Volatility
JF-Expert Member
- Aug 22, 2018
- 3,935
- 7,513
Na sasa ndio wametisha zaidi, wameenda kujificha kwenye mitambo ya nuclear.Ni kweli. Warusi wasingekuwa wanatumia mwamvuli wa kujificha kwenye makazi ya watu na vifaru vyao, hii vita ingekuwa imeshaisha na Crimea ingekuwa tayari imeshakombolewa.
Ndiyo maana Ukraine wameamua kutumia mbinu mbadala wa kuwamaliza nguvu warusi kwa kukata njia ya supplies ya silaha na kusaka mangala ya silaha ili wayaangamize. Hii itawafanya warusi waondoke wenyewe (retreat) bila kuleta madhara makubwa kwa raia na mali zao.
Tumeshuhudia vita vya maporini wanavyoangamizwa na vifaru vyao. Kwenye miji vita imekuwa ngumu sana sababu adui wanajichanganya na raia. Wanaweka vifaru kwenye fensi za watu. Warusi wanajificha kwenye nyumba za raia. Ndiyo maana Ukraine wanahitaji Drone za kutosha kutafuta vifaru na warusi kwenye makazi ya watu.
Ila mimi siwalaumu hawa warusi sababu wanadai tarehe 24 February walipoivamia Ukraine hawakuwa wakijuwa kama wanafanya uvamizi.
wanadai walipokuwa wakisikia mizinga walikuwa wanasonga mbele wakijua kwamba wanakabiliana na majeshi ya NATO, baada ya kufika UKRAINE hasa ndo wakakuta hakuna NATO wala sisimizi bali raia wasio na hatia wa Ukraine.
Yaani kwa sasa, wote watatu, Raia wa Ukraine, Wanajeshi wa Ukraine na Wanajeshi wa Urusi wote ni wahanga wa Ukichaa wa Putin.
wote wanaviziana kuuana, sababu hawaaminiani.