Spika Ndugai amesema kuna upotoshaji mwingi unaendelea nchini, adai kuna wakati sheria za hovyo zinapitishwa bungeni

Spika Ndugai amesema kuna upotoshaji mwingi unaendelea nchini, adai kuna wakati sheria za hovyo zinapitishwa bungeni

Amesema ukweli mtupu. Hali ndio iko hivyo. Bunge linadharaulika kwa sababu hiyo tu. Sheria nyingi za Tanzania, source yake ni cabinet; Na cabinet hupokea kutoka kwa watendaji waliopo chini ya wizara yake. Na bunge linapokea bila kufanya critical analysis na changes kwa maslahi mapana ya Taifa.
Sasa bunge kama chombo cha wananchi si ndio kilitakiwa kihakikishe hizo sheria mbovu hazipiti.
Na spika anaachaje wabunge wanasambaratika?
 
Ni upuuzi kusingizia ukabila, in other hand hi's right.
 
Kwa 100% kuna matatizo ya uteuzi au kuwachagua viongozi wa muhimili mbalimbali, historia zao, uwezo wao na weledi wao haviangaliwi kwa makini ndio maana tunakuwa na viongozi kila kukicha wanaropoka hovyo na hawakawii kuja kukana kauli zao!
Tuchukue hatua
 
Akiwa kwenye kongamano lililokuwa limeandaliwa na vijana wenyeji wa dodoma ambapo alialikwa kama mgeni rasmi katika kongamano hilo, spika Ndugai amedai kuwa kuna upotoshaji mwingi sana unaendelea nchini.

Akitolea mfano suala la yeye kupingwa, Ndugai amesema anapingwa si kwa sababu ana pungufu lolote isipokuwa ni kwa sababu anatoka kwenye kabila la wagogo.

"Kuna baadhi wananiandika kila kukicha siyo kwa sababu nina pungufu lolote ila ni kwakuwa mimi ni mgogo" alisema.

Pia, alisema wengi wanaomchafua na kupotosha ni vijana wenye elimu ya juu 'digrii' kwamba badala ya wao kufanya kazi wanatumia simu zao za mkononi kumtukana mitandaoni.

" Darasa la saba ndiye mtoto mwenye maana kwa mzazi kwa sababu ukimwambia lima ana lima ila huyu wa digrii yeye ana simu ya mkononi, yupo kwenye makundi ya kutukana utasikia wanasema huyu spika bure kabisa huyu kisa wana digrii" alisema Spika Ndugai na kuongeza.

Katika hatua nyingine spika Ndugai amesema kuna upotoshaji unafanyika wakati wa upitishwaji wa sheria bungeni. Amesema kuna muda bungeni zinapitishwa sheria za hovyo kabisa.

Akitolea mfano wa marekebisho ya sheria mbali mbali 'miscellaneous amendments' amedai kuwa zinawasilishwa bungeni zikiwa vipande vipande tena kipindi ambacho wabunge wamesambaratika sehemu mbali mbali hivyo sheria hizo zinapata mwanya wa kupita kutokana na kutokuwepo kwa organization ya wabunge na pale mambo yanapoharibika linalaumiwa bunge kumbe kanuni zinakuwa zimetungwa na kupitishwa na wakurugenzi, taasisi na mawaziri wa wizara husika
View attachment 2061917
Jamani si ndiyo huyu huyu, aliyepitisha azimio la kpongeza kushinda kiti cha MWENYEKITI wa sadcc, kawati akijua ni uongo mtupu, kiti hakishindaniwi Bali ni kwa majibu wa Kati a ya jumuia hiyo. Sasa Omani kwake itatoka wapi?
 
Kwa 100% kuna matatizo ya uteuzi au kuwachagua viongozi wa muhimili mbalimbali, historia zao, uwezo wao na weledi wao haviangaliwi kwa makini ndio maana tunakuwa na viongozi kila kukicha wanaropoka hovyo na hawakawii kuja kukana kauli zao!
Tuchukue hatua
Nchi kama ipo serious haiwezi kuwa na Spika mpuuzi kama huyu mzee
 
Anachotaka kusema hapa ni kuwa serikali inapitisha miswada kwa kuvizia attendance ya wabunge??

Kama ameliona hilo anapaswa kuwakatalia kwa kuhakikisha kuwa miswada inajadiliwa kukiwa na mahudhurio ya kutosha ya wabunge.

Hapo tunaanza kuulizana National Interest ni ipi??
 
Amesema ukweli mtupu. Hali ndio iko hivyo. Bunge linadharaulika kwa sababu hiyo tu. Sheria nyingi za Tanzania, source yake ni cabinet; Na cabinet hupokea kutoka kwa watendaji waliopo chini ya wizara yake. Na bunge linapokea bila kufanya critical analysis na changes kwa maslahi mapana ya Taifa.
MH SIAMINI HAYA KABISA KWELI KABISA SUPIKA WETU WA BUNGE ANAWEZA KUSEMA SHERIA MBOVU ZINAPITISHWA KWENYE BUNGE LAKE?!?!!? HALAFU YEYE MWENYEWE AZILALAMIKIE?!? HIVI TUULIZANE NI NANI ANYEPELEKA SHERIA ZILIZOPITISHWA NA BUNGE KWA RAIS?!?. NAANZA KUAMINI SUPIKA KUNA KITU KICHWANI MWAKE KIMELEGEA SUKURUBU IMEACHIA MEDULA OBLANGATA, ANAHITAJI KURUDI INDIA!!. HIVI KWELI SUPIKA NAKIMBILIA KWENYE UGOGO,UKABILA?!?!, USOMI, DARASA LA SABA?!?! HIZO NI HOJA KWELI ZA KUTULETEA HAPA KAMA VILE SISI WATZ WOOOTE NI MBUMBUMBU!!??!, NO HATUKO MAZEZETA KIASI HICHO
 
MH SIAMINI HAYA KABISA KWELI KABISA SUPIKA WETU WA BUNGE ANAWEZA KUSEMA SHERIA MBOVU ZINAPITISHWA KWENYE BUNGE LAKE?!?!!? HALAFU YEYE MWENYEWE AZILALAMIKIE?!? HIVI TUULIZANE NI NANI ANYEPELEKA SHERIA ZILIZOPITISHWA NA BUNGE KWA RAIS?!?. NAANZA KUAMINI SUPIKA KUNA KITU KICHWANI MWAKE KIMELEGEA SUKURUBU IMEACHIA MEDULA OBLANGATA, ANAHITAJI KURUDI INDIA!!. HIVI KWELI SUPIKA NAKIMBILIA KWENYE UGOGO,UKABILA?!?!, USOMI, DARASA LA SABA?!?! HIZO NI HOJA KWELI ZA KUTULETEA HAPA KAMA VILE SISI WATZ WOOOTE NI MBUMBUMBU!!??!, NO HATUKO MAZEZETA KIASI HICHO. NAANZA KUKUMBUKA ISSUE YA PROF. ASSAD KUANZIA REPORT YAKE YA UKAGUZI MPAKA HOJA YA BUNGE NI DHAIFU. SUPIKA KATUHAHAKISHIA ASILIMIA MIAMOJA BILA KUBAKIZA KWAMBA KWELI BUNGE NI DHAIFU HASWAA!! KWA KUSEMA SHERIA MBOVU ZILIPITISHWA BUNGENI
 
Back
Top Bottom