Sitosahau UKIMWI ulichofanya mtaani kwetu. Nyie watu wa mapenzi kuweni makini

Siku hizi ARV inasaidia sana , ule UKIMWI wa Sofia haupo tena. Wanakufa watu na vitambi vyao bila vipele wala kuharisha na maambukizi kwa watumia dawa ni kidogo sana.

Tatizo la HIV unaweza ukatulia wewe na kuwa makini sana lkn mwezi wako akakuletea ndani ya nyumba hasa mkioana Malaya na waongo waongo 😭😭😭
 
Huu ugonjwa haukuwa na mchezo na tumepoteza watu wengi sana, kwa sasa ni jambo la kushukuru mungu maana hizi ARV ukila vizuri na ukajiangalia vizuri kiafya unaweza kusihi maisha ya kawaida kabisa mpaka ukawa mzee bila matatizo, sio death sentence kama miaka ile, kwa sasa mambo ya pressure, kisukari, cancer ni hatari kuliko hata ukimwi, binadamu hatuko salama tunashambuliwa kila kona
 
Familia ilihamia kikazi mji ule kumbe tulienda mazikoni, kuweni makini na Mafinga wafanyakazi mnaoenda hapo, bahati yenu kumetulia ila miaka ile asee hapana.
Asante kwa ushauri mujarabu mkuu. BTW kumbuka unaweza kuvaa kondomu ukafa lakini ukapiga kavu uka survive. Kuvaa kondomu sio guarantee ya kutoambukizwa.
 
Katika kitu namshukuru Mungu nlikuwa well grounded kwenye elimu ya jinsia na mahusiano! Kulikuwa na programs nyingi zilikuwa funded na wajapan kupitia world vision Tanzania, mwaka 2009 nkiwa darasa la tatu nlishapelekwa kwenye semina tunaandaa ngonjera na Kazi mbali mbali Sanaa ambapo tar December 1 ndo inakuaga maadhimisho yake.

Pia tulikua tunaenda semina za wiki Moja au mbili kuhus mambo ya watoto na tar 16/6 tulikua tunashiriki maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika.

Haya yote yalitamatika nlipomaliza elimu ya msingi 2013 though vilinijenga Sana kua na fikra pana
 
Nimejikuta nakuonea huruma sana mkuu.Kitendo cha mkeo kuwa na trip daily ina leta confussion sana.Mara nying hata stability ya family huwa inakua at jeopardy sana

Nafikiria nimwambie kazi na ndoa/watoto ipi bora?
Haiwezekani kwa mwezi tunaonana kwa siku 7 tu imefikia hatua watoto wamemzoea dada wa kazi
 
Sasa niukwae mara ngapi jamani sixteen years and counting hamna arv wala nini siri ni mazoezi chakula na kitokuoa maana ukiwa na mke unaongeza uharaka wa kulifikia kaburi lako [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] oh plus maji kwa wingi pia
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Dah so sad kuna jamaa yetu hapa mtaani juzi aliamua kujinyonga kisa ana Ukimwi😭.
Ni ugonjwa hatari sana unahitaji maombi na umakini wa hali ya juu kuuepuka... Ukishaupata unapoteza ramani ya maisha kabisa...... Inauma na isikitisha ni gonjwa linalogusa kila familia kwa sasa.

Rip my beloved bro!.
 
Mkuu huo ugonjwa kwa % kubwa huletwa na married couple hususani wanawake wenye tamaa ya pesa na ngono za nje kwa kisingizio cha kulizishwa, pia mchunge mkeo ukiona dalili zozote za kuchepuka usimsamehe achana nae immediately.
Hiyo iko wazi kama ya mbuzi, nishamwambia nikikudaka ni no sorry
 
Hapa ndo mwengi hawana uelewa wa Nini maana ya HIV. Huu si ugonjwa ni upungufu wa Kinga hivyo magonjwa yote yatakufata Kinga ikipungua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…