Pre GE2025 Stephen Wasira atua kibabe na Ndege ya kibabe Mkoani Songwe. Kuwasha moto kwa siku tatu mfululizo bila kupumzika

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Chuma cha Reli, Mwamba Mwenyewe ,Nguli wa Siasa na Jabali la siasa Stephen Wasira Makamu Mwenyeki wa CCM Taifa Ametua kibabe kwelikweli katika uwanja wa ndege wa Songwe . kwa ajili ya kuanza ziara katika mkoa wa Songwe. Ambako anatarajiwa kuwasha Moto πŸ”₯ mkali kwelikweli kwa siku tatu mfululizo bila kupumzika.

Kabla ya kuweka miguu yake chini alipokelewa na kulakiwa na viongozi mbalimbali ngazi ya mkoa wakiwemo Mkuu wa Mkoa wa songwe Mheshimiwa sana Daniel Chongolo , Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Songwe Ndugu Radwell Mwampashe na viongozi wengine wengi sana wakiwepo wabunge mbalimbali wa Mkoa wa Songwe.

Akiwa mwenye tabasamu ,furaha na bashasha,nguvu na stamina Mheshimiwa Wasira alisalimiana na viongozi hao kikakamavu kabisa kama komandoo aliyetoka Kumaliza mafunzo yake na kufaulu vyema kabisa.

Tayari wananchi wa mkoa wa songwe wanashauku kubwa sana ya kumsikiliza na kumpokea Makamu wetu wa CCM Taifa. Hii ni kutokana na kutambua uchapakazi wake,uhodari wake na uzalendo wake uliotukuka katika utumishi wa umma na namna alivyojitoa na kujitolea Maisha yake kwa ajili ya chama na Taifa letu.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Hiyo ndege ndiyo latest model ya Gulfstream 700. Ndiyo G700 pekee Africa.
 
Marehemu stieven wasira....
 
CCM inafanya siasa na wapiga kura CHADEMA inafanya siasa na watu wa Angola.Mkishindwa uchaguzi mbaanza kulalamika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…