Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Mimi naona huku ni kudhalilishana kweli. Hawa ni watu walioomba wenyewe hiyo kazi, hawakutufanyia favour kwamba alikuwa mahali tukamuomba aje atusaidie. Huyu aliwatumikia raia wa nchi hiyo kwa utashi wake. Sasa haya ya shukrani zilizopitiliza zinatoka wapi?

Hakuna Rais mstaafu ambae hakuna nyumba yake binafsi ( wengine zaidi ya moja). Hamna Rais mstaafu asie na uwezo wa kujinunulia gari anayoitaka kutokana tu na posho yake ambayo ni asilimia 80 ya mshahara wa Rais aliyekuwepo. Rais mstaafu anapewa magari mawili na yanabadilishwa kila baada ya miaka mitano. Analipiwa mpaka dobi. Yote hayo bado tunaona ana shida sana kiasi cha kutaka waboreshewe mafao yao! Kusema leo tunamjengea nyumba Rais mstaafu na kumnunulia gari ni kumdhalilisha kuwa ni maskini kiasi hicho.

Kwa wenzetu Marekani Rais mstaafu anajinunulia nyumba. Sijasikia waziri mkuu wa uingereza au India wakipewa nyumba au magari baada ya kustaafu. Wao kama ilivyo kwa watumishi wengine wa umma wanatarajiwa kuwa wamejipanga kwa ajili ya maisha ya ustaafu.

Mimi ningeunga serikali kama ingetenga fungu ( milioni 500) ambazo mstaafu ataweza kutumia kujenga kitu chenye faida kwa jamii kama kumbukumbu yake, vitu kama maktaba, sehemu ya utafiti n.k.

Haya ya nyumba na magari ni kuwafedhehesha tu. Aidha, itaonekana kama Rais aliyepo anayapigia debe kwa vile anajua yeye pia atanufaika.

Amandla....
Sawa....nini mnataka kifanyike
Kuondoa mambo haya

Ova
 
Jana Rais Samia kwenye uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Mwinyi, alitangaza kuwa katika pia kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Rais wetu huyo wa zamani aliyetimiza miaka 96, serikali imempatia gari [jipya?] aina ya Mercedes Benz iliyo chini [sedan] kwa sababu aliyokuwa akiitumia [nadhani ni SUV] ilikuwa inampa shida kuipanda na kushuka kutokana na umri wake mkubwa kwa sasa pamoja na kimo chake [hapa nahisi Rais Samia alisema kwa utani].

Tangazo hilo la Rais Samia limezua sokomoko kubwa, hususan mitandaoni.

Mimi sina tatizo na ‘zawadi’ hiyo kwa Rais wetu huyo mstaafu. Kwa maelezo machache aliyoyatoa Rais, sina pingamizi lolote lile.

Ila kuna wengine hawakufurahishwa na jambo hilo. Wamehoji kwamba iweje mtu kama Rais Mwinyi, ambaye katumikia taifa kwa muda mrefu na katika nafasi za juu kabisa, mtu mwenye istihaki nyingi hivyo, ashindwe kujinunulia gari linalomfaa kwa matumizi yake.

Rais Mwinyi keshawahi kuwa waziri. Keshawahi kuwa Rais wa Zanzibar. Na alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Sina hakika kama pia huwa anapata marupurupu ya utumishi wake kama Rais wa Zanzibar au la. Naamini ya urais wa Jamhuri ya Muungano anayapata.

Sasa mimi nina maswali kadhaa:

1. Je, hilo gari alilopewa hivi sasa ni la kwake? Limesajiriwa kwa jina lake? Yeye ndo analilipia bima?
Mimi muda wote huu nimekuwa nikidhani kuwa marais wastaafu huwa wanapewa gari ya matumizi na serikali na kwamba magari hayo huwa ni mali ya serikali.
Yaani, Rais mstaafu huwa anapewa gari, ofisi, watumishi wa ofisi, walinzi, na kadhalika.

2. Kama hivyo ni ndivyo, ni kapewa au wamembadilishia tu gari ya matumizi na siku atayoacha kuitumia itarudishwa ilikotoka?

3. Kama wamembadilishia tu gari, Rais angesema ‘tumembadilishia’ gari la matumizi kuliko kusema ‘tumempa’ gari jipya kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa, ingekuwa ni bora zaidi na isingezua sokomoko?

Tatizo nilionalo hapa ni kuhusu timing, optics, na word choice tu.

Zaidi ya hapo kelele zilizopigwa sizioni kama ni hoja zilizo compelling.

Rais Mwinyi siyo raia wa kawaida. Hawezi kulinganishwa na wazee wengine ambao hawajawahi kuwa marais.

Rais Samia kusema ile majuzi kuwa serikali haina hela za kutosha kuwapa posho wazee, hiyo haina maana serikali haina hela za kuwatunza marais wa zamani.

So this is much ado about nothing.

Go ahead and click that ‘Like’ button if you agree with me. Even if you don’t agree but you appreciate the content, go ahead and smash that button.

Happy Sunday and most importantly, have a very happy Mother’s Day!
Kwanini wanasiasa wastaaafu wanajipanga marupurupu kama ya wale wa nchi zilizoendelea ila sisi tunaambiwa pesa haitoshi. Juzi juzi mwinyi alikabidhiwa nyumba ya zaidi ya shs bil 7!
 
Kwanini wanasiasa wastaaafu wanajipanga marupurupu kama ya wale wa nchi zilizoendelea ila sisi tunaambiwa pesa haitoshi. Juzi juzi mwinyi alikabidhiwa nyumba ya zaidi ya shs bil 7!
Sijui!

Labda uwaulize wenyewe..
 
Sawa....nini mnataka kifanyike
Kuondoa mambo haya

Ova
Nimesema hapo juu. Badala ya kupewa magari na kujengewa nyumba watengewe fungu ambalo watatumia kujengea mradi wenye faida kwa jamii ambao utakuwa kama ukumbusho wake.

Amandla...
 
Nadhani gari litabakia la serikali lile v8 litabakia nyumbani yeye apande benz ajili fupi ...apande kirahisi
 
MATAGA wanapata tabu sana na mama Samiah Suluhu.MATAGA&Sukuma -Gang ni watu wenye roho mbaya sana!
 
Hata mm nimejiuliza kama ile kubwa ilikuwa ndefu kuipanda ina maana hata mtoto wake alishindwa kumnunulia gari linaloendana na umri wake? Kuna mengi ambayo hamujajui. Bora uzima.yetu macho.
 
Sasa 450 m mbona unaziona si mali kitu wakati 38 m zilikuuma!? Au matumizi ya 38 m yalifanya jambo lisilo na manufaa kwa taifa lakini 450 zimefanya jambo muhimu, zito, la lazima na manufaa kwa taifa!?
Hizo milioni 450 mmezitoa wapi?
 
Kwa maoni yangu zawadi sio jambo la msingi sana kujadiliwa, tunapoteza malengo na makusudio.

nadhani hata yeye mwenyewe Mzee wetu Babu yetu wa Taifa Mzee Ruksa atafarijika zaidi akiona tunajikita kujadili MAUDHUI ya kitabu chake alicho kiandika badala ya kujadili ZAWADI aliyo pewa.
 
Tatizo ni kuwa, bimkubwa juzi tu kawaambia wazee wa dar kuwa hakuna fedha ya kuwapa walau 30,000 kwa mwezi. Jana amemtunuku mzee Mwinyi Benz, watu wanamaind hilo pia.

Tujue tu kuwa mwenye nacho anaongezewa, Hussein angeweza kumnunulia mzee wake hiyo Benz coz hashindwi, mzee anapata pensheni nono kila mwezi....
Kwa nini unasema Hussein hawezi kushindwa kumnunulia mzee wake hilo Benzi?

Hussein ana hela nyingi sana au kwa sababu yeye ni Rais wa Zanzibar?
 
Unauhakika watanzania hawakuhoji? Au genye zimekujaa... watu walipiga kelele kuwa ni rushwa na tena aliendelea hadi uchaguzi ulipokuwa unakaribia jiwe anamwaga tu pesa barabarani wapinzani walipiga kelele... hivi mlikuwa wapi hadi muongee as if watu kuwa walikaa kimya watu hawakumuogopa Meco japo alikuwa anapoteza watu mashujaa walikomaa tu... ukifanya upuuzi mbele za watu utapondwa tu... naomba unyamaze kitendo cha jana ni upuuzi wa kutia hasira.. kama huna pesa fanya yasiyo gharama na kama pesa ipo toa kwa wote
Ahsante ndugu!

Jamaa kala kona mazima baada ya mimi kuweka ushahidi ambao upo kinyume na uzushi wake.

Ndo maana sasa nimeamini kuwa hata nyumbu wana akili nyingi zaidi kuwashinda hawa watu wa aina ya huyo jamaa uliyemnukuu.
 
Kwa nini unasema Hussein hawezi kushindwa kumnunulia mzee wake hilo Benzi?

Hussein ana hela nyingi sana au kwa sababu yeye ni Rais wa Zanzibar?
Mzee "kibongobongo" baba akienda age vijana wanachukua hatam. Sasa ni zamu ya Hussein kumhudumia mzee wake.
 
Bima!!!? kwani kuna askari anaweza kulikagua hilo gari?? sheria huwa zipo kwenye makaratasi na huwa zinatumika kwa wanyonge sio kwa level hiyo.
 
La juu haliwezi, wamempa la chini, well and good.

Hatutaki aibu ya kusikia rais Mwinyi kaumia au hata kibaya zaidi kimetokea kwa sababu kajikwaa akipanda gari refu ambalo limekuwa likimpa shida kupanda, tutaonekana wajinga dunia nzima kwa kushindwa kuhudumia wazee wetu.

Lakini je, wamempa la chini, hilo la juu wamelichukua kwa sababu linampa shida?

Au ndiyo kiendacho kwa mganga hakirudi?

Kwa sababu kama wamelichukua hilo la juu, hapo wamembadilishia tu.

Na kama hawajalichukua, kwa nini wameliacha gari lenye matatizo hivyo?
Ndo maana nikauliza kama kama wamempa au wamembadilishia tu..

Siku zote nimekuwa nikidhani Rais mstaafu hupewa usafiri wa serikali kwa matumizi yake.

Na kwamba huo usafiri ni mali ya serikali na si mali yake binafsi.

Tatizo letu ni uwazi. Haya mambo yangekuwa yako wazi wala watu tusingehoji sana hii leo.

Au labda yapo wazi lakini ni sisi tu ambao hatujui…
 
Binti wa Profesa Yule Simba damu mtaalam wa mifupa anadai Rais kashauriwa vibaya. Kwa maana ya muda wa kuongea na wazee kuwa karibu na kumpa zawadi mzee mwingine.
Kwani Rais yeye hana akili yake mwenyewe ya kuweza kujua kisichofaa na kinachofaa?

Rais akishauriwa ajambe hadharani atakubali tu kwa vile kashauriwa hivyo?
 
Kwani Rais yeye hana akili yake mwenyewe ya kuweza kujua kisichofaa na kinachofaa?

Rais akishauriwa ajambe hadharani atakubali tu kwa vile kashauriwa hivyo?
Milioni 450 inaonekana ni pesa nyingi lakini ni ndogo sana kwa matumizi ya marais linapokuja suala la usafiri wao.

Mama wanamletea zengwe ili mradi tu nafsi za baadhi ya watu ziweze kuridhika.
 
Mimi naona huku ni kudhalilishana kweli. Hawa ni watu walioomba wenyewe hiyo kazi, hawakutufanyia favour kwamba alikuwa mahali tukamuomba aje atusaidie. Huyu aliwatumikia raia wa nchi hiyo kwa utashi wake. Sasa haya ya shukrani zilizopitiliza zinatoka wapi?

Hakuna Rais mstaafu ambae hakuna nyumba yake binafsi ( wengine zaidi ya moja). Hamna Rais mstaafu asie na uwezo wa kujinunulia gari anayoitaka kutokana tu na posho yake ambayo ni asilimia 80 ya mshahara wa Rais aliyekuwepo. Rais mstaafu anapewa magari mawili na yanabadilishwa kila baada ya miaka mitano. Analipiwa mpaka dobi. Yote hayo bado tunaona ana shida sana kiasi cha kutaka waboreshewe mafao yao! Kusema leo tunamjengea nyumba Rais mstaafu na kumnunulia gari ni kumdhalilisha kuwa ni maskini kiasi hicho.

Kwa wenzetu Marekani Rais mstaafu anajinunulia nyumba. Sijasikia waziri mkuu wa uingereza au India wakipewa nyumba au magari baada ya kustaafu. Wao kama ilivyo kwa watumishi wengine wa umma wanatarajiwa kuwa wamejipanga kwa ajili ya maisha ya ustaafu.

Mimi ningeunga serikali kama ingetenga fungu ( milioni 500) ambazo mstaafu ataweza kutumia kujenga kitu chenye faida kwa jamii kama kumbukumbu yake, vitu kama maktaba, sehemu ya utafiti n.k.

Haya ya nyumba na magari ni kuwafedhehesha tu. Aidha, itaonekana kama Rais aliyepo anayapigia debe kwa vile anajua yeye pia atanufaika.

Amandla....
Fundi…umesema kuwa Rais mstaafu huwa anapewa magari mawili na huwa yanabadilishwa kila baada ya miaka 5.

1. Hayo magari mawili huwa ni ya aina gani? Yanayofanana au yasiyofanana?

2. Ina maana Rais Mwinyi sasa kapata gari ya tatu au wamembadilishia tu moja kati ya hayo mawili uliyosema wanapewa?

Narudia tena kusema kuwa huendi tatizo hapa ni timing, optics, word choice, na labda setting…
 
Back
Top Bottom