Kite Munganga
Platinum Member
- Nov 19, 2006
- 1,773
- 952
Kwabahati mbaya unaongea habari za kigoma ila unaonekana si mwanakigoma, nakama ndio basi umeongea kimahaba zaidi.
Kigoma washenzi sana kila atakaeenda atajaza watu kwasababu walewale wanaokuja kwenye mkutano wa JPM ndio watakaokuja kwa LISU. Huwa wanapenda sana kumsikiliza mtu anasemaje hata kama hawampendi ili badae wakabishane vijiweni.
Nakukumbusha 2015 kawawa ilijaa hadi wengne wakapanda juu ya ukuta ila mwisho wa siku ubunge na madiwani wakampa Act.
Pili Kigoma kampeni za ndani (Nyumba kwa nyumba) ndo huwa zina mpa maamuzi mpiga kura. Hawategemei sana kampeni za majukwaa wao wanaenda kwenye mkutano ila washajua kula wanapiga wapi. 2005 kilitokea hichi kwa Kaburu baada yakujaza watu kwenye mikutano afu akapigwa chini.
Tatu Kigoma kula za Uraisi ni za Magufuri kwasababu kule Chadema ilipoteza Nguvu baada yakumtoa ZITTO. Ukizingatia wanajua kabisa membe hawezi kupita.
4: Kigoma hasa pale mjini udini na ukanda huwa unamuamulia mpiga kura wapi apeleke kura yake.
5: ZITTO anajua sana jinsi yakucheza na akili zao. Mana huwa anayoahidi 75% yanafanyika ko haijalishi nani kafanya ila wanajua yeye kafanya mana huwa anakua wakwanza kusemea.
Ko kung'oa ZITO kigoma sio kazi rahisi kama unavyofikiria labda irumike nguvu ya Ziada ya gori la mkono.
Kigoma ni ya wana Kigoma, wale watu hawana tofauti kabisa na Wapemba wa kule visiwani kwani unaongea nao na kukupigia makofi lakini moyoni wana chaguo lao
Na safari hii ndio kabisaa kwani pamoja na kutokuungana kwa Chadema na ACT kisheria lakini ni wazi Zitto ni rafiki binafsi wa Lissu mpaka aliweza kwenda kumsalimia Nairobi na Belgium? sasa hapo sioni kwamba Lissu atakuwa hayawani kuingia kwenye ngome yake na kumsambaratisha bali leo Lissu atapigilia msumari wa mwisho kama alivyofanya Zanzibar