Getang'wan
JF-Expert Member
- Apr 9, 2015
- 3,076
- 3,416
Tuubebe tu ndo tupate akili maana hakuna namna. Wakati Kafulila analipigania hili suala bungeni watu walikuwa wanamkejeli kwamba katumwa. Haya, sasa Std Chartered Bank na IPTL nao wametumwa tuone kama mtabisha. Ili tukae sawa na deni liwahi kuisha kila anayetumia umeme anunue unit kwa shilingi 3000/-Watu walishasema watakao bebeshwa huo mzigo wa kulipa hayo madeni ni wananchi.
Ni heri warudishe service charge kuliko hiki kitu wanachotaka kufanya.
Duuuh mkuu ni laana sana kuzaliwa kwenye nchi yenye maamuzi ya hovyo kama TanzaniaMasiki wee!! Yule rais wa wanyonge sijui yuko wapi? Kafulila alimwambia hakusikia walijifanya hawaoni wala kusikia, maisha yalivyotaiti natabiri wapo wananchi wataanza kuvaa chupi kichwani,
Watoto wao mmewanyima mikopo, mmewafutia posho na marupurupu vikaoni, mmewapandishia asilimia wadaiwa Heslb, huku mtaani T.R.A, halmashaur na Majembe(vishoka wa t.r a) wanapishana tu maduka na vibanda vinatiwa makofuli tu, huku baadhi ya bidhaa zikipaa bei, tunaendlea kumuomba Mungu mvua inyeshe tukalime nako matumaini ni kidogo maana mpska muda huu jua ni kali sana mbaya zaidi yule rais wetu sisi masikin alishaapa hatatoa chakula cha msaada kwa halmashauri yeyote alisema ni uzembe kukosa mavuno
NI MUNGU PEKEE AJUAE TUENDAKO
Yes of courseIs getting too much ila hakuna namna, tulipe tu. Watanzania hatuna utamaduni wa kufanya maandamano ya kupinga 'mambo ya hovyo' kushinikiza viongozi kuwajibika,hatuna uchungu na kodi zetu ambazo serikali & Co wanazitapakanya hovyo na kukwapua. Hadi siku watu wengi watakapokuwa tayari kupigania Taifa lao, naamini hata vyombo vya dola vitakuwa upande wa wananchi.
KADA
Watu waisome plate number vizuri wajiifunze kudai haki zaoMi naona wacha ipande tuumie mpaka tukome.tena wapandishe hasa.
Bank ya standard chartered ya hong Kong uenda ikaifilisi TANESCO.
Ni baada ya kuiomba mahakama TANESCO isitishe kwanza kuilipa IPTL mpaka pale itakapoilipa bank hiyo kiasi cha bilioni 320.
Zilizokwapuliwa kupitia bank hiyo hivyo TANESCO itaamuliwa kulipa deni hilo huku waliendelea kuweka pesa kwa ajiri wa kuilipa IPTL
View attachment 432820
My take: Kumbe siri ya kupanda umeme January ndio hiyo TANESCO wanahaha kuhakikisha wanawakamua wananchi ili kulipa deni la IPTL na standard chartered yaani kiufupi TANESCO sasa wanadaiwa Mara mbili.
Masikini Tanzania nawaonea huruma sana wanachi hasa wa vijijini waliowekewa umeme kwa mbwembwe kwa miradi ya Umeme vijijini sasa wanazidi kukamuliwa na serikali kupitia Tanesco.
waHivi hakuna uwezekano wa kuwa na mashirika mengi ya umeme kama yalivyo makampuni ya mitandao ya simu?
Kwani yamezuiliwa?
wa
Sasa hivyo viwandavitajengwa kweli wakati umeme unapanda?[/QUOTE
UMEME WA UHAKIKA SAFARI YA UCHMI WA VIWANDA.
TANESCO Sasa wanaimarisha na kuboresha miundombinu yao i
Inashangaza mno,vitu sen7sitive kama hivi vinakosa mantiki kwa sababu hii nchi kila kitu kimekuwa ni siasa...hili suala watu waliwajibika..mbele ya muhimili wa nchi..walishindwa kwa hoja..facts zili prove escrow ilikuwa ni "deal"...muhongo akaachia ngaz..maswi akangatuka..CAG na TRA walithibitisha kwa kutoa tafsir kuwa zile ni pesa za wananchi..yan za serikali..chakushangaza..aliyesema..anakuja kusaidia wananchi..wanyonge..kuinua hali ya kiuchumi..ndio huyo huyo aliewarudishia uongoz maswi na muhongo...ham a jipya hapa...sitegemei jipya kutoka huko!
Haaaah uo ni utetezi thaifu mnoTAARIFA KWA UMMA
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa iliyotolewa katika vyombo mbalimbali vya habari kuhusu ombi la kurekebisha bei za umeme kwa mwaka 2017.
Ombi la mabadiliko ya bei za umeme liliwasilishwa EWURA kulingana na Agizo la kubadilisha bei za umeme la mwaka 2016 lililoanza kutumika tarehe 1 April 2016. Ifahamike kuwa bei za umeme (Electricity Tariffs) zinazotumika zilitolewa zitumike mpaka tarehe 31/12/2016, hivyo itakapofika Januari 2017, inatakiwa bei mpya za umeme (New Electricity tariff) kutolewa kwa mujibu wa sheria.
Hivyo TANESCO ilitakiwa kufanya tathmini ya gharama za uzalishaji , usafirishaji na usambazaji umeme na kupeleka mapendekezo hayo kwenye Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji(EWURA), ili kupitiwa na kufanyiwa taftishi(kupata maoni ya wadau) ikiwa ni pamoja na Baraza la Ushauri la Serikali . Hivyo basi ikiwa bei za umeme zitapanda au kutopanda, hiyo itategemea na mapitio ya tathmini ya gharama za kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme tulizo wasilisha EWURA.
TANESCO haiwezi kuamua yenyewe kupandisha au kutopandisha bei za umeme. Kwa mujibu wa sheria, EWURA inapaswa ifanye mapitio ya bei za umeme kwa kila robo mwaka (Periodic Tariff Adjustment).
Tunapenda Umma ufahamu kuwa kupanda au kushuka kwa gharama za umeme ni suala la kisheria na ni jambo la kawaida kwani bei ya umeme imeshawahi kushuka katika vipindi tofauti kwa mfano Mwaka 2015 (robo ya kwanza ya mwaka) bei ilishuka kwa asilimia 2.5. Vivyo hivyo Mwezi Aprili mwaka 2016 pia gharama za umeme zilishuka kwa asilimia 1.6
IMETOLEWA NA: Mhandisi FELCHESMI MRAMBA
Mkurugenzi Mtendaji
Shirika La Umeme Tanzania (TANESCO)
08 Novemba 2016
Tanesco yetu tarehe 11/08/2016
Haiwezekani kwa sababu umeme hausafiri hewani kama mawimbi ya simu!Hivi hakuna uwezekano wa kuwa na mashirika mengi ya umeme kama yalivyo makampuni ya mitandao ya simu?
Nchi zingene wamefanikiwa vipi kuwa na umeme wa uhakika?Haiwezekani kwa sababu umeme hausafiri hewani kama mawimbi ya simu!
Kuwalazimisha watanzania kulipa deni wasilo na maslahi nalo kwa sababu ya wajanja wachache! Inauma sana!!!
Hii ndio Tanzania ya Ccm.
Hii nchi imejaa dhuruma kila mahala,wao ccm waendelee tu kutawala hakuna shida.