Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Katika hali isiyo ya kawaida mhombea wa CCM John Magufuli akiwa njiani Nguruka kuelekea Urambo Tabora amampa nafasi Husna Mwilima aliyekuwa mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini kumwombea kura mgombea wa CCM bwana Nashon, wakati Mwilima akiomba kura akamkumbisha Magufuli changamoto ambazo mgombea Nashoni amesahau kumweleza Magufuli, ndipo Magufuli bila ajizi akamwambia umekuwa mbunge hapa kwa miaka mitano ulishindwa nini kutatua shida hii ndogo ya shule.

Hapa ndipo huwa namwelewa sana Magufuli huwa hamezi maneno sehemu ambayo hajaridhika.

Maendeleo hayana chama
Ukipiga kura ya rais kwa Tundu Lissu, ujue unapiga kura ya katiba mpya, ujue unapiga kura kwa rais ambaye atarudisha uhuru na haki za wananchi, ujue unapiga kura kwa rais ambaye hatawasimanga..".Tundu Lissu. #Uchaguzi2020

Achana na takataka za ccm
 
Ukipiga kura ya rais kwa Tundu Lissu, ujue unapiga kura ya katiba mpya, ujue unapiga kura kwa rais ambaye atarudisha uhuru na haki za wananchi, ujue unapiga kura kwa rais ambaye hatawasimanga..".Tundu Lissu. #Uchaguzi2020

Achana na takataka za ccm
 
Mizengo Pinda Anapasha joto Arusha,Manyara na Kilimanjaro huku Samia Suluhu akitoa sauti mororo huko kusini Peramiho.
Dada Ummy Mwalimu Kaishika Tanga kisawasawa.
Kaskazini Unguja Kwa utulivu Mwinyi Juniour anamwaga Sera .
 
..Profesa.Juma Athumani Kapuya anagombea ubunge?
Usishangae ndugu yangu! Jahazi linazama na mizimu yote iliyoitafuna taifa hili inabidi ifukuliwe isaidie kuliokoa. Timu toka 1995 hadi 2020 lazima zifukuliwe ili kama ni kuzama wazame pamoja kwa pigo moja la Mh. Tundu Antiphas Lissu. Watakaokosa ni wale tu waliotangulia mbele ya haki. CCM ni ile ile.
 
Hayo maneno aliyotamka Magufuli hapo juu yanaonesha wazi HAFAI kuendelea kuwa Rais wa Tanzania, hana hekima, ni mropokaji na mkurupukaji.
 
Huyu mzee sijui kwanini hataki kubadilika kadri oktoba 28 inavyokaribia ndio anazidi kuvuruga
 
Dr Magufuli amewataka wakazi wa Kaliua kutofanya makosa ya kuchagua mbunge wa upinzani tena kwani duniani kote hakuna Upendo wa kumpa chakula mtoto wa jirani wakati wa kwako ana njaa.

Dr Magufuli amesema hata barabara ya Kaliua imejengwa kwa heshima ya mzee Kapuya hivyo wasimwangushe.

Tundu Lisu atakuwa na wakati mgumu sana mkoani Kagera kwa sababu CCM imefanya kampeni kisayansi sana na Dr Bashiru anaendelea kufukia mashimo.

Maendeleo hayana vyama!
Yaani Lissu ana wakati mgumu Kagera????😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Kagera ipi ya Chato au hii ambayo Bashiru anawatisha wana CCM kuwa wasikihujumu Chama au watamalizwa????
 
Sihaelewa ...unasema Kapuya anagombea Ubunge!Aisee Kama ndivyo Basi Wanyamwezi Kuna shida!
 
Wapi Butiku, Wapi Mangula, Wapi Kinana, Wapi makamba,Wapi Warioba.

Popote walipo hawa wazee mbona mwaka 2015 walikuwa busy Sana kusema Lowassa ni fisadi.

Vipi wamepata majibu tulipo waambia tatizo la nchi hii ni CCM na mfumo mbovu waliouhasisi?.

Njooni Mtetee vitambulisho vya Machinga wenye mitaji ya elfu 15 halafu wanatozwa kitambulisho Cha elf 20.

Njooni mtetee uwanja wa ndege chato.

Njooni mtetee Mbuga ya wanyama chato...

Nasema njooni tafadhari maana siwaoni majukwaani mkivitetea hivi vitu.

Tundu Lissu atawashangaza sana Mwaka huu lazima turudishe nchi yetu kwenye Uhuru Haki na maendeleo yao.

Hatuwezi kuendelea kuacha nchi chini ya Ngedere.

Tukutane October.
Hujui majukumu ya hao wazee uliowataja kaa kimya.Mfano mdogo tu, unataka Butiku ampigie kampeni mgombea wa ccm, je unajua wadhifa wake na ni taasisi gani.Fanya home work yako.
 
Dr Magufuli amewataka wakazi wa Kaliua kutofanya makosa ya kuchagua mbunge wa upinzani tena kwani duniani kote hakuna Upendo wa kumpa chakula mtoto wa jirani wakati wa kwako ana njaa.

Dr Magufuli amesema hata barabara ya Kaliua imejengwa kwa heshima ya mzee Kapuya hivyo wasimwangushe.

Tundu Lisu atakuwa na wakati mgumu sana mkoani Kagera kwa sababu CCM imefanya kampeni kisayansi sana na Dr Bashiru anaendelea kufukia mashimo.

Maendeleo hayana vyama!
Ni vizuri mida hii mngeitumia kumfundisha magufuli wenu aache kutoa maneno ya kuwabagua watanzania kimaendeleo wakati watanzania wote wanalipa kodi
 
Mizengo Pinda Anapasha joto Arusha,Manyara na Kilimanjaro huku Samia Suluhu akitoa sauti mororo huko kusini Peramiho.
Dada Ummy Mwalimu Kaishika Tanga kisawasawa.
Kaskazini Unguja Kwa utulivu Mwinyi Juniour anamwaga Sera .
Makamanda uchwara wamekaa wakimtegemea mnyoa kiduku na buti lake la jeje awaletee ushindi. Kazi ipo mwaka huu.
 
Mizengo Pinda Anapasha joto Arusha,Manyara na Kilimanjaro huku Samia Suluhu akitoa sauti mororo huko kusini Peramiho.
Dada Ummy Mwalimu Kaishika Tanga kisawasawa.
Kaskazini Unguja Kwa utulivu Mwinyi Juniour anamwaga Sera .
Pinda kumpa kanda ya Kaskazini mmemuonea, ni sawa na sisimizi tu, haonekani wala hasikiki.

Samia kanda ya Kusini nae anajifurahisha tu, watu wana hasira na korosho zao mlivyowachezea hata hawana hamu nae, nadhani unamuona Salma Kikwete anavyohangaika kuchambua mchele kwenye nyumba za watu huko kusini, hadi vidole vitaota sugu.

Ummy Tanga labda mumfanyie mpango tu kwasababu ndie "kipepeo" cha "jiwe".

Huko Zanzibar ndio kabisa, kila siku mnawaengua wagombea wa ACT angalau mpate nafuu, naskia mmeshapeleka wanajeshi wakapige kura tarehe 27.10. "20, bila kuchovya vidole vyao kwenye wino, halafu warudie tena kupiga kura 28.10."20.
 
Back
Top Bottom