Special thread: Mgogoro kati ya Urusi na NATO
 
China imeweka wazi kuwa haitahudhuria mkutano wa Ukraine Peace Conference utakaofanywa nchini Switzerland June 15-16, 2024

Wajumbe 160 wamealikwa kwenye mkutano huo kutoka nchi za G7, G20 na BRICS. Lakini Russia haikualikwa.

Sababu ya China kukataa kuhudhuria mkutano huo ni kutoalikwa kwa Russia.

Wanadiplomasia wa China wanasema ikiwa Russia wangealikwa kwenye mkutano huo basi kungekuwa na ushiriki sawa wa pande zote na majadiliano ya haki.
 
Maandamano ya amani huko Budapest, Hungary makumi ya maelfu wakiandamana kupinga ushiriki wa NATO katika vita hivyo.

Harakati za amani zinazokataa kuwa "silaha ni njia ya amani" na badala yake zinataka kurejea kwa diplomasia na mazungumzo.

20240602_210253.jpg
 
Alichosema Zelensky kwenye Shangri-La Dialogue nchini Singapore

Zelensky: "Xi Jinping aliniahidi China itasimama kando na haitaiunga mkono Urusi kwa silaha. Lakini, leo dalili kutoka kwa huduma za kijasusi, zikiwemo zetu kwamba kuna silaha zinaenda nchini Urusi kutoka China. Baadhi ya silaha zinatoka China."

Zelensky:
"Kwa sababu ya uungaji mkono wa China kwa Urusi, vita vitadumu kwa muda mrefu zaidi. Hii ni mbaya kwa ulimwengu wote."
 
Vipande vya kombora la Kimarekani la GMLRS lililorushwa na Jeshi la Ukraine vilivyopatikana katika eneo la Belgorod nchini Urusi baada ya kupokea kibali kutoka kwa Biden kutumia aina hizi za silaha kwenye maeneo ya Urusi.

Kwa sasa, Marekani bado haijaruhusu matumizi ya makombora ya masafa marefu ya ATACMS.

20240602_214523.jpg
20240602_214526.jpg
 
Uzi huu unaangazia kile kinachoendelea kuhusu mgogoro ulioibuka sasa wa NATO na Russia katika vita vya Ukraine.

Ikumbukwe kuwa katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg, alitaka silaha za misaada kwa Ukraine sasa zianze kutumika kushambulia moja kwa moja ndani ya mipaka ya Russia hasa miltary targets. Kitaalamu mashambulizi haya yanaitwa long range strikes.

Tangu NATO wakubaliane kuhusu hilo, dunia ilikuwa ikisubiria tamko kutoka Moscow.

Hatimaye aliyewahi kuwa raisi wa taifa hilo ambaye kwa sasa ni deputy chief of Russia’s Security Council, Dmitry Medvedev amezungumza haya kufuatia tamko la NATO

Medvedev: "Nchi za Magharibi, ambazo zinadaiwa kuidhinisha matumizi ya silaha zao za masafa marefu kwenye eneo la Urusi (bila kujali kama inahusu sehemu za zamani au mpya za nchi yetu), lazima zielewe yafuatayo:

1. Vifaa vyao vyote vya kijeshi na wanajeshi wanaopigana dhidi yetu vitaharibiwa katika eneo la Ukrainia na katika maeneo ya nchi nyingine ikiwa mashambulizi yataanzishwa kutoka huko dhidi ya eneo la Urusi.

2. Urusi inatambua kwamba silaha zote za masafa marefu zinazotumiwa na Ukraine kwa sasa zinadhibitiwa moja kwa moja na wanajeshi wa NATO. Huu sio msaada wa kijeshi bali ni kushiriki katika vita dhidi yetu.

3. Msaada wa taifa moja moja kama huo kutoka kwa nchi za NATO dhidi ya Urusi, iwe ni kudhibiti makombora yao ya masafa marefu au kutuma wanajeshi Ukraine, itaongeza mzozo huu. Ukraine na washirika wake watakabiliwa na jibu la nguvu.

4. Baadhi ya maafisa wa NATO wanazungumza kwamba Urusi haitatumia silaha za nyuklia zisizo za kimkakati dhidi ya Ukraine achilia mbali nchi za NATO. Maisha yanaweza kuwa mabaya zaidi kuliko mawazo yao ya kipuuzi."


Kuna kauli nzito ambayo ameiotoa kama red alert
"West risks miscalculating the chances of nuclear weapons being used."

Tumebaki tukisubiri hatma na kupata majibu ya maswali haya:

Je, NATO wataogopa baada ya kauli hizo thabiti kutoka kwa Russia na kuachana na mpango wa silaha zao zitumike kushambulia ndani ya mipaka ya Russia?

Silaha za NATO zikitumika kushambulia ndani ya mipaka ya Russia, je, Russia watafanya kama alivyosema Medvedev?

Je, tutapata maana ya hii kauli ya Medvedev "West risks miscalculating the chances of nuclear weapons being used."

Je, itakuwa mwanzo wa vita kuu ya tatu ya dunia na kushuhudia matumizi ya silaha hatari za nyuklia?

Acha tuone yatakayojiri kwa updates mbalimbali.



VIONGOZI WA NCHI ZA MAGHARIBI WAKUTANA MADRID, SPAIN KUFANYA MKUTANO WA SIRI MOJA YA AJENDA KUIZUNGUMZIA RUSSIA

Wakati sintofahamu ikiendelea kati ya Russia na NATO na suala la geopolitical kati ya mataifa mawili yenye uchumi mkubwa duniani Marekani na China likiendelea kufukuta.

Wawakilishi wachache walialikwa kutoka Marekani, nchi wanachama wa NATO zilizopo Ulaya na Ukraine walikutana tarehe May 30–June 2, 2024 katika jiji la Madrid, kwenye hotel ya Eurostars Suites Mirasierra.

Mkutano unaisha leo lakini hakuna mainstream media yoyote imeutangaza, ndio ujue usiri wa mkutano huu ulivyo mkubwa. Kwani waalikwa huapa kwamba watahakikisha yaliyojadiliwa yanabaki kuwa siri.

Mkutano huu hufanywa kila mwaka tangu mwaka 1954 ulipoanzishwa. Unaitwa the Bilderberg Meeting. Wajumbe huwa ni political and business elites.

Ni mkutano wa siri ambao hakuna nafasi ya waandishi wa habari kualikwa hivyo hakuna taarifa yoyoye itakayotolewa baada ya mkutano huo na vyombo vya habari.

Ajenda za mkutano wa mwaka huu zilikuwa:
●Russia
●China
●Middle East
●Ukraine and the world
●State of AI
●AI Safety
●Changing Faces of Biology
●Climate
●Future of Warfare
●Geopolitical Landscape
●Europe's Economic Challenges
●US Economic Challenges
●US Political Landscape

Kwa nini Russia, China na Middle East ziwe ajenda kwenye mkutano huo?

Tuuachie muda nafasi tutapata jibu la swali hilo.

Ikumbukwe pia hivi karibuni raisi wa China aliwaalika viongozi wa nchi za Kiarabu jijini Beijing kwenye mkutano wa China-Arab Forum.

Pia ni ndani ya kipindi kisicho kirefu Xi na Putin walifanya mazungumzo jijini Beijing.

Miongoni mwa wahudhuriaji waliolikwa kwenye mkutano huu wa siri ni pamoja na:

●US Deputy Treasury Secretary Wally Adeyemo
●US Deputy National Security Advisor Jonathan Finer
●Finnish President Alexander Stubb ●European Council President Charles Michel
●NATO Secretary General Jens Stoltenberg,
●Prime ministers of the Netherlands and Estonia
●Foreign ministers of Spain, Ukraine, Sweden, and Poland
●The deputy prime minister of Ireland.

From the world of business:
●Pfizer CEO Albert Bourla
●BP CEO Murray Auchincloss
●Former Google CEO Eric Schmidt
●Several AI executives from Google, Microsoft, and Anthropic
PBC
Time will tell
 
Alichosema Zelensky kwenye Shangri-La Dialogue nchini Singapore

Zelensky: "Xi Jinping aliniahidi China itasimama kando na haitaiunga mkono Urusi kwa silaha. Lakini, leo dalili kutoka kwa huduma za kijasusi, zikiwemo zetu kwamba kuna silaha zinaenda nchini Urusi kutoka China. Baadhi ya silaha zinatoka China."

Zelensky: "Kwa sababu ya uungaji mkono wa China kwa Urusi, vita vitadumu kwa muda mrefu zaidi. Hii ni mbaya kwa ulimwengu wote."
KABLA ya vita ilitakiwa Mr Zerensiky aingie google kutazama nafasi ya Urusi Kijeshi.
 
Umefika wakati inatakiwa hivi vita vya kijinga vimalizike sasa na dunia isonge mbele.
 
Alichosema Zelensky kwenye Shangri-La Dialogue nchini Singapore

Zelensky: "Xi Jinping aliniahidi China itasimama kando na haitaiunga mkono Urusi kwa silaha. Lakini, leo dalili kutoka kwa huduma za kijasusi, zikiwemo zetu kwamba kuna silaha zinaenda nchini Urusi kutoka China. Baadhi ya silaha zinatoka China."

Zelensky:
"Kwa sababu ya uungaji mkono wa China kwa Urusi, vita vitadumu kwa muda mrefu zaidi. Hii ni mbaya kwa ulimwengu wote."
Huyu nae kunya anye Bata akinya kuku kahara yy mbna anaomba wazwaz anategemea nini?..kila mtu na washirika wake other wise wakae chini wayamalize kwa sababu n ndg.
 
Inchi za ulaya zimepanic kila wakiipa Ukraine msaada hausaidii kitu sasa wameona bora waipe ukraine ruhusa ya kutumia silaha zao ndani kabisa ya ardhi ya urusi na putin amesha onya

na kusema inchi zao zina maeneo madogo kijiografia

Hapa waafrica tujianda kupokea wakimbizi wengi kutoka ulaya
NATO wslizingua kitambo kwa kumfunga mikono Ukraine. Tangu mwanzo walitakiwa kumpa silaha na kumuacha azitumie kwa uhuru.
 
Binafsi napenda sana vita,VITA INALETA HESHIMA NA AMANI YA KUDUMU, nilikuja gundua Demokrasia iliishashindwa. Ili kuweka mambo sawa inabidi wapigane kwanza, kisha tutafanya tathmini baadaye. Kwasasa kuzungumza kutafuta suluhu ni uongo, vita hiyo hai epukiki.

Cha msingi tujuzwe wanaanza lini kutwangana, tutapata shida lakini ikiisha tutatulia muda mrefu sana bila vita. Na ikiwa huu utakuwa mwanzo wa vita kubwa, basi na iwe, maana imeshaonekana hakuna suluhu, bora kuanza mapema tufahamu kuna vita.

Akishinda Russia, hakutatulia duniani itabidi tuhamishiwe Mars kwa muda mpaka hali itakapo kuwa shwari.
 
Kwanza Nashangaa Hivi Urusi inashindwa nini kumalizana na huyu Msanii halafu itulie kwanza mana yuko tu anajificha poland pale KGB imalizane nae kwanza
malengo ya SMO yalikua ni denazification na demilitarization,

ili ufikie malengo hayo unatakiwa kuwaondoa wanajeshi, sasa utawapunguzaje ukiamua kupiga vita vya kimaangamizi kama anavyofanya US?

mpk leo jeshi la ukraine lipo kwenye breaking point, wamekufa wanajeshi wengi mnoo kiasi saizi wanahangaika na kukamata wanaume wote waende jeshini, hii maana yake russia anafanikiwa ktk lengo lake la kuwamaliza wanajeshi wa ukraine (wear them down),

kwa sasa ni mercenaries wa nato ndio wapo kwa % kubwa,
 
Wao wa Rusia hawafi?

Ni kwamba West wanaenda kwa mahesabu katika hii vita. Kubwa zaidi ni kumdumaza Putin kiuchumi na hilo haliwezi kutokea kwa ghafla.
Subiri miaka 5 ijayo uone vilio kutoka kwa Putin.
malengo ya SMO yalikua ni denazification na demilitarization,

ili ufikie malengo hayo unatakiwa kuwaondoa wanajeshi, sasa utawapunguzaje ukiamua kupiga vita vya kimaangamizi kama anavyofanya US?

mpk leo jeshi la ukraine lipo kwenye breaking point, wamekufa wanajeshi wengi mnoo kiasi saizi wanahangaika na kukamata wanaume wote waende jeshini, hii maana yake russia anafanikiwa ktk lengo lake la kuwamaliza wanajeshi wa ukraine (wear them down),

kwa sasa ni mercenaries wa nato ndio wapo kwa % kubwa,
a
 
Back
Top Bottom