Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Maendeleo ya kweli ni maendeleo ya watu. Na maendeleo ya watu, jambo la kwanza ni uhuru, haki na utu wake. Hivyo vitu vitatu visipokuwepo, chochote utakachokifanya hakina mantiki kwa ustawi wa mwanadamu.

Tangu enzi za kale, tangu enzi za wayahudi, watu wanaongelea uhuru. Wayahudi walimsubiri masiha kwa miaka elfu 40, wakiamini kuwa huyo masiha atawafanya wawe watu huru. Hawakumsubiria ili awajengee barabara, nyumba, reli au umeme, maana hayo waliamini hata mkoloni wao Mrumi alikuwa ana uwezo wa kuwafanyia. Alichowanyima Mrumi ni uhuru wao.

Magufuli kokote aliko, ajue kuwa hata angefanikiwa kutengeneza reli ya angani lakini akaendekeza siasa za kuwanyima watu uhuru, siasa za kuwadhalilisha watu, siasa za kuwabagua na kuwapendelea watu, siasa za kuwanyima watu haki, kamwe hatakumbukwa kwa mema bali kwa mabaya yake. Na atakuja kuwekwa kwenye historia kuwa ndiye alikuwa kiongozi wa kwanza mbaya kwa Taifa letu.

Rais Magufuli anatakiwa ajue kuwa katika ubinadamu wake, hakuna anachowazidi wanadamu wengine. Pamoja na kuwa kwamba yeye ni Rais lakini bado ni mwanadamu, tena mwenye mapungufu mengi, na wengi wanamzidi katika mengi, kuanzia akili, maarifa na uelewa wa mambo mengi. Asijione kama yeye ana mamlaka ya kuamua nani aishi na nani afe, nani awe huru na nani atekwe au kupotezwa. Mabaya aliyoyafanya ayajutie na atubu kwa dhamira na siyo kwa unafiki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha blah blah njoo na hoja za maana.
Kama kumtaja mungu, hata wauaji na wachawi humtaja mungu, tena kwa unyenyekevu na kutetemeka.
Magufuli hamtaji tu alifunga na kuomba na taifa siku tatu Corona iondoke nchini na siku zingine tatu za kumshukuru Mumgu wakati wewe ulikuwa katika siku hizo unataja Mungu huku ukifakamia chips kuku
 
Toka lini jiwe akajua kuongea??? Huyo mzee mdomoni hakuna kitu
Hivi huyu jamaa zinamtosha kichwani kweli? Tumechagua rais timamu kweli? Mbona hana kauli za kiuongozi?

Najuta kumfahamu.
 
Atuoneshe kwanza Kaburi la Beni Saanane na Azory
 
Maswali ya kitoto yakiulizwa na mtoto tunasema muulizaji ana akili ya kitoto ila swali la kiutu uzima likiulizwa na mtoto tunasema mtoto anakuwa
Ina maana hujui wakati unabadilika mwisho n mbinu hubadilika pia
 
Kwa maelezo hayo, Magufuli hahitaji kufanya kampeni. Lakini kwa taarifa, anahitaji kuleta mapya ambayo yatajibu mapungufu yaliyojitokeza miaka hii 5, na pia mapya yatakayotoa mwelekeo wa miaka 5 ijayo. Majibu yako yanaonesha upungufu mkubwa katika strateji. Kama mastratejisti wa Magufuli ndio wanawaza hayo pia, basi kazi ipo
 
Ukali wa maneno?!?! Ni namna wewe ulivyoipokea habari...ukiwa positive hakuna ukali wa maneno hapo...ila ukiwa negative na kutafuta makosa ya JPM ndipo utaona kuna ukali wa maneno...it is about perception ...
Kwahiyo Magufuri alivyoitwa dicteta uchwara ni matusi au kuna ukali wa maneno wowote!
 
Ukali wa maneno?!?! Ni namna wewe ulivyoipokea habari...ukiwa positive hakuna ukali wa maneno hapo...ila ukiwa negative na kutafuta makosa ya JPM ndipo utaona kuna ukali wa maneno...it is about perception ...
Je kuna utofauti wa ukali wa manone kuzaa au kujifungua ikiwa unamuongelea binadamu!

Swali la ziada..mkuu umeshawahi kusoma lugha?
 
Anatunza nguvu za kulimia magimbi baada 28102020 ni msimu wa kilimo huko kwao chato
 
Ukali wa maneno?!?! Ni namna wewe ulivyoipokea habari...ukiwa positive hakuna ukali wa maneno hapo...ila ukiwa negative na kutafuta makosa ya JPM ndipo utaona kuna ukali wa maneno...it is about perception ...
Kwahiyo hata TBC wanaokatiza hotuba za wapinzani wana wrong perception kwa wapinzani, so ndiyo?

Maana kwa mujibu wa maelezo yako ukali wa maneno unategemea na tafsiri ya mlengwa au msikilizaji na siyo kwa mujibu wa tafsiri ya jumla inayokubalika katika jamii..mkuu utakuwa haupo serious.
 
Unataka adanganye kuwa atajenga reli hewani ili kukufurahisha ama??

Of course hakuna jipya chini ya hili jua ,

Ila tunamtaka kiongozi sampuli ya Magufuli anayeishi maneno yake.

Magufuli amejitahidi sana kutimiza ahadi zake ,

Sioni sababu ya kumnyima awamu nyingine,

Kuna mengi mazuri anapaswa kuyamalizia na kuyakabidhi yakiwa yamekamilika.
 
Maswali ya kitoto yakiulizwa na mtoto tunasema muulizaji ana akili ya kitoto ila swali la kiutu uzima likiulizwa na mtoto tunasema mtoto anakuwa
Ina maana hujui wakati unabadilika mwisho n mbinu hubadilika pia
Umejibu kwa ukali mno
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…