Spika Ndugai ahoji kwanini pesa zinakwama Wizara ya Fedha. Amtaka Waziri kujiandaa akisema "Siku ya Wizara yake nitakamata shilingi mwenyewe"

Spika Ndugai ahoji kwanini pesa zinakwama Wizara ya Fedha. Amtaka Waziri kujiandaa akisema "Siku ya Wizara yake nitakamata shilingi mwenyewe"

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai leo amehoji kwanini Fedha zinakwama Wizara ya Fedha akimtaka Waziri kujiandaa akisema, "Siku ya Wizara yake nitakamata Shilingi mimi mwenyewe"

Ndugai ametoa kauli hiyo Bungeni Dodoma wakati Bunge likijadili Hotuba ya Wizara ya Nchi - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Ameeleza, "Bunge tunaweza kuweka 'pressure' lakini sio vizuri tuiweke mahali ambapo hakuna sababu. Waziri nataka majibu, Fedha zinazokuja kwa ajili ya mazingira zinakwama Wizara ya Fedha kwa sababu gani? Mpaka inafika mahali zinataka kurudishwa"

Ameongeza, "Kwanini Fedha inaombwa inakuja katika Nchi yetu Wizara ya Fedha mnakalia eti kisa Kamati haijakaa. Katika jambo hilo tunataka badiliko"
 
Kwa hiyo hata mama aliposema kuhusu hilo suala bado wanaendeleza mambo yao?
 
Na wadanganyika wanaamini,kuna msemo unatumika huko Zenji waarabu wa Pemba wanajuana kwa vilemba,kauli ya ****** unaweza kuichomeka hapo kati yake na mwiguru.
 
Sio fedha za mazingira tu zinazokwama huko wizarani bali fedha za misaada kwa miradi yote. Kwa kutambua changamoto hii wafadhili waliamua kutoipa pesa moja kwa moja wizara ya afya kwa ajili ya mradi wa kupambana na usugu wa vimelea dhidi ya antibiotiki (Antimicrobial Stewardship Program). Badala yake gharama zote za kuendesha mradi huu zinalipwa juu kwa juu na wafadhili wenyewe.
 
Sio fedha za mazingira tu zinazokwama huko wizarani bali fedha za misaada kwa miradi yote. Kwa kutambua changamoto hii wafadhili waliamua kutoipa pesa moja kwa moja wizara ya afya kwa ajili ya mradi wa kupambana na usugu wa vimelea dhidi ya antibiotiki (Antimicrobial Stewardship Program). Badala yake gharama zote za kuendesha mradi huu zinalipwa juu kwa juu na wafadhili wenyewe.
Wizara ya fedha ni janga kubwa sn
 
Nyie endeleeni kudemka huko mjengoni, Sie tuko ktkharakati za kulisuka upya Binge na kupata spika makini.
 
Kumbe wazalendo walikuwa wanaomba fedha kwa mabeberu tu pamoja na kelele zote zile?!
 
Hizo fedha nyingi Tanganyika wametembeza bakuli la omba omba toka nchi kiarabu Oman na kwengineko ambako walikuwa wakimsema maalim seif kwamba waarabu wabaya sijui watarudi kuitawala zanzibar., Sasa tunaona waarabu wanainyemelea Tanganyika kuitawala badala yake
 
Back
Top Bottom