Skendo gani imewahi kukuandama ukahisi kuchanganyikiwa? Uliimalizaje?

Skendo gani imewahi kukuandama ukahisi kuchanganyikiwa? Uliimalizaje?

hiii Dunia hii kila unachokifanya hua Kuna mtu anakuona aiseee Kuna mtu alinitaja yaan alisimulia kila nlichofanya pale nlianza na nn nikamaliza na nn nlihojiwa nikagoma sio mm lkn nlikuwa mm....nlipitisha miaka miwili Kuna maeneo siendi mwenyw
Duniani huwezi fanya jambo kwa siri aisee
 
Natamani kueleza ila roho inasita mtanijua ila itoshe kusema wafanyakazi wa Temeke hospitali Mungu anawaona na katu siachi kuwaombea mabaya maana mlijua kunidhalilisha kijana wenu alafu nikiwa ndiyo kwanza naanza ajira .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Mbona yako inaonekana ya kusisimua mkuu... tupe story ilikuaje kuaje 😃😃
 
Skendo nyingi huwa ni za kutengenezwa na watu ili kukuchafua na kuonekana kwenye jamii kuwa wewe ni mtu wa ovyo sana

Skendo ambayo staisahau kwenye maisha yangu nilipozushiwa kuwa nina mahusiano ya kimapenzi na mwanaume shoga, na nikaambiwa na tarehe na sehemu tulipofanyia hicho kitendo,iliniuma sana nikajificha ndani haikusaidia,nikazima simu haikusaidia ..

Ili skendo iishe niliamua kukaa kwa watu walipo na kila aliyekuwa ananiuliza nilikubali yaishe, ila iliniuma sana

Je wewe mwenzangu umewahi kushushiwa skendo gani na uliikabilije kwenye jamii?
Naona umegeuza story inaonesha uliliwa wewe
 
Nakumbuka wakati niko shule nilizushiwaga nadate na mwalimu wa physics ile skendo ilinitesaga sana nilifikia hatua hadi nikawa najifelisha makusudi maana nilikua nikifaulu tu watu wanasema nimevujishiwa paper,, toka nimeenda shule msosi wa shule nilikua sili ila ikafikia hatua ilibidi nianze kula tu hatakama situmii malage na sipendi kande maana ilikua nikinunua hata chips wanasema hela nimehongwa na mwalimu, nilikuaga kiongozi lakini ikabidi nijihudhuru tu maana ilikua nikisimama assembly hata kutangaza naona kama shule nzima inanizomea🤦‍♀️🤦‍♀️...iliniumiza na kunitesa sana kisaikolojia ukizingatia na mwalimu mwenyewe alikua mkali hata kuanza kumuuliza naogopa naanzia wapi,, nilimwomba mzee anihamishe shule alikataa hadi nikatamani nitoroke😂😂😂.. Nilikuja kujifunza baadae sana kwamba inabidi uishi tu maisha ya kawaida ambayo almost kila mtu anaishi maana ukijiweka tofauti tu watu wanaanza kufanya assumptions za kipuuzi
Na ndo Mana uko jf Bila shaka wewe Ni single mom
 
Mimi miaka ya 90 kuna msichana nilimpenda mtaani lakini kutokana na utoto nikashindwa kumwambia nikawa nampa pesa tu, siku moja nilimpa pesa shilingi ishirini , kumbe kuna mtu aliniona akaenda kuwaambia wazazi wake yule binti.
Wazazi wake wakorofi wakanijazia watu mtaani wakanitukana sana kwamba namtom** binti yao.
Mwishoni wakasema huyu mtoto ni popobawa kabisa kabisa hafai.
Ikumbukwe miaka ile ya tisini ndio ile kadhia ya popo bawa ilikuwa imepamba moto.
Kuanzia hapo nikawa naitwa jina la popobawa.
Kwakweli nilikuwa naumia na kusononeka sana.

Sasa si ungempopobawa tu uyo manzi ili uzushi uwe kweli
 
Nilisingiziwa eti nimefumaniwa na mke wa mtu mtaa wa pili!
Kumbe hata sio Mimi ni mtu mwingine majina tu yanafafa, nilijitetea lakini wapi, hiii ishu iliniharibia sana hadi kazini
 
Nakumbuka wakati niko shule nilizushiwaga nadate na mwalimu wa physics ile skendo ilinitesaga sana nilifikia hatua hadi nikawa najifelisha makusudi maana nilikua nikifaulu tu watu wanasema nimevujishiwa paper,, toka nimeenda shule msosi wa shule nilikua sili ila ikafikia hatua ilibidi nianze kula tu hatakama situmii malage na sipendi kande maana ilikua nikinunua hata chips wanasema hela nimehongwa na mwalimu, nilikuaga kiongozi lakini ikabidi nijiudhuru tu maana ilikua nikisimama assembly hata kutangaza naona kama shule nzima inanizomea[emoji2356][emoji2356]...iliniumiza na kunitesa sana kisaikolojia ukizingatia na mwalimu mwenyewe alikua mkali hata kuanza kumuuliza naogopa naanzia wapi,, nilimwomba mzee anihamishe shule alikataa hadi nikatamani nitoroke[emoji23][emoji23][emoji23].. Nilikuja kujifunza baadae sana kwamba inabidi uishi tu maisha ya kawaida ambayo almost kila mtu anaishi maana ukijiweka tofauti tu watu wanaanza kufanya assumptions za kipuuzi
Poleee sana.
 
Back
Top Bottom