Sita wasomewa mashtaka ya mauaji ya Milembe Seleman aliyekuwa Afisa wa GGM, akiwemo aliyekuwa "mkewe"

Sita wasomewa mashtaka ya mauaji ya Milembe Seleman aliyekuwa Afisa wa GGM, akiwemo aliyekuwa "mkewe"

Watu sita wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Geita wakishtakiwa kwa kosa la kumuua aliyekuwa mfanyakazi wa kampuni ya madini ya dhahabu (GGM) Milembe Seleman (43).

Watuhumiwa waliopandishwa mahakamani katika kesi namba 12/2023 ni Dayfath Maunga(30), Safari Labingo(54), Genja Lubingo(30), Musa Lubingo (33), Maige Fundikira (37) na Ceslia Macheni (55).


Mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Johari Kijuwile, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Scolla Teffe ameieleza Mahakama hiyo kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa la mauji kinyume na kifungu cha 196 & 197 cha kanuni ya adhabu .

Amedai Aprili 26, 2023 Dayfath Maunga na wenzake watano huko katika maeneo ya Mwatulole wakishirikiana kwa pamoja walimuua Milembe Seleman.

Washtakiwa hao hawakupaswa kuzungumza chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 7, 2023 itakapotajwa na washtakiwa wote wamerudishwa mahabusu.


Pia Soma > Afisa Ugavi wa mgodi wa Geita, Milembe Suleiman auawa na viganja vyake kukatwa
mzazi wa marehemu Milembe Suleman aongea mazito
Kukatisha uhai wa mtu ni kosa dhidi ya jamhuri.

Mahakama itimize wajibu wake muhimu
 
Kuna ulazima wa kupelekwa kwenye mahakama isiyo na uwezo kusikiliza kesi yao?

Si ni kupoteza muda? Ni halali kumsomea mtu mashtaka bila kumpa nafasi ya kujibu, hata kukana tu?
Kuna ulazima wa wewe kufika mahakamani na kujifunza maana ya hizo hatua. Hizo Mahakama za chini kazi yake ni kukusanya taarifa zote na kuzifaili kwenda Mahakama Kuu baada ya kuwa zimekamilika. Lengo ni kusaidia mahakama za juu kutokuwa na mlolongo mrefu wakati wa kusikilizwa kesi husika.

Kazi kubwa ya mshtakiwa hapo ni kuwafahamu mashahidi na vielelezo ili ajipange jinsi ya kukabiliana nao huko juu. Offcoz hii ni stage ya muhimu sana kwa mshtakiwa pengine kuliko anayeshtaki japo unaona kama anaonewa hivi kwa kuwa hapewi nafasi ya kujibu.
 
Kuna ulazima wa kupelekwa kwenye mahakama isiyo na uwezo kusikiliza kesi yao?

Si ni kupoteza muda? Ni halali kumsomea mtu mashtaka bila kumpa nafasi ya kujibu, hata kukana tu?

Ni utaratibu wa kisheria , ukisubiria committal proceedings kwenda mahakama kuu. Huo muda ofisi ya DPP inakuwa inaandaa ushahidi wa kutosha kuwafungulia kesi hao watuhumiwa.
 
Waje na humu jf kuna walioshangilia kweli ukute ni ndugu wa hiyo familia hapo juu wakidhani mkono wa serikali ni mfupi,

Natamani Lemutuz angekua hai aone hao wauaji aliokua anawashangilia kwa kumuua msagaji wanavyopigwa mvua ya maisha,

Na hii iwe fundisho kwa wajinga wote hakuna aliye juu ya sheria, ukikoswa na sheria ya Dunia basi Mungu mwenyewe atakuadhibu kwa kujipa majukumu yasiyokua yako (ref, kwa Lemutuz hakuchukua hata mwezi)

Hongera jeshi letu la polisi, hongera serikali ya Mama Samia, naona hata humu nyuzi za Ushoga zimeisha kabisa watu wameufyata kama Mbwa kaona Chatu [emoji23][emoji23][emoji23]

Tuombee DPP apate ushahidi wa kufungua kesi mahakama kuu, isije ikatumika siasa kuiondoa hiyo kesi. Maana mpaka muda huu jalada lipo chapa kwenye ofisi ya DPP.
 
Back
Top Bottom