Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Tatizo hapa ni ufinyu wa taarifa!

Aliyemnunulia Mwinyi hilo gari ni Samia au ni serikali?

Wewe umesema ni Samia. Unaposema ni Samia unamaanisha ni Samia kama Samia au ni Samia kwa niaba ya serikali?
Ufinyu wa taarifa, na ndio maana watu wanajadili. Kungekuwa na taarifa inayojitosheleza huenda mjadala usingefika huku.

Kama ingekuwa SASHA kamnunulia mzee kwa pesa zake hapo hakuna mjadala, kama katumia pesa za serikali basi tujue..
 
Ni mamoja ni mali ya serikali au amepewa binafsi kutoka kwenye hazina ya umma.
Msimamo wa dini ya Kiislamu katika jambo hili ni mkali sana. Huwezi kuchukua mali ya watu ukaitumia upendavyo.
Bwana mmoja aliwahi kwenda kwa Khalifa Omar bin Al Khattab, usiku. ( Omar alikuwa ndiye rais wa Waislamu wote wakati huo waliofikia takriban milioni 4 na mali zilizokadiriwa dola bilioni 7 (kwa sasa) wakitawala mataifa ya Rumi (wazungu) na Waajemi (Iran). Akamkuta anafanya mahesabu ya pesa zilizoletwa kama Zaka kutoka mikoa ya Syria na Yemen. Yule bwana akamwambia, nimekuja kwa mzungumzo nawe. Omar akamwuliza, mazungumzo binafsi au ya masuala ya umma? Akasema, ya binafsi. Omar akachukua ile koroboi ilyokuwa inawaka, akaizima. Akamwita bwana yule asogee, gizani. Yule akauliza, vipi, mbona umezima taa? Omar akasema, ndiyo, mafuta ya taa hii yamenunuliwa kwa mali ya umma, si mali yangu. Na wewe una mazungumzo nami ya haja zako binafsi. Nahofia Mwenyezi Mungu atakwenda niuliza juu ya matumizi haya ya mali ya umma!

Huo ndio Uislamu usiofuatwa!
 
ACHENI KULIALIA NA KULALAMIKA
NYIE PAMBANENI NA HALI ZETU,
TAFUTENI MALI KIVYENU!
HAO MNAOWAONEA GERE WAKO KWENYE
MFUMO WAO NA FAMILIA ZAOOOOO

ova
 
Tuwe na roho ya utu, huruma na upendo.
Mzee Mwinyi amefanya mangapi kwa watanzania? Leo tunahoji mzee Mwinyi kupewa gari ambalo anaweza kupanda na kushuka vzr sawa na umri wake wa miaka 96?

Tukumbuke kuwa wanae hawajashindwa kununua Benzi kwa ajili ya Baba yao.

Na Serikali isingeshindwa kununua/kugawa gari kimya kimya, limefanyika kwa uwazi kwa sbb si la nia ovu.

Suala la kumpatia mzee Mwinyi gari halina lengo baya ni kuzidi kutambua mchango katika uongozi wake.
Urais ni ajira usisahau hilo bwashee!
 
Hata mm nimejiuliza kama ile kubwa ilikuwa ndefu kuipanda ina maana hata mtoto wake alishindwa kumnunulia gari linaloendana na umri wake? Kuna mengi ambayo hamujajui. Bora uzima.yetu macho.
Isije kuwa baba ntu kapewa zawadi ya hepi bethi dei, vijimaneno navyo huwa haviishi huku kitaa...
 
Zinatoka kwenye picha hii na mahesabu haya



109,750 x 2300 = 252,425,000/=
Ukiweka kodi ndiyo inafika 450 milioni. Sawa, hatujapigwa; siyo!?

====
Sijasahau swali, ipi imekuuma zaidi pesa ya matumizi ya 38 milioni au pesa ya matumizi ya 450 milioni!?
Hakuna hata moja iliyoniuma.
 
Jana Rais Samia kwenye uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Mwinyi, alitangaza kuwa katika pia kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Rais wetu huyo wa zamani aliyetimiza miaka 96, serikali imempatia gari [jipya?] aina ya Mercedes Benz iliyo chini [sedan] kwa sababu aliyokuwa akiitumia [nadhani ni SUV] ilikuwa inampa shida kuipanda na kushuka kutokana na umri wake mkubwa kwa sasa pamoja na kimo chake [hapa nahisi Rais Samia alisema kwa utani].

Tangazo hilo la Rais Samia limezua sokomoko kubwa, hususan mitandaoni.

Mimi sina tatizo na ‘zawadi’ hiyo kwa Rais wetu huyo mstaafu. Kwa maelezo machache aliyoyatoa Rais, sina pingamizi lolote lile.

Ila kuna wengine hawakufurahishwa na jambo hilo. Wamehoji kwamba iweje mtu kama Rais Mwinyi, ambaye katumikia taifa kwa muda mrefu na katika nafasi za juu kabisa, mtu mwenye istihaki nyingi hivyo, ashindwe kujinunulia gari linalomfaa kwa matumizi yake.

Rais Mwinyi keshawahi kuwa waziri. Keshawahi kuwa Rais wa Zanzibar. Na alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Sina hakika kama pia huwa anapata marupurupu ya utumishi wake kama Rais wa Zanzibar au la. Naamini ya urais wa Jamhuri ya Muungano anayapata.

Sasa mimi nina maswali kadhaa:

1. Je, hilo gari alilopewa hivi sasa ni la kwake? Limesajiriwa kwa jina lake? Yeye ndo analilipia bima?
Mimi muda wote huu nimekuwa nikidhani kuwa marais wastaafu huwa wanapewa gari ya matumizi na serikali na kwamba magari hayo huwa ni mali ya serikali.
Yaani, Rais mstaafu huwa anapewa gari, ofisi, watumishi wa ofisi, walinzi, na kadhalika.

2. Kama hivyo ni ndivyo, ni kapewa au wamembadilishia tu gari ya matumizi na siku atayoacha kuitumia itarudishwa ilikotoka?

3. Kama wamembadilishia tu gari, Rais angesema ‘tumembadilishia’ gari la matumizi kuliko kusema ‘tumempa’ gari jipya kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa, ingekuwa ni bora zaidi na isingezua sokomoko?

Tatizo nilionalo hapa ni kuhusu timing, optics, na word choice tu.

Zaidi ya hapo kelele zilizopigwa sizioni kama ni hoja zilizo compelling.

Rais Mwinyi siyo raia wa kawaida. Hawezi kulinganishwa na wazee wengine ambao hawajawahi kuwa marais.

Rais Samia kusema ile majuzi kuwa serikali haina hela za kutosha kuwapa posho wazee, hiyo haina maana serikali haina hela za kuwatunza marais wa zamani.

So this is much ado about nothing.

Go ahead and click that ‘Like’ button if you agree with me. Even if you don’t agree but you appreciate the content, go ahead and smash that button.

Happy Sunday and most importantly, have a very happy Mother’s Day!
Kabla ya kuandika hili bandiko reeefu... ungeangalia kwanza aina ya hao wanaolipigia kelele hilo "benz la chini" wana akili za aina gani? Je ni walewale walioshangilia wakati mwendazake akiwagawa "wale ndege wa ikulu" apendavyo kana kwamba ni mali yake binafsi au ni wale waliokaa kimya?
Nadhani sasa midhali mitandao imefunguliwa ingelikuwa vema tujadili vitu vyenye afya kwa Taifa...
 
That’s what I thought too…
Serikali haigawi zawadi mali ya umma, bali serikali inagawa stahiki zilizopo kwa mujibu wa sheria.

Mwinyi kapewa zawadi siyo stahiki.
Stahiki zimeorodheshwa, zinajulikana na zina utaratibu wake.

Wapi na ni lini mzee ruksa kaomba serikali impe Benz?.

Ni daktari gani wa Mzee ruksa aliyerecommend Benz?.

Samia kajuaje kuwa Benz ndo inayomfaa mzee ruksa na siyo gari nyingine?.

Lile gari ambalo mzee ruksa analo sasa, litarudi serikalini au nalo lunakuwa lake binafsi?
 
Serikali haigawi zawadi mali ya umma, bali serikali inagawa stahiki zilizopo kwa mujibu wa sheria.

Mwinyi kapewa zawadi siyo stahiki.
Stahiki zimeorodheshwa, zinajulikana na zina utaratibu wake.

Wapi na ni lini mzee ruksa kaomba serikali impe Benz?.

Ni daktari gani wa Mzee ruksa aliyerecommend Benz?.

Samia kajuaje kuwa Benz ndo inayomfaa mzee ruksa na siyo gari nyingine?.

Lile gari ambalo mzee ruksa analo sasa, litarudi serikalini au nalo lunakuwa lake binafsi?
Unayo majibu ya hayo maswali yako?
 
Unayo majibu ya hayo maswali yako?
Ni rhetoric questions ambazo tukio la jana linaonyesha mzee kapewa surprise tu ya "Birthday gift"

Ingekuwa imefata official Channel ya mzee kuomba gari serikalini kama sehemu ya package ya stahiki zake basi lisingetolewa kama Zawadi, kuvalishwa gift ribbon, maana ingekuwa siyo gift bali ni haki ya mtu!

Kiufupi kwa maelezo ya Samia, Samia mwenyewe kaona mzee anapata tabu ya kupanda gari na kushuka basi akaamua ampe "Zawadi" ya benz
.
Sasa angempa kwa fedha zake za mfukoni hatuna shida, lakini kutwaa mali ya umma na kumpa (nje ya package ya stahiki za mzee), sisi tunaona ukakasi
 
Ni rhetoric questions ambazo tukio la jana linaonyesha mzee kapewa surprise tu ya "Birthday gift"

Ingekuwa imefata official Channel ya mzee kuomba gari serikalini kama sehemu ya package ya stahiki zake basi lisingetolewa kama Zawadi, kuvalishwa gift ribbon.

Kiufupi kwa maelezo ya Samia, Samia mwenyewe kana mzee anapata tabu ya kupanda gari na kushuka basi akaamua ampe "Zawadi" ya benz
.
Sasa angempa kwa fedha zake za mfukoni hatuna shida, lakini kutwaa mali ya umma na kumpa (nje ya package ya stahiki za mzee), sisi tunaona ukakasi
Unajuaje kuwa hajampa kwa fedha zake [Samia] za mfukoni?

Au unasadiki hajampa kwa fedha zake toka mfukoni?
 
Jana Rais Samia kwenye uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Mwinyi, alitangaza kuwa katika pia kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Rais wetu huyo wa zamani aliyetimiza miaka 96, serikali imempatia gari [jipya?] aina ya Mercedes Benz iliyo chini [sedan] kwa sababu aliyokuwa akiitumia [nadhani ni SUV] ilikuwa inampa shida kuipanda na kushuka kutokana na umri wake mkubwa kwa sasa pamoja na kimo chake [hapa nahisi Rais Samia alisema kwa utani].

Tangazo hilo la Rais Samia limezua sokomoko kubwa, hususan mitandaoni.

Mimi sina tatizo na ‘zawadi’ hiyo kwa Rais wetu huyo mstaafu. Kwa maelezo machache aliyoyatoa Rais, sina pingamizi lolote lile.

Ila kuna wengine hawakufurahishwa na jambo hilo. Wamehoji kwamba iweje mtu kama Rais Mwinyi, ambaye katumikia taifa kwa muda mrefu na katika nafasi za juu kabisa, mtu mwenye istihaki nyingi hivyo, ashindwe kujinunulia gari linalomfaa kwa matumizi yake.

Rais Mwinyi keshawahi kuwa waziri. Keshawahi kuwa Rais wa Zanzibar. Na alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Sina hakika kama pia huwa anapata marupurupu ya utumishi wake kama Rais wa Zanzibar au la. Naamini ya urais wa Jamhuri ya Muungano anayapata.

Sasa mimi nina maswali kadhaa:

1. Je, hilo gari alilopewa hivi sasa ni la kwake? Limesajiriwa kwa jina lake? Yeye ndo analilipia bima?
Mimi muda wote huu nimekuwa nikidhani kuwa marais wastaafu huwa wanapewa gari ya matumizi na serikali na kwamba magari hayo huwa ni mali ya serikali.
Yaani, Rais mstaafu huwa anapewa gari, ofisi, watumishi wa ofisi, walinzi, na kadhalika.

2. Kama hivyo ni ndivyo, ni kapewa au wamembadilishia tu gari ya matumizi na siku atayoacha kuitumia itarudishwa ilikotoka?

3. Kama wamembadilishia tu gari, Rais angesema ‘tumembadilishia’ gari la matumizi kuliko kusema ‘tumempa’ gari jipya kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa, ingekuwa ni bora zaidi na isingezua sokomoko?

Tatizo nilionalo hapa ni kuhusu timing, optics, na word choice tu.

Zaidi ya hapo kelele zilizopigwa sizioni kama ni hoja zilizo compelling.

Rais Mwinyi siyo raia wa kawaida. Hawezi kulinganishwa na wazee wengine ambao hawajawahi kuwa marais.

Rais Samia kusema ile majuzi kuwa serikali haina hela za kutosha kuwapa posho wazee, hiyo haina maana serikali haina hela za kuwatunza marais wa zamani.

So this is much ado about nothing.

Go ahead and click that ‘Like’ button if you agree with me. Even if you don’t agree but you appreciate the content, go ahead and smash that button.

Happy Sunday and most importantly, have a very happy Mother’s Day!
Mkuu Nyani Ngabu heshima kwako. Bandiko lako limenifanya "Nitabesamu" kidogo na kunifanya niwaze kidogo " Nje ya Box". Hongera sana.
 
Back
Top Bottom