Sitashiriki kamwe chaguzi yoyote nchini Tanzania kwa sababu ya Viongozi wa Serikali za Mitaa na Wizara ya Ardhi

Sitashiriki kamwe chaguzi yoyote nchini Tanzania kwa sababu ya Viongozi wa Serikali za Mitaa na Wizara ya Ardhi

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Kipimo kikuu cha akili na ustaarabu wa binadamu yeyote yule ni namna anavyopangilia maeneo yake anayoishi na kufanya shughuli zake.

Haijalishi kama anajenga nyumba za kitajiri au za kimaskini ila namna gani alivyopima na kupangilia makazi yake ndicho kielelezo pekee kinachoweza kukwambia kuwa huyu binadamu ana akili sawa na amestaarabika kweli.

Nchi ya Tanzania imeharibiwa na watu wengi sana!

Ila tukisema leo tufanye uchambuzi hakuna watu waliochangia kuiharibu hii nchi na kuifanya kuwa ya hovyo kama Viongozi wa Serikali za Mitaa na Wizara ya Ardhi.

Kipimo kikuu cha uharibifu wa Tanzania ni namna ilivyojengwa hovyo na inavyozidi kujengwa hovyo bila mpangilio wowote ule.

Sababu kuu zilizopelekea hii nchi yetu kujengwa hovyo kwa uchafu bila mpangilio ni Wizara ya Ardhi na watu wanaoitwa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Wizara ya Ardhi kama Wizara ambayo ina jukumu la kupima na kupanga maeneo yote nchi hii na kuhakikisha wananchi wote wa nchi hii wanaishi katika maeneo yaliyopimwa na kupangwa vizuri haifanyi hilo jukumu lake la msingi kisawasawa. Badala yale Wizara hii imekuwa ikihangaika kila aiku kushughulikia migogoro ya ardhi ambayo ukitizama kama una akili nzuri migogoro hiyo inasababishwa na tatizo kuu la wao kutotimiza wajibu wao wa kupima na kupanga maeneo ya nchi hii.

Tukija kwa Viongozi wa Serikali za mitaa hawa ndo mashetani wanaofanikisha matokeo ya ujinga unaofanywa na Wizara ya Ardhi.

Hawa kwa miaka mingi ndo wamekuwa wakisimamia uuzaji na ugawaji wa maeneo bila kuzingatia uwepo wa barabara, maeneo ya wazi, pamoja na maeneo ya shughuli za kibinadamu.

Maeneo yote yaliyojengwa hovyo nchini Tanzania katika mikoa mbalimbali wanaosimamia uuuzwaji na ukatwaji holela wa viwanja kwenye maeneo hayo bila kuwaelekeza na kuwasimamia wananchi vizuri katika kuacha barababra za kupita magari na vyombo vya moto ni Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Leo hii ukitembea mikoa ya Tanzania kama Mwanza, Arusha,Dar es Salaam, Mbeya, Manyara na kwingineko ni kama unapita katika jalala kwa namna makazi ya wananchi yalivyojengwa hovyo bila mpangilio.

Wizara ya Ardhi ambayo ingepaswa hata kutoa mwongozo wa ujengwaji wa nyumba na uuzwaji wa maeneo kwa Viongozi wa Serikali za Mitaa kutokana na kushindwa kusimamia ipasavyo zoezi la upimaji na upangwaji wa nchi hii nayo imeshindwa kutoa huo mwongozo na kupelekea nchi yetu hii leo hii kuwa kama takataka.

Mbaya zaidi huwezi badilisha chochote kwenye haya kwa njia ya uchaguzi maana hapa Tanzania uchaguzi umeshahodhiwa na kikundi cha watu wachache ambacho ndicho kinateua watu wanaofanya haya. Hawajali umemchagua nani ila wanachagua wenyewe mtu wanayemtaka wao na hao wanaowachagua ndo wanafanya haya.


Mungu ananiona. Nisije tu kuwa Rais wa Nchi hii ila kuna uwezekano nikija kuwa Rais nikawafunga watu wote waliowahi kuwa Viongozi wa Serikali za Mitaa na Wafanyakazi wa Wizara ya Ardhi bila kusahau waliowahi kuwa Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara ya Ardhi.

Lord denning

Qatar
 
Kweli kabisa, inasikitisha Sana jinsi miji yetu ilivyojengwa. Unajiuliza Kama tunashindwa kupangilia makazi yetu tutaweza nini Sasa?
 
Kwani ukiacha kushiriki utakuwa unamkomoa nani? Wewe ukikitoa, hayo mabadiliko unayotaka yatokee nani atayaleta? Waswahili wanasema, ukiona vinaelea, ujue vimeundwa. Ukitaka kuona mabadiliko, lazima ushiriki kuyaleta.
 
Mabadiliko wa kuyaleta niwe mimi? Na Katiba hii tuliyonayo inayokupa nafasi ya kupiga kura ila mshindi anaamuliwa na anayehesabu kura?
Kwani ukiacha kushiriki utakuwa unamkomoa nani? Wewe ukikitoa, hayo mabadiliko unayotaka yatokee nani atayaleta? Waswahili wanasema, ukiona vinaelea, ujue vimeundwa. Ukitaka kuona mabadiliko, lazima ushiriki kuyaleta.
 
Magufuli ni rais bora wa karne ya 21, nimeliona hili baada ya kutembelea SGR na bwawa la umeme
 
Andiko refu, lakini umezunguka zunguka tu mule mule na maneno mengi bila ya sababu!

Nchi inapo kuwa na mfumo tunao jidai sasa tunaukubali, bila ya kuwepo na taratibu za udhibiti maalum, matokeo yake ndiyo hayo unayo yaeleza wewe.
Na hapa umejikita kwenye sehemu moja tu; hujagusa kwingine kokote.

Na wala hujasema chochote kuhusu "kutoshiriki kwako katika chaguzi..."!
Je, kutoshiriki huko ndiko kutakako fanya maswala unayo lalamikia kuwa na nafuu?
 
Andiko refu, lakini umezunguka zunguka tu mule mule na maneno mengi bila ya sababu!

Nchi inapo kuwa na mfumo tunao jidai sasa tunaukubali, bila ya kuwepo na taratibu za udhibiti maalum, matokeo yake ndiyo hayo unayo yaeleza wewe.
Na hapa umejikita kwenye sehemu moja tu; hujagusa kwingine kokote.

Na wala hujasema chochote kuhusu "kutoshiriki kwako katika chaguzi..."!
Je, kutoshiriki huko ndiko kutakako fanya maswala unayo lalamikia kuwa na nafuu?
Kati ya mambo yanayonikera nchi hii la kwanza ndo hili ujenzi holela na makazi yasiyo na mpangilio.

Na kwa sababu hizo huku ukizingatia na Katiba hii tuliyonayo inayofanya tupigw kura ila wanaotuchagulia Viongozi ni watu wengine, bora niendelee kukaa hivi hivi bila kupiga kura na kushiriki uchaguzi wa aina yeyote ile.
 
Kila mtu na fikra zake kuna mwingine anafikiria akipata nafasi viongozi wote na wanachama wa CCM akina mwashambwa baadhi unawafirisi na kuwafunga wengine unawaua kabisa.
 
Ni ujinga kutojiandikisha kipiga kura.
Upige kura ambayo haiamui mshindi bali kikundi cha watu wachache ndo kikuamulie nani ashinde hapo kuna haja ya kupiga kura?

Alafu hao watu ndo wanafanya mambo ya kipuuzi namna hii
 
Mfano hai Nkuhungu broad acre Dodoma
Eneo lilikuwa limepangwa kwa ustadi Mkubwa sana
Mabadiliko yalitakiwa yafanywe kitaalam
Lakini kilichofanyika ni aibu ya aibu

Rushwa rushwa kutumia tume kibao za kuthibiti vibaka waliotengenezwa kisiasa kupitia wataalamu wezi wezi
 
Kati ya mambo yanayonikera nchi hii la kwanza ndo hili ujenzi holela na makazi yasiyo na mpangilio.

Na kwa sababu hizo huku ukizingatia na Katiba hii tuliyonayo inayofanya tupigw kura ila wanaotuchagulia Viongozi ni watu wengine, bora niendelee kukaa hivi hivi bila kupiga kura na kushiriki uchaguzi wa aina yeyote ile.
Utanisamehe kwa kusema haya nitakayosema hapa:
Uamzi wako huo, wa kususa kupiga kura ni kama "umeaga dunia"!

Kama wewe bado ni binaadam mwenye uhai ndani yake, kamwe huwezi kuachia maisha yako yaende ende tu na kuendeshwa endeshwa tu na watu wengine, bila ya wewe mwenyewe kujishughulisha katika maisha hayo.

Kususa ni kumwachia CCM aendeshe maisha yako bila ya usumbufu wowote. Wanaipenda sana hali hiyo huko CCM.

Kushiriki kwenye kupiga kura ni sehemu moja tu ya hatua za kutafuta njia za kuwaondoa CCM. Uharibifu wa hizo kura zinazo pigwa ni sababu muhimu ya wananchi kuchukua hatua nyinginezo kuwaadabisha wahalifu hawa.
Kama wewe unasubiri njia zingine za kuwaondoa CCM madarakani kwa nguvu, utaanzia wapi kama hutaki kutumia sababu na ushahidi ulio wazi kama uharibifu wa kura zinazo pigwa.

Ni wananchi wattakao iondoa CCM madarakani, na wananchi wenyewe ni pamoja na wewe.
 
Mkuu, ukiamka, tutakupa elimu ya haya mambo, wizara ardhi imegatua sana, ukiona uharibifu, basi wanafanya washkaji zako hapo mtaani
 
Angalia plani za zilizofanywa wakoloni vile miji ilivyo kuwa imenyooka hata vile vijiji walivyo kuwa wanaita trading centers ilikua na barabara za kutosha zimenyooka mpangilio wa soko na maduka na mitaro ya maji ikija mvua.
 
Utanisamehe kwa kusema haya nitakayosema hapa:
Uamzi wako huo, wa kususa kupiga kura ni kama "umeaga dunia"!

Kama wewe bado ni binaadam mwenye uhai ndani yake, kamwe huwezi kuachia maisha yako yaende ende tu na kuendeshwa endeshwa tu na watu wengine, bila ya wewe mwenyewe kujishughulisha katika maisha hayo.

Kususa ni kumwachia CCM aendeshe maisha yako bila ya usumbufu wowote. Wanaipenda sana hali hiyo huko CCM.

Kushiriki kwenye kupiga kura ni sehemu moja tu ya hatua za kutafuta njia za kuwaondoa CCM. Uharibifu wa hizo kura zinazo pigwa ni sababu muhimu ya wananchi kuchukua hatua nyinginezo kuwaadabisha wahalifu hawa.
Kama wewe unasubiri njia zingine za kuwaondoa CCM madarakani kwa nguvu, utaanzia wapi kama hutaki kutumia sababu na ushahidi ulio wazi kama uharibifu wa kura zinazo pigwa.

Ni wananchi wattakao iondoa CCM madarakani, na wananchi wenyewe ni pamoja na wewe.
CCM ana njia mbili tu za kuondoka Madarakani!
1. Maandamano yatakayoitishwa na Viongozi wa Dini.


2. Mapinduzi ya Kijeshi au siku TISS akiamua basi hawabebi tena kwenye sanduku la Kura.

Vinginevyo haya yote tunayoita uchaguzi ni maigizo ya mtu mweusi kwenye sanduku la kura!
 
Angalia plani za zilizofanywa wakoloni vile miji ilivyo kuwa imenyooka hata vile vijiji walivyo kuwa wanaita trading centers ilikua na barabara za kutosha zimenyooka mpangilio wa soko na maduka na mitaro ya maji ikija mvua.
Kwa kifupi mambo yalikoma kufanywa kiakili nchi hii pale tu mkoloni alipoondoka.

Saivi kuishi eneo lililopimwa na kupangwa imekuwa kama ni anasa au special privilege wakati ni suala linalopaswa kuwa la kawaida sana kwa binadamu wenye akili na upeo mzuri.
 
Back
Top Bottom