LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Lakini situli kubaliana Ukraine peke yake ndo alikuwa anaitoa jasho Urusi na ni super power uchwara?
 
Wanajaribu kumlazimisha Rais Zelensky afanye wanachokitaka, japo walishindwa kumshirikisha kwenye mazungumzo kule Saud Arabia.
Unamshirikishaje mtu kwenye mchezo wakati hana karata?

Zelenskyy alikubali kutumika, sasa anaonja joto la jiwe.

Hata hivyo mzigo mkubwa uko kwa raia wa Ukreni sasa na wakati ujao, maana jamaa yeye amejinufaisha vya kutosha kupitia rushwa, ubadhirifu na uporaji wa mali ya umma na misaada ya kijamii na kijeshi.

Yuko kwenye dilemma; anashindwa amsikilize Putin, NATO, Marekani au matakwa ya wananchi wake.

Tunaweza kusema kwamba Zelenskyy anataka kile kile wanachotaka NATO na Marekani, yaani kuwalipa fadhila za ile misaada yao kupitia rasilimali zake, ila tu jamaa anaogopa athari zitakazompata kutoka kwa raia wake kwa sababu ya kitendo cha kuiharibu, kuitoa kafara na kuigawa nchi yake.
 
Hii ishu ya kusitisha msaada ndio naina inataka kumpeleka Macron U.S.
Sababu hata hizo silaha nyingi wanazopeleka E.U nyingine ni za U.S au joint venture.
Ila hili la intelligence na starlink ndio lina madhara makubwa na yanayoonekana kwa haraka kuliko hata silaha, maana hata E.U hawataweza kushare na Ukraine taarifa zenye mkono wa U.S
Hii ndio dawa ya jeuri kibuli, tajiri hanuniwi
 
Urusi anasaidiwa na Iran,Korea Kaskazini kupigana na Ukraine
Bahati nzuri ukweli unaujua ila unajitoa ufahamu ili kujifariji.
Tuliwaambia haitawezekana nchi za magharibi kuishinda Urusi kwenye uwanja wa mapambano nyinyi mkakaza kichwa.
Kwa hiyo Tz tukiingia vitani tutahesabika tuna saidiwa na nchi zinazo tuuzia silaha?
Urusi hasaidiwi silaha bali ananunua silaha kutoka nchi hizo na penyewe si kwamba ameishiwa silaha bali ni anajaribu kupunguza gharama za vita kwa sababu silaha za nchi hizo zinatumia gharama ndogo kuzitengeneza.
Urusi mpaka sasa ni muuzaji mkubwa wa silaha duniani ukiitoa Marekani sasa itakuwaje akose silaha za kupigana kwenye vita ya Ukraine mpaka ategemee silaha kutoka Iran?
Haya tukubaliane na hoja yako sawa Urusi inasaidiwa na N.korea na Iran sasa iweje mataifa matatu ambayo kwa mujibu wenu ni mataifa masikini na waganga njaa wayashinde mataifa zaidi ya 50 ambayo ndo masuper wa dunia?
 
Haya yote tuliwaambia ila mkatuona wajinga.
Leo majibu yamekuja sahihi kabisa.
Kwamba Ukraine ilikua inapewa misaada ya Kila ilichotaka toka USA na all collective west.
 
,πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ€πŸ€πŸ€πŸ€πŸ€πŸ€πŸ€πŸ€
Da umeingiaje kwenye mawazo yangu?
Hasa pale kwenye point ya nchi masiki.

Siku zote humu Pro west husema Korea kaskazini ni nchi masikini sana hapa duniani Leo iweje nchi masikini kama hiyo iwe na uwezo wa kuisaidia Urusi kwenye vita kubwa namna hiyo barani Ulaya baada ya WWII?
Vita ambayo inahusisha matajiri wote wa Dunia dhidi ya Urusi?
Maana ndani ya west wote Kuna USA baba lao,Kuna EU,Kuna G7 na Kuna NATO.
Haya Mataifa yote yanapigana bila mafanikio na nchi zilizokua zinaitwa masikina mfano Urusi ambayo wao wanakuqmbia Inazidiwa uchumi na California,Korea kaskazini ni nchi masikini sana na Iran ni third world na iliyowekewa vikwazo miaka zaidi ya 40.
Hawa jamaa zetu safari hii Trump mwenyewe kawa prove wrong.
Katusaidia kumaliza ubishi.
 
Urusi anasaidiwa na Iran,Korea Kaskazini kupigana na Ukraine
Ningekua Mimi ndio wewe wala nisinge ng'ang'ania kauli hii ya kua Urusi inasaidiwa na Iran na Korea kaskazini kwa sababu kauli hii inawaaibisha sana west.
Nadhani Pro west wenzako wanaona aibu wenyewe Kwa kauli Yako hii ambayo unaipenda sana lakini wanashindwa kukuziba midomo maana inaaibishano uwezo wa west dhidi ya Urusi.
Kwa sababu kauli Yako hii inaprove uwezo mkubwa wa Urusi na kuprove wrong uwezo wa west wote.
Kwa sababu kumbe na Kwa maana Yako na kwa kilio chako Cha muda mrefu ni sawa na kusema kua

I) Urusi peke yake ni sawa na nchi zote za west kijeshi.

ii)na kwa sababu west wamemshindwa Urusi basi ni Kwa sababu ya msaada wa Iran na Korea kaskazini.
Sasa sisi wachambuzi uchwara tunajiuliza huo ukubwa wa west kijeshi tuliokua tunaaminishwa uko wapi?
Kibaya zaidi hizo nchi Tatu TU yaani Urusi Iran na Korea kaskazini mlikua mnatuaminisha ni nchi masikini na third world countries.sasa Leo nchi masikini Tatu zimeweza kuzisimamisha nchi tajiri donor kantris 50.
Aisee kumbe tulipigwa pakubwa.
Namkubuka Putin alikua akisema huku anacheka kua,

"Katika vita vya propaganda hakuna nchi inaweza kuishinda USA na west."

Hivyo hiyo kauli Yako ya kua Russia inasaidiwa na Iran na Korea kaskazini inazidhalilisha mno nchi za First World,NATO,EU na west wote ambao humu hua tunaambiwa ni doner countries,Kuna watu humu hua hawaishi kusema hivi Urusi imewahi kutoa misaada Gani kwa Afrika?
Ooh Korea kaskazini ni nchi masikini sana raia wake wanatoroka nchi,ooh Iran ni third world country.
Sasa Leo hawa masikini watatu ndio wa kuwazidi akili matajiri wa Dunia?

Sasa Leo Mimi najiuliza hivi ilikuaje pale Urusi ilipokua kamili yaani USSR ambayo ndani yake kulikua Kuna akina Ukraine, Georgia, Lithuania, Beralus, Estonia,Moldova,Latvia, Azebaijan, Kyugistan, Tajikistan, Turkmenistan, Kazakhstan n.k?ambazo zote hizi ukiongeza na Russian federation ndio unapata USSR.
Sasa hapa ukiongeza na wazee wa Warsaw pact akina chekoslovakia,Hungary,Romania,Burgaria,Poland n.k unafikiri NATO walikua na Hali Gani?
 
Urusi anasaidiwa na Iran,Korea Kaskazini kupigana na Ukraine
Haya ona Sasa aibu nyingine ya kauli Yako hii pendwa.

Kwa hiyo wewe ulipendelea Urusi peke ipigane na Ukraine inayosaidiwa na nchi 59? Ndani ya hizo 59 yumo Giant wa Dunia USA,na akina UK German France Canada Italy Poland, Denmark, Norway Sweden Finland Belgium Holland Spain Turkey Australia etc?

Na je unakumbuka mwanzo mlikua mnasema Urusi Haina washirika?
Mkasema china hawezi kuingilia kijeshi sababu yeye anajali uchumi wake ,Sasa Leo hivi vi nchi dhaifu vya Korea kaskazini na Irani ndio vinawapa mawazo namna hii?
Ukuu wa west uko wapi Sasa hapo kulingana na kauli na kilio chako hiki pendwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…