Suala la Bandari TEC hawakupata kama walivyozoea

Hivi ukiwa muislamu ni lazima uwe mjinga? Maana kati ya wajinga 10 basi utakuta 10 ni waislamu!
Ryzen,
Utafiti huu wa kati ya wajinga 10 utakuta 10 ni Waislam umeufanyaje ili nami niurudie kuhakikisha matokeo ya utafiti wako.

Hebu tuangalie hapa chini:

Katika waasisi tisa wa African Association 1929 Dar es Salaam sita ni Waislam: Kleist Abdallah Sykes, Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima na Suleiman Majisu.

Hawa ndiyo waliojenga ile nyumba kilipozaliwa chama cha TANU 1954.
Ujinga wa Waislam uko wapi?

Wajumbe wa TAA Political Sub Commitee 1950 walikuwa saba wanne Waislam na yumo Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Hamza Mwapachu na Abdul Sykes.

Hawa ndiyo walijenga msingi wa kuunda chama cha TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ujinga wa Waislam uko wapi?

Wanachama shupavu wa TANU Dar es Salaam: Sheikh Suleiman Takadir, Jumbe Tambaza, Mshume Kiyate, Mwinyijuma Mwinyikambi, Rajabu Diwani, Makisi Mbwana, Sheikh Haidari Mwinyimvua, Iddi Faizi Mafongo, Idd Tosiri, Sheikh Mohamed Ramia, Iddi Faizi, Iddi Tulio, Mashado Ramadhani Plantan na Schneider Abdillah Plantan.

Ujinga wa Waislam uko wapi?
Tuje kwa wanawake.

Sijui kama umepata kuyasikia majina haya katika wanachama wa mwanzo wa TANU: Tatu bint Mzee, Halima Khamis, Mwamtoro bint Chuma, Hawa bint Maftah, Nyange bint Chande, Zarula bint Abdulrahman, Shariffa bint Mzee, Mama bint Mwalimu, Fatma Matola, Amina Kinabo, Halima Selengia, Sophia Mustafa kwa kuwataja wachache.

Hawa wote naijua michango yao katika kupigania uhuru wa Tanganyika ukiwa utapenda naweza nikakuwekea hapa.

Ujinga wa Waislam uko wapi?
Waswahili tuna msemo, ''Akutukanae hakuchagulii tusi.''

Leo uhuru umepatikana na mnafaidika nao ijaza yetu ni kututukana?

Mama zetu na shangazi zetu wengi walinunua kadi za TANU kujiunga na mapambano ya kudai uhuru wa Tanganyika kutoka kwa Bi. Tatu bint Mzee.


Tatu bint Mzee Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya TANU

Mwamtoro bint Chuma​
 
Mohamed, nimekushauri sana kwamba kuna sehemu ya jamii inakuona ni ''KOL'
Kauli au maandishi yako kuna wakati yanakuwa si maoni yako bali ya jamii .

Nilikusihi katika bandiko # 46 kwamba ulifute bandiko lako #1.. Katika bandiko # 47 ukasema sijasema lolote kuhusu video ya Ansbert na kwamba niliona ni salama ufute. Katika bandiko# 54 nikajibu hoja zaidi ya 5 kutoka bandiko #1.

Kinachosikitisha ni wewe kutotaka kujadili uliyoyaleta hapa jamvini kama hoja #1 inavyosema.
Inashangaza unaleta mambo nje ya mada. Kama kawaida picha na visivyo na uhusiano na mada ili kukwepa hoja.

Mara nyingi umejinasibu kuhusu paper ulizoandika na kuziwasilisha. Kwa staili hii ya mjadala unaacha maswali mengi kuliko majibu. Ningependa niwe peke yangu katika fikra hizo! niamini kuna tatizo!

Mohamed ukileta jambo hapa uwe tayari kwa mjadala na si mjadala tu bali pia kutetea hoja zako kwa mantiki.

Umeweka mada, halafu unatuletea habari za kumuona Nyerere, Mtikila n.k. miaka 20 hawapo Duniani.
Ukitazama wanahusiana vipi na Ziara ya Rais Vatican hakuna jibu.

Niishie hapa maana! dah
 
Nguruvi3,
Unajua tofauti kubwa kati yako na mimi ni kuwa wewe uko hapa umeficha jina lako, sura yako na sauti yako.

Mimi niko hapa kwa jina langu halisi, kwa sura na sauti.

Wewe umejificha mimi sijajificha.
Hebu jitokeze ufahamike.
 
Walikurupuka kudai uhuru
 
Leo nimethibitisha yale niliyoshuku kwa muda mrefu. Mohamed una tatizo la schizophrenic disorder wahi hospitali
 
Duh...!. Mkuu Mohamed Said, kwa idhini yako naomba kupandisha bandiko based on this dataz!.

P
 
Leo nimethibitisha yale niliyoshuku kwa muda mrefu. Mohamed una tatizo la schizophrenic disorder wahi hospitali
Mwenye tatizo hilo si mimi.
Ngoja nikupe stori.

Kwa mara ya kwanza mimi kuandika makala na ikachapwa Ulaya ilikuwa mwaka wa 1988.

Makala hii "In Praise of Ancestors," ilichapwa na Africa Events na ilikuwa inaeleza historia ya Abdul Sykes katika kuunda chama cha TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Gazeti lote lilikusanywa kutoka kwa wauzaji mitaani wakipita watu na kununua nakala zote kwa wauza magazeti.

Sasa katika hali kama hii mgonjwa nani?

Leo najibu video anakuja mtu ananiambia nifute majibu yangu yaliyoko JF na tayari mtandaoni yanasomwa.

Naweka video la somo hilo hilo la Waarabu na bandari ili nieleweke zaidi unakuja wewe na hoja kuwa nahitaji kupewa kitanda hospitali kwani nina maradhi.

Ajabu yake ni hii.
Wengine wakinisoma wananialika kwenye vyuo vikuu vyao nikazungumze.

Wengine wananiomba waniingize katika miradi yao ya uandishi wa historia ya Afrika.

Wachapaji vitabu wanachapa miswada yangu inakuwa vitabu wanauza.
Mimi akili yangu timamu na imekamilika.

Alhamdulilah.

 
Hapa, nilidhani ungemjibu wa post #54 kuhusu;
1. Mahusiano ya maoni ya CHADEMA na TEC juu ya vifungu vya mkataba wa DP na udini?
2. Maoni yako binafsi, kifungu kwa kifungu, juu ya vile vifungu vilivyolalamikiwa, ili uje utuonyeshe kwamba ile ilikuwa ni vita ya kidini na Waislamu wameshinda.
3. Uhusiano wa UBORA wa mkataba wa bandari na udini

Ukiyajibu haya, unaweza kutushawishi. Na unapojibu, usikimbilie kwa Mwl Nyerere na waanzilishi wa TAA, wala Mtikila na Mwinyi, wala historia yako ya uandishi, na tuzo, na mialiko yako. Tushawishi kwa hoja za mkataba wa bandari, vipi uislamu umeshinda. Zaidi ya hapo, unajiaibisha mzee wangu
 
Van...
Unataka nikujibu kama utakavyo wewe?
Hili mbona haliwezekani?

Binadamu tumeghitililafiana katika kuwaza.
Wala sikimbilii kwa yoyote awaye yule.

Huo ndiyo msingi wa kuelewa vipi wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika hatukuwaona TEC na mfano wa TEC au Mtikila na mfano wa Mtikila.

Hapo ni wewe kujiuliza kwa nini hawakuwapo katika harakati za kupigania uhuru?

Kitu kikubwa katika kalamu yangu ni kule kukupeni historia ambayo nyinyi hamkupata hata siku moja kuisikia ikisomeshwa si shule ya msingi, sekondari na vyuoni.

Kwengine ninapoalikwa kuzungumza maswali nipatayo ni tofauti sana na maswali nipokeayo hapa.

Hapa historia hii inawakasirisha.
Huko kwengine historia hii inawashangaza.

Mathalan wataniuliza inakuwaje Idara ya Historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na katika vyuo vikuu vingine havijaweza kutafiti na kuandika historia hii?

Wananiuliza kuhusu mashujaa waliopigania uhuru wa Tanganyika baada ya mimi kuandika historia zao kimetokea nini?

Wametambuliwa na juhudi zimefanywa kusomesha historia hii?

Hawanishutumu kwa udini.

Kalamu yangu haijapata kuniabisha.
Kalamu yangu imeniletea mengi.

Hapa JF angalia nimekuwa Mwandishi Bora mara mbili mfululizo mwaka wa 2021 na 2022.

Waislam wamenipa nishani mara mbili kwa kuandika historia ya Tanganyika kama inavyostahili kuandikwa.

Yapo mengi tu ya kufurahisha la kupata aibu hili sijakumbana nalo na namsshukuru Mungu.



Unamjua huyu Bwana Mkubwa Kabisa?

Library of Congress Washington DC
Ukimuona mtu anaingia humu basi jua ni mtu wa vitabu
 
Unazidi kuthibitisha hoja yangu
 
Unazidi kuthibitisha hoja yangu
Kinyungu,
Hilo si tatizo.

Wewe una hoja unaiweka hapa sote tunaisoma nami nakujibu kwa hoja yangu nayo inasomwa.

Hii ya kuthibitisha hoja itapendeza tukiwaachia wengine waseme.

Sababu ya kusema hivi ni kuwa mdomo haumkatai bwana wake.
 
ni kitu kibaya na cha huzuni sana kuwa mzee halafu unakuwa huna akili, miaka yote uliyoishi unakuwa haujajifunza, na haujawa na faida.

Mohamedsaid analalamika sana na anaamini waislam wanafelishwa tu kwenye mitihani, amesahau kuwa waalimu wanaofundisha na kusahihisha mitihani ya taifa ni wa dini zote, waislam pia wanasahihisha mitihani ya taifa ambayo huyu mzee anailalamikia. au tuamue siku moja tuwape marks za bure wote, hata waliopata zero.

pili, Zanzibar waalimu wote ni waislam, shule/skuli zao zinafundishwa na waislam, mitihani ya taifa inasahihishwa na waislam, na ni waaminifu kwelikweli marks wanaziweka sahihi, wanashika mkia miaka yote.

shida sio ubongo wa mwanadamu Muislam, shida ni tamaduni, utamaduni wa Muislam umewekwa kiupinzani sana na shule ya elimu dunia kiasi kwamba ukiwawe watu wawili mmoja mwenye utamaduni wa kiislam na mwingine utamaduni wa kikristo, mmoja atamzidi mwenzake kimasomo. ushahidi mzuri angalia wale waislam wasomi, wale ambao hawapotezi muda mrefu kwa mtoto wao kusoma madrasa, mtoto anaanza kusoma chekechea tangu akiwa mdogo anaunganisha primary badala ya kupoteza muda mrefu kumsubject kwenye madrasa na kukariri kuran. angalia nchi kama Uturuki ambako uislam wao sio wa siasa kali, wanajali elimu na hawapotezi muda kwenye mambo ya ajabu hayo. hayo yanawapotezea muda sana.

mwisho, Nyerere ili kuwafurahisha mashehe alinyang'anya shule nyingi sana za wakristo akazifanya za serikali ili tu tufanane, wote tusome. ajabu yake, hapakuwa na shule ya waislam hata moja ya kunyang'anya, wakristo tu ndo walinyang'anywa shule zilizojengwa kwa pesa ya sadaka za wazungu, wala sio pesa ya wabongo. ila hadi leo watu hawaridhiki. wamepewa chuo cha morogoro ili nao basi waonekane, lakin bado wanashindwa kushindana na st. augustine na vyuo vingine vya kikristo ambayo vinapokea hadi watoto wao, na kile cha morogoro kimejaa waislam watupu. lakini bado wanalalamika. hili zee ni mbumbumbu sana na yale mavitabu yake ya kusadikika. na ni mtu hatari kwa taifa hili.

huyu ndiye mzee aliyekuwepo kwenye fujo tangu za mwembechai kipindi kile, na siku zote amekaririwa akiwaita wakristo makafiri na anaamini hatutakiwi kuwa na umoja. kama unabisha sema niweke clip hapa. haya ndio mashetani ya amani ya Tanzania hii.
 
Hivi ukiwa muislamu ni lazima uwe mjinga? Maana kati ya wajinga 10 basi utakuta 10 ni waislamu!
Hahaaa mkuu hii comment yako mzee kaenda anzishia uzi fb nimecheka kama mwehu🤣🤣
 
Mkuu naomba hiyo clip
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…