Soko la Hisa la Dar es Salaam na orodha ya makampuni yaliyosajiliwa

Soko la Hisa la Dar es Salaam na orodha ya makampuni yaliyosajiliwa

Sure mkuu Co. Ikipata hasara na wewe unapata hasara, shareholders ikitokea Co. Imefilisika wao hua wa mwisho kulipwa kwenye kile kinachobakia baada ya wengine kua wamelipwa!! Jinsi ya kujua faida kuna namna mbili kupitia dividend/gawiwo na capital gain sijui kiswahili tunaiitaje! Faida kupitia gawiwo unalipata pale kwa mfano unamiliki hisa 5000 then Co. Ikatangaza kwenye kila hisa 1 utapata gawiwo la sh.100 then hapo utapata faida ya(5000×100)= sh.500,000# mkuu na Capital gain ni pale kwa mfano ulinunua kila hisa 1 kwa sh.500 na unahisa 5000 then ulitumia(500×5000)= sh.2,500,000 kama mtaji wako so ikitokea leo ukauza hisa zako na kila hisa ukauza kwa sh.1000 manake itakua ni 1000×5000(idadI ya hisa unazomiliki)=5,000,000 then faida yako hapo ni ile pesa uliyopata kipind umeuza hisa zako 5,000,000 kutoa pesa ulizonunulia hisa zako 2,500,000=2,500 000 pole kwa maelezo marefu mkuu wangu!!

kaka asante nimekuelewa, wiki ijayo nitaanza mchakato, nina kama laki tano hivi inatosha kuanzia, nitamuwekea mwanangu
 
mm mwenyewe nataka kujiingiza katika hisa hivyo nashukuru kwa mwangaza huu uliotoa hapa umenifumbua macho
asante sana ngoja niende kujiunga ila sijajua niingie kampuni gani?
 
Naomba kujua. Hii biashara inawezekana kufanyika online yaani bila kutembea physically kwa broker au dealer au DSE? Namaanisha kuifanya popote ulipo na kupata taarifa za kupanda na kushuka (fluctuations) kwa hisa za kampuni tofauti?
online bado haijaanza kwa ninavyofahamu , ila ni rahisi tu kununua kwa njia ya kawaida unless uwe nje ya nchi au nje ya dar
 
je kama kampuni ikipata hasara na mimi napata hasara?
na kwa mfano nikitaka kujua faida nafanyaje?
kujua faida unaweza kuwa unasoma ripoti zao za mahesabu ambazo unaweza zipata kwenye website ya dse.co.tz.

Pia wakitoa gawio wanaweza kukupa kupitia benki au sanduku la posta inakuja karatasi ikionyesha gawio utakalopata kwa kila hisa.

Ila kama kampuni inapata hasara hutapata gawio lakini ikiendelea pata hasara kwa muda mrefu au dalili za kupata hasara ni bora ukauza hisa mapema maana itaathiri thamani/bei ya hisa
 
kaka asante nimekuelewa,,wiki ijayo nitaanza mchakato,,nina kama laki tano hivi inatosha kuanzia,nitamuwekea mwanangu
kama unataka nunua ni bora ukaanza fuatilia soko mapema na pia brokers wanaweza kukushauri kampuni ipi ni nzuri. Maana kuna makampuni miaka yote haina gawio wala bei ya hisa haipandi
 
nakubaliana nawewe najua kwa asilimia mia, nilinunua hisa za swiss mwezi wa pili mwaka huu kwa sh 5600 lakini leo ni 6600. Wiki ijayo naenda kuuza hisa zangu zote za DCB, CRDB na NMB then nahamia SWISS mzima mzima
 
Last edited by a moderator:
mm mwenyewe nataka kujiingiza katika hisa hivyo nashukuru kwa mwangaza huu uliotoa hapa umenifumbua macho
asante sana ngoja niende kujiunga ila sijajua niingie kampuni gani?
nenda kanunue za swiss port ni bei nafuu na zinapanda kwa kasi nzuri january bei ya hisa ilikuwa 5100 leo zaidi ya 6000 na inapanda karibu kila siku
 
nenda kanunue za swiss port ni bei nafuu na zinapanda kwa kasi nzuri january bei ya hisa ilikuwa 5100 leo zaidi ya 6000 na inapanda karibu kila siku

Na 'kiwango cha chini' cha hisa unazoweza kununua kwa kampuni ya Cargo ya Swiss port ni hisa ngapi mkuu?
 
Na 'kiwango cha chini' cha hisa unazoweza kununua kwa kampuni ya Cargo ya Swiss port ni hisa ngapi mkuu?
sijajua kiwango cha chini angalau nunua hisa kuanzia 100 na kuendelea ili uje pata faida katika gawia na thamani ya hisa.

Mara ya mwisho gawio lilikuwa karibu shilingi mia kwa kila hisa, sasa kama una hisa mia hapo gawio lako litaku 10,000. Nunua nyingi kadiri uwezavyo
 
nakubaliana nawewe najua kwa asilimia mia, nilinunua hisa za swiss mwezi wa pili mwaka huu kwa sh 5600 lakini leo ni 6600. Wiki ijayo naenda kuuza hisa zangu zote za DCB, CRDB na NMB then nahamia SWISS mzima mzima
swiss kuzuri sana nilinunua wakati hisa moja ni shillingi 600, nilikuwa na plan niziuze april ila nimegairi labda november
 
Last edited by a moderator:
mkuu umenifanya nipende mno hiki kitu lakin unaweza tusaidia kujua huo mgawanyo wa faida huwa unakuaje
 
Kampuni ikishafanya biashara ikapata faida ,hiyo hela huwa ni ya wamiliki wa kampuni sasa wewe kwakuwa ni mmiliki kwa kununua hisa utabidi na wewe upate gawio.

Kampuni wakipiga hesabu wanaweza tangaza kiasi gani wamepata kwenye financial statement na gawio litakuwa kiasi gani. Haina haja ya kwenda in detail sana kama hujaamua kuwa active na soko. Kuna watu hufanya biashara wao wanatafuta taarifa tu kama kampuni inabiashara nzuri wananunua hisa mapema kwa bei ya chini wakipata gawio lao wanauza wakati huo bei ya hisa inakuwa imepanda tayari kisha anatafuta kampuni nyingine ya kununua .

Hapo kazi yake inakuwa kununua na kuuza ili apate faida. Watu kama hao ndio huwa wanafuatilia kwa makini financial reports
 
najua nimesikia CWT na wao wanaingia katika soko la Hisa wanataka kuanzisha bank,tangazo lao walisema Leo tarehe 23 mpaka 29 march,je unanishaurije niingie au
 
Last edited by a moderator:
najua nimesikia CWT na wao wanaingia katika soko la Hisa wanataka kuanzisha bank,tangazo lao walisema Leo tarehe 23 mpaka 29 march,je unanishaurije niingie au
thamani ya hisa za mabenki ukuaji wake
ni mdogo, bank kama CRDB mpaka leo hisa moja ni mia nne. Unaweza nunua ila faida itakuwa kidogo kidogo
 
Last edited by a moderator:
Kampuni ikishafanya biashara ikapata faida ,hiyo hela huwa ni ya wamiliki wa kampuni sasa wewe kwakuwa ni mmiliki kwa kununua hisa utabidi na wewe upate gawio. Kampuni wakipiga hesabu wanaweza tangaza kiasi gani wamepata kwenye financial statement na gawio litakuwa kiasi gani. Haina haja ya kwenda in detail sana kama hujaamua kuwa active na soko. Kuna watu hufanya biashara wao wanatafuta taarifa tu kama kampuni inabiashara nzuri wananunua hisa mapema kwa bei ya chini wakipata gawio lao wanauza wakati huo bei ya hisa inakuwa imepanda tayari kisha anatafuta kampuni nyingine ya kununua . Hapo kazi yake inakuwa kununua na kuuza ili apate faida. Watu kama hao ndio huwa wanafuatilia kwa makini financial reports

Ni muhimu kukumbuka kuwa GAWIO SIO LAZIMA HATA KAMPUNI IKIPATA FAIDA! gawio linaamuliwa na Board of Directors wa kampuni wanaweza kuamua kutogawa gawio lolote hata kama faida imepatikana, badala yake wanaweza kuirudisha faida kwenye kampuni kwa matumizi mengine.

Ila kampuni ikishaweka utamaduni wa kugawa dividends ni vigumu kurudi nyuma maana wanahisa wengi utakuta wanategemea kupata gawio hivyo wasipopata hisa inaweza kuporomoka.
 
Mkuu kama nataka kuinvest automatically nafanyeje kwa maana kwamba once nimeshakuwa na account naspecify amount ya kuinvest kila mwezi kutoka kwenye akaunti yangu? Kuna index trackers zozote kwa bongo? Nimesoma mahali faida ya index tracker ni kwamba kuna diversification ya investments kwa hiyo inapunguza risk sababu portfolio ni pana.

Najua kuna UTT lakinidisadvantage ya UTT ni kwamba fees lazima ziwe juu sababu ni managed fund. Je fees kwa UTT ni asilimia ngapi? Maana naona tu wana emphasize watu wainvest lakini huwa hawaongei kuhusu fees na huo huwa ni mtego unatakiwa uupuke. Maan kama fees ni kubwa ina maana zita affect reurn yako after taxes.

Natamani nione kitu kama NASDAQ na vinginevyo.
 
Naomba kujua. Hii biashara inawezekana kufanyika online yaani bila kutembea physically kwa broker au dealer au DSE? Namaanisha kuifanya popote ulipo na kupata taarifa za kupanda na kushuka (fluctuations) kwa hisa za kampuni tofauti?

Mkuu,

Taarifa juu ya bei za hisa, makampuni yaliyo sokoni n.k. unaweza kuzipata Welcome to Dar es Salaam Stock Exchange | Dar es Salaam Stock Exchange . Ni kweli unaweza ukafanya biashara bila kulazimika kuwa ofisini kwa broker kila mara. Nitakueleza kiufupi inavyowezekana. Ila ingekuwa vizuri kwa wakati wa kwanza ufike ofisini kwa broker na mzungumze na kufahamiana kwanza.

Mimi nikitaka kununua huwa ninatumia sim banking kufanya transfer ya pesa kutoka kwenye account yangu kwenda account ya Broker na ananitumia stakabadhi (receipt) kwa njia ya email - baada ya broker kuninunulia hisa, hati ya hisa ninaweza kuichukua muda wowote (hata kama ni baada ya miezi 2) au kumtuma mtu ofisini kwa broker akanichukulie...ninaamini utakuwa umesaidika kidogo.
 
Mkuu kama nataka kuinvest automatically nafanyeje kwa maana kwamba once nimeshakuwa na account naspecify amount ya kuinvest kila mwezi kutoka kwenye akaunti yangu? Kuna index trackers zozote kwa bongo? Nimesoma mahali faida ya index tracker ni kwamba kuna diversification ya investments kwa hiyo inapunguza risk sababu portfolio ni pana. Najua kuna UTT lakinidisadvantage ya UTT ni kwamba fees lazima ziwe juu sababu ni managed fund. Je fees kwa UTT ni asilimia ngapi? Maana naona tu wana emphasize watu wainvest lakini huwa hawaongei kuhusu fees na huo huwa ni mtego unatakiwa uupuke. Maan kama fees ni kubwa ina maana zita affect reurn yako after taxes. Natamani nione kitu kama NASDAQ na vinginevyo.
sijawahi kuinvest na UTT , mimi nanunua hisa tu kwa kupitia broker, ukienda kwenye office za brokers wanaweza kukusaidia zaidi. Na hayo mambo ya technology kwa soko la dse naona bado sana
 
mkuu najua kwa hiyo sisi wa precision air ndio tumeliwa sababu binafsi sijawahi tumiwa report ya jinsi gani hisa zinavyoenda na nikizingatia kua Co. haifanyi vema. Dah
 
Last edited by a moderator:
nakubaliana nawewe najua kwa asilimia mia, nilinunua hisa za swiss mwezi wa pili mwaka huu kwa sh 5600 lakini leo ni 6600. Wiki ijayo naenda kuuza hisa zangu zote za DCB, CRDB na NMB then nahamia SWISS mzima mzima

ni maamuzi mazuri kwa sababu ya perfomance ya coy. swiss. lakini katika biashara hizi za fedha wanashauri unakuwa na portfolio, maana yake kwamba unainvest sehemu nyingi kwa kununua hisa maeneo mengi ili kampuni moja ukipata hasara kampuni nyingine iliyopata faida unafidia hivyo mwishoni mwaka kapu lako litaonyesha kampuni ipi imeletq ela nyingi na ipi imeleta ela kidogo au ipi haijaleta kabisa ela kwa mwaka huo.

Still mawazo yako ni mazuri kwa sababu unaweza kutengeneza fedha nyingi .
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom