Soma hapa kabla ya kuchapisha andiko lako katika Jukwaa la Stories of Change

Soma hapa kabla ya kuchapisha andiko lako katika Jukwaa la Stories of Change

JamiiForums

JF Official Account
Joined
Nov 9, 2006
Posts
6,229
Reaction score
5,285
Kwa wote wanaotaka kushiriki shindano la Stories of Change Tafadhali someni kwa makini vigezo hivi. Hakikisha andiko lako limekidhi kabla ya kutaka kuchapisha.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  1. Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko kwenye nyanja za Elimu, Uchumi, Kilimo, Utawala, Afya, Sayansi na Teknolojia.
  2. Andiko liwe kwa Kiswahili lenye maneno yasiyopungua 800 na yasiyozidi 1000.
  3. Makala zinatakiwa kuwa habari au makala halisi zisizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Plagiarism (Wizi wa machapisho mengine) haitaruhusiwa.
  4. Mshiriki anaweza kutumia jina la kubuni ‘pseudonym’ lakini atatakiwa kutoa taarifa binafsi (jina) endapo ataibuka mshindi.
  5. Matumizi ya picha au video yanaruhusiwa ili kushibisha andiko. Endapo picha na video sio za mshiriki, atalazimika kutaja chanzo.
  6. Watendaji wa Jamii Forums na ndugu zao wa karibu hawaruhusiwi kushiriki kwenye shindano hili.
 
Upvote 73
Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko kwenye nyanja za Elimu, Uchumi, Kilimo, Utawala, Afya, Sayansi na Teknolojia.

Swali langu hapa Ni je Ni lazima andiko lihusishe mambo yote hayo au moja katika hayo mfano naweza andika andiko kuhusu elimu tu?
One
 
Habari njema hii, pia nimevutiwa kushiriki na tayari andiko langu lipo hewani "VITA YA VIJANA DHIDI YA MAENDELEO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA"
kama vijana ni andiko ambalo linaweza kuongeza kitu fulani, hivyo unaweza pitia na ukivutiwa zaidi unaweza nipigia kura.
 
Jamani, nauliza namna ya kuatach picha au video ndani ya chapisho langu mi vip?
 
Nahitaji saana nilielewe ila Kuna mahala nakwama sehemu hasa ya kuandikia Hilo jambo langu.
 
MWANDISHI: MAKI D SILWIMBA

MAADA:TISHIO LA USUGU WA DAWA NA UANDAAJWI WA MATABIBU WAJAO KATIKA KUKABILIANA NA TATIZO NCHINI TANZANIA.

Ustahimilivu wa viuavijidudu (usugu wa dawa) hutokea wakati bakteria, vimelea, virusi na fangasi wanapokuwa sugu kwa dawa . Upinzani dhidi ya viuavijasumu (dawa zinazotumika kuzuia na kutibu maambukizi ya bakteria) ni tatizo la dharura kwa sababu antibiotics ni msingi wa dawa za kisasa na taratibu nyingi za matibabu katika afya ya binadamu na wanyama hutegemea dawa hizi.
Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) linasisitiza kwamba "usugu wa dawa ni moja ya hatari kubwa kwa usalama wa chakula, maendeleo, na afya ya ulimwengu leo." Kuenea kwa bakteria sugu kumeongezeka kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya viuavijasumu(dawa) katika matibabu ya binadamu na kilimo kote ulimwenguni. Mojawapo ya sababu kuu zinazochangia kuundwa kwa bakteria sugu ni taarifa zizizo sahihi na/au matumizi mabaya ya dawa kwa wagonjwa.
Usugu wa dawa unazidi kuleta wasiwasi mkubwa, na hali inazidi kuwa mbaya zaidi katika mataifa yanayoendelea kutokana na matumizi mabaya ya madawa. Matumizi ya dawa isivyotakiwa, yanachangia kuibuka kwa usugu; Upatikanaji wa dawa za kuua viini kwenye kaunta(kiurahisi), bila agizo la daktari, na kupitia mitandao ya usambazaji isiyodhibitiwa inachochea zaidi matumizi yawe yasiyo faa katika mataifa yanayoendelea.

BAADHI YA SABABU ZINAZOCHANGIA ONGEZEKO LA TATIZO
Wasambazaji wa dawa na ubora wa dawa
Upatikanaji na matumizi mabaya ya dawa za kuua viini pia huathiriwa na ukosefu wa sheria madhubuti zinazosimamia mauzo yao. Dawa za kuua viini kwa kawaida zinaweza kununuliwa bila agizo la daktari katika mataifa maskini na kwa kawaida hutolewa na watu wasio na ujuzi mitaani. Wauzaji hawa wa dawa watauza dawa ili kupata mapato na kutosheleza mahitaji ya kifedha ya mgonjwa.

Wataalamu wa afya
Wataalamu wa afya ni muhimu katika utambuzi, matibabu, na kuzuia magonjwa, lakini wana hatari ya kuhatarisha juhudi hizi ikiwa mbinu zao hazitaungwa mkono na utafiti. Katika mataifa mengi yanayoendelea, kuna uwiano wa juu wa mgonjwa na daktari, jambo ambalo huwafanya madaktari kufanya kazi kupita kiasi na kutompa muda wa kumuelekeza mgonjwa kuhusu viwango vya ufuasi wa dawa na athari za kutofuata utaratibu wa kutumia dawa.


Wagonjwa
Uzingatiaji una changia sehemu kubwa katika ukuaji wa usugu wa dawa. Wagonjwa wanaweza kukosa dozi kwa makusudi au bila kukusudia. Baadhi ya wagonjwa wanaweza kuruka dozi wanapoalikwa kwenye karamu inayohusisha unywaji pombe kwa sababu wanafahamu madhara ya kufanya hivyo wanapotumia dawa. Taratibu hizi huweka bakteria hai kwenye viwango vya dawa chini ya viwango vya matibabu, jambo ambalo huongeza uwezekano kwamba wanaweza kupata usugu wa dawa.

Matumizi yasiyo ya binadamu ya dawa
Utumiaji wa dawa za kuua vijidudu kwa wanyama, haswa zile zinazotumika kwa uzalishaji wa chakula, una athari kubwa kwa afya ya binadamu na wanyama kwani inaweza kusababisha kuibuka kwa bakteria sugu kwa matibabu. Bakteria hawa sugu katika wanyama wanaweza kuenea kwa binadamu kwa njia ya chakula, kuwasiliana kwa karibu na wanyama wanaotumiwa kwa chakula, au usambazaji wa mazingira (kama vile maji taka kutoka kwa watu na kutiririka kutoka kwenye maeneo ya kilimo.

Ufuatiliaji duni na upimaji mdogo katika maabara.
Kutokana na matatizo ya uwezo, upimaji wa uwezekano wa antimicrobial haufanywi mara kwa mara katika maabara nyingi za vijijini. Kwa sababu viwango vya upinzani vinaweza kubadilika kwa wakati katika eneo moja la nchi, ufuatiliaji kama huo lazima ufanyike mara kwa mara na bila kukoma.

MIKAKATI YA KUDHIBITI UKUAJI WA TATIZO LA DAWA SUGU
Ukweli kwamba mashirika mengi ya kimataifa ya dawa huona kufanya utafiti juu ya usugu wa dawakama "faida ndogo" kwa hivyo, wanapendelea ufadhili wa uundaji wa dawa za magonjwa sugu kama vile kisukari na shinikizo la damu pamoja na zile zinazosaidia watu kuishi maisha yenye afya kama vile Cialis na Viagra. Kufanya tafiti, na kuja na njia bora za kuzuia maambukizi ya viumbe sugu kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine lazima iwe lengo la msingi la ufumbuzi wa muda mrefu.

Jukumu la wadau katika udhibiti wa usugu wa dawa
Wataalamu wa matibabu na wanasayansi hawawezi kuwajibika pekee yao kudhibiti usugu wa dawa. Umma kwa ujumla na washikadau wengine wana jukumu muhimu la kutekeleza, mambo kama elimu ya mara kwa mara ni muhimu katika kutatua tatizo hili. Serikali pia inapaswa kuyapa kipaumbele masuala ya afya ya umma yanayohusiana na usugu wa dawa(1).

Jukumu la mashirika ya udhibiti serikalini
Ili kuhakikisha usugu wa dawa unapungua katika vituo vyote vya huduma za afya, kilimo, na sekta ya mifugo, utafiti mkubwa na unaoendelea, sera, sheria na maendeleo zinahitajika ili kutatua tatizo la usugu wa dawa na kuajiri madaktari zaidi ili kuleta uwiano sawa kati ya idadi ya wagonjwa na madaktari.

MATABIBU WA BAADAE NA TISHIO LA USUGU WA DAWA
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa katika chuo kikuu cha Dodoma, asilimia 48.8 ya wanafunzi wanaosoma udaktari wa binadam na 27.3% ya wanafunzi wa kada zingine hawakumaliza kozi nzima inayohusu usugu wa dawa na waliacha kutumia dawa mara pale dalili za ugonjwa zinapopungua.
Kwa kuwa watakuwa wakitoa dawa kila siku bila uangalizi mara tu watakapohitimu na kupewa leseni ya udaktari, wanafunzi wa kitiba wanahitaji kujifunza jinsi ya kutoa dawa kwa usalama na kwa ufanisi. Ikizingatiwa kwamba wanafunzi wa siku za usoni wa utabibu watatumika kama kizazi kijacho cha watoa huduma za afya, ni muhimu kwamba waelezwe kikamilifu kuhusu tatizo linaloongezeka la usugu wa dawa. Kwa bahati mbaya, ni sehemu ndogo tu ya mitaala ya wanafunzi wa udaktari wa Tanzania ambayo inasisitiza juu ya usugu wa dawa, na hakuna taarifa za ASP hata kidogo. ASPs huwaelimisha watumishi wote muhimu wa mfumo wa huduma ya afya, wakiwemo madaktari, wafamasia, na wauguzi, kuhusu umuhimu wa kuzingatia maagizo ya utumizi wa dawa ili kuzuia matumizi yasiyo yasiyo faa ya viuavijasumu.

HITIMISHO
Malengo ya kujifunza yanayohusisha viuavijasumu na usugu wa dawa yanapaswa kujumuishwa katika uundaji upya wa mtaala wa kitaifa wa shule za msingi na sekondari. Katika vyuo vya tiba lazima kuwe na kozi maalum kuhusu usugu wa dawa. Kwa ujumla, ni kazi yetu kuzuia kueneza vijiumbe hai ambayo ni sugu kwa kizazi kijacho.


TUUNGANE KUDHIBITI USUGU WA DAWA….INAWEZEKANA KWA USHIRIKIANO WA ASASI ZA KIRAIA NA ZISIZO ZA KIRAIA.
 
Kwa wote wanaotaka kushiriki shindano la Stories of Change Tafadhali someni kwa makini vigezo hivi. Hakikisha andiko lako limekidhi kabla ya kutaka kuchapisha.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  1. Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko kwenye nyanja za Elimu, Uchumi, Kilimo, Utawala, Afya, Sayansi na Teknolojia.
  2. Andiko liwe kwa Kiswahili lenye maneno yasiyopungua 800 na yasiyozidi 1000.
  3. Makala zinatakiwa kuwa habari au makala halisi zisizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Plagiarism (Wizi wa machapisho mengine) haitaruhusiwa.
  4. Mshiriki anaweza kutumia jina la kubuni ‘pseudonym’ lakini atatakiwa kutoa taarifa binafsi (jina) endapo ataibuka mshindi.
  5. Matumizi ya picha au video yanaruhusiwa ili kushibisha andiko. Endapo picha na video sio za mshiriki, atalazimika kutaja chanzo.
  6. Watendaji wa Jamii Forums na ndugu zao wa karibu hawaruhusiwi kushiriki kwenye shindano hili.
Well
 
MAENDELEO NA KAGERA
Dhana ya maendeleo watu wengi huitafakari tofauti kabisa.
Wataalamu wengi husema maendeleo ni ile hali ya kutoka kwenye hali duni kwenda kwenye hali bora( hali yenye unafuu kuliko ya awali)
Watu wengine hudhani maendeleo ni mfano kupatikana kwa umeme, barabara safi tena za lami, upatikanaji wa maji safi na salama hasahasa yale maji ya bomba,hospitali nzuri n.k
Wote wako sahihi.
lakini leo ebu kidogo tujikite kidogo kwenye maendeleo yahusuyo kipato cha mtu mmoja mmoja yaani maendeleo ya kiuchumi tuaachane kidogo na maendeleo ya kijamii. Mimi naamini zaidi sana mtu akiniambia sehemu fulani imeendelea asinionyeshe majengo mazuri,barabara,hospitali tu bali twende zaidi katika kuangalia maendeleo ya mtu mmoja mmoja hasa kiuchumi(economic development).
Mkoa wa Kagera ni kati ya mikoa mitatu duni zaidi kwa mujibu wa ripoti ya serikali ya mwaka 2016, japokuwa mwaka 2018 ripoti hiyo iliusogeza mbele kidogo.
Nimekuwa nikifatilia kwa karibu maisha ya watu,mienendo,tamaduni nimegundua kuna vitu ambavyo vinachangia mkoa huu kuwa nyuma na pia kuendelea kurudi nyuma siku zinavyosonga.
Sababu hizo ni kama ifuatavyo

1.ARDHI.
Swala la umilikaji Ardhi mkoani Kagera ni kizungumkuti.Tokea enzi na enzi mkoa huu umekuwa chini ya Nyarubanja. Hii system ya kiuchumi imepitwa na wakati na haifai kuendelea kutumika kwa sasa.
Mfumo huu huusisha mzee wa ukoo kumilika ardhi ambayo uwagawia wanae wote, baadae wanae pia upata watoto na kuwagawia pia,baadae uenda hivo mpaka vitukuu.
Mfano fikilia mzee wa ukoo labda alimiliki hekari 20 ,akazaa watoto 20,kila mtoto atapata takribani hekari moja, na haohao watoto wakipata watoto wao ,ebu tuseme kila mmoja apate watano,ataendelea kuwagawia hekari moja ileile na baadae hao watoto wataigawa tena kwa watoto wao tena.
Inawezekana mzee aliyekuwa na hekari 20,saa hizi kitukuu atamiliki kitaru tu

Nini kifanyike
Kutokana kwa mkoa wa Kagera bado takribani asilimia 80 ya ardhi yake haijakaliwa na watu ni bora serikali za vijiji kwa mamlaka zilizopewa kupitia wafikilie uwezekano wa aidha kuwauzia watu ardhi,kukodisha au kuwagawia kulingana na sheria ya ardhi inavyodai.
Hapa simaanisha wauze au wagawe maeneo yote hapana maana kuna ardhi inabidi ibaki kwa vizazi vijavyo
Lakini pia pesa itakayopatikana kutokana na uuzaji au ukodeshaji wa ardhi itumike kuendeleza huduma za kijamii.

2.Kilimo
Ni ukweli usiopingika kwamba staili ya kilimo inayotumika mkoani kagera hasahasa Missenyi,Bukoba,Biharamulo na Muleba imepitwa na wakati, hapa sijaitaja Karagwe kwasababu angalau Karagwe wanajitahidi kidogo.
Miaka ya 90 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000,kilimo kilikuwa bora mkoani Kagera lakini baada ya kuingia mnyauko wa migomba pamoja na magonjwa ya kahawa kwa sasa kagera imefeli vibaya katika nyanja za kilimo.
Mwanzoni mwa miaka ya 2000,watu walilima kwa trekta hasahasa zile za KCU leo hii watu wamerudi kwenye kilimo cha jembe la mkono, maeneo yakulima vimekuwa vibustani kutokana na mfumo wa nyarubanja.

Nini kifanyike

Mapendekezo namba moja hapo juu
Pili ziwepo tafiti za kilimo kuhusu kahawa na migomba
Tatu, NGOs zijikite zaidi ktk kuelimisha juu ya mbinu bora za kitaalamu za kilimo biashara.

3.USAFIRI NA USAFIRISHAJI
Kagera inaitaji barabara za lami,meli,viwanja vya ndege. Mpango wa Ujenzi wa Uwanja wa ndege wa kimataifa sio wa kuachwa.
Kubwa kuliko Kagera inaitaji usafiri wa reli/treni.
Usafiri wa reli/treni ndio usafiri bora zaidi na wa uwakika kwa nchi zetu hizi duni

Naweza kueleweka vibaya nikisema bora meliisiwepo,uwanja wa ndege usiwepo ila kukawepo na reli
naamini wengi hawatanielewa ila kusafirisha mzigo kwa reli kutoka dar es salaam mpaka bukoba inaweza kuwa sh10000 kwa mzigo ambao mtu atasafirisha kwa laki moja kwa bus. Lakini pia usafiri wa meli unaunganisha mkoa wa Kagera na Mwanza tu wakati Kagera inatakiwa kuungwa na mikoa mingine zaidi.
Usafiri wa meli ni wa bei rahisi kweli lakini kwa treni ni bei rahisi zaidi uenda ata nauli ya kutoka bukoba mpaka Mwanza inaweza kuwa elfu 9 mpaka 10.

4.UHAMAJI WA WATU
Mkoa wa kagera ni mkoa unaoandamwa na watu wanaoamia mikoa mingine kila uchao.Hii inapunguza nguvu kazi.
Watu wanaenda mikoa mingine kutafuta mahitaji ya kijamii. Nahisi ni bora kuangalia uwezekanao wa kusogeza mahitaji hayo karibu.

5.KAHAWA NA MAZAO MBADALA
Kahawa naiongelea mara mbili hapa .Nimeisha iongelea kwenye swala la kilimo. Kahawa ilikuwa kama madini kwa kagera. Lakini kwa sasa kilimo hiki kimekufa.

NINI KIFANYIKE
napendekeza zifanyike tafiti za kutosha juu ya zao hili
pili wananchi wafundishwe juu ya kilimo cha kisasa
tatu,watafiti waje na mbege bora zinazoendana na mabadiliko ya tabia ya nchi
nne, yawepo mazao mbadala yanayoendana na hali ya Kagera.
Napendekeza mazao yafuatayo
1.KATANI
hali ya hewa ya mkoa Kagera haipishani sana na Tanga na Morogoro, kwa iyo zao la katani linaweza kustawi kwa wingi mkoani Kagera na kuchangia katika maendeleo ya mkoa.
2.ALIZETI
licha ya kwamba zao la Arizeti ulimwa sehemu zenye upungufu wa mvua ila sio kwamba halistawi kwenye maeneo yenye mvua .Mfano zao hili linalimwa Moshi,Kilimanjaro japokuwa kwa uchache.
3.PAMBA
4.UFUTA
5KARAFUU n.k

6.BEI ZA BIDHAA
Mkoani Kagera ni dhairi kwamba bei za bidhaa zipo juu sana.

NINI kifanyike
Ujenzi wa reli utasaidia gharama za usafirishaji kuwa ndogo hivo bei zitashuka
pili,Serikali iharakishe ushirikiano wa jumuiya ya africa mashariki ili biashara uria ifanyike kati ya Kagera na Uganda.

7.BEI YA PETROLI NA DIZEL
Ni ukweli kwamba mkoani Kagera bei ya mafuta hiko juu sana.Bei ya mafuta ndo utabiri gharama za maisha ziwe juu au chini.

nini kifanyike
ujenzi wa reli
pili ifanyike tathimini tena ili bei ya bidhaa hii adimu iwe chini kiasi

8.UWEKEZAJI
uwekezaji ktk mkoa kagera bado uko chini licha ya kuwepo rasilimali nyingi

nini kifanyike
zitatuliwe changamoto zoto nilizozielezea hapo juu ili kuvutia wawekezaji

9.UVUVI
Hii ni kazi nyingine muhimu mkoani Kagera laikin bado uvuvi uko chini sana ukilinganisha na Mwanza.

nini kifanyike
Taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali ziwaelimishe wqananchi juu ya uvuvi wa kisasa.
Pia changamoto za usafiri na usafirishaji zitatuliwe

10.SIASA
Mkoa kagera ni mkoa uliotawaliwa na siasa za kijani ukiachana na jimbo la bukoba mjini.
Niliwahi kusema kwamba ili mkoa wa KAGERA uendelee hauitaji CCM wala CHADEMA. Nikaenda zaidi nikasema kuwa si CCM wala CHADEMA zitakazoleta maendeleo kwa Kagera.

Lakini siku zote mkoa ukiwa chini ya chama kimoja uwa unasahauliwa kwaiyo nishauri kwamba kwa kuwa mkoa huu umekuwa chini ya kijani na bado unarudi nyuma kimaendeleo basi ni bora kuwaajibisha hawa kijani ili wajifunze wananchi wanataka nini.

ahsante
Yep
 
Kwa wote wanaotaka kushiriki shindano la Stories of Change Tafadhali someni kwa makini vigezo hivi. Hakikisha andiko lako limekidhi kabla ya kutaka kuchapisha.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  1. Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko kwenye nyanja za Elimu, Uchumi, Kilimo, Utawala, Afya, Sayansi na Teknolojia.
  2. Andiko liwe kwa Kiswahili lenye maneno yasiyopungua 800 na yasiyozidi 1000.
  3. Makala zinatakiwa kuwa habari au makala halisi zisizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Plagiarism (Wizi wa machapisho mengine) haitaruhusiwa.
  4. Mshiriki anaweza kutumia jina la kubuni ‘pseudonym’ lakini atatakiwa kutoa taarifa binafsi (jina) endapo ataibuka mshindi.
  5. Matumizi ya picha au video yanaruhusiwa ili kushibisha andiko. Endapo picha na video sio za mshiriki, atalazimika kutaja chanzo.
  6. Watendaji wa Jamii Forums na ndugu zao wa karibu hawaruhusiwi kushiriki kwenye shindano hili.
Asante kwa ufafanuzi.
 
Habari, kama unapata changamoto ya kutuma (post) makala yako basi fanya hivi;
1. Nenda kwenye menu (kushoto, pembeni ya neno JAMIIFORUMS) halafu bofya (click) hapo
2. Chagua start discussion
3. Chagua "Stories Of Change"
4. Hapo utapata uwanja wa kuandika chapisho lako.

Unaweza pitia chapisho langu lenye kichwa kisemacho "KUTOKA KUAJIRIWA MPAKA KUJIAJIRI"

Nipo tayari kwa mjadala na pia naomba kura yako.
 
Back
Top Bottom