Somo la kitunguu saumu: Nguvu yake, tiba na maajabu

Somo la kitunguu saumu: Nguvu yake, tiba na maajabu

Na tatizo la harufu wakati wa tendo la ndoa linakwisha au? Kitunguu ukikiweka mdomoni uwa kinawasha je ukiweka uko hakitawasha?
 
Heeeeeh [emoji15] [emoji15] halafu nani aweke Machine yake huko...yaani kitunguu kinavyowasha vile.!! Hatari [emoji2]
Ila pamoja Dr..ngoja tushauriane na shem hapa...
 
Kwani hospital hakuna Dawa ya uchungu? ndugu zangu.Mimi sipingi tiba za hospital na ht baadh ya wagonjwa wanapokuja kwangu uwa nawarudisha hospital na wengine huwa siwatibu mpk wanionyeshe vyeti vya hospital nijiridhishe.Sasa kama tunashangaa kitunguu swaumu mbona hatushangai wake zetu kuingizwa mikono ukeni na madr wakiume wewe ukiwa nje ya chumba cha Dr ukimsubiria mkeo. Au nasema Uongo? tiba zilw tunaona poa tu
 
Awali nilieleza namna ya kujitibu tatizo la fanagas ukeni lakini kwanini kitunguu hiki kimekuwa ni dawa?

Ndani ya kutunguu kuna aina kadhaa ya mafuta yenye kulipuka (volatile oils)kama allin, allinase,na allicin.pia ndani yake kuna diallyle. disullphide,selenium na vitamin A,B,C na E Mchanganyiko wa mafuta yenye kulipuka Dawa hizo pamoja na muunganiko wa compound za salfa ndio vitu vyenye kuvifanya vitunguu swaum kuwa na harufu iliyonayo na uwezo wa kutibu magonjwa TUTAENDELEA
 
Mods Ipelekwe Jf Doctor Ikaunganishwe Na Thread Mama Inayozungumzia Faida Za Kitunguu Swaum
Itasaidia Kufuatilia Thread Moja Ilishiba
 
Ni kweli kitunguu saumu kinatibu BAWASILI?

TIBA YAKE IKOJE?


ngoja nisaidie kujibu., inatibu bawasiri tena kwa 100 percent ila unachukua kitungu swaumu unatwanga au unasaga kisha unachanganya na ndimu hlf unapaka hapo kweny kidude il wanasema inauma.

kutokana n hathar za uzaz nikapata bawasiri jaman inauma smtms inawasha vby mpk unapagawa nikanunua mafuta ya nyonyo/castor oil ndo napaka siku hizi kuwasha kumeacha na hata hichi kidude nahisi kabisa kinapungua ukubwa yan nahis naanza kuwa mormal.

Ila hiyo ya kitunguu sijawahi kutumia
 
Chukua asali,kama lita hivi changanya na tangawizi iliyosagwa kama nusu kikombe kidogo,na vitungu swaumu vilivyopondwa, kisha changanya kwa na unga wa black seed pamoja,kila siku ule mchanganyiko wake kwa siku mara tatu kila wakat kijiko kimoja,aisee utakua na uso unaovutia,yaani uso mwororo,matatizo ya moyo,kinga mwilini,kwa marijali ndo usiseme,na pia mchanganyiko huu unaondoa uchawi kama umewahi lishwa kwa kuuozesha
 
KITUNGUU swaum ni mmea unaojulikana kitaalam kwa jina la ALLIUM SATIVUM Unaojumuisha. jamii za mimea ya KITUNGUU swaum,vitunguu maji,na vitunguu mboga.Ukiwa na historia ya kutumiwa na binadam kwa zaid ya miaka 7000 mmea wa kitunguu swaum una asili ya ASIA Ya KATI sasa twende kwenye tiba yake

Wapo dada zangu wengi sana ambao wanasumbuka na matatizo ya fangas haswa maeneo ya ukeni imefika wakati madada hawa wamekata tamaa juu ya tatizo hilo kwa kuwa wametumia dawa mbalimbali na hawajapona

TATIZO HILO HUTOKANA NA NINI?

(1)MAAMBUKIZI Kufanya mapenzi kiholela Watu hukimbilia kupima ukimwi tu wakiamin ndio gonjwa bays

(2)KUPENDELEA SANA KUVAA NGUO ZA KUSHIKA MWILI HASWA ZILE ZA MPIRA

(3)KUTOBADILISHA NGUO ZA NDANI KWA MUDA MREFU

HIZO NI MIONGONI MWA SABABU ZA TATIZO HILO


UNATUMIAJE KITUNGUU SWAUM KUONDOA TATIZO HILO?

Chukua punje moja ya vitunguu swaum kisha utaisaga na kuwa laini kabisa.Kisha utaizungushia katika kitambaa laini cha kufungia vidonda bandeji (GAUZE)baada ya kuizungushia ndani ya kitambaa hiko ingiza katika njia ya uke na kuiacha kwa masaa 8 hadi 12 kisha ubadilishe tena na kuweka nyingine. Tumia tiba hii kwa siku 2 mfululizo na tatizo la FANGASI au MUWASHO ndani uke litakwisha

HASANTENI
Mkuu je ukiwa mjamzito tiba hii inafaaa kutumiwa na mama mjamzito?
 
Back
Top Bottom