Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Lisu ameshindwa kuisaidia chadema kupata ofisi ya chama alafu eti anadai ana uchungu na Tanzania!!!
 
Kwani kabla ya magufuli kununua ndege watu walikua wanapanda bajaji kwenda marekani?

Tunazungumzia hizo pesa alizonunua hiyo midege kulikua hakuna umuhimu wowote kuunguza pesa kwa ajili ya midege ambayo asilimia 80 ya wananchi hawajui hata nauli yake.

Hizo pesa angeweza kuzitumia kufanya miundombinu itakayo mnufaisha mwananchi wenye hali ya chini. Mtu anaye panda ndege kwenda nchi za kimataifa huwezi kumuweka kwenye kundi la watu maskini ambao milo mitatu kwao ni shida.
Kwani uliambia magufulia ameacha kutengeneza miundo mbinu ? Ndege tume nunua na miundo mbinu tunatengebeza.
 
CCM mna laana nyie. Magufuli yuko kanda ya Ziwa Victoria ambako usiku wa kuamkia leo malaika wadogo wamepoteza maisha kwakuunguzwa na moto (kwakuunguzwa na moto) huko Kagera.

Ila bado wako jukwaani na wasanii wanakata mauno. Hivi hawana hata chembechembe ya huruma? Hata tamko hakuna wakati ndo wenye mamlaka?

Kwanini ndani ya muda mfupi hii ni shule ya tano ya Waislam kuwaka moto?
Kwanini Rais asionyeshe msisitizo hata kwa unafiki kukemea jambo hili na kuagiza suluhisho la haraka?

Yeye kujibu hoja za Lissu anaona sifa ila kuwaza wanetu wanaochomwa kama mishkaki mabwenini hataki hata kuwaza.
Iko Siku Mungu atashuka mwenyewe.
Ijumaa msafara wa Rais ukitoka mji wa Geita kuelekea chato , uligonga mtoto mdogo eneo la chibingo nje kidogo ya mji wa katoro na alifariki papo hapo. Unaambiwa msafara haukusimama na hakuna msemaji aliyesema kitu Hadi Sasa na mtoto amezikwa kimya kimya . Ccm Wana laana
 
Ijumaa msafara wa Rais ukitoka mji wa Geita kuelekea chato , uligonga mtoto mdogo eneo la chibingo nje kidogo ya mji wa katoro na alifariki papo hapo. Unaambiwa msafara haukusimama na hakuna msemaji aliyesema kitu Hadi Sasa na mtoto amezikwa kimya kimya . Ccm Wana laana
Innaa liLlaah wa innaa ilayh rajiu'wn

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app[/color]
 
Naona awamu hii Dr Magufuli amedhamiria kujibu mapigo ya washindani wake moja kwa moja.

Mosi, huwezi kuongoza nchi bila kutoza kodi msidanganywe.

Pili, ndege zimenyanyua mapato ya utalii hata huyo anayebeza ndege za ATCL aliporudi nchini alipanda bajaj?!

Kiukweli sasa ndio kampeni zimeanza rasmi.

Maendeleo hayana vyama!
Nimemuonea huruma Magufuli anavyomchokoza Lissu, jamaa likishusha nondo tena uvccm muanze kuhangaika mitandaoni. Mwambieni Bashiru anapowaagiza kujibu hoja amshauri na mzee apunguze kuongelea kila kitu. Akuoneeni huruma.

Halafu nimeamini nondo za Lissu zinamkita moja kwa moja na ni kweli zinamtesa sana! Anaongea kwa hasira sana na anaonesha kuteseka, eti "vitu vingine wanaongea vinaudhi sana!!!" Na bado, tuna siku 44 mbele.
 
Screenshot_20200914-132227_Chrome.jpg

Screenshot_20200914-134524_Chrome.jpg


Wakuu wa kazi hebu naombeni sana tulijadili hili jambo kwa weledi na ufasaha. Tujadili namna Mgombea wa CCM anavyofanya counter argument kwenye sera za wenzine. Namna anavyojenga hoja na kuonyesha yeye ni bora.

Mimi naona kama ukimtoa Magufuli umeweke chama kingine mfano UDP kwa namna anavyojenga hoja zake basi ataonekana mgombea kituko kuliko wote
 
Wakati Rais Magufuli anaomba kura alituambia angeibadilisha nchi kuwa ya viwanda, kuleta ajira na kukuza Uchumi wa nchi.

Lakini tangu aanze kampeni sijamsikia tena akizungumzia viwanda na wala kutuambia amejenga wapi viwanda na vimetoa ajira kiasi gani? Kipindi cha kampeni atukuahidiwa ndege wala reli ya kisasa, ili kuwa ni Tanzania ya viwanda.

Ni wakati sasa wa Rais kutuambia viwanda amejenga vingapi na vimetoa ajira kiasi gani?

Vinginevyo tulidanganywa na sasa anatudanganya.
 
CHAMA CHA MAPINDUZI CCM.
chama kimepoteza uhalali wa kushika dola
Hawa jamaa wamezoea Uongo uongo.
1. Tanzania ya viwanda Haipo.
2. SGR Anasema tunajenga kwa fedha zetu muongo.
3. Anasema maendeleo hayana vyama alafu anasema msiwachague viongozi wa upinzani muongo.
4Juzi amesema Nyererealitawala miaka 27 uongo.
Wamejaa uongo.
 
Katibu 2018 nae akaja na uongo wake alisema CCM haiwezi ikawaalika wasanii kwenye kampeni 2020 kila kona fiesta.

Katibu anatudanganya eti magufuli hataongeza Muda ni uongo.

Wamejawa na uongo
 
Kampeni zinaendelea kwa kasi sana, na mambo mengi yanaendelea kila kukicha.
Kuna mengine yanaudhi na mengine yanafurahisha, lakini mwisho wa siku bado nchi yetu ni salama kwa hilo tumshukuru sana Mungu.

Rais Magufuli amekasirishwa sana na majungu anayopigwa juu ya uwanja wa Chato, wengine wanaweza wasipendwe na uamuzi wa uwanja wa ndege pale Chato lakini lazima tujue Chato ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, panastahili kila kitu cha maendeleo.
Mbali na Magufuli kuwa Rais lakini pia ni kama mzazi wa wengi wetu kwa maana ya umri wake hivyo anastahili heshima sana kama wazazi wengine kwa umri wake tu.

Lakini pia bado ni Rais hivyo hata kama ni kumkosoa lazima adabu ifuate mkondo wake.
Kuna msemo kwamba " U DONT KNOW THE VALUE OF WHAT YOU HAVE UNTIL YOU LOSE IT kuna wakati hata kama sio leo tutamkumbuka mzee Magufuli kwa jitihada zake kwa taifa hili hata kama sio sisi wajukuu watasema. Endelea kuchapa kazi John Joseph Pombe Magufuli kuna siku nchi itakukumbuka kwa mema.
 
Kampeni zinaendelea kwa kasi sana, na mambo mengi yanaendelea kila kukicha.
Kuna mengine yanaudhi na mengine yanafurahisha, lakini mwisho wa siku bado nchi yetu ni salama kwa hilo tumshukuru sana Mungu.
Rais Magufuli amekasirishwa sana na majungu anayopigwa juu ya uwanja wa Chato, wengine wanaweza wasipendwe na uamuzi wa uwanja wa ndege pale Chato lakini lazima tujue Chato ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, panastahili kila kitu cha maendeleo.....

Usitupoze wewe majibu bado hapa

  1. Ni faida kiasi gani ndege hizo zinaleta kwa taifa?
  2. Kwanini amehamishia ndege kwenye kasma namba 20 ambayo haikaguliwi na CAG kama ambayo mashirika mengine ya umma yanakaguliwa?
  3. Kwanini hataki kuweka wazi mikataba ya manunuzi ya ndege?
  4. Kama anaweza kusafiri na gari nchi nzima wakati wa kampeni anashindwaje kusafiri kutoka mwanza airport mpaka chato?
  5. Baada ya yeye kumaliza uraisi huo uwanja utatumika kwa kazi gani?
  6. Kwa kuwa makampuni yote duniani hayanunui ndege za abiria kwa hela taslimu ( commercial aircraft leasing agreement ) ili kuweza kumudu mtaji na gharama za uendeshaji. Je biashara hii inaweza kuhimili ushindani sokoni?
  7. Mbona anakuwa anatoa majibu kiukali kwani kuna nini vile?
  8. Asititufokee, lazima ajue sisi ndiyo tunamlipa mshahara na kiinua mgongo mara akistaafu.
 
"U DONT KNOW THE VALUE OF WHAT YOU HAVE UNTIL YOU LOSE IT"

Hii ni kauli ya kweli kabisa lkn it has its exceptions!
Kwa mfano haiwezi kuhold water kwa huyu dikteta wetu.... Jiwe
 
Usitupoze wewe majibu bado hapa

  1. Ni faida kiasi gani ndege hizo zinaleta kwa taifa?
  2. Kwanini amehamishia ndege kwenye kasma namba 20 ambayo haikaguliwi na CAG kama ambayo mashirika mengine ya umma yanakaguliwa?
  3. Kwanini hataki kuweka wazi mikataba ya manunuzi ya ndege?
  4. Kama anaweza kusafiri na gari nchi nzima wakati wa kampeni anashindwaje kusafiri kutoka mwanza airport mpaka chato?
  5. Baada ya yeye kumaliza uraisi huo uwanja utatumika kwa kazi gani?
  6. Kwa kuwa makampuni yote duniani hayanunui ndege za abiria kwa hela taslimu ( commercial aircraft leasing agreement ) ili kuweza kumudu mtaji na gharama za uendeshaji. Je biashara hii inaweza kuhimili ushindani sokoni?
  7. Mbona anakuwa anatoa majibu kiukali kwani kuna nini vile?
  8. Asititufokee, lazima ajue sisi ndiyo tunamlipa mshahara na kiinua mgongo mara akistaafu.
UVCCM kazi kwenu,toeni majibu ya haya maswali acheni kupiga filimbi.
 
Back
Top Bottom