kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu, hivi ni kweli sababu ya Bunge lako kuongeza tozo kwenye miamala ya simu ni kumalizia upatikaji wa barabara, maji, madawati, madarasa, na zahanati katika kila kijiji kabla ya 2025?
Naungana na wewe 100% kuwa hakuna mfadhili atakuja kutujengea nchi yetu, hivyo ni jukumu letu kujikamua wenyewe kwa hali na mali kulijenga taifa letu kwa nguvu zetu.
Hata hivyo, Tanzania hakuna mtu asiyelipa Kodi. Kila huduma na kila bidhaa ina kodi ndani yake ambayo mtumiaji lazima ailipe. Lakini kuna Kodi za mapato, tozo, biashara na huduma pia. Mtu anayelipa PAYE atalipa tena kodi mbalimbali kwa kutumia hela yake iliyobaki baada ya kulipa PAYE.
Tatizo letu kubwa sio mapato, ni matumizi, vipaumbele, usimamizi mbaya na wizi wa fedha za umma, hata wewe unafahamu hili, ripoti za CAG zinaonyesha kila mwaka.
Kama taifa tuliamua kutumia fedha zetu kuboresha umajumuni wa Afrika badala ya kusambaza maji kwa watu wetu.
Kama taifa tunagharamia kuendesha siasa zetu kwa gharama kubwa sana bila sababu za msingi badala ya kupeleka pembejeo za kilimo na masoko kwa watu wetu ili walime kwa tija.
Kama taifa tunaanzisha miradi ambayo haisaidii kuongeza uchumi wa taifa.
Kama taifa tuna rasilimali nyingi sana, maji, ardhi, madini, wanyama pori, mifugo, na misitu ambazo hatujafanya vyakutosha kwenye rasilimali hizi kupata fedha ili kuepuka aibu ya kama Bunge kufikiria kuongeza gharama kwa machinga anaetembeza mashati 3 mkononi anayetaka kumtumia hela bibi yake aliyeko kijijini ili anunue chumvi na mafuta yaa taa. Nijuavyo mimi hela nyingi kwa kutumia simu huwa zinatumwa kutoka mijini kwenda vijijini waliko wategemezi wao ambao wana njaa, misiba, wagonjwa na shida nyingine huko vijijini.
Inatia Mashaka makubwa kuwa na Bunge lenye wabunge ambao hawawezi kufikiria namna tutakavyoweza kuchima chuma, dhahabu, kuboresha kilimo na mifugo, kuvua samaki baharini, kutumia misitu yetu na mbuga ili kupata hela kubwa ya kulihudumia taifa na watu wake badala yake wanawaza kuvitoza pesa vibabu vilivyotumiwa vijisenti vya kujikimu na wajukuu zao.
Kama ni lazima tozo hiyo iwepo, basi ingeazia kwa watu watakaotuma sh. 300,000 na kuendelea lakini sio sh. 5000, 10,000 au 50,000.
Dawa kubwa ni kuchagua kipi kijengwe Leo na kipi kinaweza kusubiri kesho.
Naungana na wewe 100% kuwa hakuna mfadhili atakuja kutujengea nchi yetu, hivyo ni jukumu letu kujikamua wenyewe kwa hali na mali kulijenga taifa letu kwa nguvu zetu.
Hata hivyo, Tanzania hakuna mtu asiyelipa Kodi. Kila huduma na kila bidhaa ina kodi ndani yake ambayo mtumiaji lazima ailipe. Lakini kuna Kodi za mapato, tozo, biashara na huduma pia. Mtu anayelipa PAYE atalipa tena kodi mbalimbali kwa kutumia hela yake iliyobaki baada ya kulipa PAYE.
Tatizo letu kubwa sio mapato, ni matumizi, vipaumbele, usimamizi mbaya na wizi wa fedha za umma, hata wewe unafahamu hili, ripoti za CAG zinaonyesha kila mwaka.
Kama taifa tuliamua kutumia fedha zetu kuboresha umajumuni wa Afrika badala ya kusambaza maji kwa watu wetu.
Kama taifa tunagharamia kuendesha siasa zetu kwa gharama kubwa sana bila sababu za msingi badala ya kupeleka pembejeo za kilimo na masoko kwa watu wetu ili walime kwa tija.
Kama taifa tunaanzisha miradi ambayo haisaidii kuongeza uchumi wa taifa.
Kama taifa tuna rasilimali nyingi sana, maji, ardhi, madini, wanyama pori, mifugo, na misitu ambazo hatujafanya vyakutosha kwenye rasilimali hizi kupata fedha ili kuepuka aibu ya kama Bunge kufikiria kuongeza gharama kwa machinga anaetembeza mashati 3 mkononi anayetaka kumtumia hela bibi yake aliyeko kijijini ili anunue chumvi na mafuta yaa taa. Nijuavyo mimi hela nyingi kwa kutumia simu huwa zinatumwa kutoka mijini kwenda vijijini waliko wategemezi wao ambao wana njaa, misiba, wagonjwa na shida nyingine huko vijijini.
Inatia Mashaka makubwa kuwa na Bunge lenye wabunge ambao hawawezi kufikiria namna tutakavyoweza kuchima chuma, dhahabu, kuboresha kilimo na mifugo, kuvua samaki baharini, kutumia misitu yetu na mbuga ili kupata hela kubwa ya kulihudumia taifa na watu wake badala yake wanawaza kuvitoza pesa vibabu vilivyotumiwa vijisenti vya kujikimu na wajukuu zao.
Kama ni lazima tozo hiyo iwepo, basi ingeazia kwa watu watakaotuma sh. 300,000 na kuendelea lakini sio sh. 5000, 10,000 au 50,000.
Dawa kubwa ni kuchagua kipi kijengwe Leo na kipi kinaweza kusubiri kesho.