Siri niliyoipata katika kufunga siku 21 kila mwanzo wa mwaka

Siri niliyoipata katika kufunga siku 21 kila mwanzo wa mwaka

JAMBO NI KUFANYA SIYO KUONGEA

Mambo haya siyo ya kuongea tu.
Mimi ninachokisema kipo kinafanyika. Wewe ni uchaguzi wako. Maarifa haya yapo na wengi huyatumia.

Kuna dini na madhehebu yapo yameandaa SALA na DUA katika maandishi. Wale watu wakikaa wiki au zaidi ya wiki wamejifungia kwa jambo hilo hilo huku wamefunga, hakika nakuambia litatokea.

Halafu haya mambo ninayoyaongelea hapa ni masuala ya IMANI. IMANI(Hisia) lazima ihusiane na MATAKWA(will)

FAITH AND WILL
vikiungana kwa pamoja lazima jambo litokee.

Wengine wanasema huwezi kumshawishi Mungu kupitia kufunga na kusali.
Watu hapa wanaongelea kitu tofauti kabisa. Hapa tunaongelea kuingia katika ulimwengu wa roho.
 
Ahsante kwa muongozo, tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
ULIMWENGU WA ROHO

Pale utakapofunga, utaufanya mwili uwe dhaifu. Mwili utaanza ku regulate namna ya kutuzakisha energy kwenye mwili kwa matumizi madogo ya chakula kilichopo kwenye mwili wako.

Kwakuwa unatumia asali na sukari huku ukiwa umevichanganya na maji, mwili utakuwa unapata kiwango kidogo cha chakula, kwahiyo mwili utaacha ku process unnecessary activities. Ndipo hapo milango ya fahamu na thought zitapunguza utendaji wake wa kazi. Ndipo hapo ulimwengu wa roho utakapoanza kuchukua nafasi.

Unaweza usiingie katika ulimwengu wa roho at the first week, lakini utakapoendelea kutenga muda wa faragha utaanza kuingia taratibu. Nakuhakikishia kabla ya siku hizo 21 kuisha utakuwa umekutana na mambo mengi.

Katika ulimwengu wa roho level one. Kuna vurugu za kila aina. Utakutana na kuzungumza na kila aina ya roho. Hakikisha lengo lako lililokufanya ufunge unalizingatia. Chanting inakuwa kama gateway ya kuingia huko.

Ni kwambie ukweli, usipo kuwa makini na kuwa mwangalifu, baada ya siku hizo utarukwa na akili. Utagudua mambo mengi ikiwamo kwamba uhalisia wetu ni ulimwengu wa roho. Utaweza kukutana na watu waliokufa na kuongea nao ana kwa ana. Na ukiwauliza wakupe evidences ya hayo wanayo yaongea watakupatia, na uta prove.

Utaweza kutembea (utaweza hata kuwasiliana na nafsi ya mtu aliyehai na kufanya jambo fulani). Hapa sasa baada ya mfungo wengine hugeuka na kuwa wachawi, wasoma nyota na waonaji.

Kumeibuka na kundi kubwa la walokole wanaojiita manabii. Ukweli ni kwamba hao ni waonaji sawa na wapiga ramli. Hao watu wanauwezo wa kukuelezea matukio yako yote yaliyopita.

Hata wewe ukifika katika ulimwengu wa roho jicho lako la tatu(spiritual eye) litaanza kufunguka. Lakini my WARNING tafuta kwenda mbali zaidi katika ulimwengu wa roho, usiishie hapo tu. Go to the most higher ili uweze kuwa enlighten. Katika level ya kwanza utakuwa na uwezo wa kuwasiliana na watu waliokufa na kuwa muonaji. Hii siyo enlightenment, enlightenment ni kujua siri kuu za spiritual world.

Utakapoanza kuona, unakutana waliokufa zamani na kuongea nao; USIOGOPE upo katika safari ya kuelekea ulimwengu wa roho level ya juu zaidi.

USIWAPE MBWA CHAKULA CHA WATOTO.

Nitatoa summary but not details.

NITAENDELEA.....
Dah sie mbwa tumenyimwa chakula cha watoto
 
Nadhani hapa unaongelea kitu tofauti kabisa na kile ninachokiongelea.

Hapa ninaongelea vitu vinavyotokea baada ya kufunga ukiwa serious.
Kwenye maongezi yangu hapa niliongelea kuwa unapofunga lazima uwe na lengo. Nikasema katika ulimwengu wa Roho kwa ninavyofahamu upo katika levels 6.

Nilieleza kuwa level ya kwanza ipo na kelele nyingi. Nikaendelea kusema katika level hiyo utaweza kukutana na watu waliokufa.

Hapa ninaongelea matokeo ya kufunga.
Hata hivyo hebu soma hapa:-

2 Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.
2 Wakorintho 12:2

3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua);
2 Wakorintho 12:3

4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene.
2 Wakorintho 12:4
Maelezo yako hayatoshelezi kujibu swali kuu. Je, unafundisha watu kufunga kwa msingi wa Mungu yupi?

Unaposema hakuna manabii una maana unapingana na maandiko katika Yoeli 2:28, 1 Wakorintho 12:10 na Warumi 12: 6
Unabii ni karama itokanayo na Roho Mtakatifu hivyo unaposema hakuna manabii maana yake unapingana na Neno la Mungu.

Kwenye suala la kuzungumza na wafu. Neno la Mungu limekataza kabisa (forbidden) kuzungumza na wafu. Soma Kumbukumbu la torati 18:10-12. Kwa kwesi ya Sauli na Samweli hili ni somo kamili lakini kwa ufupi ijulikane kuwa kabla ya Yesu kuja, kufa na kufufuka yeyote aliyekufa alikuwa anaenda kuzimu na kuzimu ilikuwa imegawanyika chini na juu, chini walienda walio na dhambi na juu walienda wasio na dhambi soma Luka 16:19-23 Sasa ileweke Samweli alienda kuzimu lakini juu na matokeo ya Sauli kuzungumza na Samweli mfu yalikuwa ni kifo soma 1 Samweli 28:1.......; hata na kesho wewe na wanao mtakuwapo pamoja nami;.... sasa maneno haya mtakuwapo pamoja nami yaliimaanisha Sauli na wanawe watakufa na kweli Sauli na wanawe walikufa keshoyake.

Utaratibu wa watu wasio na dhambi kwenda kuzimu ulikoma baada ya Yesu kufa msalabani na kushuka kuzimu kufanya vita na kumnyang'anya shetani funguo za kuzimu na mauti ndio maana saa tisa Yesu alipokata roho miili ya watakatifu ilifufuka soma Mathayo 27:52-53.

Hivyo kufunga kwetu kusitukoseshe na Mungu, na iwelewe kufunga hakubadilishi mapenzi ya Mungu ila kunakubadilisha wewe kukubali mapenzi ya Mungu yatendeke.
 
Nawasalimia wana JF wote.

Katika mwendelezo wangu wa kuwafundisha na kuwafungua macho watu, leo nimeonelea nilete siri iliyomo katika kufunga.

Kwanza kabisa nawaomba muelewe kwamba, kuna namna nyingi sana ya kufunga lakini nitaongelea namna tatu:-
1. Kufunga kwa malengo
2. Kufunga kwa mujibu wa utaratibu au sheria
3. Kufunga kwa mkumbo

Sitaelezea kila moja maana lengo la waraka huu ni kuongelea siri iliyomo katika kufunga.

Kuna njia nyingi ambazo hutumika katika kufunga lakini mimi leo ninaongelea njia moja ambayo huwa naitumia katika kufunga siku 21.

Mara ya kwanza kabisa nilifunga siku tatu mfululizo pasipi kula wala kunywa. Nilikuwa nimefunga na nimejifungia sehemu kwa ajili ya kusali na kuomba. Katika mfungo huo niligundua kuwa:-
1. Unapofunga unaufanya mwili uweze kukutii na kuanza kusikiliza kutoka ndani

2. Unapofunga unapata muda wa kuwasiliana na high self.

3. Kufunga holela pasipo utaratibu unaweza ukaathiri afya ya mwili wako.

4. Kufunga pasipo kufundishwa njia zilizomo katika ulimwengu wa roho, unaweza ukajikuta unarukwa na akili baada ya mfungo.

Ikumbukwe unapofunga unaufisha mwili ili uweze kuingia katika ulimwengu wa roho. Katika ulimwengu wa roho kuna levels 6, as I know mpaka sasa. Katika level ya kwanza utakutana na vurugu za kila namna. Hapajatulia, maana ni rahisi kwenda. Level hiyo kwa mara nyingi huwa tunaiita PEPO. Kwahiyo usipofundishwa namna ya kutembea katika ulimwengu huo; unaweza ukajikuta baada ya mfungo unakuwa mtu wa ajabu, au mara nyingine unarukwa na akili.

JINSI YA KUFUNGA UNAINGIA ROHONI PASIPO KUATHIRI AFYA

Niliweza kujifunza namna ya kufanya na kuniwezesha kila mwaka kufunga siku 21 mfululizo. Unatakiwa uwe na asali, sukari na maji.

Kila siku baada kufanya maombi ya asubuhi; chemsha maji, baada ya maji kuchemka kiwango cha chai, tia asali na sukari, kuywa kikombe kimoja mpaka viwili (Kikombe cha chai).

Ikifika jioni kama saa 12 au saa moja fanya hivyo hivyo, yaani chemsha maji tia sukari na asali.

Fanya hivyo kila siku mpaka siku 21. Mwili wako utaendelea kufanya kazi na hapo hapo utaweza kuingia ulimwengu wa Roho.

UWE NA JAMBO(MAMBO) LINALOKUFANYA UFUNGE

Utakapokuwa na jambo lililokufanya ufunge, litakusaidia kwamba utakapokuwa kwenye maombi na sala utajikita katika jambo lililokufanya ufunge. Sasa basi hii itakusaidia utakapikuwa katika level ya kwanza ya ulimwengu wa roho, hutababaika na yale yatakayokuwa yanatokea. Maana ukifunga pasipokuwa na jambo lolote, utajikuta unazagaa tu kwenye huo ulimwengu, kwahiyo chochote kitakachokuwa kinatokea ni halali yako.

Kuna nguvu katika kutamka. Tamka kwa kurudia rudia jambo unalotaka (Chanting). Liongea kwa sauti au ikiwezekana tengeneza wimbo.

Wakati wa kusali na kuomba, tafuta sehemu ya faradha.


NITAENDELEA NA SOMO HILI....
Boss chapisho hili ni zuri sana, je una maarifa juu ya tahajudi(meditation).
 
Maelezo yako hayatoshelezi kujibu swali kuu. Je, unafundisha watu kufunga kwa msingi wa Mungu yupi?

Unaposema hakuna manabii una maana unapingana na maandiko katika Yoeli 2:28, 1 Wakorintho 12:10 na Warumi 12: 6
Unabii ni karama itokanayo na Roho Mtakatifu hivyo unaposema hakuna manabii maana yake unapingana na Neno la Mungu.

Kwenye suala la kuzungumza na wafu. Neno la Mungu limekataza kabisa (forbidden) kuzungumza na wafu. Soma Kumbukumbu la torati 18:10-12. Kwa kwesi ya Sauli na Samweli hili ni somo kamili lakini kwa ufupi ijulikane kuwa kabla ya Yesu kuja, kufa na kufufuka yeyote aliyekufa alikuwa anaenda kuzimu na kuzimu ilikuwa imegawanyika chini na juu, chini walienda walio na dhambi na juu walienda wasio na dhambi soma Luka 16:19-23 Sasa ileweke Samweli alienda kuzimu lakini juu na matokeo ya Sauli kuzungumza na Samweli mfu yalikuwa ni kifo soma 1 Samweli 28:1.......; hata na kesho wewe na wanao mtakuwapo pamoja nami;.... sasa maneno haya mtakuwapo pamoja nami yaliimaanisha Sauli na wanawe watakufa na kweli Sauli na wanawe walikufa keshoyake.

Utaratibu wa watu wasio na dhambi kwenda kuzimu ulikoma baada ya Yesu kufa msalabani na kushuka kuzimu kufanya vita na kumnyang'anya shetani funguo za kuzimu na mauti ndio maana saa tisa Yesu alipokata roho miili ya watakatifu ilifufuka soma Mathayo 27:52-53.

Hivyo kufunga kwetu kusitukoseshe na Mungu, na iwelewe kufunga hakubadilishi mapenzi ya Mungu ila kunakubadilisha wewe kukubali mapenzi ya Mungu yatendeke.
Soma nilichokiandika kabla ya kuanza kujibu kitu ambacho sichakiongelea hapa.

Wapi nimesema hakuna manabii!?
Nimesema kunatofauti ya Nabii na mtu anayeweza kuona.
Nikasema wale wanaojiita manabii kwa sasa asilimia kubwa ni waonaji hawana tofauti na wapiga ramli.

Halafu hapa ninaongelea suala la kufunga. Je unaweza kuniuliza kuhusu suala hilo!?

Cha pili ungefuatilia uzi huu na ukaelewa msingi wa mtu aliyekuwa anauliza swali. Kukatazwa kuongea kwenye vitabu vya dini haiwezi ikaondoa uwepo wa ulimwengu wa roho na existence yao katika ulimwengu huo.
 
Nawasalimia wana JF wote.

Katika mwendelezo wangu wa kuwafundisha na kuwafungua macho watu, leo nimeonelea nilete siri iliyomo katika kufunga.

Kwanza kabisa nawaomba muelewe kwamba, kuna namna nyingi sana ya kufunga lakini nitaongelea namna tatu:-
1. Kufunga kwa malengo
2. Kufunga kwa mujibu wa utaratibu au sheria
3. Kufunga kwa mkumbo

Sitaelezea kila moja maana lengo la waraka huu ni kuongelea siri iliyomo katika kufunga.

Kuna njia nyingi ambazo hutumika katika kufunga lakini mimi leo ninaongelea njia moja ambayo huwa naitumia katika kufunga siku 21.

Mara ya kwanza kabisa nilifunga siku tatu mfululizo pasipi kula wala kunywa. Nilikuwa nimefunga na nimejifungia sehemu kwa ajili ya kusali na kuomba. Katika mfungo huo niligundua kuwa:-
1. Unapofunga unaufanya mwili uweze kukutii na kuanza kusikiliza kutoka ndani

2. Unapofunga unapata muda wa kuwasiliana na high self.

3. Kufunga holela pasipo utaratibu unaweza ukaathiri afya ya mwili wako.

4. Kufunga pasipo kufundishwa njia zilizomo katika ulimwengu wa roho, unaweza ukajikuta unarukwa na akili baada ya mfungo.

Ikumbukwe unapofunga unaufisha mwili ili uweze kuingia katika ulimwengu wa roho. Katika ulimwengu wa roho kuna levels 6, as I know mpaka sasa. Katika level ya kwanza utakutana na vurugu za kila namna. Hapajatulia, maana ni rahisi kwenda. Level hiyo kwa mara nyingi huwa tunaiita PEPO. Kwahiyo usipofundishwa namna ya kutembea katika ulimwengu huo; unaweza ukajikuta baada ya mfungo unakuwa mtu wa ajabu, au mara nyingine unarukwa na akili.

JINSI YA KUFUNGA UNAINGIA ROHONI PASIPO KUATHIRI AFYA

Niliweza kujifunza namna ya kufanya na kuniwezesha kila mwaka kufunga siku 21 mfululizo. Unatakiwa uwe na asali, sukari na maji.

Kila siku baada kufanya maombi ya asubuhi; chemsha maji, baada ya maji kuchemka kiwango cha chai, tia asali na sukari, kuywa kikombe kimoja mpaka viwili (Kikombe cha chai).

Ikifika jioni kama saa 12 au saa moja fanya hivyo hivyo, yaani chemsha maji tia sukari na asali.

Fanya hivyo kila siku mpaka siku 21. Mwili wako utaendelea kufanya kazi na hapo hapo utaweza kuingia ulimwengu wa Roho.

UWE NA JAMBO(MAMBO) LINALOKUFANYA UFUNGE

Utakapokuwa na jambo lililokufanya ufunge, litakusaidia kwamba utakapokuwa kwenye maombi na sala utajikita katika jambo lililokufanya ufunge. Sasa basi hii itakusaidia utakapikuwa katika level ya kwanza ya ulimwengu wa roho, hutababaika na yale yatakayokuwa yanatokea. Maana ukifunga pasipokuwa na jambo lolote, utajikuta unazagaa tu kwenye huo ulimwengu, kwahiyo chochote kitakachokuwa kinatokea ni halali yako.

Kuna nguvu katika kutamka. Tamka kwa kurudia rudia jambo unalotaka (Chanting). Liongea kwa sauti au ikiwezekana tengeneza wimbo.

Wakati wa kusali na kuomba, tafuta sehemu ya faradha.


NITAENDELEA NA SOMO HILI....
Asante kwa mada nzuri, nimeipenda sana na ninaamini itabadili maisha yangu. Swali langu kwa vile ni wa siku 21 je tunaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa na wenza? maana mwingine anaweza asielewe. Pia kama mie ni beginner, usually nafungaga ya saa 12, je siwezi nikawa nakunywa kitu kizito zaidi ya asali na maji? Mfano vegetable/green juices?
 
Nasubiria funga aina nyingine.. nimewahi kuweka nia ya kufunga na nkafunga mwaka jana kipindi cha kwa resima.

Ila ilivyofika saa 9 ntapambana na njaa na hasira na myu naye qkaja akanivuruga end of the story nkashusha hasira na kitimoto
Kwani kufunga lazima uache kula??.Mimi nafikiri kufunga inahusisha mambo mengi zaidi ya kujinyima kula, Nijuavyo Mimi unaweza kula tu kiasi kwaajili ya kuendeleza uhai,lkn ukajinyima vitu visivyo vya lazima,km vile unywaji wa bia au soda,ulaji wa Vyakula vizuri vizuri na vya gharama,n.k.Kisha pesa uliyoisevu kutokana na kujinyima kupeleka kwa wahitaji km vile kwenye nyumba za kulelea Wazee, watoto yatima, wagonjwa walioko mahospitalini au majumbani, watoto wa mitaani,n k.,Jambo jingine muhimu ni sala na kuomba toba na pia kutoa msamaha kwa waliokukosea au wewe kuomba radhi kwa wale uliowakosea.Ukiyafuata haya, naamini funga yako itakuwa na maana sana.
 
Neno la Mungu linataka ukifunga ufunge kwa Siri mtu asijue, Yani hata mdomo upakwe mafuta usipauke.

Sasa mbona mnatangaza kufunga na kujulikana fulani kuwa kafunga?
 
Hivyo kufunga kwetu kusitukoseshe na Mungu, na iwelewe kufunga hakubadilishi mapenzi ya Mungu ila kunakubadilisha wewe kukubali mapenzi ya Mungu yatendeke.

Nime note hili kufunga hakubadilishi mapenzi ya Mungu,bali kufunga kunatufanya sisi kukubali mapenzi ya Mungu yawe kama alivyokusudia.
 
Nimefuatulia bandiko lakini sijaona hitimisho la faida ambayo wewe uliipata baada ya kufanya hiyo meditation '

Yaani baada ya kumaliza huo mfungo ulinufaika kwakupata Nini ,

Let say uliamua kufunga kwaajili ya kuomba Kazi je ulipata (mfano tu )
 
Vip ndani ya hizo siku sex inaruhusiwa, au ndio itakuwa huwazi kabisa
Ukiona unaingia kwenye mfungo kama huo na bado unawaza sex basi fanya kuhairisha mpaka wakati mwingine. Maana kama una dhamira ya kweli ya kufanikisha jambo, wazo la sex huwa linapotea kabisa kichwani.

Alafu sidhani kama utakuwa na hiyo energy baada ya kama siku nne za mwanzo, wengine siku tatu tu mwili unaanza kujikataa.
 
Kwa mfungo mzuri usioweza kuathiri afya nivyema ukawa unachemsha maji asubuhi na jioni na kuweka asali na sukari. Unatumia kikombe kimoja cha chai.

Tenga muda wa kufanya sala na maombi.
Mimi nashauri uweze kuamka saa nane za usiku. Muda huo utakuwa umetulia.
Asante
 
Back
Top Bottom