Sure. Watu kama Kimei, Walitakiwa wawe wametulia sasa lakini sijui wanapambania niniSiyo ukomo wa ubunge tu sekita zote ziwe na ukomo Kama ilivyo kwenye uraisi kuanzia ubunge, uwaziri, ukuu wa wilaya, mkoa maana ni sekita za kuleta amsha amsha alafu watoke waingie wengine. Na serikali kuu na taasisi hivyo hivyo zile zinazozidisha miaka sitini ziangaliwe upya Ili vijana wakatumike.
Ngoja waandamane..watamkimbiza huyu.Amekula akashiba ameendelea kula sasa Ndugai kavimbiwa. CCM imeshindwa kutatua tatizo la ajira imebaki kusimanga tu vijana. Upumbavu mtupu wanajadili uko bungeni
Halafu pool haiingizi hela, na kisha biashara ya pool kufungwa.Leo nimejifunza kitu. Kazi ya Afisa Maendeleo ya Jamii ni kuhakikisha kila mtu anafanya kazi. Kwa vile hao Maafisa Jamii hawafanyi kazi zao kama ajira yao inavyowaelekeza, basi watu wengi wanaishia kucheza pool toka asubuhi hadi usiku. Ili kuondokana na hili tatizo, Zumbe Mkuu atawashauri na kuwaagiza Wazumbe wengine kupandisha kodi ya hizo pool. Kodi ikipanda wacheza pool wataacha kucheza mchezo huo na kuanza kufanya kazi.
Kuna watu wanayasoma haya matatizo kwenye vyombo vya habari lakini hayajawahi kuwapitia angalau karibu.Unadhani wanapenda?Hebu kafanye utafiti vizuri. Hadi watu kufikia hatua ya kunywa urabu wanakuwa wamekata tamaa.
Kuna descouragement nyingi sana katika nchi hii. From kukamatwa mifugo hadi kukatwa kwa mazao yaliyoko shambani.
Yaani kuna ile kila unapojaribu kufanya kitu, **** mtu anajiita afisa wa serikali anakwambia umevunja sheria. Anataka ulipe faini kubwa kuliko hata thamanni ya kila kitu unachomiliki hapa duniani.
Kama hayajawahi kukukuta shukuru mungu.
📌📌🔨🔨 Mbona tukibet kwa smartphone tukishinda wanakata kodi yao si watuache tuAjira washindwe kutupa hadi smartphone📱 watupangie matumizi
Watuache tutafute hela kupitia njia shirikishi
Vijana wanafuatilia jinsi nchi yao inavyoporomokea shimoni kupitia kinachofanyika hapo dodoma, vinginevyo wajitahidi kubadili hali ya mambo muda huu wa majeruhi.Dah! Maskini Tanzania yangu. Yaani haoni kabisa ajira hakuna na fao la kujitoa walilifuta. Rudisheni basi fao la kujitoa ili tujiajiri maana serikali uwezo wa kufikiri umefikia kikomo. Nilisema serikali ipo nyuma ya vifurushi vya mitandao ya simu kupanda.
Mimi nashangaa kwa sasa mjadala mkubwa duniani na kwenye baadhi ya bunge ni issue ya covid hapa kwetu hizo ndiyo akili zilipoishia.Yeye kiongozi mwenyewe anasema hajui cha kufanya.
Kwa nini asiwe sehemu ya tatizo badala ya sehemu ya ufumbuzi wa tatizo?
Marry AntoneitteWaongeze kodi!!? Hivi hawa huwa hawasomi historia? Hiyo kauli inatofauti gani na Malkia wa Ufaransa ambaye baada ya watu kulia kuwa hawana mikate akawaambia kama hawana mikate wale keki!!?.
Mtu hana ajira halafu unamuongezea kodi?!
Nakushauri kaombe special seat bungeniWatu wengi wanaofanikiwa wanatokea kwenye mazingira haya haya miaka nenda rudi wengine wanalalamika maisha magumu Vijana wengi wa kitanzania ni wavivu kuna Makundi mengi ni tegemezi hawataki kujishughulisha mfano hawa vijana wanywaji wa pombe za kienyeji ,watumiaji wa Instagram,vijana wa kubeti nk
Taifa halina mpango wowote ule kwa vijana wa rika la 18 - 30 ambao hawana nafasi ya formal education.Kutoka Dodoma.
"Tunatengeneza vijana wa kucheza Pool table, ambao wakikaa na simu wanaperuzi mitandaoni tu".
"Nafikiri labda tuongeze kodi labda itapunguza hata sijui, hivi tufanye kitu gani ili tuhakikishe kila mtu anafanya kazi, maafisa maendeleo ya jamii hawafanyi kazi" -Job Ndugai.
Nini maoni yako mdau?
Hii nchi ya hovyo sometime wakati nataka kufungua Maabara ilinichukua mieizi 4½ tangu nimeomba kibali mpaka kufungua na duka la dawa miezi 2½...wanakatisha sana tamaa hawa watu.Unadhani wanapenda?Hebu kafanye utafiti vizuri. Hadi watu kufikia hatua ya kunywa urabu wanakuwa wamekata tamaa....
Kutoka Dodoma.
"Tunatengeneza vijana wa kucheza Pool table, ambao wakikaa na simu wanaperuzi mitandaoni tu"...
Mwambieni Ndugai kua hua hatuperuzi Bali Tunatandika mikeka ndo ajira zetu zilikobakia huko ambako unakutana na mshahara wako kwa mujibu wa ongezeko la timu tu. Yaani kule tunajipangia wenyewe. Kama wao hawana ajira za kutupa.Kutoka Dodoma.
"Tunatengeneza vijana wa kucheza Pool table, ambao wakikaa na simu wanaperuzi mitandaoni tu".
"Nafikiri labda tuongeze kodi labda itapunguza hata sijui, hivi tufanye kitu gani ili tuhakikishe kila mtu anafanya kazi, maafisa maendeleo ya jamii hawafanyi kazi" -Job Ndugai.
Nini maoni yako mdau?