Sitosahau UKIMWI ulichofanya mtaani kwetu. Nyie watu wa mapenzi kuweni makini

Sitosahau UKIMWI ulichofanya mtaani kwetu. Nyie watu wa mapenzi kuweni makini

Ku
Tembea uone Ndugu yangu...kuna sehemu nilifika nikakabidhiwa nyumba full kwa sh. 3000.....nikae kwa miezi mitatu...hiyo elfu tatu nilimpa balozi alienionyesha hiyo nyumba niishi....vijijini hizo nyumba ni nyingi sana tu...
Kuna kipindi tulienda kupiga kazi Songwe kwenye mgodi wa SHANTA gold mining
Tulipokuwa tunaelekea kuna kijiji tulipita makaburi yalikuwa ni mengi sana tukawauliza wenyeji kulikoni hapa.,.,

Wenyeji wakatuambia msiguse huku kuna moto atar.,... Na makaburi yote hayo mnayoyaona wengi wao ni umeme umewondoa kwa hyo kuweni makini...
 
Upande wa mama walizaliwa kumi.Wakike 6,wakiume wanne.wajomba wote wako hai
Ila huu ugonjwa ukawabeba
Mama×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Baba nae akaenda wakatuacha wadogo sn.Huu ugonjwa hadi leo umetuathiri sn kisaikolojia.ila MUNGU ni mwema tunapambana
Polen sana ndugu
 
Naandika uzi huu huku nikiwakumbuka wengi waliokufa na gonjwa la hatari la UKIMWI kule kwetu Iringa Mafinga kwenye misitu mbao mji wa biashara mji wenye viwanda vidogo vidogo vingi vya mbao mji wa majani ya Chaibora.

Mimi nilizaliwa mwaka 1990 DSM, baadae mwaka 1995 tukahamia mafinga mjini kikazi Mafinga ikiwa bado changa sana, mwaka 1997 nikiwa na miaka saba ndo nilipoanza kusikia hii term UKIMWI.

Mama yangu alikuwa anafanya kazi hospital ya Mafinga kama nurse pale sasa mara nyingi alikuwa anakuja na viperurushi navisoma nashangaa UKIMWI ni nini.

Jamani huu ugonjwa kama hujaoana mgonjwa UKIMWI anavyokufa huwezi elewa pia utaendelea kupiga kavu, lazima ushuhudie kama week mgonjwa kabla haja kata roho ndo utajua why HIV is king of all diseases hakuna kama HIV maana linaalika magonjwa yote. HIV/AIDS NI MFALME WA MAGONJWA sio utani.

Nisipoteze muda kifo cha kwanza nilihushudia jirani yetu alikuwa mwalimu alianza mume alikonda mwaka 1997, maskini afu walikuwa na watoto mapacha waliachwa bila wazazi asee jamaa alikonda kiasi hata mimi mtoto mdogo enzi hizo niliogopa na watu walikuwa hawataki kumgusa kabisa.

Kifo cha pili ba mkubwa wangu huyo yeye hakuchukua hata round alikuwa mlevi na UKIMIW wa enzi hizo ni miezi mitatu tunazika.

Haya sasa baada hapo tukahama mtaa tukamia mtaa mpya mtaa wa mikosi mkosi mkubwa hadi naandika uzi kwa uchungu mkubwa ni tulihamia ule mtaa mwaka 2003 hadi ninavyoongea 80% ya ule mtaa wamekufa na AIDS ule mtaa jamani wafanya wa Serikali walijenga sana nyumba maana serikali ilipima na kuwaanzia kwa bei nzuri wafanyakazi wengi wakahamia huko na kujenga majumba kumbe wamehamia mtaa mtoa roho mtaa na majanga yake.

Tulianza jirani mwanajeshi huyo tunafika akavuta ila mke wake hadi leo yupo anakula ARV, kanali yule tulizika tukiwa tumehamia ule mtaa week tu.

Upande mwingine alikuwa ni hakimu yule aliishi ishi akaja na kuvuta mama wa watu alikuwa na roho nzuri nahisi sijui nae UKIMWI alitoa wapi.

Kule idara ya maji dada mmoja mchaga alikuwa mtaani kwetu nae hivi she was beautiful japo nilikuwa mdogo huyo alikufa hata mtoto hakuacha alicha nyumba tu.

Kuna jirani yetu yeye pamoja na mke wameeacha mtoto wao mvuta bangi nao hivi huyu alikuwa fundi wa magari alijenga bonge la jumba mke alikuwa mzuri sana.

Pia upande wa juu kwa mbele mwanajeshi mmoja yeye na mke walikuwaga na baa walipishana tu miaka ule mtaa jamani sina hamu HIV iliwapiga fasta ikaacha watoto wakijilea.

Kuna mwamba pia pale kitaa alikuwa usalama wa taifa yeye ndo alikufa yeye na mdogo wake, huyo ni hivi mdogo wake alikula mke wa kaka yake nae akapata kaka yake anavyokufa akamwambia kama uliniabia mke wangu tutaonana very soon walikuwa wote watatu na mke juu wakaacha nyumba na katoto kachanga sijui kako wapi.

Haya dada mmoja mzuri sana alikuwa alijenga kijumba chake kipya kabisa akifanya kazi halmashauri nae kufika tu mafinga uzuri ulimponza tukazika akapenda hela za mpasua mbao mmoja tajiri miaka hiyo sijui yuko wapi alikuwa mweupe handsome alikuwa akiindesha shangingi miaka hiyo.

Wadau mtaaa ni mkubwa mno ule 80% ya zile nyumba zimejengwa wajenzi wake HIV iliwabeba.

Kila siku tukawa tunazika majirani tukijua kwetu salama 2012 babangu nae sijui alitoa wapi ila nilifuatialia nasikia alipata miaka ya 90 nae tukazika, sikuwa na mahusiano mazuri na dingi hivyo hata msiba niliona normal tu nikamuuliza maza akasema si unajua mimi na baba ako tuliachana mmi mzima.

Basi miaka ikaenda hadi mwaka 2018 nilikuwa nimetoka zangu China nikaenda Iringa kumpa hi maza, mara kuingia chumbani nakuta ARV kasahau kitandani asee nililia sana nikamuuliza akaniambia samahani niliwaficha wanangu nikambatia kwa uchungu mkubwa sana siku kesho yake nikarudi Dar nikisema why why mama angu nurse nae anaondoka.

2020 akaanza kuumwa kumbe nae aliishia nao kimya kimya toka miaka 2000 mwanzoni, 2021 kuiukweli HIV/AIDS hapa ilionesha uwezo wake ilimua mama yangu kikatili mno siwezi simulia.

Basi wadau nasema kutoka moyo ule mtaa wetu 80% nyumba zimebaki za urithi tu siwezi taja mtaa ila una jina la herufi tu, kama uko mafinga utakuwa umeshaujua ni kwa kishua sana.

Research niliyofanya why UKIMWI uliua sana mafinga ni padogo pia na walio kufa sana ni wafanyakazi serikali ilikuwa ikileta wafanyakazi miaka ile ya 90 wanaambukizana sana bila kujua so wafanyakazi wengi mafinga miaka 90 kuna 2000 mwanzoni walikufa na HIV wengi ni wageni kutoka mikoa mingine including my mom.

Kuna makaburi yanaitwa MET 50% half ya marehemu pale watu wa UKIMWI wa miaka 90.

RIP To those beautiful souls, nimesimulia machache sana kuhusu mafinga na HIV, ni mengi mno nimeacha na niliyoshuhudia toka 1996.

Nilihama sijawahi kanyaga tena hata nyumba tuliuza kwa hasira maana majirani wote wamekufa now naishi Dar kama business man.

Huwa sipigi demu bila kupima pia mtumiaji mzuri wa condom.

Uzi wa leo asubuhi asanteni ila Mafinga never forget japo napapenda sana. Familia ilihamia kikazi mji ule kumbe tulienda mazikoni, kuweni makini na Mafinga wafanyakazi mnaoenda hapo, bahati yenu kumetulia ila miaka ile asee hapana.
HIV sio ugonjwa.
Halafu UKIMWI wa old model ulikuwa hatari ule kwa sababu ya kutokuwepo kwa dawa za kupunguza makali ya virusi. Nowdays kuna TLD, kuwatambua ni ngumu
 
Nimekaa mufindi 15 yrs niliondoka kule 2012! Napajua vizuri sana..sema basi haturuhusiwi kuweka majina huyo mamdogo wako huenda ningemfahamu.! I love the Nature kule, baridi balaaa, Napamisi Mufindi Club e.t.c..kule nilikataa kurudi tena maana HIV ipo kwa kiwango kikubwa sana
HIV kule unapishana nayo kama binadamu
 
Upande wa mama walizaliwa kumi.Wakike 6,wakiume wanne.wajomba wote wako hai
Ila huu ugonjwa ukawabeba
Mama×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Mama mdogo×
Baba nae akaenda wakatuacha wadogo sn.Huu ugonjwa hadi leo umetuathiri sn kisaikolojia.ila MUNGU ni mwema tunapambana
Pole sana mkuu.
 
Katika harakati zangu za kutafuta maisha, kuna siku nilikuwa SONGEA, nikafika mida ya jioni kama saa 12 hivi, nikachukua chumba lodge iliyokaribu na stendi.

Nikiwa room naweka vitu vyangu sawa ili nitoke, nikaona mfuko wa watsani ukiwa na vitu ndani umefungwa na kuwekwa kwenye uwazi uliopo baina ya kitanda na ukuta.

Nikauchukua nikaufungu, ndani nikakuta kikopo kidogo chenye vidonge nadhani vilikuwa kama vya kijivu hivi vikubwa kubwa kidogo. Pia nikakuta na karatasi inayoonesha muhusika alikuwa anahama hospitali ya kuchukulia ARV iliyopo DSM na kuanza kuchukulia dawa hospitali iliyopo songea. Nikakuta na night dress na hela kidgo kama 8000 hivi. Nikarudisha vile vitu halafu nikaufunga na kuweka pembeni nikiazimia nikitoka nikaupeleke mapokezi.

Baada ya dakika kadhaa mlango wangu ukagongwa niliposema karibu tu akaingia mdada moja kwa moja...dada alikuwa mzuri maashallah kajistiri vizuri na baibui pamoja na mtandio saafi. Akaenda moja kwa moja kwenye ukingo wa kitanda, nikamuona kashtuka baada ya kuona furushi lake halipo. Nikamwambia mzigo wako huu hapa chini ya meza nilipanga nikauwasilishe mapokezi. Akashukuru shukuru pale then akaondoka.

Nilipotoka mapokezi nikaulizia ilikuwaje mkanipa chumba ambacho mtu bado yupo? Wakasema HAPANA huyo dada alikuja na mtu wake wakalipia showtime na alipotoka tukakiweka sawa chumba. Nikauliza mnamjua yule dada? Wakasema eenh tunamjua vipi broo ulikuwa unamtaka uvushe nae usiku, ana bei nzuri tu....nikasema daaah WASHENZI HAWA WANANIDALALIA UKIMWI.

ANYWAY watu wameungua ndugu zangu, wameungua haswaaaa, TUENDELEE KUJILINDA.
 
Ni kweli ugonjwa anapanga mungu ila najitahidi kutembea na oral quick ili nimpime kabla ya game kwasababu kuna siku nilitaka kuyatimba.
 
Naandika uzi huu huku nikiwakumbuka wengi waliokufa na gonjwa la hatari la UKIMWI kule kwetu Iringa Mafinga kwenye misitu mbao mji wa biashara mji wenye viwanda vidogo vidogo vingi vya mbao mji wa majani ya Chaibora.

Mimi nilizaliwa mwaka 1990 DSM, baadae mwaka 1995 tukahamia mafinga mjini kikazi Mafinga ikiwa bado changa sana, mwaka 1997 nikiwa na miaka saba ndo nilipoanza kusikia hii term UKIMWI.

Mama yangu alikuwa anafanya kazi hospital ya Mafinga kama nurse pale sasa mara nyingi alikuwa anakuja na viperurushi navisoma nashangaa UKIMWI ni nini.

Jamani huu ugonjwa kama hujaoana mgonjwa UKIMWI anavyokufa huwezi elewa pia utaendelea kupiga kavu, lazima ushuhudie kama week mgonjwa kabla haja kata roho ndo utajua why HIV is king of all diseases hakuna kama HIV maana linaalika magonjwa yote. HIV/AIDS NI MFALME WA MAGONJWA sio utani.

Nisipoteze muda kifo cha kwanza nilihushudia jirani yetu alikuwa mwalimu alianza mume alikonda mwaka 1997, maskini afu walikuwa na watoto mapacha waliachwa bila wazazi asee jamaa alikonda kiasi hata mimi mtoto mdogo enzi hizo niliogopa na watu walikuwa hawataki kumgusa kabisa.

Kifo cha pili ba mkubwa wangu huyo yeye hakuchukua hata round alikuwa mlevi na UKIMIW wa enzi hizo ni miezi mitatu tunazika.

Haya sasa baada hapo tukahama mtaa tukamia mtaa mpya mtaa wa mikosi mkosi mkubwa hadi naandika uzi kwa uchungu mkubwa ni tulihamia ule mtaa mwaka 2003 hadi ninavyoongea 80% ya ule mtaa wamekufa na AIDS ule mtaa jamani wafanya wa Serikali walijenga sana nyumba maana serikali ilipima na kuwaanzia kwa bei nzuri wafanyakazi wengi wakahamia huko na kujenga majumba kumbe wamehamia mtaa mtoa roho mtaa na majanga yake.

Tulianza jirani mwanajeshi huyo tunafika akavuta ila mke wake hadi leo yupo anakula ARV, kanali yule tulizika tukiwa tumehamia ule mtaa week tu.

Upande mwingine alikuwa ni hakimu yule aliishi ishi akaja na kuvuta mama wa watu alikuwa na roho nzuri nahisi sijui nae UKIMWI alitoa wapi.

Kule idara ya maji dada mmoja mchaga alikuwa mtaani kwetu nae hivi she was beautiful japo nilikuwa mdogo huyo alikufa hata mtoto hakuacha alicha nyumba tu.

Kuna jirani yetu yeye pamoja na mke wameeacha mtoto wao mvuta bangi nao hivi huyu alikuwa fundi wa magari alijenga bonge la jumba mke alikuwa mzuri sana.

Pia upande wa juu kwa mbele mwanajeshi mmoja yeye na mke walikuwaga na baa walipishana tu miaka ule mtaa jamani sina hamu HIV iliwapiga fasta ikaacha watoto wakijilea.

Kuna mwamba pia pale kitaa alikuwa usalama wa taifa yeye ndo alikufa yeye na mdogo wake, huyo ni hivi mdogo wake alikula mke wa kaka yake nae akapata kaka yake anavyokufa akamwambia kama uliniabia mke wangu tutaonana very soon walikuwa wote watatu na mke juu wakaacha nyumba na katoto kachanga sijui kako wapi.

Haya dada mmoja mzuri sana alikuwa alijenga kijumba chake kipya kabisa akifanya kazi halmashauri nae kufika tu mafinga uzuri ulimponza tukazika akapenda hela za mpasua mbao mmoja tajiri miaka hiyo sijui yuko wapi alikuwa mweupe handsome alikuwa akiindesha shangingi miaka hiyo.

Wadau mtaaa ni mkubwa mno ule 80% ya zile nyumba zimejengwa wajenzi wake HIV iliwabeba.

Kila siku tukawa tunazika majirani tukijua kwetu salama 2012 babangu nae sijui alitoa wapi ila nilifuatialia nasikia alipata miaka ya 90 nae tukazika, sikuwa na mahusiano mazuri na dingi hivyo hata msiba niliona normal tu nikamuuliza maza akasema si unajua mimi na baba ako tuliachana mmi mzima.

Basi miaka ikaenda hadi mwaka 2018 nilikuwa nimetoka zangu China nikaenda Iringa kumpa hi maza, mara kuingia chumbani nakuta ARV kasahau kitandani asee nililia sana nikamuuliza akaniambia samahani niliwaficha wanangu nikambatia kwa uchungu mkubwa sana siku kesho yake nikarudi Dar nikisema why why mama angu nurse nae anaondoka.

2020 akaanza kuumwa kumbe nae aliishia nao kimya kimya toka miaka 2000 mwanzoni, 2021 kuiukweli HIV/AIDS hapa ilionesha uwezo wake ilimua mama yangu kikatili mno siwezi simulia.

Basi wadau nasema kutoka moyo ule mtaa wetu 80% nyumba zimebaki za urithi tu siwezi taja mtaa ila una jina la herufi tu, kama uko mafinga utakuwa umeshaujua ni kwa kishua sana.

Research niliyofanya why UKIMWI uliua sana mafinga ni padogo pia na walio kufa sana ni wafanyakazi serikali ilikuwa ikileta wafanyakazi miaka ile ya 90 wanaambukizana sana bila kujua so wafanyakazi wengi mafinga miaka 90 kuna 2000 mwanzoni walikufa na HIV wengi ni wageni kutoka mikoa mingine including my mom.

Kuna makaburi yanaitwa MET 50% half ya marehemu pale watu wa UKIMWI wa miaka 90.

RIP To those beautiful souls, nimesimulia machache sana kuhusu mafinga na HIV, ni mengi mno nimeacha na niliyoshuhudia toka 1996.

Nilihama sijawahi kanyaga tena hata nyumba tuliuza kwa hasira maana majirani wote wamekufa now naishi Dar kama business man.

Huwa sipigi demu bila kupima pia mtumiaji mzuri wa condom.

Uzi wa leo asubuhi asanteni ila Mafinga never forget japo napapenda sana. Familia ilihamia kikazi mji ule kumbe tulienda mazikoni, kuweni makini na Mafinga wafanyakazi mnaoenda hapo, bahati yenu kumetulia ila miaka ile asee hapana.
Mafinga kuzuri mkuu, mambo mengine ni hivo kama ilivo asee...
 
Sema huu uzi unaogopesha saana, ila AFYA inapaswa kulindwa kwa namna yoyote ile. UKIMWI upo na unaua. Cha kushangaza siku hizi kampeni za kuelimisha kuhusu huu ugonjwa zimepotelea kusiko julikana
 
Sema huu uzi unaogopesha saana, ila inapaswa kulindwa kwa namna yoyote ile. UKIMWI upo na unaua. Cha kushangaza siku hizi kampeni za kuelimisha kuhusu huu ugonjwa zimepotelea kusiko julikana
saivi hakufi mtu maana kuna dawa unameza unakaa sawa unanenepa na kupendeza kabisa hadi hauwezi kumjua mwenye nao
 
Shida kwenye ndoa, wanaume sio waaaminifu kabisa wakiona Msichana ametulia hawakumbuki kabisa kondomu
Wee nani alikudanganya wanandoa wakicheat wanatumia condom 🤣🤣🤣🤣
Kataa ndoa kama wapenda afya yako. Msituone sie wajinga hatutaki kuoa mnasema vijana wa hovyo 🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom