Uchaguzi 2020 Sitaki kuwa mnafiki. WanaCCM awamu hii tunaburuzwa na Mwenyekiti

Na wale wenzio vichwa ngumu watakiri tu, ngoja akili ziwakae sawa, bado wako usingizini.

Cc.
drone camera.
chagu wa malunde.

Anawachezesha kwata lakini wanamsifia tu, sijui wamelogwa na nani!.
Kwa hiyo mtoa mada ameongea nini cha maana hapo? Ccm ni kawaida kumuachia mgombea aliefanya vizuri amalizie ngwe iliyobaki na imekuwa taratibu yao zaidi ya miaka 36. Mtoa mada anawapangia Ccm wakati ni utaratibu wao? Kura alitaka zipigwe vipi? Kura zimepigwa kwa uwazi na kuhesabiwa kwa uwazi. Sasa alitaka nini zaidi? Anaongea pumba na upuuzi tu.
 
Msimsingizie. Uwezo wa kupiga kura ya hapana mlikuwa nao. Tamaa zenu na malengo yenu binafsi ndo yalowapelekea kupiga kura za ndiyo. Hamuwezi kuja huku kutudanganya kwamba mmezuiwa. Mlikuwa na hiari ya kutokwenda pia.

Kila la heri kwenye harakati zenu za kisiasa.
 
Juzi tu hapa umeogopa kuandamana na shati jeupe. Ukabaki kuandamana kwenye keyboard. Chadema kufilisika kihoja isiwe sababu ya kuhamasisha upuuzi.
 
Bila shaka wewe ni mnufaika wa ubabaishaji unaoendelea ndani ya chama
 
We kiazi soma mchakato wa kura ulivyoendeshwa na mwenyekiti wenu, wacha kukurupuka.
 
Muonyesheni jinsi ya kiyafanya kwa usahihi huko chadema
 

Huna ujualo, unadhani zile kura kupigwa pale ndio ilikuwa maamuzi ya pale? Inaonekana hujui mifumo ya kidictator inafanya vipi kazi. Ole wa mkoa wowote ambao ungepiga kura ya hapana, mbona wangempata aliyepiga hiyo kura. Uwezo wako wa kuelewa mambo naujua mpaka wake.
 
Mkuu wapinzani wa hii nchi hawana nia ya kweli kwa sababu suala la tume huru walishauriwa tangu 2016 lakini wakatia pamba sikioni imebaki miezi michache bado wanakumbushwa lakini hawana hiyo nia ya kudai mbaya zaidi misimamo hawana..hujui wanapigania nini.

Mwenyekiti wa CCM ambaye ndiye Rais wa nchii anateua tume ya uchaguzi yeye na aliwaambia wakurugenzi amewateua yeye,amewapa mshahara,gari,nyumba na posho yeye ole wao wawatangaze wapinzani lakini bado wapinzani tupo kama Nyumbu tunaenda kupigana mazingira hayo.
 
Mwaka huu ni kichekesho. Mtaongea kila uongo. Sasa hao wagombea wenu ambao hata udiwani hawawezi kupata unadhani wana Ccm wasingepiga kura zote kwa JPM kwa mambo anayofanya?
 
Juzi tu hapa umeogopa kuandamana na shati jeupe. Ukabaki kuandamana kwenye keyboard. Chadema kufilisika kihoja isiwe sababu ya kuhamasisha upuuzi.

Hakukuwa na maandamano, bali wito ilikuwa ni kuvaa nguo nyeupe, na hilo nililifanya mimi na mke wangu kwa usahihi sana. Narudia tena, iwapo wapinzani wanataka sehemu watakazopata ushindi watangazwe, basi inabidi waende na silaha za jadi.
 

Tunawacheki tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…