Uchaguzi 2020 Songwe: Dkt. Magufuli afanya kampeni Tunduma, afuta tozo ya mama kamandoo

Uchaguzi 2020 Songwe: Dkt. Magufuli afanya kampeni Tunduma, afuta tozo ya mama kamandoo

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Dkt. Magufuli anaendelea na kampeni mkoa wa Songwe na sasa yuko Tunduma.

MAGUFULI: Ninafamu kuna kero moja kwa kinamama inaitwa kampeni ya mama kamandoo ambapo wamama wanapochelewa kwenda kliniki wanatozwa 50,000. Naifuta leo moja kwa moja hiyo tozo.

Kwa hiyo pasitokee mtu yoyote kutoka wizara ya afya au mahali popote anawatoza kina mama hawa wajawazito ati kwa sababu wamechelewa kliniki, kumtoza elfu hamsini ni kumuonea mwanamama huyu ambae anahangaika miezi tisa tumboni.

Kwa hio kina mama pateni mimba zenu, nendeni mkajifungue sawasawa. Wewe mama umemuona ni mjamzito, wewe unaenda kumtoza elfu hamsini, ulimpa wewe mimba?

Kamandoo aende shambani akalime au afanye biashara nyingine. Mtu unachelewa kwenda kliniki unatozwa elfu hamsini wakati mikoa mingine hawatozwi. Hili nasema hapana kwa hio marufuku kuanzia leo.

Nilileteeni Silinde, alikuwa CHADEMA kwenye jimbo la Momba, alipokuwa kule CHADEMA alijua uozo uliomo humo akawa kila mara anabembeleza, anasema baba nimechoka niko radhi nipoteze ubunge lakini nihamie CCM hata kama nitakuwa karani, nikamshangaa kijana huyu ambae alikuwa yuko radhi apoteze mishahara na fedha za ubunge kwa ajili ya maslahi ya watu.

Alichaguliwa na wabunge wa CCM kuwakilisha katika bunge la Afrika, kijana mdogo jasiri aliye na upendo wa kweli. Alikuwa agombee Momba, nikamwambia nenda kanisaidie Tunduma kwa sababu ndio pana changamoto nyingi kubwa.

Nileteeni Silinde alafu mje mniulize maji ya hapa na ukweli nimeshaanza kuipanga hiyo miradi, tunataka tuyatoe maji Ileje yateremke mpaka hapa Tunduma, mtakunywa mpaka mtachoka.

Lakini msinichanganyie, mkiniletea hao, nasema maji hamyapati. Lazima tuambizane ukweli na mimi nazungumzaga ukweli.
 
Rais Magufuli amesema hivi ''Najua viongozi wa Serikali mnanisikia, Wizara ya Afya mnanisikia na mimi mpaka leo bado ni Rais. Kampeni ya Mama Kamandoo ni marufuku kuanzia leo, kwa hiyo wakina mama bebeni mimba zenu vizuri tuongeze idadi ya Watanzania''

Dkt. Magufuli ameongeza kuwa ''Kuna malalamiko dhidi ya kampeni ya Mama Kamandoo kuwatoza wanawake wajawazito wanaochelewa kujiandikisha kliniki Tsh. 50,00. Hii kampeni naifuta leo, kwahiyo Mama Kamandoo aende shambani akalime Mahindi aachane na tabia ya kutoza kinamama''
 
Ni wakati akiomba kura Tunduma na kumwagiza RPC kuwakamata watumishi wote watakaotoza tozo hii ya Sh. 50,000/=.
 
Hapo Magufuli amefanya jambo la maana sana
JPM wakati anapambana na Lowassa alipiga push-ups nyingi mara kadhaa, ulifahamu maana yake? Dhihaka kwa Lowassa kuhusu afya yake. Rhetorical language.

Wakati huu anapambana na amepigishwa magoti mara mbili akiomba kura, unajua maana yake??

Mataga Tafuta thamani ya X......
 
Dr Magufuli amesema mara ya mwisho alipokuja Tunduma wafuasi wa Chadema walimshangilia sana na hiyo inamaanisha kuwa maendeleo hayana vyama.

Magufuli amesema Silinde alikuwa anambembeleza toka akiwa Chadema kwamba anaomba ahamie CCM hata kama atapoteza ubunge.

Silinde alikuwa agombee Momba lakini nikamwelekeza agombee Tunduma kwa sababu kuna changamoto nyingi amesema Dr Magufuli.

Maendeleo hayana vyama!
 
JPM wakati anapambana na Lowassa alipiga push-ups nyingi mara kadhaa, ulifahamu maana yake? Dhihaka kwa Lowassa kuhusu afya yake. Rhetorical language.

Wakati huu anapambana na amepigishwa magoti mara mbili akiomba kura, unajua maana yake?

Mataga Tafuta thamani ya X......
 
Arudishe 50k niliyolipa mwezi uliopita
 
Hakujua haya ndio kayafahamu leo?

Pili hio ilikuwa Tozo ili waongeze kipato au ilikuwa kama fine / kitisho ili wasichelewe kwenda Kliniki hence kumsaidia kiumbe (mtoto) asipate matatizo sababu ya uzembe wa aina yoyote? (sijui sijafanya research ila wakati mwingine tujiulize kwanini walifanya vile kabla)
 
Back
Top Bottom