Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Hapo kuna vitu viwili
1. Zawadi
2. Stahiki

Hatuna Shida na namba 2, Kama ni Stahiki yake basi atwambie kuwa kampa stahiki yake. Na pia tunataka tujue, Stahiki yake ina ukomo upi, Je anaweza kumpa chochote kile anachoona kinafaa? —Yaani akijisikia kumpa hata private Jet anaweza ili kumrahisishia kumove around?, Je Mwinyi aliandika barua kuomba stahiki hiyo?

Kama ni zawadi tunataka kujua, Je Kodi za wananchi na mali ya Umma inaweza kugaiwa tu kama zawadi tu kwa mtu kujisikia?, Yaani rais anaweza kuamka asubuhi akachukua mali ya umma na kumpa mtu kama pipi?, Kama ana power hizo, vipi let say akiamua kumgawia mtu Kiwanda cha umma kama zawadi au what if kama akiamua kutwaa donge kubwa la mabilioni la dhahabu lililo benki kuu na kumgawia mtu?. Je kuna sheria ya Zawadi?.

Bwana Ngabu, Hii nchi ilipotoka enzi za Nyerere tulijifunza mambo ya cheo ni dhamana sitotumia cheo changu kwa manufaa binafsi, Sasa hawa akina Mzee Mwinyi enzi za ujana wao ndo walikuwa wakiimba Slogan hii kama Kasuku, Sasa Leo hii kastaafu, haipaswi atumie cheo chake cha zamani kwa manufaa binafsi, maana kapewa gari hilo kwa kofia kuwa "aliwahi kuwa rais".

Mwisho niseme, Mwinyi anao uwezo wa kujinunulia gari analohitaji, kwa sababu ana majumba, ana pensheni, ana ardhi, kiufupi hata kukopesheka anakopesheka, Kwa hiyo kutwaa mali ya umma na kumpa eti zawadi ni kutapanya kiduchu ambacho tunakihitaji kuondoa umasikini wa watu wetu wetu.

Ila kama ni Stahiki yake basi tusiambiwe kuwa ni Zawadi.
 
Tatizo kwangu ni kununuliwa gari ya kifahari kama kweli imegharimu zaidi milioni 450 kwa kodi zetu!!
Angeweza kununuliwa gari la bei ndogo linaloweza kukidhi maitaji yake.
Hii kusema amelitumikia ili taifa miaka mingi isiwe sio justification nzuri ya kupewa gari la kifahari!

Kuna manesi na madokta wamelitumia ili taifa kwa miaka mingi kwenye maisha ya magumu na wengine wamepata matatizo ya kiafya huko huko kazini Lakini leo hata dawa hawapati bure au matibabu! Hii sio sawa wengine kuishi maisha ya kifahari kwa kodi zetu na wengine wamelitumikia ili taifa kwenye mazingira magumu(kama lack of PPE) kuendelea kuteseka!

Hii tabia ya watu waliyojengewa ya kuita watu wanamawazo ya kimaskini pale wanapooji kodi zetu zinapotumika kununua luxury goods. Hii haisadi kuleta vitendea kazi kwenye mahospitali , maji mitaani, trainings kwa madokta na manesi, Lateral flow test kwenye mahospitali na mengine mengi!!

Hawa si wanajengewa nyumba za kifahari?
Na pia naomba kusahihishwa hapa; Matibabu nje na ma land cruiser si wanapewa?
Kwa nini wengine waishi maisha ya kifahari kwa kodi zetu kuliko madokta na manesi!!
 
Sema mi natamani ilo gari alilobadilishiwa rais wangu mpendwa.
 
@Waterloo,
Nakuheshimu sana mkuu, Ila hapo hakuna hoja. Jaribu kufikiria tena kwamba je, mzee Mwinyi kweli alihitaji hiyo zawadi wakati tunaambiwa taifa linapitia kipindi kigumu hata kushindwa kuongeza watu mishahara?
Anyway tuliache kama lilivyo.
 
Kikwete naye apewe au kwakuwa yeye ni wa bara!
Kikwete, ana hela nyingi mno, alozochkua when he was president. Marais wastaafu huoewa gari mbilivevery 2 years. Sasa imekuwa lazima itangazwe. What a joke. Huyu mama yupo hapo kwa manufactured ya wacache waliomuua Magufuli
 
Hivi hiyo Milioni 450 mmeipata wapi? Maana mnajibu tuu kama kasuku kila mtu 450 mia nne hamsini. Kama ni mtihani wote si mtakuwa mmefeli?
Tupe majibu Professor ipi inauma matumizi ya benzi ama kuokoa mtu asifungwe!?
 
Issue kubwa wala sio kuwa Rais issue kubwa zaidi ni kufikisha miaka 96 sio kila mtu ana uwezo huo hata wangesema kila mzee akifikisha miaka 96 apewe Benz haitakuwa hasara sana sababu wapo wachache.., Zawadi angeweza kutoa kwa niaba yake na sio kutumia pesa zetu kutoa zawadi..., hii inaweza kuleta utamaduni wa kila Birthday kupeana zawadi (walishaanza kujengeana majumba)

Tukemee hii tabia ya pesa zetu kupangiana kufanyia matumizi bila kutushirikisha (hawashindwi binafsi kwa pesa zao kumnunulia hata Ndege) Ila ziwe pesa zao
 
Kama yepi?
Mwinyi means so many people behind!! Siyo mpaka apande yeye mzee ana wapendwa zake.
Wake wawili.
Watoto wake wa kuzaa bwena
Watoto wa ndugu.
Marafiki.
Majirani.
Wahitaji msaada wa hali na mali hapo usisahau
Wajukuu bwena.vitukuu.vining'ina na vilembwe miaka90 si padogo!
Hivyo vimeoa na kuolewa na bado vinazaliwa. Yaani hii inatumikia kijiji cha Mwinyi unasikia???
think out side de box ma meeeen!!

hawa wote means u-Rais wa zamani Mwinyi.!! Kwetu sisi waafric hawa hawakosagi piga ua watakuja tuu.

Kwanza haitoshi angempa coasta. hako ka benz mzee anaenda nako wapi kutanulia? Serikali ikimualika ni ndinga za maana kutoka Ikulu baaas!

Labda vitukuu! Ndo waitumie
Inaonyesha mleta mada ni maskini mnoo!! na ametoka mazingira ya kimaskini sana.

Ameshindwa kujua zawadi Km hizi for popular figure like him means beloved ones, surrounding him its for dem! En! gonna use it effectively!! Tin'k deep!!

unachukulia Mzee Mwinyi km mtu muanza maisha kutoka mkoani anaishi chumba kimoja na sebure!! Looool!
 
Issue kubwa wala sio kuwa Rais issue kubwa zaidi ni kufikisha miaka 96 sio kila mtu ana uwezo huo hata wangesema kila mzee akifikisha miaka 96 apewe Benz haitakuwa hasara sana sababu wapo wachache.., Zawadi angeweza kutoa kwa niaba yake na sio kutumia pesa zetu kutoa zawadi..., hii inaweza kuleta utamaduni wa kila Birthday kupeana zawadi (walishaanza kujengeana majumba)

Tukemee hii tabia ya pesa zetu kupangiana kufanyia matumizi bila kutushirikisha (hawashindwi binafsi kwa pesa zao kumnunulia hata Ndege) Ila ziwe pesa zao
Hili wazo la pesa zenu! Kila siku mnalitoa wapi??
Uchoyo tuuuu! Kila mahali yeye hakufanya kazi?
Watoto wake hawafanyi kaziii tena ngumu kuliko yako hiyo ya boda boda!!

Miafrica michawi tu!! Roho mbaya zinawamiliki mpaka huku.shabash!!!
Si ajabu hujui hizo hela zinatoka wapi!
Hata hiyo boda hujui imetengenezwa na nani unajikalia tuuuu!
Acha mzee ale pensheni kwa raha!! Ndo maana mkoloni aliwachapa vichwa kumbe mijinga bado mpo!!
 
It's a PR Disaster.
Pure and simple.
Wiki ile, hakuna hela ya kuongeza kwa wafanyakazi kwani serikali haina hela.
Wiki hii , Mzee Ruksa anapewa zawadi ya birthday ambayo anaweza kununuliwa na watoto wake ambao wengine ni Marais.

Mbaya zaidi unalifocus tukio lenyewe kwa kuahirisha mechi pendwa sana.

Tunaomtetea mama mtandaoni hatumwelewi.

Hivi hizi kazi wanalazimishwa? Si waache tu
 
Yaan mambo mengine yana umiza mioyo ya wananchi ila basi tu.
Aliye nacho anaongezewa zaidi??
Tuendelee kunywa mtori, nyama zipo chini

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Kutokana na yaliyo andikwa kwenye Kitabu chake Mzee Mwinhi, inaomekana katika Marais walio pata taabu sana ktk uongozi kuanzia alipo teuliwa kuwa waziri basi ni Huyu Mzee wetu Mwinyi.

Pamoja na kuwa mwadilifu na mtiifu lkn bado alichukiwa sana na alifanyiwa fitina za hali ya juu mpaka akajiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani lkn badae alirudishwa tena ulingoni lkn bado alipigwa fitina na kubabaishwa kuwa eti ni mdini anapendelea waislamu n.k, ama hakika walimyumbisha sana lkn kutokana na uadilifu wake na ucha Mungu alibakia kuwa Imara na Hatimaye Mungu alimsaidia.

Hakika kuna mafunzo mengi sana ya kujifunza ktk kipindi cha utawala wake.

tujirekebishe kwa wale wote wenye chuki binafsi na uchu wa vyeo, tuache tabia za kuiguruga nchi yetu, tuwe wazalendo wa kweli.

tuache kutafuta vyeo kwa uchawi au kwa kuhadaa/unafiki kwani cheo/uongozi hutoka kwa Mungu.

Tusibaguane wala kuchukiana au kufanyiana fitina kisa ni mkristo au mwislamu, sisi sote walio na dini na wasio na dini tunaunganishwa na MAMA Tanzania.

tusibaguane kwa makabila au ukanda kwani sisi sote ni watanzania, hivyo yatupasa kudumisha Amani, Upendo na Utulivu kwa masilahi ya nchi yetu.
kwa nini nia, uwezo.sababu, wasaa! Wa kugombea uongozi.urais miafrica inaupachika mi jina mibaya km hivi ....
"uchu wa madaraka,.

urafi.

tamaa ya fisi

Kujipendekeza nk.

Km wewe zandrano unavosema wazi???

Kila akigombea mtu mtamzodoa weee!! km hivi!!!
wewe ni kijishetani au! Haijulikani miafrica mnataka nini!!!!

Pesa hamna

Elimu ya mawazo inasumbua.

Kulogana ndo mwake..

Mali hamna

Kupigana miti tuuu nakulibwatiana. ili unyonywe km kupe unaona rahaa!!

Sijui sababu mliuza ndugu zenu km bidhaa bila huruma!! Wakalia na kusaga meno!! Mpaka Muungwana mzungu akaingilia kati.akaikomesha

Dhambi hii inawatafuna.kizazi mpaka kizazi. Mtalogana weee!! Mpaka na hewa mtailoga kengeee

Akili rahisi tu basi ile ya kupendana hamna shetani amewakalia vibaya tena matakoni basi. Na hatoki.

Mtaongozwa na nani km si shetani??
Wenzenu wanatiana moyo wanapendana, kusaidiana lkn miafricaaaaa !!!!yooooo!!! maweeeeee!!!
 
Hili wazo la pesa zenu! Kila siku mnalitoa wapi??
Uchoyo tuuuu! Kila mahali yeye hakufanya kazi?
Watoto wake hawafanyi kaziii tena ngumu kuliko yako hiyo ya boda boda!!

Miafrica michawi tu!! Roho mbaya zinawamiliki mpaka huku.shabash!!!
Si ajabu hujui hizo hela zinatoka wapi!
Hata hiyo boda hujui imetengenezwa na nani unajikalia tuuuu!
Acha mzee ale pensheni kwa raha!! Ndo maana mkoloni aliwachapa vichwa kumbe mijinga bado mpo!!
Kweli akili yako inahitaji nyongeza...

Unajua maana au tofauti ya zetu na zangu ?, zetu ni kwamba ni fungu ambalo kila raia ana stake no matter what (sababu hata kila akinunua kitu anachangia) hilo fungu lazima matumizi yake yafanyike kwa mapatano / makubaliano ya jamii na kila mwananchi ana haki ya kuhoji...

Kuna sheria ambazo zinahakikisha kwa kazi aliyofanya anapata anachostahili (nina uhakika hilo limefanyika ) Issue sio ngapi zimetumika bali ni matumizi yake yafuate utaratibu isije kujengeka utamaduni wa kutumia hili fungu ndivyo sivyo
 
Hapo vipi? Hio Rainbow sijaipata vizuri

IMG_20210504_181351_122.jpg


IMG_20210504_181805_179.jpg
 
Kweli akili yako inahitaji nyongeza...

Unajua maana au tofauti ya zetu na zangu ?, zetu ni kwamba ni fungu ambalo kila raia ana stake no matter what (sababu hata kila akinunua kitu anachangia) hilo fungu lazima matumizi yake yafanyike kwa mapatano / makubaliano ya jamii na kila mwananchi ana haki ya kuhoji...

Kuna sheria ambazo zinahakikisha kwa kazi aliyofanya anapata anachostahili (nina uhakika hilo limefanyika ) Issue sio ngapi zimetumika bali ni matumizi yake yafuate utaratibu isije kujengeka utamaduni wa kutumia hili fungu ndivyo sivyo
akili yangu iko kamili niamini ndo maana niko mbali kiuchumi kisiasa!

hiyo kila ukinunua una changia ni huduma unazopewana sirikali za kawaida za kila siku.

Ni utamaduni wa Dunia nzima. Tangu enzi za Yesu.

Huduma gani za kijamii zimeteteleka ajili ya manunuzi hayo?
Km nchi itateteleka ajili ya kibenz cha mstaaf ife au iuzwe tu.

Una twist language kizamani sana kwani silikali haina hela zake? Una mind kodi yako?? Huo ni ulinzi unaopewa na polisi.mahakama.barabaranzuri hizo! Unazopita unajamba jamba!!

Zinatakiwa usafi.ukarabati iliziwepo ndo kikodi chako hicho kinaishia hapo.

Ina biashara nyingi sana km hujui.
Ina misaada ile misaada haiji hivihivi kuna watu wanapitisha kopo kimatonya.Ili ule bado unalindwa na familia yako bure usionewe na wanyarwanda.

Nyie ni Dunia ya tatu.hamuwezi kuendesha sirikali yenu hata mwezi tu.kwisha.hako kaboda boda kako siyo made in bongo mnapewa cheap price.

Kwanza ndani kwako hapo nambie una miliki nini made in tanzania!!
Labda ungo.mbuzi ya kukunia nazi na kigoda tu.
 
Mie binafsi kuna baadhi ya wastaafu hawatakiwi kupata chochote hata pensheni wanatakiwa wasipate, hii inatokana na jinsi walivyotumikia taifa, yaani walikula kabisa heshima ni sahihi kuwapati ila kuwaongezea mali si sawa, nakumbuka kipindi kile Mrema anashika dhahabu airport, maelezo yake hadi leo hamna, labda yapo kwenye kitabu cha ruksa, na kama hayapo, basi kitabu akijatimia!
Hapa pagumu.
Al-hajj hasemwi vibaya mkuu
 
Back
Top Bottom