Nimepita sehemu kadhaa ambapo kuna TV na mikutano ya Magufuli ikirushwa Live.
Kitu nilichonotice ni kwamba wananchi wameshakuwa saturated na kumuona Magufuli, yaani wamemuona sana yeye peke yake mpaka sasa hawana shauku ya kumuona wala kumsikiiza sana.
Nimeona watu wakila chakula migahawani huku TV ikirusha mikutano ya Magufuli lakini wananchi wakiwa hawana time nayo.
Sababu kuu huenda ni kuona mtu yuleyule akiwaambia mambo yaleyale tangu kipindi cha kampeni iliyopita ya mwaka 2015.
Ukichukua kameni za Magufuli za mwaka 2015, ukalinganisha na za sasa anaongea almost yaleyale.
Kitu kingine ni wananchi kukata tamaa na utendaji wa Magufuli.
1. Magufuli aliingia madarakani kwa hoja kuu ya kupambana na ufisadi, lakini leo hii tunaona badala ya kukamata mafisadi halisi wale walioingia mikataba ya kifisadi ya madini, tunana akikibizana na wafanyabiashara na kuwaoa kesi za uhujumu uchumi, lakini wakita hela anawaachia.
2. Magufuli alitwambia akina Deo Mwanyika wanashirikiana na Mabeberu wa ACACIA kutuibia kwenye madini, akamfungulia kesi, baada ya miaka mitatu akamfungua na kumpitisha kugombea ubunge jimbo la Mbeya Mjini. Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM iweje awapelekee mgombea fisadi wananchi wa njombe mjini?
3. Kuna matukio chungu nzima ya wagombea wa CCM waliotoa rushwa ili kupata nafasi ya kushika tiketi ya kugombea ubunge kwa chama hicho, TAKUKURU inajua na Magufuli anajua lakini kawapitisha
4. Kuna siasa za biashara ya kisiasa zilifanyika ndani ya miaka hii mitano ya utawala wa Magufuli
5. Magufuli alitutangazia kuwa Andengenye na Lugoa wameinhia mkataba wa kifisadi wa shilingi Trilion 1, baadae akasema amemsamehe Andengenye na akamteua kuwa mkuu wa mkoa.
Kwa hiyo wananchi wakikumbuka yote hayo, wanaona kuwa Hoja ya kupambana na ufisadi ni usanii mtupu
Pia kuna ahadi ambazo Magufuli na CCM mwaka 2015 waliahidi kwa wananchi baadae wakaziruka kimanga
1. Waliahidi milion 50 kila kijiji, hawakutimiza.
2. Wakiahidi kukamilisha katiba mpya, leo hii wanaikama katiba mpya kuwa siyo kipaumbele
Lakini ia kuna kukata taamaa kwa wananchi kwenye masuala ya ukosegu wa ajira, maslahi ya wafanyakazi kutozingatiwa, kuongezeka kwa makato bodi ya mikopo ya elimu ya juu, kusuasua kwa sekta binafsi ambayo ndo inaajiri watu wengi zaidi
Wananchi wakiangalia yote hayo, wanaona kama kampeni za Magufuli kama mchezo wa kisiasa tu, hawaziamini sana
wakati huohuo, Tundu Lissu anaendelea kuchanja mbuga, japo anafanyiwa kila figisu ili taarifa zake zisisambae, lakini ukweli ni kwamba taarifa zake zinasambaa mdomo kwa mdomo, watu wanatafuta clip zake, wanazichambua, wanahadithiana na kwa namna hii umma unashirikishwa, unajishirikisha kampeni ya Chadema.
Watu wana kiu ya kumsikiliza Lissu, Clip yake moja ya wiki iliyopita inaendelea kuwa chemchem ya taarifa kwa wiki nyingi zijazo, views za clip hiyo zinaongezeka kila siku na watu kuielewa zaidi.
Kiukweli kabisa kama uchaguzi utakuwa fair, Magufuli byebye!