Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

Kati ya mambo ambayo CCM watajutia ni hili la kuwafukuza na kuwavua uanachama ambao walikuwa wanachama wake.......Busara haikutumika, watundani ya chama wanatakiwa kuwa wavumilivu, kuelezana ukweli bila fitina pale mtu anapokosea na hatimae kuwa wamoja kwa kuwapa majukumu ya kuimarisha Chama kwani Mchawi mpe mtoto amleeeee.........lakini kwa hali hii ya kufukuzana wanakidhoofisha chama na wanachama hao wanaofukuzwa ni Mtaji kwa vyama vingine.............
 
wewe nawe mzigo!
unajua Sophia alipomuimbia Lowasa ilikuwa kabla EL hajahama CCM?
Unajua kuwa mwenyekiti wa wakati huo alitaka kuwaburuza wajumbe na kumuweka mgombea wake bila ya kujali utashi wa wanachama wote? je ni dhambi kumpinga mwenyekiti pale unapohisi amekosea?

Hebu wewe tufafanulie unachokiita usaliti toka kwa SOPHIA SIMBA ni kipi?
unadhani kwa nini akina Nchimbi hawakufukuzwa uanachama? Sophia simba mpaka leo ni mtiifu kwa Lowasa na bado anampinga Rais lakin Nchimbi alijirekebisha
 
Ule wimbo wa tuna imani na Lowasa kumbe uliwakera sana eh..nimesikia leo mkuu akiongelea😀😀😀😀😀😀😀
 
unadhani kwa nini akina Nchimbi hawakufukuzwa uanachama? Sophia simba mpaka leo ni mtiifu kwa Lowasa na bado anampinga Rais lakin Nchimbi alijirekebisha
kwani mtu aruhusiwi kumpinga raisi!
He is not perfect, sio yeye tu, wapo ccm wengi wanaompinga labda wanaona hawapi tumaini walitakalo, ni insecurity tu inayowasumbua otherwise kupingwa katika siasa ni jambo la kawaida sana!
 
Najaribu tu kuwaza kimya kimya hivi kama vyama vya siasa vingekuwa na utaratibu wa kuuziana wanachama kama vilabu vya mpira wa miguu vinavyofanya hali ingekuwaje? Je CCM ingewafukuza akina sophia, madabida n.k au wangewauza tu Kwa mkopo kwa TLP ACT-WAZALENDO au PONA?
 
mimi itabidi tu nikae kimya...kama wanachama wenzangu wanafukuzwa ovyo hivi mimi nitaponea wapi? tatizo mwenyekiti wetu hashauriki na wala hapingiki. kuwafukuza wanachama wenye nguvu kama sofia simba kutakipasua chama chetu.

Umekuwa mkweli..we kama unapenda kubaki CCM tulia tuliii hata ukiona ndivyo sivyo maana watakufurumusha!!
 
Madabida alikuwa Team Mwembe kwa Muda mrefu sana Akaja kuwa team Lowassa Mwishoni
 
Mageuzi haya yasiposimamiwa vizuri yatakiua chama na kukuzika rasmi ...
Kama CCM haikufa pale alipoondoka Nyerere,alipoondoka mwanachama mwenye kadi namba 5 ambae ni Kingunge,akaondoka mzee mzima LOWASSA!!na bado chama hakikufa!basi CCM haitokufa kwa kufagia wanachama wasaliti na wanafiki kama Sophia na wenzie kina Madabida!!
Waende!!Vijana tulikosa nafasi ndani ya CCM kwa ajili ya watu kama hawa kung'ang'ania madaraka..
Wacha watoke nasie tuingie!!
 
kwani mtu aruhusiwi kumpinga raisi!
He is not perfect, sio yeye tu, wapo ccm wengi wanaompinga labda wanaona hawapi tumaini walitakalo, ni insecurity tu inayowasumbua otherwise kupingwa katika siasa ni jambo la kawaida sana!
ni nani ndani ya CHADEMA anaempinga MBOWE? hebu nitajie hata mmoja mkuu kama kupingwa ni kawaida sana.....
 
Madabida akithubutu kwenda CDM ajue kesi ya ARV's feki itapamba moto,TRA watamwangukia kama mwewe,na atanyang'anywa kiwanda cha madawa Arusha

Bashe nao Maafisa Uhamiaji wanapasha kusubiri kuingia uwanjani
 
Kama CCM haikufa pale alipoondoka Nyerere,alipoondoka mwanachama mwenye kadi namba 5 ambae ni Kingunge,akaondoka mzee mzima LOWASSA!!na bado chama hakikufa!basi CCM haitokufa kwa kufagia wanachama wasaliti na wanafiki kama Sophia na wenzie kina Madabida!!
Waende!!Vijana tulikosa nafasi ndani ya CCM kwa ajili ya watu kama hawa kung'ang'ania madaraka..
Wacha watoke nasie tuingie!!
sawasawa ni muda wetu vijana na sisi tushike madaraka ndani ya chama akina Sophia na unafiki wao waende kwa bosi wao wa CHADEMA
 
MAdabida ndiye akihusika na ei ara vii feki au nimekosea?
 
Kuanzia j3 CHADEMA tunaanza kuweka sherehe ya kupokea wanachama wapya na makapi yaliyotupwa na CCM karibun nyooote tusherekee
 
Ile kauli imetimia "unajua wewe mzee mpole sana yaani watu wanaimba kabisa sijui wanamtaka nani lakini ukawaangalia tu, ningekuwa mimi...."
 
Back
Top Bottom