Ndugu zangu Watanzania,
Chuma cha Reli, Mwamba Mwenyewe ,Nguli wa Siasa na Jabali la siasa Stephen Wasira Makamu Mwenyeki wa CCM Taifa Ametua kibabe kwelikweli katika uwanja wa ndege wa Songwe na kwa ajili ya kuanza ziara katika mkoa wa Songwe.Ambako anatarajiwa kuwasha Moto 🔥 mkali kwelikweli kwa siku tatu mfululizo bila kupumzika.
Kabla ya kuweka miguu yake chini alipokelewa na kulakiwa na viongozi mbalimbali ngazi ya mkoa wakiwemo Mkuu wa Mkoa wa songwe Mheshimiwa sana Daniel Chongolo , Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Songwe Ndugu Radwell Mwampashe na viongozi wengine wengi sana wakiwepo wabunge mbalimbali wa Mkoa wa Songwe.
Akiwa mwenye tabasamu ,furaha na bashasha,nguvu ,stamina Mheshimiwa Wasira akisalimiana na viongozi hao kikakamavu kabisa kama komandoo aliyetoka Kumaliza mafunzo yake na kufaulu vyema kabisa.
Tayari wananchi wa mkoa wa songwe wanashauku kubwa sana ya kumsikiliza na kumpokea Makamu wetu wa CCM Taifa. Hii ni kutokana na kutambua uchapakazi wake,uhodari wake na uzalendo wake uliotukuka katika utumishi wa umma na namna alivyojitoa na kujitolea Maisha yake kwa ajili ya chama na Taifa letu.
View attachment 3269466View attachment 3269467View attachment 3269468View attachment 3269469View attachment 3269471
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.