Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

acha waisome namba yao mkuu wameipenda wenyewe....πŸ˜€
 
Mikutano ya CCM inawawasha washa Kwa nn , watu wanaenda kumuona raisi wao mwenye uwezo wa kutatua kero onspot , we unawatisha Tisha , nendeni Kwa Lissu raisi wenu awape ajira na awaongezee mshahara
 
Kumbe ndio maana kwenye mikutano watu wanalala na kununa. Ila cha uhakika watampa kura zote Lissu. Sisi watanzania wote kura zote kwa Lissu.
 
Mkome kuitika kila wito. Unaitwa na shetani unakwenda halafu unarudi kulialia.
 
Mmeishiwa sasa mnaanza kueneza uwongo wa kuizushia CCM. JPM kanyaga twende washaanza kupoteana huku kwenye media.
 
Salaam Wana JF.
Rais Magufuli ni kiongozi mwenye maono na aliyeonyesha uthubutu wa hali ya juu katika ya viongozi wa bara hili la Afrika, Uthubutu wake ni wa kimapinduzi na unaolenga kuwakomboa wananchi, Magufuli amethubutu kisiasa, kiuchumi na kijamii, ni kiongozi wa pekee kwa sasa anayeweza kusimama na kukemea "Ukoloni Mambo leo" Kwa maana ya unyonyaji wa mabeberu, Aidha Magufuli ni mjamaa na kiongozi anayeishi katika falsafa za kuwatumikia watu walio "Wanyonge" na Wanyonge ndio wengi, Maono ya Magufuli yapo wazi kwenye "COVID-19", "Mikataba ya Madini" na "Falsafa ya ufufuaji wa viwanda"

Kwa Mantiki hiyo Wananchi wana Kiburi cha kumchagua tena Dkt. Magufuli kwa miaka mingine mitano, kwa sababu nia na hoja za kufanya hivyo zipo wazi kulingana na matendo yake, Myonge myongeni lakini haki yake mpeni, tumpe mitano tena Dkt. Magufuli atende yaliyo mema zaidi kwa ustawi wa nchi na kizazi cha sasa na hapo badae.
 
CCM imeingia kwenye Kampeni ikiwa na wapiga Kura wa uhakika M.14+ ambapo wote ni wanachama wake, Kwa hiyo ushindi uko palepale
 
Nimeshangaa Sana baada ya Polepole kumkaribisha mzee Butiku ameanza kwa kuuliza wanafunzi waliohudhuria mkutano wanyooshe mikono na nusu ya waliohudhuria wamenyosha mikono wengine wakiwa ndani ya nguo za shule.
Vipi huko Makambako kwani wanafunzi wako likizo? Au Leo Ni Kuna holiday huko?
 
Hii ya kuwazui watoto kwenda shule na kuwapeleka kwenye kampeni, NEC hawaioni.
Yote kwa yote CCM inapobeba watu na wanfunzi kwenda kwenye kampeni inawasaidiaje?
 

Nafikiri lengo la Butiku ilikua kuwaprove wrong akina Lissu akapatikana yeye!!

Aibu nimeona mimi!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…