Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Kwa hiyo mkuu tusiwe na wasiwasi. Nyomi za CHADEMA kura hawapigi Ila za CCM.

Au vp mkuu?
CCM mikutano yao wanakwenda na nguo za kijani na wote wale ni wapiga kura.

Ni chama chenye wanachama milioni nane kwa data za 2015, ni chama chenye utaratibu wa uendeshaji wenye kueleweka. Kina hazina ya wataalam wa fani mbalimbali.
 
CCM mikutano yao wanakwenda na nguo za kijani na wote wale ni wapiga kura.

Ni chama chenye wanachama milioni nane kwa data za 2015, ni chama chenye utaratibu wa uendeshaji wenye kueleweka. Kina hazina ya wataalam wa fani mbalimbali.

Sasa mna yote hayo kwa nini mmeshindwa uwepo wa tume huru ili muwashinde kiroho safi wasiwe hata na kisingizio?

Kwa nini muwabanie vyombo vya habari?

Kwa nini kuwa engua engua?

Kwa nini mafigisu yasiyokwisha dhidi yao?
 
Amepuuza vilio vya watanzania kuhusu biashara zao kudorora, vijana kukosa ajira na kutoyakemea matukio ya utekaji, mauaji, matusi ya Musiba kwa wazee wastaafu na mengine mengi.

Alifanya maamuzi mengi kibabe. Mfano kukataza mikutano ya siasa, kukataza bunge kuwa live, n.k kwa kisingizio kuwa watanzania wachape kazi. Lakini yeye kutwa kucha yuko mubashara hata kwa mambo yasiyo na umuhimu.

Laiti kama Magufuli angekuwa msikivu, mnyenyekevu na mpenda watu, uchaguzi huu ungekuwa rahisi kwake.
Kuna watu ni kama akili zenu zimefyatuka

Pumzi ya JPM na jinsi jamii inavyo mkubali lakini bado mnajikaza tu kuja mitandao kuropoka upuuzi sijui mtafaidika nini
 
Mwingine anaweza kusema mwaka 2015 alitumia nguvu kubwa na akapita maeneo mengi kwa sababu kazi ilikuwa ngumu hata matokeo ya Uraia yalisadifu hilo.

Mwaka huu kazi ni nyepesi mno, kila mtu anaona kinachotokea, mwitikio wa Raia kwake na kwa wapinzani wake. ACT wameshanyosha mikono, CDM ndiyo Kama hivo, Juzi uliona Raia wa pwani Kama vile hawamjui, Jana Morogoro mjini umeona hali mwenyewe, kule Mheza ilikuwa aibu. Hata Makamanda tangu Mlivyoposti picha za Mbeya, hamjaposti tena, utafikiri Mgombea wenu yupo likizo naye.

Sasa kwa namna hiyo kwanini asipumzike Budha. Game imekuwa nyepesi mno.
Kama umegundua, wanachokifanya CCM baada ya uhakika wa Kushinda, ni kuhakikisha mtu anapata kipigo cha mbwa koko, hicho ndicho kinachofanyika kwa Sasa.

Angalau we ni kati ya wanaCCM wanaoweza kuandika vizuri, sijazungumzia kujenga hoja lakini. Wape semina elekeze wenzio basi wanatia aibu humu. Semeni ukweli sio kwamba kampeni ni rahisi na mzee ameamua kupumzika, la hasha! Hawezi mpera mpera huu mfululizo. Kampeni zingekuwa rahisi tusingemsikia akisema “Mkiendelea kuzomea naondoka” au “Mninyime miaka mingine mitano nimewakosea nini”? 😀

Btw, miss u nakusubiria wasapu.
 
Amepuuza vilio vya watanzania kuhusu biashara zao kudorora, vijana kukosa ajira na kutoyakemea matukio ya utekaji, mauaji, matusi ya Musiba kwa wazee wastaafu na mengine mengi.

Alifanya maamuzi mengi kibabe. Mfano kukataza mikutano ya siasa, kukataza bunge kuwa live, n.k kwa kisingizio kuwa watanzania wachape kazi. Lakini yeye kutwa kucha yuko mubashara hata kwa mambo yasiyo na umuhimu.

Laiti kama Magufuli angekuwa msikivu, mnyenyekevu na mpenda watu, uchaguzi huu ungekuwa rahisi kwake.
Huyo alimpenda Mungu na kumchukia binadamu mwezake ila sisi tutamwonesha upendo was bure kabisa
 
Angalau we ni kati ya wanaCCM wanaoweza kuandika vizuri, sijazungumzia kujenga hoja lakini. Wape semina elekeze wenzio basi wanatia aibu humu. Semeni ukweli sio kwamba kampeni ni rahisi na mzee ameamua kupumzika, la hasha! Hawezi mpera mpera huu mfululizo. Kampeni zingekuwa rahisi tusingemsikia akisema “Mkiendelea kuzomea naondoka” au “Mninyime miaka mingine mitano nimewakosea nini”? 😀

Btw, miss u nakusubiria wasapu.
Teh teh teh teh, unanichekesha hapa, mbavu Sina😂😂😂😂😂😂halafu Mimi ni CHAUMA, kule kwa Rungwe kwenye Ubwabwa usijifanye haujui. Hapa nilikuwa najaribu kueleza tu ukweli na kujaribu kuwasaidia Wanabuku7 dhidi ya Wanaserengeti
 
Teh teh teh teh, unanichekesha hapa, mbavu Sina😂😂😂😂😂😂halafu Mimi ni CHAUMA, kule kwa Rungwe kwenye Ubwabwa usijifanye haujui. Hapa nilikuwa najaribu kueleza tu ukweli na kujaribu kuwasaidia Wanabuku7 dhidi ya Wanaserengeti

We bana acha kujificha CHAUMA, ubwabwa ukija kwangu ntakupikia. Hujakubali ushauri wangu wa kuwafundisha mataga wenzio kujenga hoja na kuandika kwa ufasaha!
 
Pumzi ya JPM na jinsi jamii inavyo mkubali
Itakuwa upo bize sana na mitandaoni kujibu hoja za wanaompinga jpm na huna muda wa kuzunguka mitaani aukawasikiliza wananchi.

JPM akipata 30% ya kura ujue kaiba.
 
We bana acha kujificha CHAUMA, ubwabwa ukija kwangu ntakupikia. Hujakubali ushauri wangu wa kuwafundisha mataga wenzio kujenga hoja na kuandika kww ufasaha!
MATAGA teh teh teh teh😎😎😎😎😎😎😎😎, una mambo aloo, nakuchora tu hapa. Anyways mimi CHAUMA bwana Kama wewe ulivyo Mwanachama wa kile Chama cha Queen Sendega
 
Kusema kampeni za CCM ni ngumu ni vichekesho. Rais Magufuli hata asipopiga kampeni kuanzia leo ushindi ni 90%

Rafiki zetu wa CHADEMA mtaula wa chuya huu mwaka hampati hata mbunge.

Kampeni ya ccm ni ngumu kwa sababu tatu kubwa. Mosi, chama chenye serikali kina nafasi kubwa ya kukosolewa. Pili, baada ya uchaguzi uliopita ccm haikufanya kazi yoyote ya kisiasa bali ilikabidhi majukumu yake yote kwa serikali ambayo nayo ilijihusisha zaidi kudhoofisha ushindani. Tatu, tofauti na 2015 udhaifu wa ccm ya sasa umefahamika zaidi na upinzani umejipanga vizuri zaidi kijenga hoja za kisiasa kwa kutumia udhaifu huo. Ndiyo maana mapema tu wazee wamechukuliwa kuingia kwenye kampeni. Katika hali ya kawaida wazee wangeingia dakika za mwisho. Na kwa namna wazee wenyewe wanavyoshiriki kampeni ni dhahiri pia mambo siyo mzuri. Muda mwingi hutumika kutetea maamuzi tata ya serikali na kutoa maelezo kitu ambacho kilipaswa kufanywa na serikali yenyewe tena muda mrefu uliopita. Maana yake wahusika hawana utetezi wala maelezo ya kuridhisha hivyo kuhitaji msaada. Aidha nguvu nyingi pia hutumika kukosoa mbinu za washindani na kutoa vitisho dhidi ya mwenendo wao badala ya kupambanisha hoja.
 
Ingawa ni mgombea, bado pia ni Rais wa nchi kwa hiyo hawezi kutumia muda wote kwenye kampeini na kusahahau majukumu ya uraisi. Halafu kama angekuwa na woga, ndipo angekuwa anafanya kampeini usiku na mchana lakini kwa vile hana hofu basi anaweza kuchukua time-off ili kufanya mambo mengine.

October 28 ndiyo fainali.
Sijui kama watakuelewa hawa 'watani' zangu! Erythrocyte ,Missile of the Nation Daudi Mchambuzi na wengineo mmesikia/soma na kuelewa?
 
Kampeni ya ccm ni ngumu kwa sababu tatu kubwa. Mosi, chama chenye serikali kina nafasi kubwa ya kukosolewa. Pili, baada ya uchaguzi uliopita ccm haikufanya kazi yoyote ya kisiasa bali ilikabidhi majukumu yake yote kwa serikali ambayo nayo ilijihusisha zaidi kudhoofisha ushindani. Tatu, tofauti na 2015 udhaifu wa ccm ya sasa umefahamika zaidi na upinzani umejipanga vizuri zaidi kijenga hoja za kisiasa kwa kutumia udhaifu huo. Ndiyo maana mapema tu wazee wamechukuliwa kuingia kwenye kampeni. Katika hali ya kawaida wazee wangeingia dakika za mwisho. Na kwa namna wazee wenyewe wanavyoshiriki kampeni ni dhahiri pia mambo siyo mzuri. Muda mwingi hutumika kutetea maamuzi tata ya serikali na kutoa maelezo kitu ambacho kilipaswa kufanywa na serikali yenyewe tena muda mrefu uliopita. Maana yake wahusika hawana utetezi wala maelezo ya kuridhisha hivyo kuhitaji msaada. Aidha nguvu nyingi pia hutumika kukosoa mbinu za washindani na kutoa vitisho dhidi ya mwenendo wao badala ya kupambanisha hoja.
Duuh! Asante kwa uchambuzi wako mzuri mkuu. Nimepata kitu.
 
Back
Top Bottom