YESU aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Nyinyi ndio chumvi ya dunia.” (Mathayo 5:13) Nao Waarabu husema kwamba, “Kuna chumvi kati yetu,” na Waajemi husema kuhusu “asiye wa kweli kwa chumvi” (asiye mwaminifu au asiye na shukrani). Kwa kuwa chumvi inaweza kuhifadhi vitu, neno “chumvi” limeheshimiwa na kustahiwa katika lugha za kale na hata za leo.
Chumvi pia imekuwa alama ya uthabiti na udumifu. Hiyo ndiyo sababu, katika Biblia agano muhimu liliitwa “agano la chumvi,” na wale waliokubaliana mara nyingi walikula mlo pamoja, uliotiwa chumvi ili kuidhinisha agano hilo. (Hesabu 18:19) Chini ya Sheria ya Musa, chumvi ilitiwa kwenye matoleo madhabahuni, bila shaka ikionyesha hali ya kutokuwa na ufisadi au uharibifu wowote.
Jr[emoji769]