Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Nimepata Video nzuri Uwanja wa Vita. Urusi walikuwa wanapambana na Ukriane Umbali wa Hatua Ishirini. Walio chini ya Daraja ni Ukraine, walio juu ya Daraja hapo kwenye michanga ni Warusi. Urusi wamepelekewa moto hadi wakakimbia. Picha imechukuliwa na drone
Your browser is not able to display this video.
 
Ama kweli; shughuli ilikuwa ni pevu.Utadhani ni movie kumbe ni kitu halisi.Dah! Vita sio kitu cha kutamani hata cku moja. Ukraine ni ngangari kweli-kweli. Hongera sana.
 
Aisee! Shukrani sana Mkuu. Hii clip nimeiangalia sijui zaidi ya x 5 lakini bado sitosheki na ninachokiona hapo esp. Wanajeshi Waukraine 3 hapo kushoto darajani walivyokuwa wanarusha Hand grenades(Cjui kama ndo hizo) na Warusi wakajibu lakini majibu yao hayakufua dafu na ikabidi watimue mbio kama kawaida yao. Sikuona mizoga lakini naamini itakuwepo tu - kwa nini watimue mbio? Yaani we acha tu, Ukraine ni Moto wa kuotea mbali. Pongezi Ukraine. Shikilia hapo-hapo: PELEKA MOTOOOOoooo tena kwa Sanaa.
 
Nimekubali wanajeshi wa Ukraine [emoji1255] are the best
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…