3. Kufunga holela pasipo utaratibu unaweza ukaathiri afya ya mwili wako.

4. Kufunga pasipo kufundishwa njia zilizomo katika ulimwengu wa roho, unaweza ukajikuta unarukwa na akili baada ya mfungo.

Ikumbukwe unapofunga unaufisha mwili ili uweze kuingia katika ulimwengu wa roho. Katika ulimwengu wa roho kuna levels 6, as I know mpaka sasa. Katika level ya kwanza utakutana na vurugu za kila namna. Hapajatulia, maana ni rahisi kwenda. Level hiyo kwa mara nyingi huwa tunaiita PEPO. Kwahiyo usipofundishwa namna ya kutembea katika ulimwengu huo; unaweza ukajikuta baada ya mfungo unakuwa mtu wa ajabu, au mara nyingine unarukwa na akili.

JINSI YA KUFUNGA UNAINGIA ROHONI PASIPO KUATHIRI AFYA

Niliweza kujifunza namna ya kufanya na kuniwezesha kila mwaka kufunga siku 21 mfululizo. Unatakiwa uwe na asali, sukari na maji.

Kila siku baada kufanya maombi ya asubuhi; chemsha maji, baada ya maji kuchemka kiwango cha chai, tia asali na sukari, kuywa kikombe kimoja mpaka viwili (Kikombe cha chai).

Ikifika jioni kama saa 12 au saa moja fanya hivyo hivyo, yaani chemsha maji tia sukari na asali.

Fanya hivyo kila siku mpaka siku 21. Mwili wako utaendelea kufanya kazi na hapo hapo utaweza kuingia ulimwengu wa Roho.

UWE NA JAMBO(MAMBO) LINALOKUFANYA UFUNGE

Utakapokuwa na jambo lililokufanya ufunge, litakusaidia kwamba utakapokuwa kwenye maombi na sala utajikita katika jambo lililokufanya ufunge. Sasa basi hii itakusaidia utakapikuwa katika level ya kwanza ya ulimwengu wa roho, hutababaika na yale yatakayokuwa yanatokea. Maana ukifunga pasipokuwa na jambo lolote, utajikuta unazagaa tu kwenye huo ulimwengu, kwahiyo chochote kitakachokuwa kinatokea ni halali yako.

Kuna nguvu katika kutamka. Tamka kwa kurudia rudia jambo unalotaka (Chanting). Liongea kwa sauti au ikiwezekana tengeneza wimbo.

Wakati wa kusali na kuomba, tafuta sehemu ya faradha.


NITAENDELEA NA SOMO HILI....

Kwani wakristo mnafungaga?
 
Heeee!!!! Mkuu wa anga nani na anafanya nn mda huo? Na je mtu akiamka mda huo akaomba nn kitatokea???
Kuna maandiko yanasema mida hiyo roho ya Mungu inashuka karibu na anga la dunia, na pia kwa upande wa giza na wenyewe unakuwa kwenye peak ya utendaji wake. Kwa maana nyingine, wakati huo anga la dunia linakuwa neutral ground... sasa itategemea wewe umepanga kujihusisha na nguvu ya upande gani kwa muda huo.
 
Nawasalimia wana JF wote.

Katika mwendelezo wangu wa kuwafundisha na kuwafungua macho watu, leo nimeonelea nilete siri iliyomo katika kufunga.

Kwanza kabisa nawaomba muelewe kwamba, kuna namna nyingi sana ya kufunga lakini nitaongelea namna tatu:-
1. Kufunga kwa malengo
2. Kufunga kwa mujibu wa utaratibu au sheria
3. Kufunga kwa mkumbo

Sitaelezea kila moja maana lengo la waraka huu ni kuongelea siri iliyomo katika kufunga.

Kuna njia nyingi ambazo hutumika katika kufunga lakini mimi leo ninaongelea njia moja ambayo huwa naitumia katika kufunga siku 21.

Mara ya kwanza kabisa nilifunga siku tatu mfululizo pasipi kula wala kunywa. Nilikuwa nimefunga na nimejifungia sehemu kwa ajili ya kusali na kuomba. Katika mfungo huo niligundua kuwa:-
1. Unapofunga unaufanya mwili uweze kukutii na kuanza kusikiliza kutoka ndani

2. Unapofunga unapata muda wa kuwasiliana na high self.

3. Kufunga holela pasipo utaratibu unaweza ukaathiri afya ya mwili wako.

4. Kufunga pasipo kufundishwa njia zilizomo katika ulimwengu wa roho, unaweza ukajikuta unarukwa na akili baada ya mfungo.

Ikumbukwe unapofunga unaufisha mwili ili uweze kuingia katika ulimwengu wa roho. Katika ulimwengu wa roho kuna levels 6, as I know mpaka sasa. Katika level ya kwanza utakutana na vurugu za kila namna. Hapajatulia, maana ni rahisi kwenda. Level hiyo kwa mara nyingi huwa tunaiita PEPO. Kwahiyo usipofundishwa namna ya kutembea katika ulimwengu huo; unaweza ukajikuta baada ya mfungo unakuwa mtu wa ajabu, au mara nyingine unarukwa na akili.

JINSI YA KUFUNGA UNAINGIA ROHONI PASIPO KUATHIRI AFYA

Niliweza kujifunza namna ya kufanya na kuniwezesha kila mwaka kufunga siku 21 mfululizo. Unatakiwa uwe na asali, sukari na maji.

Kila siku baada kufanya maombi ya asubuhi; chemsha maji, baada ya maji kuchemka kiwango cha chai, tia asali na sukari, kuywa kikombe kimoja mpaka viwili (Kikombe cha chai).

Ikifika jioni kama saa 12 au saa moja fanya hivyo hivyo, yaani chemsha maji tia sukari na asali.

Fanya hivyo kila siku mpaka siku 21. Mwili wako utaendelea kufanya kazi na hapo hapo utaweza kuingia ulimwengu wa Roho.

UWE NA JAMBO(MAMBO) LINALOKUFANYA UFUNGE

Utakapokuwa na jambo lililokufanya ufunge, litakusaidia kwamba utakapokuwa kwenye maombi na sala utajikita katika jambo lililokufanya ufunge. Sasa basi hii itakusaidia utakapikuwa katika level ya kwanza ya ulimwengu wa roho, hutababaika na yale yatakayokuwa yanatokea. Maana ukifunga pasipokuwa na jambo lolote, utajikuta unazagaa tu kwenye huo ulimwengu, kwahiyo chochote kitakachokuwa kinatokea ni halali yako.

Kuna nguvu katika kutamka. Tamka kwa kurudia rudia jambo unalotaka (Chanting). Liongea kwa sauti au ikiwezekana tengeneza wimbo.

Wakati wa kusali na kuomba, tafuta sehemu ya faradha.


NITAENDELEA NA SOMO HILI....
ubarikiwe. yote unasema ya kweli. ila mimi nilichojifunza kwenye kufunga na kuthibitisha kuwa ndicho cha kweli ni hiki:

1. kufunga hakumlazimishi Mungu atende, yaani you can never force God to act upon your desires just because of fasting.

2. kufunga kunakusaidia tu kuitiisha nafsi yako/mwili wako ili kusogea mbele za Mungu kwa unyenyekevu, na hapo ndipo utapata nafasi ya kuongea na Mungu kwa unyenyekevu. Mungu anapatikana kwenye unyenyekevu na utulivu.

3. Kufunga kwa namna yeyote ile, kwafaa sana na kuna majibu. kuna baadhi ya mambo mengine huwezi kuyapata bali kwa kufunga na kuomba, ikiwa na maana kwamba, hadi utiishe sana nafsi yako kwa unyenyekevu mbele za Mungu, na Mungu kwa hiari yake baada ya kuona unyenyekevu wako anaweza kuamua kukujibu. kwa neema yake anaweza kujibu hata kabala ya wakati uliokuwa umepangwa, au akaingilia kati kwasababu ikinyenyekea sana mbele za Mungu, unakuwa umesogea sana mbele zake hivyo anakusikia sana, and as long as wewe ni mtoto wake, ukipiga kelele anakusikia na anasogea kukusaidia kwa haraka kuliko ukiwa mbali.

4. kufunga kunakusaidia kuua kiburi cha mwili na mapenzi yake. jua kwamba, mwili siku zote hushindana na roho, mwili hupenda tamaa za dunia hii na huwezi kusogea mbele za Mungu ukiwa na tabia za tamaa za mwili/dunia hii, ila ukizifisha ukasogea kwa Mungu kwa roho, hapo utamwona kwasababu Mungu ni Roho nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika Roho na kweli. pia huwezi kupata Roho Mtakatifu bila kuufisha mwili na kuiweka roho mbele. yote hayo yanakulazimu ujinyenyekeshe mbele ya mkono wa Mungu ulio hodari, kitabu cha mika pia kinaeleza kuwa Mungu anachohitaji toka kwetu ni kujinyenyekeza na kutii Neno lake. yote haya ni magumu kufanya kama huna tabia ya kufunga kwa kuutiisha mwili ili roho iinuke na kumtafakari Mungu. ubarikiwe.
 
Mleta huu Uzi siku ukifika kuzimu utaikuta hivi kazi unayoifanya...maana unayatumia maarifa vibaya ... Unafundisha mfungo wa siku 21 afu unawaambia watu wachague uchawi au (....) Mabano haujisemi wewe ni nani - mlokole au mpagani... Neno la msalaba ni upuzi kwao wanaopotea Bali kwetu sisi tunaokolewa ni nguvu ya Mungu .. Siionei haya injili ni uwezo uletao wokovu..Kol 3;
16-17 Na kila mfanyalo kwa neno au kwa tendo fanyeni yote ktk Jina la Bw Yesu mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye...Mimi ni mlokole !
 
Mleta mada uje uelezee haya mambo, kwanza unasema tupange pounti za kuomba..kivipi wakati Roho mt hutusaidia kuomba.
 
Mkuu, ni kipi unashangaa hapo?

Kwani hujui kuwa 'mwanga' na 'giza' ni kitu kimoja ila hutofautiana kwa kiasi (degree)? Ni kama joto na baridi.

Bila giza hakuna mwanga, bila giza huwezi kuelewa faida ya mwanga. Ni kama shilingi ilivyo na pande mbili, shilingi ni hiyohiyo lakini ina kichwa na mwenge. Huwezi ukatengeneza shilingi ikawa ina kichwa pekee, itakuwa haijakamilika.

Kwahiyo spiritual energy/power ni ileile. Application ya hiyo energy ndio itakuweka upande unaostahili.
 
Kabla hamjafanya hayo mambo yenu je mna uwakika na izo ibada zenu?.

Wengi wa kizazi cha leo mnauchukulia powa uwo ulimwengu wa Roho?

Kwa bahat nzuri ama mbaya hakuna wala awezaye kuingia ktk Ulimwengu huo ilihali hajafa au hayupo ktk sleeping mode, yaan hali ya nusu ufu na kuruhusu Nafsi yako kutengana na mwili na kutenganisha mawazo+fikra za mwili, kuelekea ktk ulimwengu usio onekana.

Kabla hujafanya izo ibada zako kuwa unataka kuingia ktk Ulimwengu usio ujua, unatakiwa ujuwe kuwa je unae msaidizi wa kukupa muongozo uwapo ktk uo ulimwengu?.

Naposema msaidizi namaanisha Kiumbe wa kiroho kulingana na imani yako, mfano wasaidizi hawa ni kama malaika,majini, mapepo, mashetan, ama mizimu.

Sas wew unaetamani ama unataka kuingia ktk Mipaka isiyo kuhusu, juwa kuwa unafanya kitendo cha hatari kitakacho yagharimu maisha yako, either kifo ama kuandamwa na mapepo.

Automatic unapoingia ktk ulimwengu huo lzma uwe na mwenyej atakaye kuwakilisha na kukupeleka unapostahili kwa lengo lililokupeleka huko.

Wengi hamjui kuwa Ktk ulimwengu huo kuna kila aina za viumbe wenye nguvu kubwa na wamejawa utisho wa hali ya juu, hivyo bas wew beginner unaetaka kujaribu mambo usiyoyaweza nakutahadharisha, utaumia na hutakuwa na wakumlaumu.

Enyi Viongozi wa dini acheni upotoshaji, hakuna mwenye uwezo wa kuingia huo ulimwengu kiholela namna hiyo, izo ndoto zenu na hisia mupatazo kwa kuwaza kuwa mpo ktk level ya kiroho zinawadanganya, mtapotea bure.

Namna ya kwenda huko, ni lazma uwe invited by God's willing or Satanic willing.

Ninaposema satanic willing namaanisha ni hawa wachawi,waganga, wapiga ramli na washrikina wanaoingia ktk limwengu hizo kupitia invitation ya Shetan na Ulimwengu wake, hivyo hata akiingia huko anajulikana ni wa upande wao, na wanajua anakwenda kwa madhumuni gani.

Na God's willingness ni pale Muumba wa kweli anapoamua yeye mwenyewe bila kushurutishwa na mtu na kumchukuwa mtu kiroho kupitia msaidizi wa kiroho(malaika) ambaye anakuwa mlinzi na kiongozi wa mtu huyo kumpeleka anapostahili ili akajifunze ama kupata ujumbe wa jambo fulani, ama kupata maono ya jambo fulani.

Usidanganyike na hawa matapeli kuwa huko wanajiingilia kama chooni, ndugu yangu utakufa kabra ya umri wako,

Usifanye mzaha na Mambo yaliyo juu ya uwezo wako.

Malaika wanatishaa kama huna nguvu huwez stahimili kuwaona ama kukaa nao sambamba, utakufa, hata hao viumbe wa Giza wana nguvu, huwez stahimili kuingia ulimwengu huo kama huna msaidizi ama huna nguvu za kishirikina, utakufa mapema ama ugeuke kuwa chizi.

Acheni utani nyie wafia dini, msipende kuchukulia Simplest mambo ya kiroho yanatisha, hakuna mzaha kule

Kama njaa&madhambi yamekushinda kuyahandle, sas utaweza stahimili kuingia ulimwengu usio wako? Unataka kuingiza roho yako matatani? .

Acheni mizaha someni hizo biblia zenu, hutoona watu walikuwa wakifanya mizaha na ibada za Kiroho, akina Yohana walipoingia ktk ulimwengu huo na kupelekwa kupata maono ya siku za mwisho, walikuwa na wasaidizi ambao ni malaika wenye nguvu.

Not easy
1643672491645.jpg
 
Tunaendelea...

Kama nilivyosema kufunga ni hatua ya kuutiisha mwili. Watu huweza kufanya mambo ya mwili wanapokuwa wamekula.

Lakini ninataka mpate kujua ya kwamba kufunga na kujinyima chakula pekee haitoshi. Unatakiwa unapofunga utenge muda kwa ajili ya Sala na Maombi.

SALA NI NINI
SALA ni neno la ujumla linalojumuisha maombi yote, iwe ya shukrani, mahitaji, ibada, sifa, toba,ulinzi, Baraka n.k…Kwamfano yale maombi ya Baba yetu uliye mbinguni Yesu aliyowafundisha wanafunzi wake….Ni mfano wa SALA.

KUSIFU
Unapoanza sala ni vyema ukaanza kwa kusifu. Kusifu ni pamoja na kukubali mazingira mazuri yanayokuzunguka. Nyota, wanyama, ndege na vitu vingine kuwa wewe huna uwezo wa kuvitengeneza. Unaweza kusifu kwa kuongea au kuimba. Kubali kushuka kwa kuna mambo mengi yapo juu ya uwezo wako. Hivi vyote tunavifanya ni vitendo vya kiimani. Unaweza ukataja masuala kadha wa kadha kulingana na imani yako. Lengo kuu ni kuweza kuhamisha hisia kutoka katika mwili na kuelekeza katika roho.

TOBA
Kitu kinachoweza kukukwamisha kuingia kwenye ulimwengu wa roho ni kuwa na ila ndani yako. Ile hali ya kujikataa na kuona kwamba wewe upo na makosa kadha wa kadha. Inaweza ikawa kikwazo kwako kuingia katika ulimwengu wa roho.

Kama kuna mtu amekukosea au umemkosea, tamka maneno ya toba na weka katika imani kuwa jambo hilo limekwisha. Kuna namna nyingine ya kujikataa mwenyewe. Jaribu kuongea maneno "NIPO SAFI" kwa kurudia rudia (Chanting) mpaka akili itakapo amini kuwa huna ila tena.

MAOMBI
Tamka maneno ya kutaka unachokihitaji. Iwe ni kutaka baraka, iwe ni kutaka ulinzi au kuomba kitu.

Inakuwa ni vizuri sana kama ukiwa umeandika na kuyaweka kichwani maombi yako. Yatamke hayo maombi kwa kurudia rudia. Ukiweza tengeneza wimbo wa hayo maombi yako.

Unajua mtu anaweza kukulaani au kukubariki kama atayaandika maneno fulani na kuyaongea kwa kurudia rudia kila kwa muda mrefu.
NENO HUUMBA

Ongea maneno hayo, iache hisia ivume, kama ni maneno ya kusikitisha iruhusu hisia ifanye hivyo. Ruhusu hisia itawale.
Ukiendelea hivyo kwa muda utajikuta midomo inaanza kutetemeka tu, wakati mwingine mwili utaanza kutetemeka. Wengine huwa wanahisi umeme unapita kwenye mwili wao. Mwili utakuwa haufanyi kazi tena, huwezi kusikia, huwezi kuona, huwezi kuhisi chochote katika mwili.

Ndipo sasa utaanza kuona, kusikia na kuhisi kupitia viungo vya ulimwengu wa roho. Acha ububunije.

TUTAENDELEA.....
Wew sijui nikuite mtumishi ama nani, em tafakari kabla hujawaletea hawa izo mbinu zako za kiroho kama zina madhara ama la!.

Huwez kuingia huko kiholela namna hiyo, or otherwise uingie kupitia mind tricks kama vile Third eye opening, meditation and astral projection, accidentally unapokuwa umelala, vinginevyo haiwezekani acha kuwalisha watu watango pori
 
Mleta huu Uzi siku ukifika kuzimu utaikuta hivi kazi unayoifanya...maana unayatumia maarifa vibaya ... Unafundisha mfungo wa siku 21 afu unawaambia watu wachague uchawi au (....) Mabano haujisemi wewe ni nani - mlokole au mpagani... Neno la msalaba ni upuzi kwao wanaopotea Bali kwetu sisi tunaokolewa ni nguvu ya Mungu .. Siionei haya injili ni uwezo uletao wokovu..Kol 3;
16-17 Na kila mfanyalo kwa neno au kwa tendo fanyeni yote ktk Jina la Bw Yesu mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye...Mimi ni mlokole !
Siku hizi kila mtu ni mwalimu, ndiomaana hawana uchungu wanafunzi wao wakipotoka na kupotea...kamwe usije tamani kufanya jambo ambalo huna uwakika nalo, haswa kama lahusu haya Mambo ya rohoni
 
Wew sijui nikuite mtumishi ama nani, em tafakari kabla hujawaletea hawa izo mbinu zako za kiroho kama zina madhara ama la!.

Huwez kuingia huko kiholela namna hiyo, or otherwise uingie kupitia mind tricks kama vile Third eye opening, meditation and astral projection, accidentally unapokuwa umelala, vinginevyo haiwezekani acha kuwalisha watu watango pori
Tatizo unajifanya mjuaji. Una okoteza maneno/terms huko na kuja kuwatisha watu.

Hakuna cha kuhofia zaidi ya hofu yenyewe!
 
Back
Top Bottom