JamiiForums
JF Official Account
- Nov 9, 2006
- 6,229
- 5,285
Kwa wote wanaotaka kushiriki shindano la Stories of Change Tafadhali someni kwa makini vigezo hivi. Hakikisha andiko lako limekidhi kabla ya kutaka kuchapisha.
Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
- Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko kwenye nyanja za Elimu, Uchumi, Kilimo, Utawala, Afya, Sayansi na Teknolojia.
- Andiko liwe kwa Kiswahili lenye maneno yasiyopungua 800 na yasiyozidi 1000.
- Makala zinatakiwa kuwa habari au makala halisi zisizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Plagiarism (Wizi wa machapisho mengine) haitaruhusiwa.
- Mshiriki anaweza kutumia jina la kubuni ‘pseudonym’ lakini atatakiwa kutoa taarifa binafsi (jina) endapo ataibuka mshindi.
- Matumizi ya picha au video yanaruhusiwa ili kushibisha andiko. Endapo picha na video sio za mshiriki, atalazimika kutaja chanzo.
- Watendaji wa Jamii Forums na ndugu zao wa karibu hawaruhusiwi kushiriki kwenye shindano hili.
Upvote
73