Cash Generating Unit
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 13,286
- 39,418
Mkuu mi sikatai kuwa Urusi ni taifa kubwa kieneo pengine mara 10 ya Ukraine, sikatai kuwa Urusi ina jeshi kubwa na lenye nguvu zaidi ya Ukraine, pia sikatai kuwa Urusi ana silaha hatari zaidi ya zile za Ukraine. Ila ninachozungumzia hapa ni kwamba Urusi na wapambe wake hawakutegemea kuwa wangepata upinzani mkubwa kutoka kwa vikosi vya Ukraine kwani waliamini kuwa Ukraine ina jeshi dhoofu lisilo na ujuzi wala mbinu, lisilo na silaha wala uwezo wa kujilinda na kujitetea kwa namna yoyote ile. Urusi ilitegemea kuwa baada ya kuanzisha mashambulizi jeshi la Ukraine lingeweka silaha chini na kukimbia huku wakiacha jeshi la Urusi likivinjari katika ardhi yao, na ndio maana kabla mashambulizi hayaja anza Putin alianza kutangaza kuwa anataka wanajeshi wa Ukraine waweke silaha chini ili yeye aingie tu kiwepesi wepesi kama vile mume anaeingia kwenye chumba cha mkewe kula mzigo. Sasa kilichoshangaza wengi ni kwamba jeshi la Ukraine pamoja na udogo wa nchi yao, uhafifu wa vifaa vyao vya kijeshi na udogo wa jeshi lao lakini hawakutii wala kuogopa kauli ile. Ndio kwanza walionesha na wao kujiamini kwa lolote litakalotokea, na kweli kujiamini kwao kumewasaidia maana vita ambayo Russia alitegemea ataimaliza siku moja, leo ina week haijaisha huku Urusi yenyewe ikiwa haijadhibiti kikamilifu mji hata mmoja kati ya miji miwili mikubwa ya nchi hiyo. So hauoni kama mambo bado ni magumu kwa Urusi japo wanajeshi bora na silaha kubwa kubwa?
Wapi mrussi alisema hata kutana na upinzani kutoka ukraine? Ukraine usiichukulie poa ipo vzr kijeshi mzee