Spika Dkt. Tulia: Rais mimi ndio Mbunge wa Mbeya Mjini, Wananchi wameniambia Wanakuunga mkono Uwekezaji wa Bandari!

Baada ya Tulia Ackson kusema uongo mbele ya Rais Samia Suluhu, kwamba Wakazi wa Mbeya wameridhia Mkataba wa Kitumwa wa Bandari na DP WORLD, Wakazi hao wamecharuka na kujitokeza bila kuogopa kutekwa kukanusha kauli hiyo ya Mbunge huyo.

Wengi wamependekeza Mama huyu ajiuzulu haraka Ubunge ili asiendelee kuwadhalilisha .

Baadhi yao hawa hapa

 
Duh huyu mwanamke kweli ni hamnazo kabisa kichwani kwake. Dishi limesha cheza kichwani.

Hivi, unaanzaje kuwajibia watu maelfu kwenye jambo nyeti kama hilo?

Wangekua wameridhia wana mbeya wote, basi wasigekua wao wa kwanza kwenda mahakamani kulipinga huko huko mbeya!
 
Tulia, sisi wana Mbeya tumesononeshwa sana na maneno yako eti kwamba sisi tunaunga mkono uuzwaji wa bandari ze binafsi.tu kwa Mwarabu, la hasha.

Mbeya ndio mkoa pekee wa Tanganyika ambao umepinga mahakamani biashara haramu ya rasilimali zetu.

Hiki ni kianishi tosha kuonyesha kwamba uliyoyaongea kwenye hotuba yako ni maneno ya mawazo yako wewe binafsi.

Kama unataka uone wananchi walivyo against mawazo yako, tuonane uwanja wa Sokoine wananchi wote tukapige kura za uwazi ndio utajua wana Mbeya tunataka nini.

Wananchi wa Mbeya tunasimama bega kwa bega na Mwabukusi, wakili wetu msomi.

Shujaa wa taifa letu. Huyu ni tofauti kabisa na wewe ambaye zaidi ya kusifu na kuabudu hamna unachokiweza.
 
Rais Samia Suluhu Hassan ni kama amempotezea Spika wa Bunge baada ya kuzungumza kuwa watu wa Mbeya wanaunga mkono mkataba wa uwekezaji wa Bandari na kwamba hapo Mbeya kumekuwa na maneno mengi kuhusu bandari.

Kwenye Hotuba ya Rais Samia pamoja na kutanguliziwa maneno hayo na Spika wa Bunge kuhusu bandari lakini bado kwenye hotuba yake yote ilijikita kwenye mambo ya nane nane kuhusu wakulima, wafugaji na wavuvi na kumuacha solemba Spika Tulia na ishu yake ya Bandari.

Lakini Spika kwa kukosa adabu anasema mbele ya hadhara hiyo kwamba wananchi wa Mbeya wakuunga mkono Mh Rais kwenye suala lako la uwekezaji wa Bandari. Yeye Spika ameambiwa na nani kwamba suala la uwekezaji bandarini ni la Mh. Rais na sio Serikali ya Tanzania na Duba? MoU baina ya kuhusu bandari ilisainiwa na TPA na DPW sasa Mheshimiwa Rais ametokea wapi.

Ina maana hili suala la Bandari mpotoshaji mkubwa kwa Taifa ni Tulia Ackson ndiyo maana wenzake wa CCM wamegundua wamekosea wameamua kuliacha na kusema mkataba sio msahafu wala biblia, Serikali nayo imeshajitoa Rais hajawahi kuzungumzia kwa kina suala hilo sasa limebaki na Spika na Bunge lake waliopitisha jambo ambalo hawakujua lina madhara gani.
 
Rais Samia Suluhu Hassan ni kama amempotezea Spika wa Bunge baada ya kuzungumza kuwa watu wa Mbeya wanaunga mkono mkataba wa uwekezaji wa Bandari na kwamba hapo Mbeya kumekuwa na manen mengi kuhusu bandari...
Hiyo TAKATAKA Mbeya sijui waliitoa wapi sijawahi ona mnyakyusa hayawani kama huyo ptuuuh!
 
Rais Samia Suluhu Hassan ni kama amempotezea Spika wa Bunge baada ya kuzungumza kuwa watu wa Mbeya wanaunga mkono...
Rais Samia tupo smart sana. Nadhani Spika Tulia na Chawa wengine ndio wanalizimisha.

Mama endelea kuwapotezea
 
Dk. Tulia ni Mbunge wa Jiji la Mbeya, hivyo anawasemea Wana Jiji la Mbeya waliomchagua. Wewe unayebisha una mamlaka gani uliyokasimiwa kihalali na Wana Jiji la Mbeya?
Anawasemea wanambeya hao waliofungua kesi! Akili za tulia hazijatulia.
 
kwa hiyo mbeya kuna mwananchi mmoja
 
Huyu betina lazima ni mchawi,sio bure.
 
Ee Mungu ikupendeze na mapenzi yako yatimizwe.
 
haka nako kapumbavu kama wapumbavu wenzie
 
Hapo ndipo mnapokosea viongozi wa tz kulazimisha watu vitu wazivyovitaka ,kwenye daladala watu wanapinga,kwenye bajaji watu wanapinga,mikunyiko yaina yeyote ukisikiliza wananchi wanapinga sasa sijui research hiyo mnafanya kwa kusikiliza maoni ya machawa au ya watanzania. Maana swala kama LA bandari ni pana halinabudi maoni yake yasiwe ya kiitikadi bali mapana na marefu kwa bustakabali wa kizazi kijacho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…