Sisi hatukupaswa kutoa msaada wa fedha Uturuki, tulitakiwa kutuma kikosi cha uokoaji

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Msaada wetu kwa Uturuki umechelewa sana, tunaanza kucheza wakati mziki umeisha!

Sisi hatutakiwi kutoa msaada wa kifedha kwa wale jamaa, bali tulitakiwa kupeleka kikosi cha uokoaji kwenda kusaidia uokozi kwenye majengo yaliyoporomoka na kukalia watu.

Tulikuwa wapi kutoa msaada wa aina hii mapema? Mahitaji makubwa ya Uturuki haikuwa fedha, bali vikosi vya uokozi.
 
Acha tozo zitumike!
 
Naiomba Serikali Kwanzia leo SukumaGang i orodheshe kwenye kikundi cha waasi
 
Kweli kabisa,

Mkapa aliwahi Sema, mtaji wa.....ni nguvu zake.
 
Samia ni Kiongozi ,kwanza mswahili, alafu akapata Washauri wabovuuuuu kwelikweli, wengi wa Washauri wa Samia, ni walamba Asali.
Hile hela ukifuatilia utakuta ni namna ya watu kupiga,pale wataalamu wa Money laundering wamepeleka fedha zaidi ya iyo Dola milioni moja na Balozi kaambiwa vijana watakuja kuzichukua!
Tanzania kusaidia Uturuki kifedha kweli???
 
Umesema kweli aisee!
 
Unaisaidia Uturuki hela?
 
Mpokeaji anasemaje ndio la msingi tuanzie hapo!
 
Mawazo ya mleta mada hayatakiwi kupuuzwa hata kidogo.

Tulistahili kupeleka kikosi cha uokoaji, siyo fedha. Shida ya Uturuki haikuwa fedha bali kuokoa maisha ya watu, na kutoa maelfu ya miili iliyokuwa imefunikwa na vifusi.

Nimekuwa na mawasiliano ya karibu na jamaa zangu waliopo Uturuki, wanasema makampuni na watu binafsi wamechangia pesa nyingi sana. Kuna mtu binafsi mmoja alichangia U$20 billion.

Sasa hivi AFAD imetangaza kutopokea misaada ya fedha. Tayari kumethibitika ubadhirifu mkubwa wa fedha za maafa.

The Disaster and Emergency Management Authority (AFAD) of Turkey is an institution working to prevent disasters and minimize disaster-related damages, plan and coordinate post-disaster response, and promote cooperation among various government agencies.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…