Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Jana Rais Samia kwenye uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Mwinyi, alitangaza kuwa katika pia kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Rais wetu huyo wa zamani aliyetimiza miaka 96, serikali imempatia gari [jipya?] aina ya Mercedes Benz iliyo chini [sedan] kwa sababu aliyokuwa akiitumia [nadhani ni SUV] ilikuwa inampa shida kuipanda na kushuka kutokana na umri wake mkubwa kwa sasa pamoja na kimo chake [hapa nahisi Rais Samia alisema kwa utani].

Tangazo hilo la Rais Samia limezua sokomoko kubwa, hususan mitandaoni.

Mimi sina tatizo na ‘zawadi’ hiyo kwa Rais wetu huyo mstaafu. Kwa maelezo machache aliyoyatoa Rais, sina pingamizi lolote lile.

Ila kuna wengine hawakufurahishwa na jambo hilo. Wamehoji kwamba iweje mtu kama Rais Mwinyi, ambaye katumikia taifa kwa muda mrefu na katika nafasi za juu kabisa, mtu mwenye istihaki nyingi hivyo, ashindwe kujinunulia gari linalomfaa kwa matumizi yake.

Rais Mwinyi keshawahi kuwa waziri. Keshawahi kuwa Rais wa Zanzibar. Na alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Sina hakika kama pia huwa anapata marupurupu ya utumishi wake kama Rais wa Zanzibar au la. Naamini ya urais wa Jamhuri ya Muungano anayapata.

Sasa mimi nina maswali kadhaa:

1. Je, hilo gari alilopewa hivi sasa ni la kwake? Limesajiriwa kwa jina lake? Yeye ndo analilipia bima?
Mimi muda wote huu nimekuwa nikidhani kuwa marais wastaafu huwa wanapewa gari ya matumizi na serikali na kwamba magari hayo huwa ni mali ya serikali.
Yaani, Rais mstaafu huwa anapewa gari, ofisi, watumishi wa ofisi, walinzi, na kadhalika.

2. Kama hivyo ni ndivyo, ni kapewa au wamembadilishia tu gari ya matumizi na siku atayoacha kuitumia itarudishwa ilikotoka?

3. Kama wamembadilishia tu gari, Rais angesema ‘tumembadilishia’ gari la matumizi kuliko kusema ‘tumempa’ gari jipya kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa, ingekuwa ni bora zaidi na isingezua sokomoko?

Tatizo nilionalo hapa ni kuhusu timing, optics, na word choice tu.

Zaidi ya hapo kelele zilizopigwa sizioni kama ni hoja zilizo compelling.

Rais Mwinyi siyo raia wa kawaida. Hawezi kulinganishwa na wazee wengine ambao hawajawahi kuwa marais.

Rais Samia kusema ile majuzi kuwa serikali haina hela za kutosha kuwapa posho wazee, hiyo haina maana serikali haina hela za kuwatunza marais wa zamani.

So this is much ado about nothing.

Go ahead and click that ‘Like’ button if you agree with me. Even if you don’t agree but you appreciate the content, go ahead and smash that button.

Happy Sunday and most importantly, have a very happy Mother’s Day!
Tuwe na roho ya utu, huruma na upendo.
Mzee Mwinyi amefanya mangapi kwa watanzania? Leo tunahoji mzee Mwinyi kupewa gari ambalo anaweza kupanda na kushuka vzr sawa na umri wake wa miaka 96?

Tukumbuke kuwa wanae hawajashindwa kununua Benzi kwa ajili ya Baba yao.

Na Serikali isingeshindwa kununua/kugawa gari kimya kimya, limefanyika kwa uwazi kwa sbb si la nia ovu.

Suala la kumpatia mzee Mwinyi gari halina lengo baya ni kuzidi kutambua mchango katika uongozi wake.
 
Kuna wazee wastaafu wengi tu wanapata shida kwenye usafiri wa umma mara mia ya anavyopata Mwinyi kupanda "vieite" lake.

Naishauri serikali iwape msamaha wa kodi wastaafu wote kwenye kuagiza gari at least moja.

Hii nchi ni yetu sote!
Mkuu Kame, ebu fafanua vizuri huu ushauri wako "Serikali iwape msamaha wa kodi wastaafu WOTE kwenye kuagiza gari at least moja" ushauri huu unawahusu Marais wastaafu au na wastaafu wa Umaa.
 
Kuna mambo yanachosha sana

20210421_094936.jpg
 
Anaanza kutumia madaraka yake vibaya, Mwinyi anashindwa kunua gari kwa hela yake ? Au kuna utakatishaji hapa ? Umzaniae sie kumbe ndie ,ya Mungu ni mengi ,tokea aache uraisi ni miaka mingapi,pensheni anapokea ,ukisikia ubazirifu na huu nao upo kwenye aina fulani.
 
Tatizo ni kuwa, bimkubwa juzi tu kawaambia wazee wa dar kuwa hakuna fedha ya kuwapa walau 30,000 kwa mwezi. Jana amemtunuku mzee Mwinyi Benz, watu wanamaind hilo pia.

Tujue tu kuwa mwenye nacho anaongezewa, Hussein angeweza kumnunulia mzee wake hiyo Benz coz hashindwi, mzee anapata pensheni nono kila mwezi....
 
Mkuu Kame, ebu fafanua vizuri huu ushauri wako "Serikali iwape msamaha wa kodi wastaafu WOTE kwenye kuagiza gari at least moja" ushauri huu unawahusu Marais wastaafu au na wastaafu wa Umaa.
Watumishi wote wa umma wastaafu wawe wanapewa msamaha wa kodi ili kwa watakaoamua kumiliki usafiri wapate ahueni ya gharama.
 
Kwa hela walizo nazo hawa wazee hapakua na u muhimu wa kununua gari la bei ivyo ili hali nchi yenyew ndo kama hivi
Halijanunuliwa wamelitoa bohari na bado yapo meng tu kuanzia mavieite mabenz km LA Babu manisan km ya mwendazake makosta wameyaweka kule kwa ajili ya kwao wao Bi Mkubwa tangu aingie bado hajanunua anatumia oda ya mwendazake.
 
Jana Rais Samia kwenye uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Mwinyi, alitangaza kuwa katika pia kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Rais wetu huyo wa zamani aliyetimiza miaka 96, serikali imempatia gari [jipya?] aina ya Mercedes Benz iliyo chini [sedan] kwa sababu aliyokuwa akiitumia [nadhani ni SUV] ilikuwa inampa shida kuipanda na kushuka kutokana na umri wake mkubwa kwa sasa pamoja na kimo chake [hapa nahisi Rais Samia alisema kwa utani].

Tangazo hilo la Rais Samia limezua sokomoko kubwa, hususan mitandaoni.

Mimi sina tatizo na ‘zawadi’ hiyo kwa Rais wetu huyo mstaafu. Kwa maelezo machache aliyoyatoa Rais, sina pingamizi lolote lile.

Ila kuna wengine hawakufurahishwa na jambo hilo. Wamehoji kwamba iweje mtu kama Rais Mwinyi, ambaye katumikia taifa kwa muda mrefu na katika nafasi za juu kabisa, mtu mwenye istihaki nyingi hivyo, ashindwe kujinunulia gari linalomfaa kwa matumizi yake.

Rais Mwinyi keshawahi kuwa waziri. Keshawahi kuwa Rais wa Zanzibar. Na alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Sina hakika kama pia huwa anapata marupurupu ya utumishi wake kama Rais wa Zanzibar au la. Naamini ya urais wa Jamhuri ya Muungano anayapata.

Sasa mimi nina maswali kadhaa:

1. Je, hilo gari alilopewa hivi sasa ni la kwake? Limesajiriwa kwa jina lake? Yeye ndo analilipia bima?
Mimi muda wote huu nimekuwa nikidhani kuwa marais wastaafu huwa wanapewa gari ya matumizi na serikali na kwamba magari hayo huwa ni mali ya serikali.
Yaani, Rais mstaafu huwa anapewa gari, ofisi, watumishi wa ofisi, walinzi, na kadhalika.

2. Kama hivyo ni ndivyo, ni kapewa au wamembadilishia tu gari ya matumizi na siku atayoacha kuitumia itarudishwa ilikotoka?

3. Kama wamembadilishia tu gari, Rais angesema ‘tumembadilishia’ gari la matumizi kuliko kusema ‘tumempa’ gari jipya kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa, ingekuwa ni bora zaidi na isingezua sokomoko?

Tatizo nilionalo hapa ni kuhusu timing, optics, na word choice tu.

Zaidi ya hapo kelele zilizopigwa sizioni kama ni hoja zilizo compelling.

Rais Mwinyi siyo raia wa kawaida. Hawezi kulinganishwa na wazee wengine ambao hawajawahi kuwa marais.

Rais Samia kusema ile majuzi kuwa serikali haina hela za kutosha kuwapa posho wazee, hiyo haina maana serikali haina hela za kuwatunza marais wa zamani.

So this is much ado about nothing.

Go ahead and click that ‘Like’ button if you agree with me. Even if you don’t agree but you appreciate the content, go ahead and smash that button.

Happy Sunday and most importantly, have a very happy Mother’s Day!
Hii hii benz ni miongoni mwa benzi 20 zilizoletwa na Mfalme wa Morocco King Hasssan VI, as a gift ambapo Mwendazake alijimilikisha kama mali yake binafsi. Kugawanywa leo kwa Kiongozi mstaafu nahisi zimeshataifishwa, na ni sahihi!
 
Afrika insu ni kuupata huo Urais ,ila ukifanikiwa inakuwa Mungu wa Nchi
 
Aliyekuwa anauza jogoo alikuwa ni kuongozi wa kitaifa?
Lakini pia alinunua hakutoa zawad,

Sasa.mwinyi kapewa gari, je yeye katoa mikioni mia saba ilintuone kazidisha bei ya gari?
Alitumia pesa ya jamhuri au ya kwake binafs!!?? Lkn sidhan km wanaweza weka maten pasent ktk dili km hili LA laki
 
Watumishi wote wa umma wastaafu wawe wanapewa msamaha wa kodi ili kwa watakaoamua kumiliki usafiri wapate ahueni ya gharama.
Mkuu ushauri wako uko vizuri, maana akisitafuu amekuwa amechoka tayari.. Yah ushauri poa.
 
Akiba ya fedha za kigeni baada ya Vita vya Uganda iliteremka, nchi ilikuwa haikopesheki na maahirika ya fedha kimataifa, Watanzania walikuwa wanakula mchele wa msaada wa kitumbo, unga wa yanga. Halafu vyote hivyo unavipata kwa foleni. Huko Mtwara wananchi walikuwa wanavaa mifuko ya visulphate kama mashati.

Mwinyi ndiye aliyeruhusu biashara huria, kuanzishwa kwa daladala, kuingizwa kwa mitumba kutoka Ulaya. Akaruhusu watu wafanye biashara mbali mbali. Hata kitimoto kwa wakristu kuliwa openly kwenye mabaa kilianza wakati wake.

Hata privatization ya maahirika Kama TBL na TCC ilianzia kipindi chake na uanzishwai wa TRA.

Muache babu afaidi nchi aliyosaidia kuijenga
 
Mbona nasikia Samia ni mtoto wa nje wa mzee Mwinyi.Samia Hassan .Ahaaa.Mechi imehahirishwa.
LUPEM umepotea kwa hiyo assumption yako. Binti mkubwa wa Mzee Ali Hassan Mwinyi ambaye ni mkubwa kuliko Dr Hussein, na anazaliwa na mama tofauti anaitwa Fatma mke wa Kagasheki na kasoma IDM Mzumbe mwaka 1989. Suluhu naye kasoma IDM Mzumbe mwaka 1986. Hicho ndiyo kinawachanganya

Nimesoma nao wote wawili na ninawafahamu
 
Kama yepi?
1. Kwenye uongozi wao walichukua Chao mapema, (ni matajiri)
2. Magu aliwajengea mahekalu.
Leo mtu anapewa zawadi ya kuzaliwa gari ya mamilioni
Huku wazee wetu wa mitaani wanaomba hisani ya kutibiwa bure kutoka na umri wao, hata ivo hawapati
INAKERA.
 
Akiba ya fedha za kigeni baada ya Vita vya Uganda iliteremka, nchi ilikuwa haikopesheki na maahirika ya fedha kimataifa, Watanzania walikuwa wanakula mchele wa msaada wa kitumbo, unga wa yanga. Halafu vyote hivyo unavipata kwa foleni. Huko Mtwara wananchi walikuwa wanavaa mifuko ya visulphate kama mashati.

Mwinyi ndiye aliyeruhusu biashara huria, kuanzishwa kwa daladala, kuingizwa kwa mitumba kutoka Ulaya. Akaruhusu watu wafanye biashara mbali mbali. Hata kitimoto kwa wakristu kuliwa openly kwenye mabaa kilianza wakati wake.

Hata privatization ya maahirika Kama TBL na TCC ilianzia kipindi chake na uanzishwai wa TRA.

Muache babu afaidi nchi aliyosaidia kuijenga
Hakujenga pekee yake, yeye anakila kitu wakati waliomsaidia wengi wao hawana kitu. Tuache kuwatukuza hawa viongozi!!! This thinking hautifikishi kokote inaturudisha nyuma sana
 
Back
Top Bottom