Sri Lanka: Wananchi wayatumbukiza kwenye maji, wayachoma magari ya kifahari ya wanasiasa kisa ugumu wa maisha

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Your browser is not able to display this video.
Wakati maandamano yakiendelea Nchini Sri Lanka inadaiwa kuwa hivi ndivyo baadhi ya wananchi walivyoamua kushusha hasira zao kwa familia ya Rajapaksa ambayo inatawala nchini humo.

Wameamua kuyachoma na kuyatupa ndani yam aji magari ya kifahari ya wanasiasa hasa kutoka familia hiyo

Watoto na ndugu wa familia hiyo wanamiliki magari ya mengi ya kifahari ikiwemo Rolls Royce, Lamborghini, Ferrari, Mclaren.

Wananchi wanalalamika hali ya maisha ni ngumu wakati familia hiyo inaishi kitajiri.

Your browser is not able to display this video.



Source: Newschecker.in
 


Wapumbavu hao wananchi, kwanini wanachoma magari??!! Badala ya kiyapiga mnada na pesa zinazopatikana zitumike kwa ajili ya shughuli ya umma!!!.
 
Wapumbavu hao wananchi, kwanini wanachoma magari??!! Badala ya kiyapiga mnada na pesa zinazopatikana zitumike kwa ajili ya shughuli ya umma!!!.
Wapige mnada kwa kina nani, hao watakaowauzia ndo wenye magari mkuu [emoji23]

Muda hautoshi, bora nusu shari, kuliko shari kamili

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Basi wanachofanya hao wananchi ni uhalifu.
Acha wawakomeshe hao viongozi sera zao mbovu zimeifanya nchi iingie kwenye madeni makubwa na uchumi kuanguka huku wao wakila raha.
 
Hii ilibidi ije kwenye familia ya makamba,kikwete,mwinyi.Nchi inakuwa ya kiukoo,hali mbaya kila mahali.
 
Acha wawakomeshe hao viongozi sera zao mbovu zimeifanya nchi iingie kwenye madeni makubwa na uchumi kuanguka huku wao wakila raha.


Kuharibu mali ni uhalifu pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…